Muhindi alieyeenda kukodi muuaji Afrika Kusini

South wamerithishwa tabia mbaya na wale wazungu ukiua kesi ni ndogo kuliko ukijeruhi kwa kisingizio kwamba majeruhi atatumia kodi za nchi kutibiwa lakini mfu ni kufukia tena kwa gharama za ndugu
 
Familia ya marehemu walikuwa wanatia huruma sana.Walikwenda SA na wakakaa miezi mitatu wakifuatilia hii kesi lakini mwisho wa siku waliambulia patupu wakarudi UK na majivu ya Binti yao tu.
 
Shrien dewan alimuoa anne dewan. Shrien ni mhindi mwenye uraia wa UK wazazi wake ni matajiri wanamiliki biashara ya majumba ya kutunza wazee wakati Anne Dewan alikuwa raia wa Uswiss naye mhindi. Walikutana UK, wakafall in love wakaoana fungate wakaelekea South.
Kwa madai ya aliyepanga mauaji msouth anayeitwa Tongo ndiye alidai kuwa walilipwa na Shrien kujifanya kama ilikuwa car hijack ambapo shrien walimteremsha wakaondoka na Anne ambaye alikuwa ana mkoba ambao Shrien alishawambia kutakuwa na malipo yao.
Hiki kisa kina viashairia kuwa Shrien alihusika ila pia kina mambo mengi yasiyo na majibu na ndio maana mahakama ya S.A ilimwachilia shrien maana hata polisi wa UK wanadai askari wa S.A walipoteza ushaihidi mwingi na inastaajabisha waliwahi kuingia makubaliano na Tongo haraka sana yani ndani ya siku moja kumpa kinga ya kutoshitakiwa awe kama shahidi.
Pia wanadai kesi hiyo ilikuwa na msukumo wa kutatuliwa kwa haraka kuokoa sekta ya utalii wa S.A maana mauaji hayo yalipata attention kubwa ya vyombo vya habari vya kimataifa.
Katika upelelezi iligundulika shrien ni shoga na sasa nadhani atakuwa ashaolewa maana hajifichi tena.
 
Kama shirien alikua ana hela msukumi upi ulikuwepo wa kumuua bidada?
Motive behind ilikua nini
 
Ishu inayofanana na hii iliwahi kutokea tena hukohuko Sauz. Mwanariadha mmoja maarufu wa nchini humo alimpiga risasi kwa bastola mke wake. Baada ya case kuendeshwa muda mrefu mahakamani, jamaa alijitetea kuwa hakuua kwa kukusudia, akaachiwa huru.
 
Si bora angenitupia mimi huyu mwanamke.
 
Kama shirien alikua ana hela msukumi upi ulikuwepo wa kumuua bidada?
Motive behind ilikua nini
Wanasema alikuwa anaishi double life. Alikuwa gay wa kisiri hataki jamii ijue na muda wa kuoa ulikuwa umefika. So akaoa kama ushahidi halafu akapanga kumuua mkewe maana hakuwa anamhitaji. Hiyo ndiyo motive.
Ila ukiachana na kuwa ni gay, kuna pia ushahidi unaonyesha kuwa alikuwa anampenda kweli anne dewan.
Unajua kabla hajaondoka S.A mara ya mwisho walipokutana na tongo alimpa bahasha ya ela tena walienda kupeana chooni. Polisi wanadai ndiyo yalikuwa malipo ya mwisho ya kazi ya kumuua anne dewan
 
Aisee
 
Mambo mengi yalikuwa captured na cctv camera ya hoteli waliyofikia kwa mfano, hlo la kupeana pesa chooni, baada ya mke wake kuambiwa akauawa alilia halafu baadae ikaonekana anazungumza na simu huku akicheka, masaa machache kabla ya mkewe kuuawa alimnyoshea vidole kwa ishara ya pistol kama anamshoot.
Kuna viashiria kibao lakini vyote ni circumstancial evidence
 
Daa,maisha haya jaman
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…