Wakati sakata la Flora likiendelea, bwana wake Mbasha amefunguka kwenye redio na kusema anasikitika sana mkewe kutaka kumfunga ili aendelee na uhuni wake na jamaa mmoja ambae anasema ni kigogo serikalini wakati wengi wakiongea mara Gwajima mara nani.
Mbasha amefunguka na kusema anajua mchezo mzima na aliepanga hilo na akasema hata akifungwa miaka 30 akitoka ni lazima afe na huyo kigogo liwalo.
Mbasha akaenda zaidi na kusema kuwa tokea zamani mkewe amekuwa akitongozwa na wakubwa na kumwambia mtu fudenge anataka tunda lake lakini tangu alipoanza kutukanana nae kuhusu huyo kigogo ameamua soln ni kumnyima tunda.
Sasa ameamua amfunge ili aendeelee na uhuni wake. Naamini Gwajjima atapumzika kwa statement hiyo na wengine waliohusishwa na Flora.
Nilisema na nitarudia tena sakata zima la Flora na mumewe ni wawili tu ndio wanajua chanzo na upumbavu unaoendelea juu yakee.
Akafunguka mtoto huyo wanaesema nimembaka nimemtoa mwenye kijijini na hata wanavyosema ana miaka 17 si kweli ..waende shule aliyosoma ama waangalie kadi yake ya kuzaliwa ana miaka 19.
Ujue hata mchezo wanaocheza hawana uhakika wanachoongea mwisho wa siku nawaambia watanzaniaMungu yupo na ukweli utafika utajulikana na Mungu atajiidhihirisha kwa hili, Ahsanten.
Nanukuu mbasha alivyoaga so sad kwa waliosikia hili.