Sasa huyo ndo Mwanaume sasa hana mbambamba siyo mnafiki.Bora wewe, Mie huyu Baba Kidogoli anafukuza hadi ndugu zake, hapa nilipo upande wa mume wanaona Mimi ndo nina roho mbaya, kumbe ndugu yao hana uvumilivu WA kuishi na ndugu....Yani ndugu akizingua asubuhi anakatiwa tiketi, hata Kama anasoma uhamisho utamkuta huko huko.
Nishamzoe mwenyewe, la msingi nguvu za kiume anazo, kibo na mawenzi ananifikisha wala sigombani nae, tabia zake apambane nazo mwenyewe.
Please usiwatenge ndugu zako sababu ya mume. Wanaume sisi hatutabiriki na sometimes tuna ujinga ujinga wetu wa kiume ( kuna nyapu nyingi nk nk)! Siku majanga yakikupata the only people watakaolia na wewe bila unafki ni ndugu zako wa kuzaliwa nao. So usithubutu kuwatenga kisa mume wako au unau-sugarcoat ubinafsi/ mapungufu yake!Asante kwa ushauri. Nishamwambia mara nyingi niambie
Kama nimfukuze basi ili nijue maana naona kila anachofanya ni kero. Hata mimi naumia unavosikitika najiona mimi ndo tatizo. Hajibu
Tatizo anamuamini sana mume wake as if ni malaika (hana tamaa).Wanawake bwana yaani kweli karne hii una muamini mwanaume kwa kumletea mdogo wako pisi kali nyumbani kwenu....aisee lazima nipite nae tuu.
Bado haitosaidia kwakuwa ww utafanya kwa lengo la kumuonesha mumeo ila mumeo hafany kwa lengo la kukuonesha ww kwani anajua kitu anafanyaMungu ni mwema: nimepokea mgeni kutoka kijijini kwa mume wangu kaingia mchana huu kiukweli nimefurahi na mengi. Mume wangu atajifunza Kupitia hili kwamba ukishakua mkubwa kuna mambo hayaepukiki. Picha linaanza mapokezi niliyompa haamini. Na tutakua nae hapa kwa mwezi. Labda maneno yatapungua. Ushauri wenu wa kumtoa mdogo wangu nimeupokea Mungu anipe busara ya maneno ya kumuondoa ila hadi aondoke na huyu ndugu yake aondoke atatoka na funzo kubwa sana.
Asanteni
Asante sana
Sikutaka kuchangia lkn imenilazimu.Yes na hakuonesha kukerwa.
Hii ndo comment pekee inayoshauri hivi. Yani najiuliza wangapi wamefukuza ndugu zao kwasababu ya penzi? Siku mume akikengeuka mimi ntakua mgeni wa naniPlease usiwatenge ndugu zako sababu ya mume. Wanaume sisi hatutabiriki na sometimes tuna ujinga ujinga wetu wa kiume ( kuna nyapu nyingi nk nk)! Siku majanga yakikupata the only people watakaolia na wewe bila unafki ni ndugu zako wa kuzaliwa nao. So usithubutu kuwatenga kisa mume wako au unau-sugarcoat ubinafsi/ mapungufu yake!
Hauna kwenu?umeolewa wewe sio mdogo wako...mrudishe kwenu,mambo ya kuoa mtu unakuja na ukoo yanakeraNimeamua kutumia ID mpya maana ya zamani ni maarufu sana. Nnachotaka ni wazoefu wa ndoa wanishauri ntasoma tu.
Akapange au akae hostel mambo ya kurundikana kwa shemeji sio mpangoTupo ndugu zaidi ya wawili wapi sasa? Mimi na mdogo wangu mmoja anaeenda chuo anarudi jioni, ndo kurundikana? Soma vizuri maelezo. Mtoto ambae humlipii ada, humpi nauli, mara moja moja hata chakula ananunua yeye mdogo wangu akijibana chuo anatuletea vizawadi maskini.
Kwetu hatuna shida na nyumba dar ipo lakini nauli mtoto anaweza kutumia hata elfu 10 kutoka nyumbani kwenda chuo. So sio kwamba kwetu ni kijijini lakini nyumba ya hapa dar ilipo ni mbali na chuo. Nimeshaelezea sana.
Pole sana...kiufupi mume wako ni mchoyo ile kabisakabisa. Na hii ni mbaya sana kuwa na mwenza mchoyo maana ni tabia iliojengeka tangu akiwa mdogo..na wengi wanakua ni watu waliokulia vijijini kwenye aina fulani ya umaskini (simaanishi wote walokulia kijijini wanatabia hizo). Hii hali ilimtokeaga mdogo wangu wa kike ni lecturer,mme wake akaanzaga hizo mambo na nnadhani alidhani sisi ni maskini...baadae alizima fegi mwenyewe na huwa anajubaraguza sana maana anatamani ifutike kabisa kwenye kumbukumbu zetu. Na hii huwa ni common mwanzoni mwanzoni mwa ndoa within 3 yearsHabari wakuu, nahitaji ushauri,
Mimi ni binti nimeolewa naishi na familia, mume wangu pamoja na mdogo wangu wa kike. Tatizo ni kwamba mume wangu amekuwa na kisirani sana juu ya huyu mdogo wangu wa kike. Kila anachofanya lazima mwanaume alalamike.
Na wala sijawahi kuwa na mawazo labda anamtaka, ndiyo maana anafanya hivi visirani vyote. Mazingira niliyomlea mdogo wangu namjua na ana tabia njema sana.
Mume wangu pia siwezi kumuhukumu kwa uhuni, hajanipa sababu ya kufanya hivyo. Kwahiyo kinachonichanganya ni kwanini ananipa wakati mgumu wa kumfanya mdogo wangu aishi kama yuko kwa mtu baki wakati mimi ni dada yake wa kuzaliwa naye kabisa?
Kila kitu ni lazima aseme kana kwamba huyu mtoto anamkwaza. Kinachoniuma mimi ni kwamba kila siku namuuliza hivi kama angekuwa anaishi hapa ndugu yako halafu mimi namfanyia hivi
Ungejiskiaje? Si ningeonekana mimi ndiyo mbaya sipendi ndugu wa mume?
Na kinachonishangaza, kuna kijana tunaishi naye hapa siyo ndugu wa damu wa mume wangu lakini anatusaidia kazi za hapa nyumbani, ametokea kijijini kwao. Sasa huyu hata akosee vipi mume wangu ukimwambia huyu kakosea hiki na hiki wala hutomuona akijigusa kwenda kumfokea wala kumsema.
Sana sana atajibaraguza tu ili uone ame 'react' na hii siyo mara ya kwanza. Chochote kinachomuhusu mtu wa kwao hutomuona mume wangu amekasirika, lakini ikiwa ni swala la kuhusu ndugu yangu atafoka haswa.
Inafika hatua anamnyima hadi vitu vya kutumia ndani ambavyo hata yeye anavitumia. Hiyo siyo shida, naumia kwasababu mimi huyu mtoto namchukulia kama mwanangu wa kumzaa, nimelichukua hilo jukumu kwa mama yangu tangu mdogo na kwa sasa mama haishi Dar na hatujawa na mahusiano mazuri sana na baba yetu kwa sababu ya mambo ambayo amekuwa akifanya kwetu sisi kama familia.
Kwahiyo najitahidi sana mdogo wangu asijihisi mpweke wala asione kuna pengo la kuumizwa kimalezi na baba yetu.
Na kuna siku ilikuwa sikukuu, nilimwambia mume ndugu zangu wanakuja kwasababu wazazi wetu hawaishi hapa Dar naomba sisi hapa tuwafanyie kitu kama kuwaalika wale hata chakula cha kawaida tu, akasema yeye hana hela.
Wala sikukasirika, nikajikokota nikanunua vyakula nikapika nioneshe kama mume wangu ndiyo amewaalika na wao waone wana kaka hapa mjini. Mume wangu wala hakuonesha ule ushirikiano ambao mimi huwa nautoa wakija ndugu zake, maana huwa napika haswa hadi kwenye kuni.
Nahangaika, napanga, naandaa, nikijua ndugu wa mume wangu wanakuja ila siku wamekuja wadogo zangu sikupata ushirikiano huo. Nilisema acha tu nivumilie kwasababu namheshimisha mume wangu mwenyewe.
Mara nyingine aliniliza na nikamwambia mimi huwa silii lakini unanitenda kama vile sisi kwetu ni masikini, yaani wadogo zangu walipita kutusalimia wakawa sebuleni akaniita chumbani akaniambia nataka kuja kukaa sebleni, naomba nikute siti ya kukaa. Kanakwamba wadogo zangu wamejaa pale maana walikuja kusalimia.
Kinachoniuma ni kwamba, sisi katika kukua kwetu hatujawahi kulelewa na ndugu, kama wadogo zangu wanakaa nje ya kwa baba na mama basi kwangu ndiyo pa kwanza, kwahiyo nikiona wanatendewa hivi naona kama ni mimi ndiyo napitia, sitamani wajione watu baki.
Na kuna muda huwa nawaza, ningekuwa na uwezo ningejenga nyumba yangu niwaweke wadogo zangu hadi watakapokuja kuolewa. Atakae tawanyika sawa, ila kwakuwa mzazi wetu ana uwezo ataona nampokonya wanae. Ila natamani sana wadogo zangu waishi maisha niliyotamani kuishi.
Ushauri unaohitajika;
1. Ni kosa mimi kumtetea mdogo wangu? Kwasababu ninapo jaribu kuuliza kwani tatizo lipo wapi hadi ufoke juu ya jambo dogo hivi, naonekana mkorofi au nataka kumpanda mume kichwani?!
2. Kiubinadamu, huyu mdogo wangu amekosea kuja kuishi kwangu? Nimemlea na hana tabia mbovu kwahiyo namjua, na kila siku namwambia mdogo wangu ikitokea leo dada yako nimedondoka, watoto wangu hutowaacha naamini.
Nampenda sana huyu mtoto, Mungu pekee ndiyo anajua. Kuna muda namwambia mume wangu basi nisamehe mimi naomba vumilia kidogo huyu mtoto akipata kazi ataondoka.
Kwasababu siyo kwamba kwetu tuna shida ya kifedha na wala mume wangu hamgharamii chochote zaidi ya chakula ninachokula mimi ndiyo anachokula huyu mtoto. Ni anakaa kwangu kwasababu ni karibu na chuoni anaposoma yeye.
Kwa upande wa nauli na gharama za kujikimu anatoa mzazi na mimi nikipata huwa nampa kidogo, nashindwa hata kusema namuhudumia maana biashara niliyokuwanayo ilishavurugika baada ya kumuomba mume tusimamie wote ili asiwe na wivu na wateja (stori ndefu haihusiki na mada).
Kwahiyo sina uwezo wa kumgharamia mdogo wangu kwa asilimia mia ila nikipataga 20, 30 nampa ajisogeze. Na mdogo wangu najua ananijali sana, kuna vitu ananifanyiaga huwa nahisi kama nina binti wa kike kabisa.
Yaani kiufupi sipo tayari ndoa yangu iingie doa kwasababu ya mimi kumtetea mdogo wangu na sipo tayari kugombana na mdogo wangu kwasababu yoyote, sijui kama nimeeleweka hapa?
3. Nifanyeje ili mume wangu awe na amani, mdogo wangu pia awe na amani na asijue kwamba shemeji yake huwa analalamika? Kwasababu kila ambacho mume huwa analalama mimi huwa natafuta namna ya kumuelekeza mdogo wangu kama vile mimi ndiyo nataka iwe hivyo, namwelekeza ili asije akafanya tena mume asione tunamdharau.
Na kibaya ni kwamba kuna siku mdogo wangu alisikia nikilalamika sana kwamba hii hali ya yeye mume wangu kukosa amani inaninyima raha, nataka anisaidie mawazo nifanyeje ili awe na furaha na nimuelewe ili niwe namrekebisha mdogo wangu na mimi niwe na amani, hakunijibu! Kesho yake mdogo wangu alikosa raha na sikutaka tena kuibua hiyo mada.
Kiukweli ndoa yetu haina miaka mingi lakini naumia, nilitamani sana mume wangu amlee mdogo wangu kama ambavyo mimi ningelea wa kwake. Lakini inanipa wakati mgumu sana kwamba isije ukatokea mtafaruku kati yao. Nitakae kuwa kwenye wakati mgumu ni mimi.
Uadui huwa hauishi ikiwa mmoja akijua mwengine anamchukia. Na kuna muda huwa namwambia mume, natamani hata na wewe aje ndugu yako hapa akae nikuoneshe jinsi inavyokua kuishi na familia, kuna vitu unavichukulia kama ni mwanao kafanya. Na mume kwangu ana upendo, anajitahidi sana kwakweli, kama kuna makosa ni madogo ya kiubinadamu, ndiyo maana nafukia mengine yoote.
Ninachotamani ni ushauri tu wa kumfanya mume wangu amuone mdogo wangu kama mdogo wake. Niwe na amani pia.
Naombeni ushauri.
dada umekuja kuomba ushauri au kutafuta mtu wa kuside na wewe?trust me there is something and you need to think beyondHii ndo comment pekee inayoshauri hivi. Yani najiuliza wangapi wamefukuza ndugu zao kwasababu ya penzi? Siku mume akikengeuka mimi ntakua mgeni wa nani
Nimeshasikia ushauri wa watu wote kilichobaki ni akili yangu kufanya maamuzidada umekuja kuomba ushauri au kutafuta mtu wa kuside na wewe?trust me there is something and you need to think beyond
Dah ni mtihani.Pole sana...kiufupi mume wako ni mchoyo ile kabisakabisa. Na hii ni mbaya sana kuwa na mwenza mchoyo maana ni tabia iliojengeka tangu akiwa mdogo..na wengi wanakua ni watu waliokulia vijijini kwenye aina fulani ya umaskini (simaanishi wote walokulia kijijini wanatabia hizo). Hii hali ilimtokeaga mdogo wangu wa kike ni lecturer,mme wake akaanzaga hizo mambo na nnadhani alidhani sisi ni maskini...baadae alizima fegi mwenyewe na huwa anajubaraguza sana maana anatamani ifutike kabisa kwenye kumbukumbu zetu. Na hii huwa ni common mwanzoni mwanzoni mwa ndoa within 3 years
Mwambie nawewe unaanza kuwakazia ndugu zake,japo sidhani kama itasaidia na ukizingatia si tabia yako. Kiufupi ni tabia za baadhi ya watu walokulia maisha duni afu akapata unafuu ukubwani..na pia wanakuaga na ushamba mwingiDah ni mtihani.
Dada, fanya hata vibiashara ili uondokane na hii low self esteem.Hii ndo comment pekee inayoshauri hivi. Yani najiuliza wangapi wamefukuza ndugu zao kwasababu ya penzi? Siku mume akikengeuka mimi ntakua mgeni wa nani
Hivi nnavokwambia ndugu yake yuko hapa, af vile vyote ambavyo mdogo wangu alikua anakatazwa kufanya, wa kwake anafanya. Hivi unaambiwa vumilia ndoa kwa mke kuhudumia ndugu tena ambae sio wa damu kabisa tena kwa upendo ila wa kwako ananyanyaswa. Wanawake tuna kaziMwambie nawewe unaanza kuwakazia ndugu zake,japo sidhani kama itasaidia na ukizingatia si tabia yako. Kiufupi ni tabia za baadhi ya watu walokulia maisha duni afu akapata unafuu ukubwani..na pia wanakuaga na ushamba mwingi
Pole sana aisee... Usikubali kuumia kwa kinyongo. It's either usichoke kumchana hadi aache, or nawewe ufanye waziwazi kwa ndugu zake kwa makusudi ili afeel the same. Na uache kuwachangamkia ndugu zake tena na ajue waziHivi nnavokwambia ndugu yake yuko hapa, af vile vyote ambavyo mdogo wangu alikua anakatazwa kufanya, wa kwake anafanya. Hivi unaambiwa vumilia ndoa kwa mke kuhudumia ndugu tena ambae sio wa damu kabisa tena kwa upendo ila wa kwako ananyanyaswa. Wanawake tuna kazi
Dah. Tutafika tu Mungu atupe mioyoPole sana aisee... Usikubali kuumia kwa kinyongo. It's either usichoke kumchana hadi aache, or nawewe ufanye waziwazi kwa ndugu zake kwa makusudi ili afeel the same. Na uache kuwachangamkia ndugu zake tena na ajue wazi