Asante kwa ushauri,
naweza kuwapa benefit of doubt katika kugegedana, mdogo wangu amefata nyayo zangu na ananijua vizuri tu na kiukweli uhuni hana.
Mume wangu kusema anatembea nae naweza kumtetea kwa sasa, mimi ni mtu mfatiliaji sana wa hisia so kama kuna mahusiano kati yao ntakuwa wa kwanza kujua ila kwasasa ntakua natenda dhambi kumuhukumu mume wangu siku akinipa
Hiyo sababu ntajua tu.
Sababu ambayo nahisi ni kwamba mume wangu hajawahi kuishi na familia kubwa yenye ndugu mchanganyiko kama mimi nilivyokua wazazi wetu maisha yao yoye wamekua wakiishi na ndugu zao so nilijifunza huko kuwa kila mtu ni mwanadamu mwenye uwezo wa kukosea.
Kilichonileta natamani mume wangu awe na amani na mdogo wangu naumia kuwa katika position ya kumfukuza mdogo wangu wakati mimi ndo nilishadadia aje hapa ili awe karibu na chuo. Leo namwambiaje nenda nyumbani? Ni mbali sana kutokea nyumbani kwenda chuoni kwao. So kwa hapa kwangu anarahisisha.