Mume wangu hapendi ndugu zangu

Mume wangu hapendi ndugu zangu

Haya ndio nionavyo Mimi

 Mosi, uwezo wa huyo mdogo wako kupanga chumba upo Ila unajisikia vibaya kwanini akapange na Hali wewe upo na anaweza kuishi kwako

Jibu ni rahisi mumeo hamtaki hapo kwake,Busara ni huyo kuhama hapo na mweleze ukweli mdogo wako kuwa inaonekana uwepo wako hapo mumeo hapendi na hujui sababu,hii itakusaidia mdogo wako kujua kuwa sio mapenzi yako yeye kuhama Ila Kero zimezidi toka Kwa mumeo.

 Pili, unapenda Sana mumeo aonekane ni mtu mzuri kwenu ndio maana unajitahidi kuficha upuuzi wake,Hilo ni Jambo zuri lakini wakati mwingine sio Sawa aonekane yeye ni Malaika,nahisi ndio maana unahisi mdogo wako alienda kupanga basi mumeo ataonekana sio mtu mzuri,Kwa mazingira hayo kuwa muwazi sema kweli kuwa mumeo hapendi uwepo wa mdogo wako pale.


Tatu, ambalo ndio kubwa na wanabodi wengi wamesema ni kuwa mumeo anataka kumla supu huyo mdogo wako,na hivyo mdogo wako amegoma kuliwa supu,hiyo ndio sababu kubwa Kwa sababu zifuatazo:

* Mumeo hamhudumii huyo binti Kwa nauli wala Karo ya chuo na mambo mengine,kwahiyo wala sio mzigo kwake hata kidogo useme labda Maisha magumu ndio maana hamtaki hapo

* Huyo binti Mda mwingi yupo chuoni sio kwamba anashinda hapo na kuwafanya msiwe huru na nyumba yenu .


* Kama unavyosema huyo binti ana Tabia njema hivyo naamini hajawahi kuvunja heshima ya nyumba yenu.


Kitu pekee ambacho kimebakia hapo ni kuliwa supu na huyo mumeo.

Raisi mstaafu aliwahi kutuambia akili za kuambiwa changanya na zako.
Hoja yako ya kwanza sio poa.
Haifai umwambie ndg yako kuwa mmewe hapendi aishi pale...utasababisha ndg wote wamchukie
 
Dada yangu angekua mtu wa mitandao ningesema ni wewe aisee
Ila nyie Kuna wanaume wana gubu na roho mbaya🙌..majuzi nimepata taarifa mume wa Dada Katia chumvi juice za mdogo wangu😂😂😂😂Jamani ..mwezi uliopita Katia simu kwenye ndoo ya maji...ngachokaaa
 
Asante kwa ushauri,

naweza kuwapa benefit of doubt katika kugegedana, mdogo wangu amefata nyayo zangu na ananijua vizuri tu na kiukweli uhuni hana.

Mume wangu kusema anatembea nae naweza kumtetea kwa sasa, mimi ni mtu mfatiliaji sana wa hisia so kama kuna mahusiano kati yao ntakuwa wa kwanza kujua ila kwasasa ntakua natenda dhambi kumuhukumu mume wangu siku akinipa
Hiyo sababu ntajua tu.

Sababu ambayo nahisi ni kwamba mume wangu hajawahi kuishi na familia kubwa yenye ndugu mchanganyiko kama mimi nilivyokua wazazi wetu maisha yao yoye wamekua wakiishi na ndugu zao so nilijifunza huko kuwa kila mtu ni mwanadamu mwenye uwezo wa kukosea.

Kilichonileta natamani mume wangu awe na amani na mdogo wangu naumia kuwa katika position ya kumfukuza mdogo wangu wakati mimi ndo nilishadadia aje hapa ili awe karibu na chuo. Leo namwambiaje nenda nyumbani? Ni mbali sana kutokea nyumbani kwenda chuoni kwao. So kwa hapa kwangu anarahisisha.
We kipindi ulimshirikisha kweli mumeo au ulijiamulia mwenyewe kuwa nimchukue??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpangishie chumba huyo mdogo wako. Umri wa mwanachuo unatosha kujitegemea
 
Huyo ni mbinafsi aliyepitiliza,
Ukishamjua mtu hakusumbui Tena,
Anza kutomchukulia serious kweye hayo mambo yake ya uselfish, mpuuze na usiruhusu moyo wako uumie simply umeshamjua, act matured and normal anapokupa changamoto kama hii.

Akiona haujali atabadilika mwenyewe na kuacha ubinafsi japo itachukua muda ila matunda utayaona.
Never gaslight hasa katika hiki kizazi, utavuna mabua. Ubinafsi amekuja ujulia ndani ya ndoa, muulize sababu ni nini hasa maana mwanamke sikuzote hujitoa ndani ya picha mbaya. Aseme ni nini hasa lasivyo hata process za ndoa zisingeenda na mwanaume mbinafsi hutambulika mapema sana kuliko mwanamke.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, amini maneno yangu. Ikitokea siku mumeo na mdogo wako wakaja kupatana na kucheka pamoja.

Elewa umeshachelewa. Ameshapigwa mtu tako 3000.

Mimi ni mwanaume na nimeshapitia yote hayo. Kuanzia kutongoza mashemeji na hata marafiki wa mke.
Hapo mumeo katoswa na mdogo wako hilo ndy tatizo. Hamisha mdogo wako, au kubali kushare mapenzi.

Ukweli mchungu.
Yap, ndiyo maana nasema asitafute picha mbaya kumpaka mmewe bali atafute tatizo haswa ni nini. Hapo kajump to conclusions tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naungana na mdau mmoja hapo juu. Ukishaona situation kibinadamu umeshindwa, ngumu, imekutatiza na huoni njia ya kutokea isiyoleta ugomvi, peleka kwa hakimu asiepokea hongo.

You need spiritual intervention. Washirikina weng wanajua hii formula. Mapema tu wanamtafuta fundi. Wanaroga si kitoto. Because kuna some matters solution yake ni spiritual. Kwa nilivyokusoma wewe ni mtu wa Imani. Sina experience sana lakin nachoweza kusema Pray...

Kwa Imani yangu kuna neno utasoma ktk Isaya 11:6-9. Its possible for the impossibles to happen. Naamini ukiomba kwa kumaanisha na ukalitolea sadaka utaweza. Yumkini ni maroho tena ya kurithi kabisa. We utahangaika kumbe shetani the mastermind yuko nyuma hapo.

Anataka usikie uchungu usiweze kureason kwa hekima au busara. Wewe ukiumia ni rahis kumchukia your partner. Utajikuta unaongea maneno ya uchungu. Ugomvi polepole unaanza. Unakuja kushtuka mlango ulifunguliwa kitambo..mkampa adui nafasi. Kuna mdau hapo juu kashauri dogo either apangiwe au arudi nyumbani kwanza. Mungu alimwambia kaini kama ukitenda vyema hutapata kibali?? Kuna vibali mpaka vije lazima uhustle..chek majaliwa. Ilimbidi ajirisk maisha yake ili apate kibali (if its true..if not watajijua wenyewe). So its a hustle. Keep in mind shetani hapendi ndoa, hapendi amani, hapendi maelewano, hapendi umoja. See the real enemy...deal wit the problem from the root.....
 
Kwanza huyo Jamaa anapata wapi muda wa kuonana na watu wa nyumbani,mie huwa nikiondoka nyumbani SAA 12:30 kurudi ni SAA 3-6 usiku hadi watoto huwa wananimisi.
Ndugu akija nyumbani anaweza akamaliza wiki nzima ndio akaniona has a Jumapili.
 
Tupo ndugu zaidi ya wawili wapi sasa? Mimi na mdogo wangu mmoja anaeenda chuo anarudi jioni, ndo kurundikana? Soma vizuri maelezo. Mtoto ambae humlipii ada, humpi nauli, mara moja moja hata chakula ananunua yeye mdogo wangu akijibana chuo anatuletea vizawadi maskini.

Kwetu hatuna shida na nyumba dar ipo lakini nauli mtoto anaweza kutumia hata elfu 10 kutoka nyumbani kwenda chuo. So sio kwamba kwetu ni kijijini lakini nyumba ya hapa dar ilipo ni mbali na chuo. Nimeshaelezea sana.
Kwa Ni mtoto asikae hostel?Kuna Sababu gani za kumtesa mtoto kisaikolojia hapo nyumbani.......by the way Kuna possibility kubwa huyo Bwana kaomba nanihino Sasa kwa vile umesema binti anatabia njema utakuwa kanyimwa Sasa Ni gubu kwa kwenda mbele
 
Habari wakuu, nahitaji ushauri,

Mimi ni binti nimeolewa naishi na familia, mume wangu pamoja na mdogo wangu wa kike. Tatizo ni kwamba mume wangu amekuwa na kisirani sana juu ya huyu mdogo wangu wa kike. Kila anachofanya lazima mwanaume alalamike.

Na wala sijawahi kuwa na mawazo labda anamtaka, ndiyo maana anafanya hivi visirani vyote. Mazingira niliyomlea mdogo wangu namjua na ana tabia njema sana.

Mume wangu pia siwezi kumuhukumu kwa uhuni, hajanipa sababu ya kufanya hivyo. Kwahiyo kinachonichanganya ni kwanini ananipa wakati mgumu wa kumfanya mdogo wangu aishi kama yuko kwa mtu baki wakati mimi ni dada yake wa kuzaliwa naye kabisa?

Kila kitu ni lazima aseme kana kwamba huyu mtoto anamkwaza. Kinachoniuma mimi ni kwamba kila siku namuuliza hivi kama angekuwa anaishi hapa ndugu yako halafu mimi namfanyia hivi
Ungejiskiaje? Si ningeonekana mimi ndiyo mbaya sipendi ndugu wa mume?

Na kinachonishangaza, kuna kijana tunaishi naye hapa siyo ndugu wa damu wa mume wangu lakini anatusaidia kazi za hapa nyumbani, ametokea kijijini kwao. Sasa huyu hata akosee vipi mume wangu ukimwambia huyu kakosea hiki na hiki wala hutomuona akijigusa kwenda kumfokea wala kumsema.

Sana sana atajibaraguza tu ili uone ame 'react' na hii siyo mara ya kwanza. Chochote kinachomuhusu mtu wa kwao hutomuona mume wangu amekasirika, lakini ikiwa ni swala la kuhusu ndugu yangu atafoka haswa.

Inafika hatua anamnyima hadi vitu vya kutumia ndani ambavyo hata yeye anavitumia. Hiyo siyo shida, naumia kwasababu mimi huyu mtoto namchukulia kama mwanangu wa kumzaa, nimelichukua hilo jukumu kwa mama yangu tangu mdogo na kwa sasa mama haishi Dar na hatujawa na mahusiano mazuri sana na baba yetu kwa sababu ya mambo ambayo amekuwa akifanya kwetu sisi kama familia.

Kwahiyo najitahidi sana mdogo wangu asijihisi mpweke wala asione kuna pengo la kuumizwa kimalezi na baba yetu.

Na kuna siku ilikuwa sikukuu, nilimwambia mume ndugu zangu wanakuja kwasababu wazazi wetu hawaishi hapa Dar naomba sisi hapa tuwafanyie kitu kama kuwaalika wale hata chakula cha kawaida tu, akasema yeye hana hela.

Wala sikukasirika, nikajikokota nikanunua vyakula nikapika nioneshe kama mume wangu ndiyo amewaalika na wao waone wana kaka hapa mjini. Mume wangu wala hakuonesha ule ushirikiano ambao mimi huwa nautoa wakija ndugu zake, maana huwa napika haswa hadi kwenye kuni.

Nahangaika, napanga, naandaa, nikijua ndugu wa mume wangu wanakuja ila siku wamekuja wadogo zangu sikupata ushirikiano huo. Nilisema acha tu nivumilie kwasababu namheshimisha mume wangu mwenyewe.

Mara nyingine aliniliza na nikamwambia mimi huwa silii lakini unanitenda kama vile sisi kwetu ni masikini, yaani wadogo zangu walipita kutusalimia wakawa sebuleni akaniita chumbani akaniambia nataka kuja kukaa sebleni, naomba nikute siti ya kukaa. Kanakwamba wadogo zangu wamejaa pale maana walikuja kusalimia.

Kinachoniuma ni kwamba, sisi katika kukua kwetu hatujawahi kulelewa na ndugu, kama wadogo zangu wanakaa nje ya kwa baba na mama basi kwangu ndiyo pa kwanza, kwahiyo nikiona wanatendewa hivi naona kama ni mimi ndiyo napitia, sitamani wajione watu baki.

Na kuna muda huwa nawaza, ningekuwa na uwezo ningejenga nyumba yangu niwaweke wadogo zangu hadi watakapokuja kuolewa. Atakae tawanyika sawa, ila kwakuwa mzazi wetu ana uwezo ataona nampokonya wanae. Ila natamani sana wadogo zangu waishi maisha niliyotamani kuishi.


Ushauri unaohitajika;

1. Ni kosa mimi kumtetea mdogo wangu? Kwasababu ninapo jaribu kuuliza kwani tatizo lipo wapi hadi ufoke juu ya jambo dogo hivi, naonekana mkorofi au nataka kumpanda mume kichwani?!

2. Kiubinadamu, huyu mdogo wangu amekosea kuja kuishi kwangu? Nimemlea na hana tabia mbovu kwahiyo namjua, na kila siku namwambia mdogo wangu ikitokea leo dada yako nimedondoka, watoto wangu hutowaacha naamini.

Nampenda sana huyu mtoto, Mungu pekee ndiyo anajua. Kuna muda namwambia mume wangu basi nisamehe mimi naomba vumilia kidogo huyu mtoto akipata kazi ataondoka.

Kwasababu siyo kwamba kwetu tuna shida ya kifedha na wala mume wangu hamgharamii chochote zaidi ya chakula ninachokula mimi ndiyo anachokula huyu mtoto. Ni anakaa kwangu kwasababu ni karibu na chuoni anaposoma yeye.

Kwa upande wa nauli na gharama za kujikimu anatoa mzazi na mimi nikipata huwa nampa kidogo, nashindwa hata kusema namuhudumia maana biashara niliyokuwanayo ilishavurugika baada ya kumuomba mume tusimamie wote ili asiwe na wivu na wateja (stori ndefu haihusiki na mada).

Kwahiyo sina uwezo wa kumgharamia mdogo wangu kwa asilimia mia ila nikipataga 20, 30 nampa ajisogeze. Na mdogo wangu najua ananijali sana, kuna vitu ananifanyiaga huwa nahisi kama nina binti wa kike kabisa.

Yaani kiufupi sipo tayari ndoa yangu iingie doa kwasababu ya mimi kumtetea mdogo wangu na sipo tayari kugombana na mdogo wangu kwasababu yoyote, sijui kama nimeeleweka hapa?

3. Nifanyeje ili mume wangu awe na amani, mdogo wangu pia awe na amani na asijue kwamba shemeji yake huwa analalamika? Kwasababu kila ambacho mume huwa analalama mimi huwa natafuta namna ya kumuelekeza mdogo wangu kama vile mimi ndiyo nataka iwe hivyo, namwelekeza ili asije akafanya tena mume asione tunamdharau.

Na kibaya ni kwamba kuna siku mdogo wangu alisikia nikilalamika sana kwamba hii hali ya yeye mume wangu kukosa amani inaninyima raha, nataka anisaidie mawazo nifanyeje ili awe na furaha na nimuelewe ili niwe namrekebisha mdogo wangu na mimi niwe na amani, hakunijibu! Kesho yake mdogo wangu alikosa raha na sikutaka tena kuibua hiyo mada.

Kiukweli ndoa yetu haina miaka mingi lakini naumia, nilitamani sana mume wangu amlee mdogo wangu kama ambavyo mimi ningelea wa kwake. Lakini inanipa wakati mgumu sana kwamba isije ukatokea mtafaruku kati yao. Nitakae kuwa kwenye wakati mgumu ni mimi.

Uadui huwa hauishi ikiwa mmoja akijua mwengine anamchukia. Na kuna muda huwa namwambia mume, natamani hata na wewe aje ndugu yako hapa akae nikuoneshe jinsi inavyokua kuishi na familia, kuna vitu unavichukulia kama ni mwanao kafanya. Na mume kwangu ana upendo, anajitahidi sana kwakweli, kama kuna makosa ni madogo ya kiubinadamu, ndiyo maana nafukia mengine yoote.

Ninachotamani ni ushauri tu wa kumfanya mume wangu amuone mdogo wangu kama mdogo wake. Niwe na amani pia.

Naombeni ushauri.
Wakati wa kumleta mdogo wako ulimshilikisha mmeo?au ulimleta kwa mabavu
 
..Inawezekana ni kutokana na familia alikotokea yeye, kubwa/ndogo

labda ndoa yenu bado changa ~huenda huyo binti anamkosesha kujinafasi atakavyo yeye ,mtoto wa kike na wa kiume ni tofauti ktk mazingira flani ...
(kumbuka mmoja ni ndugu, mwngne msaidizi wa kazi, kwahyo hawana nafasi sawa)

...huyo binti ana umri gani? Maana umemtaja sana kama mtoto, kama wadau wanavyosema, hilo la mapenzi nalo linawezekana pasipo wewe kujua

...inawezekana unampenda sana na kumthamini mdogo wako kuliko mme wako by the way

...inawezekana ndugu zako nao wanamtegemea yeye kwa kiwango kikubwa (kinyume na ulivyosema)
fikiria hili neno "nakuja sebuleni kukaa nikute seat" (maana yake 'boss')

hebu fatilia zaidi
 
Mimi naona sawa ndugu waje wasalimie na kuondoka wakikaa sana wataleta mazoea.isije tokea kama yule jamaa wa moro aliekuwa analalamika kutukanwa na shemegi
 
Ndoa bado changa ila watapatikana tu
Sasa ndoa changa unaanza kuleta an outside person kweli. Hapo iwe ndugu wa mume au mke. Jenga ndoa na ndugu zako wahudumie kwasehemu yao. Usichanganye mafaili ya undugu na ndoa, mwanaume kashaona hii ndoa itafeli maana ndugu hawataisha. Ndugu zako siwake na wake siwako. Unasema it's simple as that kwasababu hamjaanza kuwa na watoto ila mkishakuwa nao believe me it's not simple. I know you love your siblings but never let it interfere with your marriage soon or later, you will have to choose.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari wakuu, nahitaji ushauri,

Mimi ni binti nimeolewa naishi na familia, mume wangu pamoja na mdogo wangu wa kike. Tatizo ni kwamba mume wangu amekuwa na kisirani sana juu ya huyu mdogo wangu wa kike. Kila anachofanya lazima mwanaume alalamike.

Na wala sijawahi kuwa na mawazo labda anamtaka, ndiyo maana anafanya hivi visirani vyote. Mazingira niliyomlea mdogo wangu namjua na ana tabia njema sana.

Mume wangu pia siwezi kumuhukumu kwa uhuni, hajanipa sababu ya kufanya hivyo. Kwahiyo kinachonichanganya ni kwanini ananipa wakati mgumu wa kumfanya mdogo wangu aishi kama yuko kwa mtu baki wakati mimi ni dada yake wa kuzaliwa naye kabisa?

Kila kitu ni lazima aseme kana kwamba huyu mtoto anamkwaza. Kinachoniuma mimi ni kwamba kila siku namuuliza hivi kama angekuwa anaishi hapa ndugu yako halafu mimi namfanyia hivi
Ungejiskiaje? Si ningeonekana mimi ndiyo mbaya sipendi ndugu wa mume?

Na kinachonishangaza, kuna kijana tunaishi naye hapa siyo ndugu wa damu wa mume wangu lakini anatusaidia kazi za hapa nyumbani, ametokea kijijini kwao. Sasa huyu hata akosee vipi mume wangu ukimwambia huyu kakosea hiki na hiki wala hutomuona akijigusa kwenda kumfokea wala kumsema.

Sana sana atajibaraguza tu ili uone ame 'react' na hii siyo mara ya kwanza. Chochote kinachomuhusu mtu wa kwao hutomuona mume wangu amekasirika, lakini ikiwa ni swala la kuhusu ndugu yangu atafoka haswa.

Inafika hatua anamnyima hadi vitu vya kutumia ndani ambavyo hata yeye anavitumia. Hiyo siyo shida, naumia kwasababu mimi huyu mtoto namchukulia kama mwanangu wa kumzaa, nimelichukua hilo jukumu kwa mama yangu tangu mdogo na kwa sasa mama haishi Dar na hatujawa na mahusiano mazuri sana na baba yetu kwa sababu ya mambo ambayo amekuwa akifanya kwetu sisi kama familia.

Kwahiyo najitahidi sana mdogo wangu asijihisi mpweke wala asione kuna pengo la kuumizwa kimalezi na baba yetu.

Na kuna siku ilikuwa sikukuu, nilimwambia mume ndugu zangu wanakuja kwasababu wazazi wetu hawaishi hapa Dar naomba sisi hapa tuwafanyie kitu kama kuwaalika wale hata chakula cha kawaida tu, akasema yeye hana hela.

Wala sikukasirika, nikajikokota nikanunua vyakula nikapika nioneshe kama mume wangu ndiyo amewaalika na wao waone wana kaka hapa mjini. Mume wangu wala hakuonesha ule ushirikiano ambao mimi huwa nautoa wakija ndugu zake, maana huwa napika haswa hadi kwenye kuni.

Nahangaika, napanga, naandaa, nikijua ndugu wa mume wangu wanakuja ila siku wamekuja wadogo zangu sikupata ushirikiano huo. Nilisema acha tu nivumilie kwasababu namheshimisha mume wangu mwenyewe.

Mara nyingine aliniliza na nikamwambia mimi huwa silii lakini unanitenda kama vile sisi kwetu ni masikini, yaani wadogo zangu walipita kutusalimia wakawa sebuleni akaniita chumbani akaniambia nataka kuja kukaa sebleni, naomba nikute siti ya kukaa. Kanakwamba wadogo zangu wamejaa pale maana walikuja kusalimia.

Kinachoniuma ni kwamba, sisi katika kukua kwetu hatujawahi kulelewa na ndugu, kama wadogo zangu wanakaa nje ya kwa baba na mama basi kwangu ndiyo pa kwanza, kwahiyo nikiona wanatendewa hivi naona kama ni mimi ndiyo napitia, sitamani wajione watu baki.

Na kuna muda huwa nawaza, ningekuwa na uwezo ningejenga nyumba yangu niwaweke wadogo zangu hadi watakapokuja kuolewa. Atakae tawanyika sawa, ila kwakuwa mzazi wetu ana uwezo ataona nampokonya wanae. Ila natamani sana wadogo zangu waishi maisha niliyotamani kuishi.


Ushauri unaohitajika;

1. Ni kosa mimi kumtetea mdogo wangu? Kwasababu ninapo jaribu kuuliza kwani tatizo lipo wapi hadi ufoke juu ya jambo dogo hivi, naonekana mkorofi au nataka kumpanda mume kichwani?!

2. Kiubinadamu, huyu mdogo wangu amekosea kuja kuishi kwangu? Nimemlea na hana tabia mbovu kwahiyo namjua, na kila siku namwambia mdogo wangu ikitokea leo dada yako nimedondoka, watoto wangu hutowaacha naamini.

Nampenda sana huyu mtoto, Mungu pekee ndiyo anajua. Kuna muda namwambia mume wangu basi nisamehe mimi naomba vumilia kidogo huyu mtoto akipata kazi ataondoka.

Kwasababu siyo kwamba kwetu tuna shida ya kifedha na wala mume wangu hamgharamii chochote zaidi ya chakula ninachokula mimi ndiyo anachokula huyu mtoto. Ni anakaa kwangu kwasababu ni karibu na chuoni anaposoma yeye.

Kwa upande wa nauli na gharama za kujikimu anatoa mzazi na mimi nikipata huwa nampa kidogo, nashindwa hata kusema namuhudumia maana biashara niliyokuwanayo ilishavurugika baada ya kumuomba mume tusimamie wote ili asiwe na wivu na wateja (stori ndefu haihusiki na mada).

Kwahiyo sina uwezo wa kumgharamia mdogo wangu kwa asilimia mia ila nikipataga 20, 30 nampa ajisogeze. Na mdogo wangu najua ananijali sana, kuna vitu ananifanyiaga huwa nahisi kama nina binti wa kike kabisa.

Yaani kiufupi sipo tayari ndoa yangu iingie doa kwasababu ya mimi kumtetea mdogo wangu na sipo tayari kugombana na mdogo wangu kwasababu yoyote, sijui kama nimeeleweka hapa?

3. Nifanyeje ili mume wangu awe na amani, mdogo wangu pia awe na amani na asijue kwamba shemeji yake huwa analalamika? Kwasababu kila ambacho mume huwa analalama mimi huwa natafuta namna ya kumuelekeza mdogo wangu kama vile mimi ndiyo nataka iwe hivyo, namwelekeza ili asije akafanya tena mume asione tunamdharau.

Na kibaya ni kwamba kuna siku mdogo wangu alisikia nikilalamika sana kwamba hii hali ya yeye mume wangu kukosa amani inaninyima raha, nataka anisaidie mawazo nifanyeje ili awe na furaha na nimuelewe ili niwe namrekebisha mdogo wangu na mimi niwe na amani, hakunijibu! Kesho yake mdogo wangu alikosa raha na sikutaka tena kuibua hiyo mada.

Kiukweli ndoa yetu haina miaka mingi lakini naumia, nilitamani sana mume wangu amlee mdogo wangu kama ambavyo mimi ningelea wa kwake. Lakini inanipa wakati mgumu sana kwamba isije ukatokea mtafaruku kati yao. Nitakae kuwa kwenye wakati mgumu ni mimi.

Uadui huwa hauishi ikiwa mmoja akijua mwengine anamchukia. Na kuna muda huwa namwambia mume, natamani hata na wewe aje ndugu yako hapa akae nikuoneshe jinsi inavyokua kuishi na familia, kuna vitu unavichukulia kama ni mwanao kafanya. Na mume kwangu ana upendo, anajitahidi sana kwakweli, kama kuna makosa ni madogo ya kiubinadamu, ndiyo maana nafukia mengine yoote.

Ninachotamani ni ushauri tu wa kumfanya mume wangu amuone mdogo wangu kama mdogo wake. Niwe na amani pia.

Naombeni ushauri.
Kamnyima naniliiii
 
Mmeo ni mbinafsi,mchoyo ,tho mbaya Kwa wageni ,anapenda muwe nae tu ndani bila buguzi,

Ebu eleza maisha kabla ya mdogo wako kuhamia hapo yalikuwaje ? Nikimaanisha kujiachia ndani na mengineyo,labda dogo anawaharibia ndio maana mume wako hapendi buguzi.,
 
Back
Top Bottom