Mume wangu hapendi ndugu zangu

Mume wangu hapendi ndugu zangu

Tupo ndugu zaidi ya wawili wapi sasa? Mimi na mdogo wangu mmoja anaeenda chuo anarudi jioni, ndo kurundikana? Soma vizuri maelezo. Mtoto ambae humlipii ada, humpi nauli, mara moja moja hata chakula ananunua yeye mdogo wangu akijibana chuo anatuletea vizawadi maskini.

Kwetu hatuna shida na nyumba dar ipo lakini nauli mtoto anaweza kutumia hata elfu 10 kutoka nyumbani kwenda chuo. So sio kwamba kwetu ni kijijini lakini nyumba ya hapa dar ilipo ni mbali na chuo. Nimeshaelezea sana.
Huyo mdogo wako alifikaje fikaje hapo kwako? Mlikaa na mumeo mkakubaliana au alifika kwa kulazimisha wewe?
 
Chagua moja hapo kati ya kumtoa ndugu au mume 7bu hakuna uwezekano wa hayo mawili kwa wakat mmoja
 
Bora wewe, Mie huyu Baba Kidogoli anafukuza hadi ndugu zake, hapa nilipo upande wa mume wanaona Mimi ndo nina roho mbaya, kumbe ndugu yao hana uvumilivu WA kuishi na ndugu....Yani ndugu akizingua asubuhi anakatiwa tiketi, hata Kama anasoma uhamisho utamkuta huko huko.
Nishamzoe mwenyewe, la msingi nguvu za kiume anazo, kibo na mawenzi ananifikisha wala sigombani nae, tabia zake apambane nazo mwenyewe.
 
NDOA NI YA WATU WAWILI TU.MAMBO YA KULETA SIJUI MDOGO WANGU,KAKA YANGU NA BLAABLAA NYINGINE NIKUJITAFUTIA MIGOGORO WEWE MWENYEWE.

Marko 10:6-9
6Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke. 7Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; 8na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. 9Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.
 
Habari wakuu, nahitaji ushauri,

Mimi ni binti nimeolewa naishi na familia, mume wangu pamoja na mdogo wangu wa kike. Tatizo ni kwamba mume wangu amekuwa na kisirani sana juu ya huyu mdogo wangu wa kike. Kila anachofanya lazima mwanaume alalamike.

Na wala sijawahi kuwa na mawazo labda anamtaka, ndiyo maana anafanya hivi visirani vyote. Mazingira niliyomlea mdogo wangu namjua na ana tabia njema sana.

Mume wangu pia siwezi kumuhukumu kwa uhuni, hajanipa sababu ya kufanya hivyo. Kwahiyo kinachonichanganya ni kwanini ananipa wakati mgumu wa kumfanya mdogo wangu aishi kama yuko kwa mtu baki wakati mimi ni dada yake wa kuzaliwa naye kabisa?

Kila kitu ni lazima aseme kana kwamba huyu mtoto anamkwaza. Kinachoniuma mimi ni kwamba kila siku namuuliza hivi kama angekuwa anaishi hapa ndugu yako halafu mimi namfanyia hivi
Ungejiskiaje? Si ningeonekana mimi ndiyo mbaya sipendi ndugu wa mume?

Na kinachonishangaza, kuna kijana tunaishi naye hapa siyo ndugu wa damu wa mume wangu lakini anatusaidia kazi za hapa nyumbani, ametokea kijijini kwao. Sasa huyu hata akosee vipi mume wangu ukimwambia huyu kakosea hiki na hiki wala hutomuona akijigusa kwenda kumfokea wala kumsema.

Sana sana atajibaraguza tu ili uone ame 'react' na hii siyo mara ya kwanza. Chochote kinachomuhusu mtu wa kwao hutomuona mume wangu amekasirika, lakini ikiwa ni swala la kuhusu ndugu yangu atafoka haswa.

Inafika hatua anamnyima hadi vitu vya kutumia ndani ambavyo hata yeye anavitumia. Hiyo siyo shida, naumia kwasababu mimi huyu mtoto namchukulia kama mwanangu wa kumzaa, nimelichukua hilo jukumu kwa mama yangu tangu mdogo na kwa sasa mama haishi Dar na hatujawa na mahusiano mazuri sana na baba yetu kwa sababu ya mambo ambayo amekuwa akifanya kwetu sisi kama familia.

Kwahiyo najitahidi sana mdogo wangu asijihisi mpweke wala asione kuna pengo la kuumizwa kimalezi na baba yetu.

Na kuna siku ilikuwa sikukuu, nilimwambia mume ndugu zangu wanakuja kwasababu wazazi wetu hawaishi hapa Dar naomba sisi hapa tuwafanyie kitu kama kuwaalika wale hata chakula cha kawaida tu, akasema yeye hana hela.

Wala sikukasirika, nikajikokota nikanunua vyakula nikapika nioneshe kama mume wangu ndiyo amewaalika na wao waone wana kaka hapa mjini. Mume wangu wala hakuonesha ule ushirikiano ambao mimi huwa nautoa wakija ndugu zake, maana huwa napika haswa hadi kwenye kuni.

Nahangaika, napanga, naandaa, nikijua ndugu wa mume wangu wanakuja ila siku wamekuja wadogo zangu sikupata ushirikiano huo. Nilisema acha tu nivumilie kwasababu namheshimisha mume wangu mwenyewe.

Mara nyingine aliniliza na nikamwambia mimi huwa silii lakini unanitenda kama vile sisi kwetu ni masikini, yaani wadogo zangu walipita kutusalimia wakawa sebuleni akaniita chumbani akaniambia nataka kuja kukaa sebleni, naomba nikute siti ya kukaa. Kanakwamba wadogo zangu wamejaa pale maana walikuja kusalimia.

Kinachoniuma ni kwamba, sisi katika kukua kwetu hatujawahi kulelewa na ndugu, kama wadogo zangu wanakaa nje ya kwa baba na mama basi kwangu ndiyo pa kwanza, kwahiyo nikiona wanatendewa hivi naona kama ni mimi ndiyo napitia, sitamani wajione watu baki.

Na kuna muda huwa nawaza, ningekuwa na uwezo ningejenga nyumba yangu niwaweke wadogo zangu hadi watakapokuja kuolewa. Atakae tawanyika sawa, ila kwakuwa mzazi wetu ana uwezo ataona nampokonya wanae. Ila natamani sana wadogo zangu waishi maisha niliyotamani kuishi.


Ushauri unaohitajika;

1. Ni kosa mimi kumtetea mdogo wangu? Kwasababu ninapo jaribu kuuliza kwani tatizo lipo wapi hadi ufoke juu ya jambo dogo hivi, naonekana mkorofi au nataka kumpanda mume kichwani?!

2. Kiubinadamu, huyu mdogo wangu amekosea kuja kuishi kwangu? Nimemlea na hana tabia mbovu kwahiyo namjua, na kila siku namwambia mdogo wangu ikitokea leo dada yako nimedondoka, watoto wangu hutowaacha naamini.

Nampenda sana huyu mtoto, Mungu pekee ndiyo anajua. Kuna muda namwambia mume wangu basi nisamehe mimi naomba vumilia kidogo huyu mtoto akipata kazi ataondoka.

Kwasababu siyo kwamba kwetu tuna shida ya kifedha na wala mume wangu hamgharamii chochote zaidi ya chakula ninachokula mimi ndiyo anachokula huyu mtoto. Ni anakaa kwangu kwasababu ni karibu na chuoni anaposoma yeye.

Kwa upande wa nauli na gharama za kujikimu anatoa mzazi na mimi nikipata huwa nampa kidogo, nashindwa hata kusema namuhudumia maana biashara niliyokuwanayo ilishavurugika baada ya kumuomba mume tusimamie wote ili asiwe na wivu na wateja (stori ndefu haihusiki na mada).

Kwahiyo sina uwezo wa kumgharamia mdogo wangu kwa asilimia mia ila nikipataga 20, 30 nampa ajisogeze. Na mdogo wangu najua ananijali sana, kuna vitu ananifanyiaga huwa nahisi kama nina binti wa kike kabisa.

Yaani kiufupi sipo tayari ndoa yangu iingie doa kwasababu ya mimi kumtetea mdogo wangu na sipo tayari kugombana na mdogo wangu kwasababu yoyote, sijui kama nimeeleweka hapa?

3. Nifanyeje ili mume wangu awe na amani, mdogo wangu pia awe na amani na asijue kwamba shemeji yake huwa analalamika? Kwasababu kila ambacho mume huwa analalama mimi huwa natafuta namna ya kumuelekeza mdogo wangu kama vile mimi ndiyo nataka iwe hivyo, namwelekeza ili asije akafanya tena mume asione tunamdharau.

Na kibaya ni kwamba kuna siku mdogo wangu alisikia nikilalamika sana kwamba hii hali ya yeye mume wangu kukosa amani inaninyima raha, nataka anisaidie mawazo nifanyeje ili awe na furaha na nimuelewe ili niwe namrekebisha mdogo wangu na mimi niwe na amani, hakunijibu! Kesho yake mdogo wangu alikosa raha na sikutaka tena kuibua hiyo mada.

Kiukweli ndoa yetu haina miaka mingi lakini naumia, nilitamani sana mume wangu amlee mdogo wangu kama ambavyo mimi ningelea wa kwake. Lakini inanipa wakati mgumu sana kwamba isije ukatokea mtafaruku kati yao. Nitakae kuwa kwenye wakati mgumu ni mimi.

Uadui huwa hauishi ikiwa mmoja akijua mwengine anamchukia. Na kuna muda huwa namwambia mume, natamani hata na wewe aje ndugu yako hapa akae nikuoneshe jinsi inavyokua kuishi na familia, kuna vitu unavichukulia kama ni mwanao kafanya. Na mume kwangu ana upendo, anajitahidi sana kwakweli, kama kuna makosa ni madogo ya kiubinadamu, ndiyo maana nafukia mengine yoote.

Ninachotamani ni ushauri tu wa kumfanya mume wangu amuone mdogo wangu kama mdogo wake. Niwe na amani pia.

Naombeni ushauri.
Pole sana kwa changamoto hiyo ya kifamilia, atakuwa mchawi huyo
 
Afu pia ikiwa huoni sababu jua kabisa huyo mumeo kashaomba tunda ila amechomolewa japo hulikubali hili ila ndo chanzo na usitegemee kama huyo ndugu yako atakuja kukuambia mana atahisi atawagombanisha ww hatakam mpelelezi vp ila jua hao ni watu wazima hasa kwenye ishu za kutongozana unaweza kukaa hata mwaka bila kujua kwahy hakuna sababu nyingne hapo
 
Nina hisia huyo mwanaume anampenda kimapenzi mdogo wako... hii naongelea kwa experience,kuna shemeji yangu alikua na tabia kama hizo nilivyomaliza form six nilienda kwa dada yangu kuwapa hi .shem akawa ni mtu wa kununa nuna tuu kugomba gomba hovyo, mara nikiongea na simu anamwambia sister aniangalie nimeshaanza anza mambo ya wanaume..nikitoka kdg hata kwenda dukani anamwambia sisy huyu mdg wako asije kutuletea mimba humu na mengine mengiii wkt mi mwenyewe enzi hizo namaliza six wala hata sijaanza matusi 😀 . Basi bwana sisy alikuja kusafiri alienda msibani akatuacha hapo na wtt wake na msichana wa kazi si ndo bwa shemeji kunambia live kuwa ananipenda sana na vile kunimind mind ni kwa sbb anaona wivu mara anashindwa kuvumilia so nimtunuku. Aisee siku hyo alijuta kunambia nilimuogesha matusi yote na nikamwambia naenda kusema na kutangaza kwa ndugu. Na kesho yake nikasepa nikamwambia sisy nawahi kuaaply tempo mahali. So my dear usikaze shingo kusema mumeo hawezi fanya hivyo... mwanaume ni mwanaume tuu dont under estimate him.
 
Very simple ukweli mchungu mtu anaekupenda hawezi kuchukia ndugu zako hata kidogo dada hapo cha kufanya mpeleke mdogo wako hostel basi kuepusha kero zisizo na kichwa wala miguu...mimi pia naishi na mdogo wangu na mume wangu anamchukulia kama mdogo wake

Ila tusihukumu upande mmoja, ukute shosti Hampi mume attention, attention anampa mdogo wake....ukizingatia hawana mtoto, unaweza kukuta muda wa kutafuta mtoto yeye yuko chumbani Kwa mdogo wake wanapiga Stori za utotoni.....wakati wa Kula ukute badala ya kumlisha mumewe yeye anataka ale jikoni na mdogo wake, mume lazima ajione ametengwa na atamchukia huyo mdogo mtu Kwa kuona anaingilia mahaba.
 
Very simple ukweli mchungu mtu anaekupenda hawezi kuchukia ndugu zako hata kidogo dada hapo cha kufanya mpeleke mdogo wako hostel basi kuepusha kero zisizo na kichwa wala miguu...mimi pia naishi na mdogo wangu na mume wangu anamchukulia kama mdogo wake
Hakuna cha gubu wala nini.Ndugu ni kikwazo cha ndoa kwa namna yoyote ile.
Mimi kwangu najihitaji mimi mwenyewe,mke wangu na wanangu basi,ndugu wapite tu kusalimia na kusepa.Wakiwa na na shida ya pesa waseme niwape.Kifupi nyumbani kwangu ninahitaji uhuru wa hata kumtukana mke wangu,kumfokea,kumkumbatia any time,kumgegeda popote pale ndani ya nyumba yangu.Na ndiyo maana watoto nimepeleka boarding huko.
 
Kwa nini hamna mtoto mpaka sasa? There's possibly something wrong with your husband fertility and thus loosing his self confidence and hence resorts to intimidating.
 
Watu kama hawa katika familia wapo sana, wanapenda sifa na kuonekana wema bila kujali anaumiza upande wa mume.
Mimi binafsi napenda privacy sana.
Kwangu hawezi kukaa ndugu yangu wala upande wa pili.
Nitasaidia wakiwa mbali.
Kama kuja kwetu wasalimie na kukaa siku kadhaa wasepe.
Kukaa na ndg ni mzigo, watakufanya uishi maisha wayatakayo wao, watataka special treatment na mimi huo ujinga sinaga kabisa.
Nikiwa kwangu mimi ndiye mfalme sitakagi mbambamba za ndg.

Kwa misimamo yangu nitawaudhi kwani sitaki kuuishi uongo uongo
Ndiyo mwanaume wa kweli alivyo.Tunahita uhuru tukiwa majumbani mwetu.
 
Duh.

Mwamba atakuwa aliteseka sana kisaikolojia.

Iliishaje hii?
Nilivyoondoka nikaenda home mambo ya chuo yakaja nikasoma nikamaliza nikaolewa. So huyu ni moja ya mashemeji wanaoniheshimu sana maana sijawahi mwambia mtu yoyote siri yake. Na sikutaka kuvunja au kutoa amani ya ndoa yao.
 
Me nakushauri mrudishe dogo kwanza home. Halafu jipe muda wa kukaa na mwenzako kujua shida ipo wapi.

Hapo ni kwake kama hataki kukaa na ndugu jitahidi ujue sababu ni ipi kwa utaratibu na umakini usijegombana nae.

The way umeandika ni kama unamuelewa zaidi mdogo wako kuliko mume wako. Nadhani ni busara kujali hisia za mwenzako zaidi na kujua anasumbuliwa na nini. Mdogo wako na yeye ataolewa atakuwa na mji wake, je utaenda kukaa nae huko au utabaki kwako?!

Sasa mbona unahangaika na mambo ambayo si lazima. Kumjali mdogo wako kama mwanao inauhusianaje hapo. Mbona kama unalazimisha kuwa mama kwa mdogo wako na ana mama yake ? Sasa umemuacha mama yako anakaa na nani we unachukua mdogo wako unaishi nae?!

Inaonyesha hauna mtoto bado. Kwann usitafute watoto ili uwe busy nao na kuwapenda na kuwapa hiyo attention?!


Mdogo wako atabakia kuwa mdogo wako na atatakiwa kuwa na kwake siku moja, msaidie kujiandaa na maisha yake ila sio kumkumbatia kama kinda as if ni mtoto wako.
 
Me nakushauri mrudishe dogo kwanza home. Halafu jipe muda wa kukaa na mwenzako kujua shida ipo wapi.

Hapo ni kwake kama hataki kukaa na ndugu jitahidi ujue sababu ni ipi kwa utaratibu na umakini usijegombana nae.

The way umeandika ni kama unamuelewa zaidi mdogo wako kuliko mume wako. Nadhani ni busara kujali hisia za mwenzako zaidi na kujua anasumbuliwa na nini. Mdogo wako na yeye ataolewa atakuwa na mji wake, je utaenda kukaa nae huko au utabaki kwako?!

Sasa mbona unahangaika na mambo ambayo si lazima. Kumjali mdogo wako kama mwanao inauhusianaje hapo. Mbona kama unalazimisha kuwa mama kwa mdogo wako na ana mama yake ? Sasa umemuacha mama yako anakaa na nani we unachukua mdogo wako unaishi nae?!

Inaonyesha hauna mtoto bado. Kwann usitafute watoto ili uwe busy nao na kuwapenda na kuwapa hiyo attention?!


Mdogo wako atabakia kuwa mdogo wako na atatakiwa kuwa na kwake siku moja, msaidie kujiandaa na maisha yake ila sio kumkumbatia kama kinda as if ni mtoto wako.
Na anamuamini sana mume wake kuwa hawezi mtongoza mdogo wake.
 
Na anamuamini sana mume wake kuwa hawezi mtongoza mdogo wake.
Aaaah mambo mengine ni kuibua changamoto zisizo na ulazima. Ukishaolewa mtu pambana na kujenga familia yako. Ndugu na familia yako wasaidie kwa makubaliano na mwenzako au kwa namna ambayo haita athiri mahusiano yenu.

Kuna familia ni stress na zipo dysfunctional. Umetoka huko unaanza kuvuta tena changamoto hizo kwenye ndoa yako. Ishi na ufocus na ndoa yako. Ndio maana mahusiano haya dumu siku hizi sababu unakuta mtu analazimishia ndugu zake kuwa part ya familia mpya na hajakaa na mwenzake wakapanga lolote. Sasa kwann uliolewa au kuoa si ungebakia kwenu muishi milele.
 
Nashukuru sana. Mtoto akija anafanya vishughuli vidogo vya nyumbani then anaingia kulala. Kukaa sebleni ni hadi mimi ni lazimishe
Ila kuna mdau anasema kwa ushuhuda na umemtokea yeye akiwa kwa Shem

Shem mkali kujionyesha kumbe ni wivu na anamtamani ( mdogo mtu)

Angalia pande zote pia hamu ina Vishawishi vingi sana mchunguze mmeo au mwondoe mdogo wako hapo

Huo ni ushauri tu kwani kila kitu linawezekana chini ya Jua

Dunia hii haijaanza leo na machafu ni mengi ila yanatofautiana
Pole sana ila natumaini umepata picha kubwa hapa kwa wadau

Usikurupuke bali uwe mwangalifu pia
Dua zangu
 
Unaolewa na mtu wa kijijini ndiyo shida hapo. Wanakuwa na ushamba mwingi sana. Vumilia, yakizidi mueleze mdogo wako hali halisi na mwambie akaze roho. Walau akijua hapendwi atajua namna ya kuishi.
 
Aaaah mambo mengine ni kuibua changamoto zisizo na ulazima. Ukishaolewa mtu pambana na kujenga familia yako. Ndugu na familia yako wasaidie kwa makubaliano na mwenzako au kwa namna ambayo haita athiri mahusiano yenu.

Kuna familia ni stress na zipo dysfunctional. Umetoka huko unaanza kuvuta tena changamoto hizo kwenye ndoa yako. Ishi na ufocus na ndoa yako. Ndio maana mahusiano haya dumu siku hizi sababu unakuta mtu analazimishia ndugu zake kuwa part ya familia mpya na hajakaa na mwenzake wakapanga lolote. Sasa kwann uliolewa au kuoa si ungebakia kwenu muishi milele.
Kibongo bongo hilo ni swala ambalo familia nyingi kama imekua kawaid na kuna koo au makabila fulani kukaa na ndugu ni kama lazima hivi. So ili kuepusha matatizo ni vyema iwe kuja na kusalimia kidg na kusepa
 
Back
Top Bottom