olando da costa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2018
- 505
- 379
Watu wengi humu haulizi maswali kwa maana ya kutaka kujifunza wasichokijua bali kwa mtazamo wa kutaka kuchallenge.
Imagine wewe ni mwanafunzi/mwanachuo umeenda darasani kwa lengo tu la kutaka kuchallenge mwalimu/lecturer wako HAKUNA namna utakaa uelewa somo lake. Utabakia vile ulivyo.
Wewe ni mwanadamu tena u mavumbi tuu kisha unataka kuyachallenge mambo ya Mungu (divinity) kabla ya kumwamini, HAKUNA namna utakaa uyaelewe pasipo kumwamini kwanza. Utabakia na ujinga wako huku ukijiona mwerevu mbele zake.
Kaa chini uwe tayari kujifunza.
Nyuzi zako nyingi ni kukosoa mambo ya dini za kigeni,nakushauri uanzishe dini ya asili ya mizimu mbona utapata wafuasi wengi.Kuna Mambo Yapo Ulimwenguni ukiyatafakari kwa Kina hayaingii Akilini ndugu waafrika wenzangu
Kuna Historia katika Vitabu kwamba Mungu alimtoa Mwanae Ili aje Kuikomboa Dunia katika Dhambi (ambazo zipo mpaka Leo)
Ukiangalia kwa Undani Historia hii ya kuzaliwa kwake inatia Shaka sana kabla ya Kujua Majibu ya kuzaliwa kwake inakuja Historia kwamba hana Baba. Kabla hujapata Majibu ya Baba ni nani Inakuja Kwamba ni Uwezo wa Mungu ndio akazaliwa. Yanakuwa Maswali juu ya Maswali
Kumbuka Yusufu na Mariam si kwamba Walikuwa ni Wachumba la hasha bali walikuwa tayari wapo Ndani (wameoana) wanaishi pamoja. Hakuna wachumba Wanaoishi pamoja kwa Utaratibu wa Kuishi. Ukichumbia wewe utakaa kwako na Huyo mchumba atakaa kwao. Kama Waliishi pamoja maana Yake waliweza Kushiriki Tendo la Ndoa yao na Ukifuatilia kwa Makini Yusuf alikuwa Pamoja na Mariam kila Sehemu hakuna Sehemu inayosema Alikuja Kumuoa mariam Ikiwa na Maana Kwamba Tayari alikuwa keshaoa maana yake ule uchumba ulio andikwa Tayari ukayeyuka
Binadamu huzaliwa Kwa Mwanaume na Mwanamke hili halina ubishi. Ila Kuna Kuja Utata wa Hapa Kwamba Yesu alizaliwa bila Mfumo maalumu wa Uzazi wa Baba na Mama ila Roho Mtakatifu kama Wanavyodai (kumbuka Hata Huko india Wapo Watu wenye Hadithi hizi hizi za Kuzaliwa bila Baba)
Sasa Hapa Unajiuliza Maswali. Mungu huyo aliyeweza Kumuumba Mwanadamu wa Kwanza Bila Kutumia mifumo ya Uzazi Inakuwaje leo aje Aanze Kumuumba Binadamu mwingine anayedaiwa ni Mwanae kwa Mifumo ya Uzazi na Akaenda kwa Mariam ambaye alikuwa teyari ana Mume(kumbuka Hapa Mungu hazai na Wala Hakuzailiwa)
Sasa Anamzaa mwanae kupitia Mariam mara Yusufu atake kumkimbia Mariam maana Kuna Siri May be Yusufu aliiona akaona Hapa Nimepigwa na Baada ya Yesu kuzaliwa Yusuf Anapotea Ghafla kwenye Maandiko na Historia yake inaishia Hapo hapo
Mungu anamtoa Mwanae. Anakuja Mnamkataa, mnampiga, mnamtesa anawahubiria mnagoma Kukubali maneno yake mnamfukuza kwenye masinagogo yake, Anaenda Kusali mlimani peke yake, anakusanya wanafunzi wake. Hao wanafunzi nao mnawakataa mnawafukuza. Hivi Mungu hapo anawaogopa Nyie kisa Nini mpak Awafanyie Haya Yote Nyie Viumbe wake
Yaani Mungu mpaka Anatoa Mtoto wake Wa Pekee ili awabembeleze nyie mmrudie Yeye na Mnakataa. Sasa Hapo Mungu Anakuwa na Ule Uwezo na Kutoshindwa Kitu kweli. Kama Kawatumia Mwanae na Mmemgomea kawatumia Manabii na Mitume mmemgomea Tena na hamtaki kumrudia. Hivi Mungu anawalemba Hivyo Ili Iweje
Si kila Mtu anayezaliwa bila Baba Yake basi Baba Yake ndio Mungu. Wachawi wanazini na Binadamu kila Siku na Wachawi hao hao ndio Binadamu wenzenu. Wanawake wanabeba Mimba zingine wasizozijua zimetoka wapi
Basi Mjue Kwamba Hapo Mwenye Enzi Mungu hayupo na Mnaozeshwa Akili zenu ndugu zangu. Kaeni Chini Mtafakari kwa Akili zenu Timamu. Mungu hawezi kufanya hayo Kwa Viumbe wake. Yeye hayupo Hivyo
[emoji3507]Mungu si Mmoja
[emoji3507]Mungu si Wengi
[emoji3507]Mungu si Baba
[emoji3507]Mungu si Mama
[emoji3507]Mungu si Kiumbe
[emoji3507]Mungu hachukii Viumbe
[emoji3507]Mungu hapendi Viumbe wake ila Ana Enzi na Viumbe wake (usijione wewe Kiumbe Mtu unapendwa na Mungu Kuliko Viumbe wake wengine aliowaumba)
[emoji3507]Mungu hakuzaa wala Kuzaliwa
Yachunguzeni maandiko Yenu mtajua kwamba si Maandiko ya kiucha Mungu ila Maandiko ya Viumbe wenye Tamaa
ASANTENI
Hata ungepewa facts 1000 za maandiko matakatifu kama hujafungua ufahamu na moyo kumwamini Yesu Kristo kuwa ni Mungu alikufa na kufufuka kwa ajili yako huwezi kuokoka wala kumwelewa Mungu.Jamani nyieeee Mungu hazaliwi nyie
Walokuleteeni iyo dini saivi wanaslimu kwa kasi huko
Wewe ndio unasema kwamba kuzaa ni sifa ya kiumbe ila maandiko yanasema Mungu anazaa.
Waebrania : 1 : 5 - Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?
Maandiko hayo hapo Mungu anazaa. Lete andiko katika biblia Mungu anasema hazai tujue mbivu na mbichi leo
Mungu hazai ukimpa Hiyo Sifa Basi Baba Yako na Mama Yako Pia Ni Mungu si Wanazaa bhana. Nyie kila Siku mnaimba Hafafani na Yeyote ila Mnampa Sifa Ya Kuzaa Mungu akishazaa Basi Hana Tofauti na Wewe NA wanyama Wengine wanaozaa pia.
Unakimbilia Maandiko yako wakati Hata Huko hakuna Andiko linalosema Mungu kazaa[
Mada imeisha
Mungu anazaa na ana mwanawe anaitwa Yesu Kristo
Kwa taarifa yako
BILA YESU MBINGUNI HUTOBOI
Siri Nyingi sana Zimefichwa kwa Hawa Viumbe wanaokuja Kukupa Taarifa za Mungu hapa Dunianikwa hiyo kuna uwezekano kuna siri imefichwa?
hujanitajia alomzaa ila m ninavojua alimzaa ni Mariam kwaio Mariam ndo Mungu wa Yesu?
hhhhhh kwaio unalazimishwa kwanza uamini hlf ndio usomeshwe imani si kulazimishana huko sasaHata ungepewa facts 1000 za maandiko matakatifu kama hujafungua ufahamu na moyo kumwamini Yesu Kristo kuwa ni Mungu alikufa na kufufuka kwa ajili yako huwezi kuokoka wala kumwelewa Mungu.
Imani ya kikristo inaaminiwa kwanza sio kusomewa kwanza.
mbona unaleta maswali juu ya maswali jibu ilo swali kwanzaWewe unavyojua ila sio maandiko yanavyosema.
Kwa taarifa yako
Yohana : 8 : 58 - Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Sasa tuambie kati ya ibrahim na Mariam nani alianza kuwepo
mmmh noma sanaSiri Nyingi sana Zimefichwa kwa Hawa Viumbe wanaokuja Kukupa Taarifa za Mungu hapa Duniani
Mungu Ana Mwana
Mungu Ana Hasira
Mungu ana Wivu
Mungu ana Sikia
Mungu ana Mkono mrefu unafika Popote
Hizo Sifa Zote ni za Viumbe siyo Mungu kwahiyo wao wanampa Sifa Walizonazo wao
Huyu hapa Allah ameshasamehe dhambi zote zilizo pita na zijazo , waislamu wapo huru kufanya dhambi wanazo penda.Aisee kila mtu atabeba mzigo.wake msijidanganye kabisaaa ety kafa kwa ajili.ya dhambi zetu
Yni uue,uzini,uibe hlf useme kuna mtu kashanitubia dhambi zangu its non sense
Sasa mbona mnaenda makanisani ili msamehewe dhambi zenu? Na ubaya zaidi ety Pastor au Padri ndie anaesamehe dhambi wakati yy hpo anamichepuko kibao
kusema ukweli wakristo jitafakarini bhna mumeingizwa chaka na iyo imani yenu
Mungu anaishi katika nafsi 3
MUNGU BABA
MUNGU MWANA
ROHO MTAKATIFU
Nafsi ya pili ndio ilikuja duniani kwa mwili wa binadamu, ikaonekana waziwazi na wanadamu.
Aliyekufa na kufufuka ni Yesu kristo. Wakati amekufa nafsi nyingine zinafanya kazi.
Allah kasema ameshawasamehe dhambi zilizo pita na mtakazo fanya , mbona bado mnaenda msikitini kutubu?Jibu hoja izo m sina shida ila kwanini mseme mshabebewa dhambi zenu hlf mnaenda makanisani kutubu?
Hata ungepewa facts 1000 za maandiko matakatifu kama hujafungua ufahamu na moyo kumwamini Yesu Kristo kuwa ni Mungu alikufa na kufufuka kwa ajili yako huwezi kuokoka wala kumwelewa Mungu.
Kuamini Kunakuja Baada ya Kuambiwa Ukweli ukisema Ukweli unaoingia Akilini watu watakuamini sana Tu.Imani ya kikristo inaaminiwa kwanza sio kusomewa kwanza.
kama Shetani hasamehewi dhambi kwanini anaendelea kuachwa akiendelea kudanganya watu Ili Hali uwezo wa kumwangamiza asiendelee kuhadaa upo?Hawaogopi. Anawapenda wanadamu
Kumbuka aliiitengeza Dunia kwa lengo tu amuumbe mwanadam aje aishi hu
Mbona hujiulizi kwa Nini Shetani anamng'ang'ania mwanadamu amkoseshe asitende mapenzi ya Mungu Kuna Nini humo?
Ngoja nikuambie Shetani ana wivu sana na mwanadamu kwa sababu Mwanadamu anasanehewa dhambi. Shetani hasamehewi dhambi kwa hiyo anataka aende jehanam na wanadamu wengi sana
So anapofusha fikra zao wasielewe mpango wa Mungu waendelee kucheza na dhambi mwisho wake jehanam mile
Kumbuka mshahara wa dhambi ni mauti Bali karama ya Mungu ni uzima wa milele
Yohana 5 (Biblia Takatifu)Hata ungepewa facts 1000 za maandiko matakatifu kama hujafungua ufahamu na moyo kumwamini Yesu Kristo kuwa ni Mungu alikufa na kufufuka kwa ajili yako huwezi kuokoka wala kumwelewa Mungu.
Imani ya kikristo inaaminiwa kwanza sio kusomewa kwanza.
mbona unaleta maswali juu ya maswali jibu ilo swali kwanza
Kwanini isije wakati tunasema mungu anao uwezo wa kufanya chochote?Viumbe vyote vinazaliwa tena ni kwa matokeo ya mimba ambayo hutungwa kutokana na tendo maalumu la mwanamke na mwanamume sasa hiyo theory ya kupuliziwa udongo kiumbe kitokee unaona inakuja kweli?
Ukitaka kujadili usiwe unampinga Muhammad , muheshimu, kati ya unabii wake kasema wazi uislamu ulianza kama kituko na utarudi kuwa kituko, ulianza kama dini ndogo na utarudi kuwa dini ndogoJamani nyieeee Mungu hazaliwi nyie
Walokuleteeni iyo dini saivi wanaslimu kwa kasi huko
Mariam Yeye alizaa nini Sasa Kama Mungu wako Keshamzaa YesuYesu ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. Kabla hakijakuwako kitu chochote Mungu alimzaa Yesu