Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Hawaogopi. Anawapenda wanadamu
Kumbuka aliiitengeza Dunia kwa lengo tu amuumbe mwanadam aje aishi hu

Mbona hujiulizi kwa Nini Shetani anamng'ang'ania mwanadamu amkoseshe asitende mapenzi ya Mungu Kuna Nini humo?

Ngoja nikuambie Shetani ana wivu sana na mwanadamu kwa sababu Mwanadamu anasanehewa dhambi. Shetani hasamehewi dhambi kwa hiyo anataka aende jehanam na wanadamu wengi sana
So anapofusha fikra zao wasielewe mpango wa Mungu waendelee kucheza na dhambi mwisho wake jehanam mile
Kumbuka mshahara wa dhambi ni mauti Bali karama ya Mungu ni uzima wa milele
 
Tungekua tunatafuta kuujua ukweli kabla ya kubisha tusiyoyajua tungekua na amani sana
Na tungekua tunaujua mpango wa Mungu ni kwa kila aliyemuumba na yeye ni wa wote tusingejidai kumbinafsisha
Jibu hoja izo m sina shida ila kwanini mseme mshabebewa dhambi zenu hlf mnaenda makanisani kutubu?
 
Wacha ubaguzi na uharibifu kwa kigezo cha kummiliki mungu kupitia wewe.

Kama yeye Mungu aliyetuumba hakutubagua, alimpa Ishmail baraka zake na Isaka baraka zake wewe nani uje umbinafsishe Mungu awe wako mwenyewe?

Acha udini Mungu habinafsishwi

Pambana kuacha uovu uelewane na Mungu sio upambane kusema wewe ni bora kuliko wale hala Mungu akukatae


Mwanzo 17: 1-10; 15-19

Abrahamu alipokuwa mtu wa miaka tisini na kenda, Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu. Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe, nami nitakuzidisha sana sana.
Abrahamu akaanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema, Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi, wala jina lako hutaitwa tena Abrahamu, lakini jina lako litakuwa Ibrahimu, kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi.

Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako.
Agano langu nitalifanya imara kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako.
Nami nitakupa wewe na uzao wako baada yako nchi hii unayoikaa ugeni, nchi yote ya Kanaani, kuwa milki ya milele; nami nitakuwa Mungu wao.
Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada yako.
Hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa.

Mungu akamwambia Ibrahimu, Sarai mkeo, hutamwita jina lake Sarai, kwa kuwa jina lake litakuwa Sara.
Nami nitambariki, na tena nitakupa mwana kwake, naam, nitambariki, naye atakuwa mama wa mataifa, na wafalme wa kabila za watu watatoka kwake.

Ndipo Ibrahimu akaanguka kifudifudi akacheka, akasema moyoni, Je! Mtu wa umri wa miaka mia, kwake atazaliwa mtoto? Naye Sara mwenye umri wa miaka tisini atazaa?

Ibrahimu akamwambia Mungu, Lau kwamba Ishmaeli angeishi mbele yako.
Mungu akasema, Sivyo, lakini Sara mkeo atakuzalia mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Isaka. Nami nitafanya agano langu imara kwake kuwa agano la milele kwa ajili ya uzao wake baada yake.

Na kwa habari za Ishmaeli nimekusikia, nimembariki, nitamzidisha, nami nitamwongeza sana sana. Atazaa maseyidi kumi na wawili, nami nitamfanya awe taifa kuu.
Ubaguzi uko wapi? unajua uko nyuma tumejibizana vipi au unasema tuu

Mungu sio mbaguzi na wapi mm nimefanya ubaguzi? au kudhihirisha imani yangu ndo nimefanya ubaguzi?
 
Habari za humu ndani!

Nawakaribisheni watu wote wakristo, waislamu, na watu wa dini zote kabisa katika majibu ya maswali ambayo yamekuwa yakiwatatiza sana kuhusu Uungu na Ubinadamu wa Yesu Kristo.

Maswali ya msingi kama;
1. Yesu ni nani? Ni Mungu au ni mwanadamu?
2. Kwa nini anaitwa mwana wa Mungu? Alifanyikaje mwana wa Mungu? Je Mungu anazaa? Mungu ana mke?
3. Nini maana ya kusema Mungu alizaliwa? Alizaliwa na nani?
4. Mungu anaishi wapi? Mbinguni ama Duniani? Je hapo alipoziumba mbingu na nchi alikuwa wapi kabla? Nini maana ya mbingu na nchi?
5. Mungu ana watoto? Watoto wake ni kina nani? Wanapatikanaje?
6. Kwa nini Yesu alikufa kwa ajili ya wanadamu? Je aliuwawa au aliamua kufa mwenyewe? Alifufukaje? Nini uthibitisho yupo hai leo? Ni kaburi wazi? Au ni zaidi ya hilo?
7. Ni wakati gani mtu anaokoka? Ni mambo gani yanatakiwa kuaminiwa ili mtu kuokoka?
8. Umeokoka? Uliamini nini? Unaweza kuelezea kwa maneno rahisi nini maana ya kuokoka?

Kumfahamu Yesu Kristo ndio ufunguo wa kufahamu mambo yote ya Mungu.

Huwezi kujifunza hili kwa dondoo/tips au memes. Hata masomo ya darasani huajifunzi na kufaulu kwa namna hiyo.

Kujifunza kunahitaji nidhamu na uvumilivu. Lazima uwe tayari na kusikiliza mpaka mwisho. Kwa miaka mingi Biblia imeonekana kama kitabu ambacho ni complex na chenye mkanganyiko lakini complexity na mikanganyiko hiyo ipo kwenye fahamu za wasomaji na si kwenye biblia. Kwa sababu ya watu kutokufundishwa kwa usahihi na kutumia kimakosa biblia.

Maswali yote hapo juu na mengine mengi yanajibiwa kwa ufasaha kabisa katika series za masomo ya audio yaliyo katika website yenye link hii https://kainosmedia.org/mafundisho/hapo-mwanzo-part-1/

Anza na somo la kwanza Hapo Mwanzo: Kuelezea “Yesu ni Mungu” (In The Beggining: Explaining “Jesus is God”) zipo sehemu 6. Tafadhali zisikilize zote kwa umakini kabisa. Nakuhakikishia ufahamu wako hautakuwa kama mwanzo tena.

Baada ya kusikiliza karibu kwa swali pale ambapo hujaelewa vizuri.

Furahia shule yako.
Watu wengi humu haulizi maswali kwa maana ya kutaka kujifunza wasichokijua bali kwa mtazamo wa kutaka kuchallenge.
Imagine wewe ni mwanafunzi/mwanachuo umeenda darasani kwa lengo tu la kutaka kuchallenge mwalimu/lecturer wako HAKUNA namna utakaa uelewa somo lake. Utabakia vile ulivyo.

Wewe ni mwanadamu tena u mavumbi tuu kisha unataka kuyachallenge mambo ya Mungu (divinity) kabla ya kumwamini, HAKUNA namna utakaa uyaelewe pasipo kumwamini kwanza. Utabakia na ujinga wako huku ukijiona mwerevu mbele zake.

Kaa chini uwe tayari kujifunza.
 
Kabla ya Yesu kuja duniani, Mungu alikuwa anazungumza moja kwa moja na mwanadamu, baada ya kuja Yesu Mungu na mwanadamu wanazungumza kupitia Yesu Kristo.

Ndio msingi wa watu kuomba msamaha kila siku, sababu kama binadamu kukosea ni jambo lililo gumu kukwepeka kwa hiyo kila siku unaomba upatanisho na Mungu. Andiko sikupi sababu hata ukipewa hutaamini.
lete andiko kua Mungu alikua anazungumza na binadamu moja kwa moja
 

Mt 11:25-26 SUV​

Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako.
 
Biblia ni mkusanyiko wa vitabu. Yesu alisoma torati iliyoandikwa na manabii kama Isaya, kwa hiyo jibu kwa swali lako ni NDIYO
Sasa huo mkusanyiko uyo Yesu wenu hakuusoma alishushiwa injili tu na Mungu wake

hlf kaangalie kwenye iyo biblia yako Maana ya hekalu hlf utanambia uyo Yesu alikua anaswali wapi na nyinyi mnaswali wapi
 
Watu wengi humu haulizi maswali kwa maana ya kutaka kujifunza wasichokijua bali kwa mtazamo wa kutaka kuchallenge.
Imagine wewe ni mwanafunzi/mwanachuo umeenda darasani kwa lengo tu la kutaka kuchallenge mwalimu/lecturer wako HAKUNA namna utakaa uelewa somo lake. Utabakia vile ulivyo.

Wewe ni mwanadamu tena u mavumbi tuu kisha unataka kuyachallenge mambo ya Mungu (divinity) kabla ya kumwamini, HAKUNA namna utakaa uyaelewe pasipo kumwamini kwanza. Utabakia na ujinga wako huku ukijiona mwerevu mbele zake.

Kaa chini uwe tayari kujifunza.
Mungu alitaka kuwa mtu wa familia, basi Mungu akasema kama mtu mwenye familia lazima familia yangu inifahamu lakini kama Mungu hivi nilivyo hawawezi kunijua. Kwa sababu katika namna yangu kama Mungu mimi ni Nuru isiyoweza kufikiwa na mwanadamu mwenye mwili wa kufa.

Kwa hiyo Mungu aliketi na Mungu akatoka nje ya Mungu na Mungu akamtazama Mungu. Mungu akasema na Mungu. Wewe nenda! Mimi nasubiri hapa.

"Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, hata niwaweke adui zako kuwa chini ya miguu yako?" Mathayo 22:44 [Zab. 110:1.]

Mungu alikuwa akiongea na yeye mwenyewe. Basi Mungu mwingine akaingia katika tumbo la mwanamke (Bikira Maria).

Kuzaliwa kwa Yesu mara ya kwanza hakukuwa kuzaliwa kihalisi kwa maana halisi ya kuzaliwa bali kudhihirishwa.

16 Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu: *Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho,
Akaonekana na malaika,
Akahubiriwa katika mataifa,
Akaaminiwa katika ulimwengu,
Akachukuliwa juu katika utukufu.
1 Timotheo 3:16

Mungu alidhihirishwa haina maana ya kuzaliwa kama "kuzaliwa" bali kudhahirishwa.

Kwa hiyo kuzaliwa kwa Yesu mara ya kwanza ilikuwa ni KUONEKANA KWA MUNGU KWA MARA YA KWANZA KATIKA UMBO LA BINADAMU.

Karibu katika familia ya Mungu. Unakuwa mtoto wa Mungu na Mungu anakuwa Baba yako. Kuamini katika kazi kamilifu ya Yesu Kristo ni kupata haki yako halisi ya uzaliwa sio kuasiliwa.

Duniani na mbinguni hushangilia wewe kuwa mwana wa Mungu. Mungu akiishi ndani yako milele.

Nakutakia Kujifunza kwema
 
Hahahahah unafurahisha sana kwamba mtoto wa pekee angetakiwa kuwa Adam. Soma maandiko ndugu uyaelewe na siyo kuja na majibu yako kichwani.

Kwanj Majibu yako ndugu unayatoa Wapi. Maana Kama Huwezi Shirikisha Ubongo wako sahau kuja Kujua Yaliyojificha Kwenye Maandiko hayo unayoyatoa na Kuyaamini sana. Mmepotoshwa Ndio maana hamuwezi Kujua Ukweli ulipo mnakomaa kuomba Maandiko

Kama Yesu ndio mwanae wa Pekee Adam si Alikuwa Binadamu pia na Yesu si Mwanadamu aliyekuwa Hapa Duniani leo hii huo Upekee wa Yesu unakuwaje Ni mkubwa Kuliko upekee wa Adam!?

Yaani wewe uzae Watoto Halafu mtoto wa Pekee aje kuwa Mwanao wa Mwisho. Utakuwa na Akili timamu kweli





Yesu ndio mwana pekee wa Mungu. Yesu ndio MWANZO. Amekuwepo kabla ya Adam na nikupe siri moja ambayo huijui,
Yesu alishiriki uumbaji wa Adam

Hakuna Siri inayowekwa Kwenye Kitabu Kilichosambaa Dunia Nzima. Na Ukisema Siri maana Yake Ni Kitu kilichofichwa ukishakijiua siyo Siri hiyo.

Yesu awezi kuwa Mwana na Hapo hapo Akawa Tena Mungu muumbaji . Yaani ni Sawa na Wewe kujiita Mwana wa Fulani halafu Ukataka Tena Uwe Baba. Huwezi kuitwa Mwana da costa halafu hapo hapo wakakuita Da costa

Tutumieni Akili kuchambua Mnayoletewa
 
Bwana eeh.. mi siku izi nimeacha kuhangaika na haya mambo. Kama mungu aliniumba ili aje anichome moto mwishoni hiyo ni juu yake maana tunaambiwa yeye anatujua kabla hatujazaliwa na pia anajua mwenyewe alipopanga kutupeleka baada ya maisha haya... 😐
 
Ndugu yangu unajua Kwamba Kuzaa Ni Sifa Ya Kiumbe. Huoni kama Unamtukana Mungu tusi kubwa Sana Kusema Anazaa. Maana Yake Yesu ana Mama Yake si Ndio?amabye Yupo huko alipo Ambaye si Mariam



Umetoa Wapi haya Kwamba Alishiriki. Wakati Mungu Hashirikiani na Viumbe wake katika Uumbaji

Wewe ndio unasema kwamba kuzaa ni sifa ya kiumbe ila maandiko yanasema Mungu anazaa.
Waebrania : 1 : 5 - Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?

Maandiko hayo hapo Mungu anazaa. Lete andiko katika biblia Mungu anasema hazai tujue mbivu na mbichi leo
 
Habari za humu ndani!

Nawakaribisheni watu wote wakristo, waislamu, na watu wa dini zote kabisa katika majibu ya maswali ambayo yamekuwa yakiwatatiza sana kuhusu Uungu na Ubinadamu wa Yesu Kristo.

Maswali ya msingi kama;
1. Yesu ni nani? Ni Mungu au ni mwanadamu?
2. Kwa nini anaitwa mwana wa Mungu? Alifanyikaje mwana wa Mungu? Je Mungu anazaa? Mungu ana mke?
3. Nini maana ya kusema Mungu alizaliwa? Alizaliwa na nani?
4. Mungu anaishi wapi? Mbinguni ama Duniani? Je hapo alipoziumba mbingu na nchi alikuwa wapi kabla? Nini maana ya mbingu na nchi?
5. Mungu ana watoto? Watoto wake ni kina nani? Wanapatikanaje?
6. Kwa nini Yesu alikufa kwa ajili ya wanadamu? Je aliuwawa au aliamua kufa mwenyewe? Alifufukaje? Nini uthibitisho yupo hai leo? Ni kaburi wazi? Au ni zaidi ya hilo?
7. Ni wakati gani mtu anaokoka? Ni mambo gani yanatakiwa kuaminiwa ili mtu kuokoka?
8. Umeokoka? Uliamini nini? Unaweza kuelezea kwa maneno rahisi nini maana ya kuokoka?

Kumfahamu Yesu Kristo ndio ufunguo wa kufahamu mambo yote ya Mungu.

Huwezi kujifunza hili kwa dondoo/tips au memes. Hata masomo ya darasani huajifunzi na kufaulu kwa namna hiyo.

Kujifunza kunahitaji nidhamu na uvumilivu. Lazima uwe tayari na kusikiliza mpaka mwisho. Kwa miaka mingi Biblia imeonekana kama kitabu ambacho ni complex na chenye mkanganyiko lakini complexity na mikanganyiko hiyo ipo kwenye fahamu za wasomaji na si kwenye biblia. Kwa sababu ya watu kutokufundishwa kwa usahihi na kutumia kimakosa biblia.

Maswali yote hapo juu na mengine mengi yanajibiwa kwa ufasaha kabisa katika series za masomo ya audio yaliyo katika website yenye link hii https://kainosmedia.org/mafundisho/hapo-mwanzo-part-1/

Anza na somo la kwanza Hapo Mwanzo: Kuelezea “Yesu ni Mungu” (In The Beggining: Explaining “Jesus is God”) zipo sehemu 6. Tafadhali zisikilize zote kwa umakini kabisa. Nakuhakikishia ufahamu wako hautakuwa kama mwanzo tena.

Baada ya kusikiliza karibu kwa swali pale ambapo hujaelewa vizuri.

Furahia shule yako.
Jamani nyieeee Mungu hazaliwi nyie
Walokuleteeni iyo dini saivi wanaslimu kwa kasi huko
 
vizuri sana
Enheeee yesu kazaliwa na nani?

Waebrania : 1 : 5 - Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?
 
Wakolosai : 1 : 15 - naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
Wakolosai : 1 : 16 - Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.
Yesu katika Mahubiri yake haymjawahi Kuzungumza Haya mnayoyasema. Mwandishi wa Hicho kitabu Hata Hakuwa Mwanafunzi wake wala Kuwahi kuwa Karibu yake.

Leo hii anakuandikia hayo unayaamini. Yaani ni sawa na Mzungu kutoka ulaya Aje Tanzania akusimulie Historia ya Wangoni.
 
Tabia yako naijua vizuri , unataka andiko ukilitewa unaanza thibitisha kama Luka amemuona Yesu , Kuna kipindi nilikuuliza hafs alimuona muhammad , na Pia niikuuliza Muhammad alimuona Issa? kama hakuwahi kuwaona habari alizitoa wapi?
Ukiacha Hypocrisy ndio utaweza jadili na watu
Wewe jibu kwanza swali langu kisha uniulize kuhusu Mtume, ili uone tofauti yangu na yako iko wapi.
 
Waebrania : 1 : 5 - Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?
hujanitajia alomzaa ila m ninavojua alimzaa ni Mariam kwaio Mariam ndo Mungu wa Yesu?
 
Mimi siamini Hao Manabii unaowaamini wewe ndugu yangu. Na Ukiona Hivyo kwamba Yona Kamgomea Mungu basi Huyo Mungu hana Uwezo mana Hata Viumbe wake wanamgomea.

Kwa Akili Timamu huwezi sema Mungu hashindwi kitu Chochote kwake kinawezdkana Halafu uje Uniletee Stori za Nabij Yona Alimgomea Mungu.

QUOTE="olando da costa, post: 41840660, member: 497168"]
Andiko linafafanuliwa na andiko. Lete maandiko kwamba Mungu hazai na hana mwana tujue mbivu na mbichi leo.

Mungu hazai ukimpa Hiyo Sifa Basi Baba Yako na Mama Yako Pia Ni Mungu si Wanazaa bhana. Nyie kila Siku mnaimba Hafafani na Yeyote ila Mnampa Sifa Ya Kuzaa Mungu akishazaa Basi Hana Tofauti na Wewe NA wanyama Wengine wanaozaa pia.

Unakimbilia Maandiko yako wakati Hata Huko hakuna Andiko linalosema Mungu kazaa[/QUOTE]

Mada imeisha
Mungu anazaa na ana mwanawe anaitwa Yesu Kristo
Kwa taarifa yako
BILA YESU MBINGUNI HUTOBOI
 
Kuna Utata mkubwa Sana Katika kuzaliwa kwa Yesu kutokana Na Maandiko ya Biblia. Ila Kwa Akili Timamu Binadamu yeyote lazima Azaliwe kwa Mifumo maalumu ya Mbegu ya Kiume kuungana Na Mbegu ya Kike Tofauti na Hapo Binadamu hawezi Kutokea
kwa hiyo kuna uwezekano kuna siri imefichwa?
 
Back
Top Bottom