Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Mungu anawaogopa nini Wanadamu mpaka awatolee Sadaka ya Mwanae?

Baba akiitwa mwanasheria mtoto pia ataitwa mwanasheria?
Au tuseme baba akiwa hakimu mtoto pia ataitwa hakimu?
Au tuseme baba akiitwa rais mtoto pia ataitwa rais?
[emoji2377][emoji2377][emoji2377]
Kwanini hamtaki kukubali kuwa baba na mtoto hawako sawa??
Ni ngumu kwao kukubali Hilo ingawa Moyoni wanajua Ukweli Ulipo ila Hawataki kukubaliana Na Ukweli kwamba Wamepotoshwa sana na Wameharibikiwa

Hata Jina La Yesu Halikutabiriwa katika Maandiko ila Aliyetabiriwa alikuwa ni Emanueli
 
Mkuu me nasoma biblia ila sipotezi mda wangu kusoma story sijui za waisrael, sijui wakina ESTA , au story za makabila ya waisrael ,cjui washeba, mara sijui wanan , Mimi huwa napenda mistari inayoniongezea busara na maarifa kama hekima ,enjili nk
Umechagua Jambo Jema. Tafuta Hekima Itakayokufaa katika Vitabu ila Kuwa Muumini wa Akili Timamu tu Ndugu hakuna Malaika waongo... Majini waongo watakaokusumbua
 
Mutah girl koran bila Hadith na tafsir haieleweki inaacha maswali yasiyo na majibu

Mfano Aya hii
Koran 66:4. Kama nyinyi wawili hamkutubia kwa Mwenyezi Mungu, basi nyoyo zenu zimekwisha elekea huko. Na mkisaidiana dhidi yake muhammad, basi hakika Allah ndiye kipenzi chake, na Jibrili, na Waumini wema, na zaidi ya hayo Malaika pia watasaidia.

Utajiuliza maswali
1. hao wawili ni kina nani? ,
2. Wamefanya dhambi gani mpaka waambiwe watubu? ,
3. Wakisaidiana dhidi ya Muhammad kwani Muhammad kafanya nini? ,
4. Kwa nini Allah asaidiane na Malaika wote , jibril na waumini wote kupambana na hao wawili?
5. Awa wawili wana nguvu gani mpaka Allah asaidiwe

Jibu unalipata Kwenye Hadith
1. Wawili ni Aisha na hafsa
2. Walikuwa wanamkataza Muhammad kubaka House girl
3. Muhammad alikuwa ana mbala house girl anaitwa maria
4. Allah hana nguvu
5. Walikuwa wanammandi Muhammad mpaka Allah akaingilia kati kumruhusu kutembea na house girl

Hadith inamajibu
Muhammad had a female slave with whom he had intercourse, but 'Aishah and Hafsah would not leave him alone until he said that she was forbidden for him. Then Allah, the Mighty and Sublime, revealed:
"O Prophet! Why do you forbid (for yourself) that which Allah has allowed to you.' until the end of the Verse. Sunan an-Nasa'i 3959
Huo ni ujuha wako tu. Qur'an inajitosheleza. Hakuna neno la Binaadam lishindane na la Allah. Kuamini kuwa hadith (maneno ya binaadam) ndio yanatafsiri maneno ya Mwenyeezi Mungu ni kufanya shirki.

Qur'an ni "criterion", yenyewe inasema imekuja kuweka sawa palipotiwa mikono ya watu, sasa tuendeleze ujinga huohuo wa kutia mikono yetu na kuiona kuwa Qur'an haijitoshelezi? Kwa mtazamo wangu huo ni ujuha tu.

Qur'an haina shaka.
 
Soma uelewe kwanza.. umeambiwa kama unaona Miungu ya babu zenu inafaa nendeni mkaiabudu. HAUJALAZIMISHWA KUIAMINI BIBLIA.
Hujui Kwamba Huko Ndiko kuna Miungu Tofauti tofauti kuliko unaposema Mababu wa Miungu.Mababu walikuwa na Mungu si Miungu

Hamjui kwamba Huko Mnaabudu Miungu mitatu (utatu)
 
Huo ni ujuha wako tu. Qur'an inajitosheleza. Hakuna neno la Binaadam lishindane na la Allah. Kuamini kuwa hadith (maneno ya binaadam) ndio yanatafsiri maneno ya Mwenyeezi Mungu ni kufanya shirki.

Qur'an ni "criterion", yenyewe inasema imekuja kuweka sawa palipotiwa mikono ya watu, sasa tuendeleze ujinga huohuo wa kutia mikono yetu na kuiona kuwa Qur'an haijitoshelezi? Kwa mtazamo wangu huo ni ujuha tu.

Qur'an haina shaka.
Jibu Aya maswali bila Hadith wala tafsir

Mfano Aya hii
Koran 66:4. Kama nyinyi wawili hamkutubia kwa Mwenyezi Mungu, basi nyoyo zenu zimekwisha elekea huko. Na mkisaidiana dhidi yake muhammad, basi hakika Allah ndiye kipenzi chake, na Jibrili, na Waumini wema, na zaidi ya hayo Malaika pia watasaidia.

maswali
1. hao wawili ni kina nani? ,
2. Wamefanya dhambi gani mpaka waambiwe watubu? ,
3. Wakisaidiana dhidi ya Muhammad kwani Muhammad kafanya nini? ,
4. Kwa nini Allah asaidiane na Malaika wote , jibril na waumini wote kupambana na hao wawili?
5. Awa wawili wana nguvu gani mpaka Allah asaidiwe
 
Kuna Mambo Yapo Ulimwenguni ukiyatafakari kwa Kina hayaingii Akilini ndugu waafrika wenzangu

Kuna Historia katika Vitabu kwamba Mungu alimtoa Mwanae Ili aje Kuikomboa Dunia katika Dhambi (ambazo zipo mpaka Leo)

Ukiangalia kwa Undani Historia hii ya kuzaliwa kwake inatia Shaka sana kabla ya Kujua Majibu ya kuzaliwa kwake inakuja Historia kwamba hana Baba. Kabla hujapata Majibu ya Baba ni nani Inakuja Kwamba ni Uwezo wa Mungu ndio akazaliwa. Yanakuwa Maswali juu ya Maswali

Kumbuka Yusufu na Mariam si kwamba Walikuwa ni Wachumba la hasha bali walikuwa tayari wapo Ndani (wameoana) wanaishi pamoja. Hakuna wachumba Wanaoishi pamoja kwa Utaratibu wa Kuishi. Ukichumbia wewe utakaa kwako na Huyo mchumba atakaa kwao. Kama Waliishi pamoja maana Yake waliweza Kushiriki Tendo la Ndoa yao na Ukifuatilia kwa Makini Yusuf alikuwa Pamoja na Mariam kila Sehemu hakuna Sehemu inayosema Alikuja Kumuoa mariam Ikiwa na Maana Kwamba Tayari alikuwa keshaoa maana yake ule uchumba ulio andikwa Tayari ukayeyuka

Binadamu huzaliwa Kwa Mwanaume na Mwanamke hili halina ubishi. Ila Kuna Kuja Utata wa Hapa Kwamba Yesu alizaliwa bila Mfumo maalumu wa Uzazi wa Baba na Mama ila Roho Mtakatifu kama Wanavyodai (kumbuka Hata Huko india Wapo Watu wenye Hadithi hizi hizi za Kuzaliwa bila Baba)

Sasa Hapa Unajiuliza Maswali. Mungu huyo aliyeweza Kumuumba Mwanadamu wa Kwanza Bila Kutumia mifumo ya Uzazi Inakuwaje leo aje Aanze Kumuumba Binadamu mwingine anayedaiwa ni Mwanae kwa Mifumo ya Uzazi na Akaenda kwa Mariam ambaye alikuwa teyari ana Mume(kumbuka Hapa Mungu hazai na Wala Hakuzailiwa)

Sasa Anamzaa mwanae kupitia Mariam mara Yusufu atake kumkimbia Mariam maana Kuna Siri May be Yusufu aliiona akaona Hapa Nimepigwa na Baada ya Yesu kuzaliwa Yusuf Anapotea Ghafla kwenye Maandiko na Historia yake inaishia Hapo hapo

Mungu anamtoa Mwanae. Anakuja Mnamkataa, mnampiga, mnamtesa anawahubiria mnagoma Kukubali maneno yake mnamfukuza kwenye masinagogo yake, Anaenda Kusali mlimani peke yake, anakusanya wanafunzi wake. Hao wanafunzi nao mnawakataa mnawafukuza. Hivi Mungu hapo anawaogopa Nyie kisa Nini mpak Awafanyie Haya Yote Nyie Viumbe wake

Yaani Mungu mpaka Anatoa Mtoto wake Wa Pekee ili awabembeleze nyie mmrudie Yeye na Mnakataa. Sasa Hapo Mungu Anakuwa na Ule Uwezo na Kutoshindwa Kitu kweli. Kama Kawatumia Mwanae na Mmemgomea kawatumia Manabii na Mitume mmemgomea Tena na hamtaki kumrudia. Hivi Mungu anawalemba Hivyo Ili Iweje

Si kila Mtu anayezaliwa bila Baba Yake basi Baba Yake ndio Mungu. Wachawi wanazini na Binadamu kila Siku na Wachawi hao hao ndio Binadamu wenzenu. Wanawake wanabeba Mimba zingine wasizozijua zimetoka wapi

Basi Mjue Kwamba Hapo Mwenye Enzi Mungu hayupo na Mnaozeshwa Akili zenu ndugu zangu. Kaeni Chini Mtafakari kwa Akili zenu Timamu. Mungu hawezi kufanya hayo Kwa Viumbe wake. Yeye hayupo Hivyo

[emoji3507]Mungu si Mmoja
[emoji3507]Mungu si Wengi
[emoji3507]Mungu si Baba
[emoji3507]Mungu si Mama
[emoji3507]Mungu si Kiumbe
[emoji3507]Mungu hachukii Viumbe
[emoji3507]Mungu hapendi Viumbe wake ila Ana Enzi na Viumbe wake (usijione wewe Kiumbe Mtu unapendwa na Mungu Kuliko Viumbe wake wengine aliowaumba)
[emoji3507]Mungu hakuzaa wala Kuzaliwa

Yachunguzeni maandiko Yenu mtajua kwamba si Maandiko ya kiucha Mungu ila Maandiko ya Viumbe wenye Tamaa

ASANTENI
Haileti maana yoyote pale tunapoambiwa Mungu anajua hadi wakati ujao. Alafu huyo huyo anaweka mpango siku moja aumbe binadamu huku akijua watamuasi na itambidi amtoe mwanae wa pekee kama sadaka.
 
Haileti maana yoyote pale tunapoambiwa Mungu anajua hadi wakati ujao. Alafu huyo huyo anaweka mpango siku moja aumbe binadamu huku akijua watamuasi na itambidi amtoe mwanae wa pekee kama sadaka.
Ndivyo watu wanaishi kwenye Hizo Imani
 
Hujui Kwamba Huko Ndiko kuna Miungu Tofauti tofauti kuliko unaposema Mababu wa Miungu.Mababu walikuwa na Mungu si Miungu

Hamjui kwamba Huko Mnaabudu Miungu mitatu (utatu)
Nilisha kuonya ukitaka kujua Imani ya watu kaisome kwanza uelewe, Mungu wa wakristo unatakiwa uelewe yupoje ili kuepuka maswali ya kitoto

Mungu ni Roho na ana nafsi tatu toka uwepo wake , ana Nafsi Baba , Mwana na Roho mtakatifu na nafsi zake zote ni divine

Mungu alitengeneza mwili humani flesh ambayo ilipitia kwa maria ambayo ndio aliitoa sadaka na kufuta sadaka zote za damu za wanyama

Aliitoa nafsi yake moja ya mwana ndio ikavaa mwili human flesh huo mwili iliopitia kwa maria

Mungu hazai wala hajazaliwa , Mungu hafi
Mwili alikuwa nao nafsi mwana ndio ulikufa na aliufufua mwenyewe huo mwili
Alikuja kwetu kutufunza jinsi ya kuishi utakati na jinsi tunatakiwa kumuabudu Mungu

Kuna mda Yesu alikuwa anaongea kama human flesh na kutenda kama human
Na Kuna mda alikuwa anaongea nafsi ya Mungu ambayo ilikuwa ndani yake kama miujiza , kufufua wafu , kusamehe dhambi n.k

Unaposoma biblia unatakiwa ujue wapi Yesu anaongea kama human flesh na wapi anaongea kama Mungu

Ndio maana Kuna watu niliwakanya hapa wasiingize nature ya Mungu wao kwa Mungu wa wakristo na wewe nakukanya usilete nature ya Mungu wako kwa Mungu wa wakristo

You a demonic possessed
 
Alafu hapo hapo anaweka na moto wa milele. Yani alijua kabisa atamuumba mtu na mtu atazingua na itabidi kumchoma moto ila akamuumba ili aone shoo ya moto wa milele imekaaje.[emoji17]
Wakija Watakuambia Unakufuru. Yaani Unatengeza Kitu kama Gari aj Baskeli halafu Kikikuangusha Unakichoma Moto na Kusema Umekikomesha na Kitasaga Meno
 
Watu hawawezi kuelewa bila mfano....kuzihirishwa kwa yesu ulikkua mfano tosha kwa maisha ya mwandamu.
 
Hizo porojo zako binafsi, weka ushahidi wa maandiko, kama huna ni heri ukae kimya tu.

Waebrania : 1 : 4 - amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao.
Waebrania : 1 : 8 - Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.

Maandiko hayo hapo
Baba anamuita mwana Mungu.
 
Jibu Aya maswali bila Hadith wala tafsir

Mfano Aya hii
Koran 66:4. Kama nyinyi wawili hamkutubia kwa Mwenyezi Mungu, basi nyoyo zenu zimekwisha elekea huko. Na mkisaidiana dhidi yake muhammad, basi hakika Allah ndiye kipenzi chake, na Jibrili, na Waumini wema, na zaidi ya hayo Malaika pia watasaidia.

maswali
1. hao wawili ni kina nani? ,
2. Wamefanya dhambi gani mpaka waambiwe watubu? ,
3. Wakisaidiana dhidi ya Muhammad kwani Muhammad kafanya nini? ,
4. Kwa nini Allah asaidiane na Malaika wote , jibril na waumini wote kupambana na hao wawili?
5. Awa wawili wana nguvu gani mpaka Allah asaidiwe
Aisee mbona unachukua aya moja tu katafute aya toka ya kwanza ndo utajua maana yake
 
Nilisha kuonya ukitaka kujua Imani ya watu kaisome kwanza uelewe, Mungu wa wakristo unatakiwa uelewe yupoje ili kuepuka maswali ya kitoto
Una Ucha Mungu Mkubwa Sana ila Unatetea Imani Za Wengine ambazo huzijui ndugu yangu. Unapomuita Mungu Baba na Kumwita Yesu Mungu Mwana Hao Ni Miungu Miwili tayari

Na Ki Utu... Baba Ni Jinsia ya Kiume ya Viumbe. Mungu Hawezi akawa na Sifa za Kiumbe yeye Hafanani na Chochote kile wala Kiumbe chochote kile



Mungu ni Roho na ana nafsi tatu toka uwepo wake , ana Nafsi Baba , Mwana na Roho mtakatifu na nafsi zake zote ni divine

Mungu alitengeneza mwili humani flesh ambayo ilipitia kwa maria ambayo ndio aliitoa sadaka na kufuta sadaka zote za damu za wanyama

1.Mungu hakuwa na Haja Ya Kufanya Hayo Yote wakati aliweza Kumuumba Adam unayemwamini kama Mwanadamu wa Kwanza Kutoka Kwenye Udongo. Mimba ya Mariam ina utata maana Malaika Aliyekuja Kumjuza Alimwambia Mtoto atamwita Yesu wakati Isaya Alitabiri ataitwa Emanueli angetakiwa Kumuita Kama ilivyotabiriwa na Isaya kwanza

2. Wayahudi waliendelea na Ibada za Wanyama na Kuendelea na Torati. Yesu Hakuziondoa Hizo Sadaka



Aliitoa nafsi yake moja ya mwana ndio ikavaa mwili human flesh huo mwili iliopitia kwa maria

Mungu hazai wala hajazaliwa , Mungu hafi
Mwili alikuwa nao nafsi mwana ndio ulikufa na aliufufua mwenyewe huo mwili
Alikuja kwetu kutufunza jinsi ya kuishi utakati na jinsi tunatakiwa kumuabudu Mungu

Kuna mda Yesu alikuwa anaongea kama human flesh na kutenda kama human
Na Kuna mda alikuwa anaongea nafsi ya Mungu ambayo ilikuwa ndani yake kama miujiza , kufufua wafu , kusamehe dhambi n.k

Unaposoma biblia unatakiwa ujue wapi Yesu anaongea kama human flesh na wapi anaongea kama Mungu

Ndio maana Kuna watu niliwakanya hapa wasiingize nature ya Mungu wao kwa Mungu wa wakristo na wewe nakukanya usilete nature ya Mungu wako kwa Mungu wa wakristo

You a demonic possessed
Acha Kupanic ndugu yangu
Mie Maswali yangu Ndugu ni Haya

1. Wewe ulifanya Nini Mpaka Akatoa Nafsi yake Ije Duniani na Aitoe Sadaka

2. Alikuja Kukufundishajw Kuabudu wakati Musa Alikuwa na Torati tayari iliyokuwa na Miongozo Mingi

3. Na Inakuwaje Yesu alipopatwa na Magumu alienda Kuongea na Musa na Elia wakati nafsi mbili aliziacha Mbinguni. Kwanini Asingeongea na Mungu mwenyewe
 
Baba akiitwa mwanasheria mtoto pia ataitwa mwanasheria?
Au tuseme baba akiwa hakimu mtoto pia ataitwa hakimu?
Au tuseme baba akiitwa rais mtoto pia ataitwa rais?
[emoji2377][emoji2377][emoji2377]
Kwanini hamtaki kukubali kuwa baba na mtoto hawako sawa??

Maandiko yanasema Baba anaitwa Mungu na mwana pia anaitwa Mungu

Waebrania : 1 : 8 - Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.
 
Ndugu Dira Ilikuwepo Ila Kutokana Na Kuja Kwa Wakoloni wakaita Ni Ushenzi na Uchawi. Sasa hivi Watu wanakesha Waangalia Kwaya na Kwenda Kusali Ijumaa. Jumamosi na Jumapili huo Muda wa Kusema Au Kutafuta Ukweli wa Ki Utu na Dira ya Kiafrika wataupta Wapi

Tena Akifika Huko wanaanza Kukemea Mizimu ya Mababu zao. Unategema Watakuwa Salama Hao zaidi ya Kuharibikiwa
Hivi kwanini huwa mnawatazama watu wa dini tu tena wakristo na waislamu tu, wenye imani tofauti na hizo mbona hamuwatizami? na wale wasioamini Mungu au dini mbona hamuwaubilii?
 
Hivi kwanini huwa mnawatazama watu wa dini tu tena wakristo na waislamu tu, wenye imani tofauti na hizo mbona hamuwatizami? na wale wasioamini Mungu au dini mbona hamuwaubilii?
Wapagani- hawa ni Watu wasioegemea Upande wowote ule wa Ki dini. Wanaweza Wakawa wanajua Ukweli ila Wakaa pembeni tu Hawajihusishi na Chochote

Wakristu na Waislamu wao Hujinadi wanamjua Mungu na Ndio wenye Mungu wa Kweli kuliko Wengine na uwahubiria Watu wengine wamepotea na Watachomwa Moto kama Hawatomwamini Mungu wao

Wakati Ukweli ni Kwamba Ni Dini zilizoletwa na Viumbe wapotofu na Hazina Ukweli ndani yake. Ukweli upo kwenye Jadi na Elimu ya Mwanzo ya Wazee wetu waliomjua Mungu kabla ya Hizo Dini Kuja
 
Utaanzishaje Dini Yako au Imani yako Ndugu wakati hujui Mwanzo kulikuwaje. Hata Watu wakikuuliza Umetokea Wapi utawajibuje Wakati Dini yako Umeianzisha 2022.
Kwani hao wazee wetu afrika tunajua hizo imani zao walizipata wapi na kwa vp? hapa kinachoonekana lengo ni kuwa na kitu chetu wenyewe waafrika na kuacha kutumia vitu vya kuletewa ndio maana uislamu na ukristo tunaita ni imani za kuletewa sio asili yetu. Kwahiyo na sisi tuanzishe dini yetu yenye kubeba mambo ya kiafrika na kwa sasa tuna nafasi nzuri tunaweza kuandika hivyo hata vizazi vyetu vijavyo watakuta maandiko ya dini ya mababu zao.
 
Kwani hao wazee wetu afrika tunajua hizo imani zao walizipata wapi na kwa vp?
Kwani Wewe ndugu yangu Tz Mbongo. Unajua Elimu za Mababu wa Israeli kina Musa.. Elia.. Isaya walizipataje.!? Au umesoma Tu kwamba Walipata Kwa Mungu na Wewe ukaamini Bila Kuhoji

hapa kinachoonekana lengo ni kuwa na kitu chetu wenyewe waafrika na kuacha kutumia vitu vya kuletewa ndio maana uislamu na ukristo tunaita ni imani za kuletewa sio asili yetu. Kwahiyo na sisi tuanzishe dini yetu yenye kubeba mambo ya kiafrika na kwa sasa tuna nafasi nzuri tunaweza kuandika hivyo hata vizazi vyetu vijavyo watakuta maandiko ya dini ya mababu zao.

Elimu Yetu ipo Inaitwa SENDE ESUPRY DEWO OCHI. Ni Kibantu kikimaanisha NGUVU ILIYODUMU KATIKA JADI
 
Back
Top Bottom