Mwamuzi wa Tanzania
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 15,486
- 45,256
Habari!
Mbele za Mungu sisi wanadamu ni kama majani na upepo tu.
Yes ametuumba na anatulinda ila kuna wakati anatutazama kwa namna nyingine. Yaani anatusort kulingana na agano lake na mtu husika, au anatusort kulingana na maisha na mienendo yetu.
Kama humchi Mungu , Mungu anaweza kukutumia wewe ili kufanikisha jambo la mtu mwingine huku wewe akikuacha umeumia, kuteseka au hata kufa.
Siku moja nilishikwa na polisi Songea stand asubuhi na mapema kwa kosa nisilolifahamu, nilihisi ni uzurujaji.
Ndo nilikuwa nimefika Songea kwa mara ya kwanza kama mtafutaji huku nikiwa sina hata sh. Mia, pesa yote iliisha , ni stori ya kutia hudhuni na baadaye ilileta furaha, nililala nje siku 5 baadaye nikapata mpenyo nikaishi vizuri.
Ndani ya selo tulikuwa kama 15 hivi.
Sikuwa na simu, kitabu changu chenye namba za simu kiliibiwa pamoja na vitu vichache nikiwa safarini.
Sikuwa na ticket maana niliingia usiku na Lori.
Sikuwa na ndugu Songea
Sikuwa na namba ya simu kichwani labda niwajuze ndugu zangu nyumbani.
Pasi na shaka nilikuwa nakwenda kufungwa miezi 6 kwa sheria ndogo za manispaa chap.
Sasa huku nataka nijitetee roho wa Mungu akanizuia nisiongee chochote.
Mara Nikasikia sauti kutoka desk la nje ambapo mkuu wa kituo mama mmoja mwenye cheo cha MRAKIBU kama sijakosea akiongea na radio call . Alikuwa akijuzwa kuwa basi la super Feo limepata ajali nje kidogo ya manispaa ya Songea na watu kadhaa wamekufa papo hapo.
Akaamuru dereva aje haraka atuchukue tupelekwe central police station Songea ili Askari wa pale wakasaidie huko kwenye ajali .
Ikaja gari haraka tukaamuliwa tutoke nje kwa mstari kisha tupande karandinga haraka.
Mimi nikawa wa mwisho katika mstari ule wa kuelekea nje kupanda karandinga.
Wakapanda wote about 10 na ushehe hivi .
Imefika zamu yangu kupanda nikasimama tu karibu na gari huku nimekaa kimya.
Wakapanda maaskari kwenye gari kisha ikawashwa ikaondoka na watuhumiwa huku Mimi wameniacha chini. Askari wengine walibaki pale kituoni kuendelea na shughuli zingine.
Kwa kweli sikujua nini kiliendelea.
Nilichogundua ni kuwa Mungu humpa thamani kubwa sana mtu wake mwenye agano naye, yuko tayari aue wengi ili akutetee.
Kwa tukio Lile, niliuona utukufu wa Mungu.
Nikasepa zangu.
Mbele za Mungu sisi wanadamu ni kama majani na upepo tu.
Yes ametuumba na anatulinda ila kuna wakati anatutazama kwa namna nyingine. Yaani anatusort kulingana na agano lake na mtu husika, au anatusort kulingana na maisha na mienendo yetu.
Kama humchi Mungu , Mungu anaweza kukutumia wewe ili kufanikisha jambo la mtu mwingine huku wewe akikuacha umeumia, kuteseka au hata kufa.
Siku moja nilishikwa na polisi Songea stand asubuhi na mapema kwa kosa nisilolifahamu, nilihisi ni uzurujaji.
Ndo nilikuwa nimefika Songea kwa mara ya kwanza kama mtafutaji huku nikiwa sina hata sh. Mia, pesa yote iliisha , ni stori ya kutia hudhuni na baadaye ilileta furaha, nililala nje siku 5 baadaye nikapata mpenyo nikaishi vizuri.
Ndani ya selo tulikuwa kama 15 hivi.
Sikuwa na simu, kitabu changu chenye namba za simu kiliibiwa pamoja na vitu vichache nikiwa safarini.
Sikuwa na ticket maana niliingia usiku na Lori.
Sikuwa na ndugu Songea
Sikuwa na namba ya simu kichwani labda niwajuze ndugu zangu nyumbani.
Pasi na shaka nilikuwa nakwenda kufungwa miezi 6 kwa sheria ndogo za manispaa chap.
Sasa huku nataka nijitetee roho wa Mungu akanizuia nisiongee chochote.
Mara Nikasikia sauti kutoka desk la nje ambapo mkuu wa kituo mama mmoja mwenye cheo cha MRAKIBU kama sijakosea akiongea na radio call . Alikuwa akijuzwa kuwa basi la super Feo limepata ajali nje kidogo ya manispaa ya Songea na watu kadhaa wamekufa papo hapo.
Akaamuru dereva aje haraka atuchukue tupelekwe central police station Songea ili Askari wa pale wakasaidie huko kwenye ajali .
Ikaja gari haraka tukaamuliwa tutoke nje kwa mstari kisha tupande karandinga haraka.
Mimi nikawa wa mwisho katika mstari ule wa kuelekea nje kupanda karandinga.
Wakapanda wote about 10 na ushehe hivi .
Imefika zamu yangu kupanda nikasimama tu karibu na gari huku nimekaa kimya.
Wakapanda maaskari kwenye gari kisha ikawashwa ikaondoka na watuhumiwa huku Mimi wameniacha chini. Askari wengine walibaki pale kituoni kuendelea na shughuli zingine.
Kwa kweli sikujua nini kiliendelea.
Nilichogundua ni kuwa Mungu humpa thamani kubwa sana mtu wake mwenye agano naye, yuko tayari aue wengi ili akutetee.
Kwa tukio Lile, niliuona utukufu wa Mungu.
Nikasepa zangu.