Mungu kama upo unapaswa kuniomba msamaha

Hatuwezi kulazimishana kuhusu haya mambo ya imani n ahata siamini kama yanatakiwa kuwa hivyo ila kwa sasa naomba utafute msaada wa kiafya. Waone madaktri au mshirikishe mtu unayemuamini jambo lako.

Nakutakia siku njema.
 
Ulimuuliza mama yako akasema mungu ndo alimgegeda ukazaliwa wewe?
 
Sun is Sun Sijajua kama ni jokes au ulichokiandika kimetoka katika akili Yako timamu, Ayubu alipokuwa katika nyakati ngumu alishawahi kulaani siku aliyozaliwa
Ayubu 3:1&3
[1]Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake.
[3]Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi,
Na ule usiku uliosema,
Mtoto mume ametungishwa mimba. Hii ni baada ya Ayubu kuwa katika Hali ya majuto katika alichokuwa akipitia Kwa Wakati ule, Lakini licha ya hayo Ayubu hakutoka kwenye njia yake ya kumtumikia Mungu mwenyezi, ikiwa ulichokiandika upo katika utimamu wa akili Yako tafuta njia nyingine ya kuwasilisha hitaji lako mbele za Mungu, Lakini kama ulichokiandika ni msukumo tu wa hisia, Kwa sababu tumepewa mamlaka juu ya matamko na nguvu ya maneno na kinywa Natamka "Mungu akusamehe"
 
Ipo hatari kubwa sana ya hili tatizo la afya ya akili. Akitoka hapo atamlaumu mzazi wake
 
Mithali 30 : 9

Nisije nikashiba nikakukana, Nikasema, Bwana ni nani? Wala nisiwe maskini sana nikaiba, Na kulitaja bure jina la Mungu wangu.

Umaskini huleta kufuru kwa Mungu
 
Jifunze kuomba, sio kukufuru
 
Mkuu umekunywa??
 
Dhambi waga inarithisha, mpaka umefikia kusema hivo Kuna Babu mzaa Babu Yako,Babu Yako ,baba Yako alafu Kuna wewe, alafu atakuja mwanao, tafakari kwa Nini umewaza hivo , utagundua siyo kosa lako, ila jua hujawaza hivo Bure,jua una kazi ya kufanya ili wanao wasiwaze hivo
 
Katika utafiti nilioufanya, Nimekuja na hitimisho kuwa wanaojifanya kumuamini Mungu kwa asilimia kubwa ndio wanaongoza kwa unafiki na nahisi hata dhambi wananizidi.

Mungu anajua alichonifanyia ndio maana bado nina kesi naye.

Hamuwezi kujua nyie, Kaeni kwa kutulia alaaaah😉
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…