Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Waliomba chakula, wakapewa mama. Wamekula miaka na miaka..wamechoka,.wakataka kitu cha tofauti..Mungu akawaua kwa kutaka kitu tofauti na mana.Kwani hiyo Mana waliomba Mungu awape au Mungu ndo akiamua kuwapa Aina hiyo chakula ?
Je unafikiri Mungu hakujua umuhimu wa hiyo Mana kulingana na mazingira waliokuwa nayo ?
means Mungu WA huruma Ni propagandaMatukio yote uliyo orodheshwa ni wanadamu walichagua kifo kwa kukaidi.
Mungu na shetani wote hawapo. Hawa ni wahusika tu katika hadithi ya kutungwa na watu.Ndugu WanaJF,
Mungu ni muuaji ambaye amefanya mauaji ya halaiki mara kwa mara na wote tumeyasoma kwenye simulizi za biblia.
Pamoja na hivyo, bado shetani analaumiwa zaidi kwa kudaiwa kusababisha mauaji, magonjwa na mambo ya hivyo yasiyompendeza binadamu.
Tutumie agano la kale kujionea wenyewe jinsi huyu mungu mwenye 'huruma' alivyowatenda wanadamu.
Matukio Ambapo Mungu Aliua Watu Katika Agano la Kale
1. Gharika – Idadi ya vifo: Haijulikani, inakadiriwa 1,000,000+
Rejea: Mwanzo 6:5-7
“BWANA akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani, na kwamba kila kusudi analoliwaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. BWANA akasema, Nitamfuta mwanadamu, niliyemuumba, usoni pa nchi; mwanadamu, na mnyama, na kitambaacho, na ndege wa angani; maana, najutia ya kwamba nimewafanya.”
2. Uharibifu wa Sodoma na Gomora – Idadi ya vifo: 1,000
Rejea: Mwanzo 19:24-25
“Ndipo BWANA akanyesha juu ya Sodoma na Gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa BWANA; akaangusha miji hiyo, na Bonde lote, na wote waliokaa katika miji hiyo, na yote yaliyomea katika nchi ile.”
3. Mke wa Lutu – Mtu 1
Rejea: Mwanzo 19:26
“Lakini mkewe Lutu akaangalia nyuma akawa nguzo ya chumvi.”
4. Mapigo ya Misri – Idadi ya vifo: Inakadiriwa 50,000
Rejea: Kutoka 12:29-30
“Ikawa usiku wa manane, BWANA akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, tangu mwana wa kwanza wa Farao aketiye juu ya kiti chake cha enzi, hata mwana wa kwanza wa mfungwa aliyekuwa gerezani; na wazaliwa wote wa kwanza wa wanyama. Farao akaondoka usiku huo, yeye na watumwa wake wote, na Wamisri wote; kukawa na kilio kikuu katika Misri, maana hapakuwa na nyumba pasipokuwa na maiti.”
5. Kisa cha Ndama wa Dhahabu – Watu 3,000
Rejea: Kutoka 32:27-28
“Akaawaambia, BWANA, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kila mtu na ajifunge upanga wake pajani mwake; mpitieni na kuupitia marago toka lango hili mpaka lango lile, kila mtu amwue ndugu yake, na rafiki yake, na jirani yake. Wana wa Lawi wakafanya kama vile Musa alivyosema; wakaanguka watu kama elfu tatu siku ile.”
6. Uasi wa Kora – Watu 14,950
Rejea: Hesabu 16:31-35, 49
"Ikawa, alipokwisha kusema maneno hayo yote, nchi ikapasuka iliyo chini yao; nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na nyumba zao, na watu wote waliokuwa wa Kora, na vyombo vyao vyote. Wakatumbukia ndani ya shimo, wao na wote waliokuwa nao hai, nchi ikawafunikiza, wakapotea katika mkutano.”
“Nao waliokufa kwa ile tauni walikuwa watu kumi na nne elfu na mia saba, zaidi ya wale waliokufa kwa sababu ya Kora.”
7. Malalamiko Katika Jangwa – Idadi ya vifo: Inakadiriwa 100
Rejea: Hesabu 11:1-3
“Watu walikuwa kama wanaonung’unika kwa ajili ya mabaya masikioni mwa BWANA; BWANA akasikia, hasira zake zikawaka, moto wa BWANA ukawaka kati yao, ukateketeza katika mipaka ya marago.”
8. Tauni kwa Kulalamikia Mana – Idadi ya vifo: Inakadiriwa 500
Rejea: Hesabu 11:33-34
“Kama nyama ilikuwa bado kati ya meno yao, kabla haijatafunwa, hasira za BWANA zikawaka juu ya watu, BWANA akawapiga watu kwa mapigo makuu sana. Kwakuo walipaita pale Kibroth-Hataava, kwa sababu hapo ndipo walipowazika watu waliokuwa na tamaa.”
9. Adhabu kwa Kuabudu Baali-Peori – Watu 24,000
Rejea: Hesabu 25:9
“Nao waliokufa kwa hiyo tauni walikuwa ishirini na nne elfu.”
10. Nyoka Wenye Moto – Idadi ya vifo: Inakadiriwa 200
Rejea: Hesabu 21:6
“BWANA akatuma nyoka za moto kati ya watu, wakawauma; wakaanguka watu wengi katika Israeli.”
11. Adhabu kwa Sababu ya Sensa – Watu 70,000
Rejea: 2 Samweli 24:15
“Basi BWANA akaleta tauni katika Israeli tangu asubuhi hata wakati ulioagizwa; wakafa watu sabini elfu miongoni mwa watu toka Dani mpaka Beer-Sheba.”
Jumla ya Vifo Vilivyosababishwa na Mungu: Inakadiriwa 1,100,000+
-
Vifo vilivyosababishwa na Shetani Katika Agano la Kale
1. Watoto wa Ayubu – Watu 10
Rejea: Ayubu 1:18-19
“Alipokuwa bado akinena, akaja mwingine, akasema, Wana wako na binti zako walikuwa wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa; kumbe, upepo mkubwa ukatoka upande wa jangwani, ukaipiga hiyo nyumba pembe zake nne, ikaanguka juu ya hao vijana, nao wamekufa; nami peke yangu nimepona ili nikuambie.”
Jumla ya Vifo Vilivyosababishwa na Shetani: 10
Kwa mantiki hii, Mungu ni muuaji mkubwa sana. Anachojali ni kuogopwa tu. Ni mkatili na ana tabia za psychopaths.
Mungu ni dikteta, character yake ni kama ya wakina Adolf Hitler au wale drug lords wa cartels za Amerika ya kusini.
Anyways, ni fiction tu. Waamini msijenge chuki. Twajua hata ninyi hamumpendi Mungu, ni hofu tu imewatawala, mnaogopa kuchomwa moto.
Siku njema mkiendelea kutafakari ukatili wa Mungu wa Yakobo.
Mungu na shetani waliwahi kukubaliana kujaribu muumini, sikumbuki Ni kifungu ganMahali popote penye ushetani ni Mungu karuhusu, hivyo Mungu ndiye muuwaji.
Tunalinganisha katika muktadha wa hadithi tu.Mungu na shetani wote hawapo. Hawa ni wahusika tu katika hadithi ya kutungwa na watu.
Ila, kama tunalinganisha wahusika katika hiyo hadithi, kama tunachambua riwaya, Mungu kaua zaidi.
Hutakiwi kumlinganisha mtu aliyeumba kifo, aliyekiruhusu kiwepo, na mwingine anayeua tu.
Huyo Mungu aliyeumba kifo, aliyekiruhusu kiwepo, siku zote atakuwa ameua zaidi.
Kwa sababu anahusika katika kila kifo, yeye ndiye chanzo cha vifo vyote, asingeruhusu kifo kiwepo, kungekuwa hakuna kifo. Hakuna ambaye angeweza kuua.
Kama kifo Ni adhabu,Kifo ni matokeo ya Uasi ,unapopanda mbegu lazima uvune haijalishi itachelewa au itawahi
Mshahara wa dhambi ni mauti,
Kifo ni adhabu hivyo huwezi kujipangia Muda wa kupewa adhabu yako Ila hakimu ndo huamua
Na Mungu ndo anamua Muda wa kupata adhabu na huwezi kuchagua iwe kwa namna gani
Akiamua iwe gharika ni maamuzi yake
Akiamua iwe moto ni yeye hakimu
Kwa hiyo ACha kupangia mahakama ya Mungu juu ya Adhabu uliyochagua mwenyewe
Mungu ni mwenye haki lazima akulipe haki yako unayostahili
mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.
Kutoka 34:7
Imani wanaruhusiwa kuamini, ni haki yao ya kikatiba na kibinadamu.Tunalinganisha katika muktadha wa hadithi tu.
Japo tuna mchanganyiko.
Wengine tunachanganua hadithi na characters wake, ila wapo wengine wanatetea imani zao.
Umewahi kusoma philosophy of religion, formally or informally, na kukutana na kitu kinaitwa "the problem of evil" au "Epicurean Paradox" ?Kifo ni matokeo ya Uasi ,unapopanda mbegu lazima uvune haijalishi itachelewa au itawahi
Mshahara wa dhambi ni mauti,
Kifo ni adhabu hivyo huwezi kujipangia Muda wa kupewa adhabu yako Ila hakimu ndo huamua
Na Mungu ndo anamua Muda wa kupata adhabu na huwezi kuchagua iwe kwa namna gani
Akiamua iwe gharika ni maamuzi yake
Akiamua iwe moto ni yeye hakimu
Kwa hiyo ACha kupangia mahakama ya Mungu juu ya Adhabu uliyochagua mwenyewe
Mungu ni mwenye haki lazima akulipe haki yako unayostahili
mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.
Kutoka 34:7
Kifo ni chaguo na matokeo ya Adam na uzao wake wote aliyachagua kwenye bustani ya EdenKama kifo Ni adhabu,
Kwanini watoto wachanga wanafariki?
Wametenda kosa gani mpk wauwawe?
Wamekaidi maagizo gani mpk awaue?
Kama hawana kosa, Basi uyo Mungu wako Ni GAIDI.
Yaani TERRORIST
Wewe ambae huamini hata uwepo wa Mungu Sina haja kukueleweshaUmewahi kusoma philosophy of religion, formally or informally, na kukutana na kitu kinaitwa "the problem of evil" au "Epicurean Paradox" ?
Your totally confused and you will never understand nothingMungu na shetani wote hawapo. Hawa ni wahusika tu katika hadithi ya kutungwa na watu.
Ila, kama tunalinganisha wahusika katika hiyo hadithi, kama tunachambua riwaya, Mungu kaua zaidi.
Hutakiwi kumlinganisha mtu aliyeumba kifo, aliyekiruhusu kiwepo, na mwingine anayeua tu.
Huyo Mungu aliyeumba kifo, aliyekiruhusu kiwepo, siku zote atakuwa ameua zaidi.
Kwa sababu anahusika katika kila kifo, yeye ndiye chanzo cha vifo vyote, asingeruhusu kifo kiwepo, kungekuwa hakuna kifo. Hakuna ambaye angeweza kuua.
Vhagar
Unajua tofauti ya kulalamika na kuomba ???Kwa hiyo waisrael walikosea kulalamika?
Watu wakilalamika tu Mungu anawaua?
Hakimu anapopitisha hukumu ya kifo yule hakimu anakua ni muuji ???Kwa andiko hili unathibitisha kwamba mungu ni muuaji ila tunajaribu kujustify kuwa anawaua watu kwa kutofuata masharti yake?
Unajua Mungu hawezi kufanya lolote duniani bila kumtumia Mwanadamu na shateni hawezi kufanya lolote duniani bila kumtumia Mwanadamu ????Mahali popote penye ushetani ni Mungu karuhusu, hivyo Mungu ndiye muuwaji.
Unaweza kunipa fact za uwepo wako ???Imani wanaruhusiwa kuamini, ni haki yao ya kikatiba na kibinadamu.
Ila, wakianza kuitetea kama ukweli inabidi tuende kwenye uhakiki wa fact.
Unajuaje kwamba wewe ndiye utanielewesha mimi na si mimi ndiye nitakuelewesha wewe?Wewe ambae huamini hata uwepo wa Mungu Sina haja kukuelewesha
Wewe jifunze kuandika Kiingereza kwanza kabla ya kujishaua mengine.Your totally confused and you will never understand nothing