Mungu wa Lissu ni Mungu aliye hai, kumbe wanaotukana Serikali na Viongozi ni Wao wenyewe

Mungu wa Lissu ni Mungu aliye hai, kumbe wanaotukana Serikali na Viongozi ni Wao wenyewe

Bush Dokta

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2023
Posts
24,831
Reaction score
45,154
Kwa miaka mingi kumekuwa na jitihada za kuhadaa umma kwamba watu wanaotukana serikali na viongozi ni Wapinzani.

Ukifatilia kwa umakini utaelewa kuwa wapinzani kazi yao imekuwa ni kukosoa, kushauri, kupendekeza na inapobidi kutekeleza na kutoa majibu ya Changa moto mbali mbali zinazoikabili Nchi yetu.

Lakini baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM na serikali wamekuwa wakitaka kudanganya umma kwamba wapinzani ndio wabaya na wanapinga kila kitu pale wanaposhindwa kujibu hoja zao.

Mh Tundu Lissu amekuwa Target in the list licha ya Mwanasiasa huyu ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa na aliyekuwa Rais wa Tanganyika Law Society kujikita kwenye mambo mtambuka, magumu na mazito yanayohitaji fikra pevu. Wapinzani wake wakimtuhumu kuwa anatukana serikali.

Sasa hatimaye kama waswahili wanavyosema Muda ni Mwalimu, sasa muda umeongea.

Wamegundua kuwa Tundu Lissu si mbabaishaji bali wenyewe kwa wenyewe wanageukana.

Hoja nyingine ni kuwa viongozi badala ya kujikita na kuweka nguvu nyingi kupambana na mambo ambayo sisi wananchi tunayaita UDAKU ni bora kujikita kuwatafuta watu wanaoiba mali na fedha za serikali, wanaopora maliasili za Taifa na kutumia ofisi za umma kwa masalahi binafsi.

Maswala ya upotevu wa fedha nyingi za Taifa ndani ya chama na serikali wameyafumbia macho na hatujajawahi kuona kiongozi yeyote wa juu wa chama au serikali akitishia kuwataja Mafisadi na wanyonyaji hawa.

Sasa leo kuwataja watukanaji wa mitandaoni ina tija gani kwa Wananchi wanaohangaika na changamoto mbali mbali kama kukosekana kwa misingi ya haki na utawala bora, Njaa, kupanda bei za bidhaa, mafuta kuadimika, umeme wa kusuasua na ubovu wa miundombinu ya Barabara na majitaka?

Mungu wa Tundu Lissu ni Mungu aliye hai. Na Mwenye nguvu.
 
CCM hawawezi kuwa wamoja tena, yaani sasa hivi ni mwendo wa kuviziama - kinachosaidia ni dola kuwa within.
Mda si mrefu watauana. Sidhani kama itafka uchaguz mkuu mmoja hajapita hivi. Ogopa sana kuona mawaziri wakitembea na waganga wao kwenye ma V8.
 
Sasa leo kuwataja watukanaji wa mitandaoni ina tija gani kwa Wananchi wanaohangaika na changamoto mbali mbali kama kukosekana kwa misingi ya haki na utawala bora, Njaa, kupanda bei za bidhaa, mafuta kuadimika, umeme wa kusuasua na ubovu wa miundombinu ya Barabara na majitaka?
Muhimu waisome hii machawa na makunguni wa CCM
 
Kwa miaka mingi kumekuwa na jitihada za kuhadaa umma kwamba watu wanaotukana serikali na viongozi ni Wapinzani.

Ukifatilia kwa umakini utaelewa kuwa wapinzani kazi yao imekuwa ni kukosoa, kushauri, kupendekeza na inapobidi kutekeleza na kutoa majibu ya Changa moto mbali mbali zinazoikabili Nchi yetu.

Lakini baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM na serikali wamekuwa wakitaka kudanganya umma kwamba wapinzani ndio wabaya na wanapinga kila kitu pale wanaposhindwa kujibu hoja zao.

Mh Tundu Lissu amekuwa Target in the list licha ya Mwanasiasa huyu ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa na aliyekuwa Rais wa Tanganyika Law Society kujikita kwenye mambo mtambuka, magumu na mazito yanayohitaji fikra pevu. Wapinzani wake wakimtuhumu kuwa anatukana serikali.

Sasa hatimaye kama waswahili wanavyosema Muda ni Mwalimu, sasa muda umeongea.

Wamegundua kuwa Tundu Lissu si mbabaishaji bali wenyewe kwa wenyewe wanageukana.

Hoja nyingine ni kuwa viongozi badala ya kujikita na kuweka nguvu nyingi kupambana na mambo ambayo sisi wananchi tunayaita UDAKU ni bora kujikita kuwatafuta watu wanaoiba mali na fedha za serikali, wanaopora maliasili za Taifa na kutumia ofisi za umma kwa masalahi binafsi.

Maswala ya upotevu wa fedha nyingi za Taifa ndani ya chama na serikali wameyafumbia macho na hatujajawahi kuona kiongozi yeyote wa juu wa chama au serikali akitishia kuwataja Mafisadi na wanyonyaji hawa.

Sasa leo kuwataja watukanaji wa mitandaoni ina tija gani kwa Wananchi wanaohangaika na changamoto mbali mbali kama kukosekana kwa misingi ya haki na utawala bora, Njaa, kupanda bei za bidhaa, mafuta kuadimika, umeme wa kusuasua na ubovu wa miundombinu ya Barabara na majitaka?

Mungu wa Tundu Lissu ni Mungu aliye hai. Na Mwenye nguvu.
huyo kibaraka awe target ya nani acha upotoshaji kamanda 🐒

yaan inafahamika kabisa huyo ni puppet halafu mnababaika nae tena, wanini sasa, khaa🐒

lakini umeendelea kupotosha zaidi,

ati kazi ya upinzani humu nchini imekua ni kukosoa, kushauri, kupendekeza mipango mbadala na kutoa majibu ya changamoto mbalimbali 🤣

ingekua ni hivyo si tungeuipiku Singapore kimaendeleo 🐒

hii ya kulalamikia, kugoma, kuzira, kususa, maandramano, ghadhabu, mihemko na matusi hua ni nani anafanya 🐒

without fear of contradictions, Tz ingekua zaidi Singapore kimaendeleo, kama tu, pangelikuapo na united, vibrant, visionary, committed and focused opposition 🐒

Lakini hii tuliyonayo sidhani kama ni opposition, maybe it is something else 🐒
 
Mwigullu Nchemba anajitia kuvaa skafu ya bendera ya taifa kumbe ndiye analipa wanaomtukana Rais wetu.
 
ati kazi ya upinzani humu nchini imekua ni kukosoa, kushauri, kupendekeza mipango mbadala na kutoa majibu ya changamoto mbalimbali 🤣
Huoni kama ccm inatekeleza Ilani ya Chadema?

Hakuna mpango ambao ccm hawajakopi kutoka Chadema
 
without fear of contradictions, Tz ingekua zaidi Singapore kimaendeleo, kama tu, pangelikuapo na united, vibrant, visionary, committed and focused opposition 🐒
Yaani mali za umma waibe ccm na rushwa watoe wao maendeleo yaletwe na Vibrant opposition??
Shame on you.
 
Back
Top Bottom