Muonekano Mpya wa TAZARA Flyover

Muonekano Mpya wa TAZARA Flyover

Halafu anakuja Mtu Mzima Na akili zake anasema Tangu uhuru Hakuna kulichofanyika

John Magufuli anahitajiwa Sana Tanzania Kuliko kipindi chochote Kile
 
TAZARA FLY OVER katika Muonekano Mpya ikiwa katika hatua za Mwisho kukamilika. ... Huyu Ndiye MAGUFULI anayechukiwa na kikosi cha Wapiga dili, Vibaka na Misheni town, wakwepa Kodi n.k ...

Huyu Ndiye Rais Magufuli aliyepoteza umaarufu kwenye Makaratasi ya Watafiti na Wanasiasa uchwara .... Na hii ndiyo Tanzania Mpya tunayoitaka.

Watapata tabu sana.
Najivunia

View attachment 813205

Dalili za ujinga ni kushabikia vitu vya kijinga!!
 
Halafu anakuja Mtu Mzima Na akili zake anasema Tangu uhuru Hakuna kulichofanyika

John Magufuli anahitajiwa Sana Tanzania Kuliko kipindi chochote Kile
Kwakuwa watu wasioujulikana hawajagusa maisha yako wala ya ndugu zako.

Huko Ethiopia waliokoandama kumtoa dikteta kuna ndege nyinyi tu na miuindombinu mizuri lakini havikupumbaza wananchi.

Acheni ushamba na kuwa wajinga!!
 
Hii ni sawa na mtu ambaye zamani hakuwa na uwezo hata wa kununua suruali. Baadaye akaweza akanunua suruali, anaenda anapiga kelele mtaa mzima kuwa amekuwa tajiri. Anaowapigia kelele, japo zamani walikuwa sawa, sasa wana nyumba za ghorofa.
 
Kwakuwa watu wasioujulikana hawajagusa maisha yako wala ya ndugu zako.

Huko Ethiopia waliokoandama kumtoa dikteta kuna ndege nyinyi tu na miuindombinu mizuri lakini havikupumbaza wananchi.

Acheni ushamba na kuwa wajinga!!

Hata Libya watu waliandamana Sana Baada ya kuchoka Maisha mazuri Na Sasa hawaandamani Tena Kwa Kuwa Shida walizopigania wamezipata

Usikariri kila wakiandamana maana yake wana logic ya wanachopigania
 
Hii ni sawa na mtu ambaye zamani hakuwa na uwezo hata wa kununua suruali. Baadaye akaweza akanunua suruali, anaenda anapiga kelele mtaa mzima kuwa amekuwa tajiri. Anaowapigia kelele, japo zamani walikuwa sawa, sasa wana nyumba za ghorofa.

Kama ulikuwa Na nyumba tatu Za ghorofa Baada ya Miaka miwili unabaki nayo Moja lakin Mwenzio Miaka mitatu ya Nyuma hakuwahi kumiliki Suruali isiyo Na vilaka lakin Baada ya Miaka mitatu anamiliki Suruali mbili Mpya Nani hapo ame advance?
 
Overpass - Wikipedia

[emoji115][emoji115][emoji115][emoji115]
Hebu tumalize utata kidogo, ukisoma hapo utaelewa hiyo ya Tazara ni flyover au siyo. Overpass au Flyover kama inavyojulikana na waingereza. article yake hiyo hapo
 
Umeongea kwa kufanya utafiti au chuki dhidi ya Serikali ya mheshimiwa JPM? Maana ungejua advantage za kujenga fly over usingukuja na blah blah.

Kwa kukusaidia tafuta hotuba ya Waziri kivuli wa mawasiliano na uchukuzi(MBATIA) kwa upande upinzani ya mwaka wa fedha 2016/2017 anaongelea umuhimu wa barabara za juu(fly over) tena ilikuwa inashauri serikali kwa ijenge barabara za juu ili ujue ina multi impact gani kwa maendeleo ya kiuchumi kama nchi na wananchi kiujumla.
Huko Ulaya na kwingineko wana miundombinu mizuri lakini kila siku waanandamana kudai ajira, nyongeza za mishahara,kupanda kwa gharama za maisha, n.k


Watu wanapunguzwa makazini, vijana wanamaliza vyuo hawana ajira, watumishi wanasahaulika, wavuvi wanalia, wakulima wanalia, n.k nyie mnaendekeza ushamba tu.

Endeleeni kupuuza maendeleo ya watu mtakuja kuona matokeo yake maana mnafikiri Tanzania ni kisiwa.
 
"Ubwege unaanziaga palee,wanapobishana kuhusu nguo,wakati wamezaliwa uchi"
 
TAZARA FLY OVER katika Muonekano Mpya ikiwa katika hatua za Mwisho kukamilika. ... Huyu Ndiye MAGUFULI anayechukiwa na kikosi cha Wapiga dili, Vibaka na Misheni town, wakwepa Kodi n.k ...

Huyu Ndiye Rais Magufuli aliyepoteza umaarufu kwenye Makaratasi ya Watafiti na Wanasiasa uchwara .... Na hii ndiyo Tanzania Mpya tunayoitaka.

Watapata tabu sana.
Najivunia

View attachment 813205
Kama sikosei mradi huu ulianzishwa na kipindi cha awamu ya nne.........wamu ya tano wamemalizia mradi wenyewe....pongezi ziende kwao wote.
 
Huko Ulaya na kwingineko wana miundombinu mizuri lakini kila siku waanandamana kudai ajira, nyongeza za mishahara,kupanda kwa gharama za maisha, n.k


Watu wanapunguzwa makazini, vijana wanamaliza vyuo hawana ajira, watumishi wanasahaulika, wavuvi wanalia, wakulima wanalia, n.k nyie mnaendekeza ushamba tu.

Endeleeni kupuuza maendeleo ya watu mtakuja kuona matokeo yake maana mnafikiri Tanzania ni kisiwa.
Mkuu kumbe unajua hata Ulaya kuna changamoto, kwani Tanzania nani isiwe na changamoto?



Sent from my SM-G610F using JamiiForums mobile app
 
Hata Libya watu waliandamana Sana Baada ya kuchoka Maisha mazuri Na Sasa hawaandamani Tena Kwa Kuwa Shida walizopigania wamezipata

Usikariri kila wakiandamana maana yake wana logic ya wanachopigania
Waliandamana kwasababu waliochoka udikteta wake na kufanya nchi mali yake.
 
Sasa naanza kuwaelewa hawa wapiga makofi hata jiwe akicheka tu wao watavunjika mbavu na kupiga makofi hadi mikono ikatike, hili ni daraja tu lakuvusha magari kama mtoni mtongani, ruvu isipokua treni ndio linapita Juu, ndio maana kumbe huyu hero wenu anatembea na kamera za tbc kila aendapo na kila uchao hata akiwa na shughuli ya kawaida kabisa anapelekewa ripoti kurugenzi ya mawasiliano inatangaza wiki kabla eti tusitoke kwenye tv zetu tuwetayari kwenye mitandao nk HAKUNA kitu special kwa Kikwete kuomba msaada kwa Japan ili kujenga hiyo flyover kitakacho mfanya jiwe ajione yeye ndio mungu, hakuna tofauti yoyote na Mzee Mwinyi alieomba msaada Japan hizi barabara za Dar city centre ziwekwe lami na Konoike corp, au Salender bride lijengwe na Kajima, na hakuna sifa yoyote kwa jiwe, kwa Kikwete alivyo omba world bank mkopo akakubaliwa ili ajenge ile ubungo exchange hata Nyerere aliomba mkopo world bank akajenga Mtera Hydro Power System ni ushamba tu unawazuzua ninyi na hiyo jiwe wenu, mnatufanya sie wengine kuona aibu kwenye jumuia ya kimataifa anapopita paka mashangilia tembo! siku mtakayo muona mbwa hakika balaa lake mpaka kuzimu watasikia!
 
Tatizo la sie watanzania ni kelele ...Mradi wa wastani watu hao si CCM si vyama vingine wanapaza sauti Mi nategemea tubadilike fikra zetu tuwe tunapima vitu kwa TIJA,Tumenunua vindege na Ndege Moja(Boeing) kelele kibao..Kwa nini tunapenda sifa kuliko uhalisia.Miradi inatakiwa kusifiwa ikileta Tija bila hivyo naona ni sawa na kujihangaisha, pia Serikali inapaswa kuyafanyia kazi maoni ya vyama vingine (serikali sio ya CCM tu bali Watanzania)kwa kuwekeza zaidi kwenye miradi na kuhakikisha Tija inakuwepo.Kwa kiasi chake Daraja hili la juu litasaidia sio swala la kubeza..Tuache kelele kwenye hili daraja labda kama litakuwa halina uimara mje na hoja
 
na wewe mpe tuzo ya fly over ili moyo wako utulie! Watu hatuna hela we unaleta mambo ya fly over, yaani ni kama watoto wa kota wanapoenda uswahilini na stori za isidingo! Leta uchumi mefukoni shubamitii..!
Chakarika kijana, hutokosa doo, baki hapo ukilia lia
 
Back
Top Bottom