Muosha Magari apatisha ajali gari lenye thamani zaidi ya Milioni 100. Akutwa anaruka sarakasi

Muosha Magari apatisha ajali gari lenye thamani zaidi ya Milioni 100. Akutwa anaruka sarakasi

huyo jamaa anapata kichaa cha nini wakati gari ina comprehensive insurance
hio comprehensive insurance wabongo wachache wanayo wngi wanatumia tu hizi third party za laki 1, huwa zinahusisha tu watu au mali za watu utaowasababishia madhara mfano kugonga mtu au wanyama au gari,

Ila ikitokea ana comprehensive income, bado sughuli ni pevu maana kuna mibadala mitatu tofauti na watu wanavyodhani .

1. kufanyiwa marekebisho, watapeleka gari likanyoshwe kwenye gereji wanazozijua wao, kwa hii ford wanaweza kuipeleka kenya ikarudi ipo fresh.

2. kununuliwa gari kama iliyopata ajali, hapa wanaweza kukununulia gari huko be forward, tena kwa mile age na uchakavu unaoendana na gari kabla halijapata ajali.

3. kupewa cash uwende kununua gari mwenyewe, hapa huwainatokea kama wamekosa fundi wa kurekebisha au wamekosa gari za mtumba huko be forward 😂

Hapo watakomaa kuipeleka gereji ikanyooshwe tu, hawana pesa za mchezo kukununulia nyingine ama kukupa cash, Bongo Nyoso!!
 
huyo jamaa anapata kichaa cha nini wakati gari ina comprehensive insurance
Bima hii imekwisha siku 228 zilizopita

Acha dogo aendelee kujidai chizi ila ingekua gari yangu akili ingemkaa sawa ndan ya dakika 15
20210803_123410.jpg
 
ila hizo sarakasiii hahaaaa

..ukute gari mkopo haujamaliziwa kulipwa...

nimejifunza, nkienda maeneo ya kuoshea gari, namkabidhi funguo bosi, yeye ndo awape vijana wake ufunguo
mkuu gari ni lawama usije muazima mtu mi juzi kati nimemuazima gari mtu kailudisha usiku kimya kimya kumbe kakwanyua side mirror yote imetoka kaniachia msala
 
Hahahhaha mambo mengine yanachekesha ila ni mahatma

Embu tupe stori
Ngoja niwape story yangu, Mimi niliazima tayota ist kwa rafiki yangu ili niwahi safari nioliokuwa naiendea, baada kupewa Gari Safi kabisa bado mpya Ina week mbili nikanyoosha goti vizuri safari yangu nikaenda maana ilikuwa mkoa Hadi mkoa mwingine.

Wakati narudi kutoka safari yangu nikiwa njiani nipo kwa road la vumbi na speed ya 70 hivi ghafla Ng'ombe mbele yangu anakatiza Barabara nilitupia mgu kwa brake Gari ikakubali lakini ikaenda pembeni kidogo, bwana we sijui ibilisi gani kanijaa nikajikuta nimetupia mguu kwenye Moto tena la haula Gari iliruka na kuzunguka Kama Mara 4 hivi ikatulia ndugu yangu natoka pale Sina hili Wala lile nikaangalia huku na kule hakuna mtu kucheki Gari ya mtu imeisha yaani.

Nilichomoka mbio hizo alafu sijui naenda wapi na Sina mpangilio wowote kichwani nakuja kusimama najishangaa kwanza Sasa naenda wapi alafu nimeacha kila kitu kwenye gari na documents muhimu ambazo hatakiwi mtu kuziona looh nikarudi Tena speed nikafika nikakunja doc zangu kwanza nikavua vyatu nikaanza kutembea peku nilikuwa nimefunga tai aisee


Itaendeleaa.............😢😢😢😢😢
 
Lakini kwa nini unanunua gari la gharama kubwa halafu hutaki kuliwekea bima comprehensive, hata kama kwa bei nusu yake?

Mimi mwenyewe nilikuwa na harrier aerotourer enzi zileee, mwaka mmoja nikaamua kuweka third party na ndiyo nilipata accident zilinitoka kama milioni 3 kutengeneza.

Kuanzia hapo mimi na comprehensive hata kama ni IST.
 
Back
Top Bottom