Musiba ni Mufilisi kisheria hivyo hapaswi kudaiwa

Musiba ni Mufilisi kisheria hivyo hapaswi kudaiwa

Kampuni zote za Musiba zilishafilisika hata mishahara hawezi kulipa, na anadaiwa na watumishi wake kitambo.

Hivyo hizi amri za kulipa aliowac hafua pesa hazitekelezeki sababu kampuni zake lilishaishiwa pesa.

My take; Tusikenue meno tukadhania amepatikana kumbe hakuna chochote atakachopoteza.
Labda nikusaidie kitu kwa manufaa ya uliowamislead. In short, Mufilisi ni mtu au kampuni inayosimamia ufilisi wa kampuni nyingine kusimamia Mali na madeni kabla kampuni iliyofilisiwa haijafungwa rasmi.

Kuna aina mbili ya ufilisi moja ni wakurugenzi au directors wanafanya maamuzi (board resolution) kwa hiari (voluntary liquidation) au kwa njia ya wadai kupitia Mahakama kulazimisha kuifunga kampuni ili madeni yao walipwe ( involuntary/Court liquidation).

Hivyo basi, anayeweza kutamka kwamba kampuni fulani imefilisika ni Mahakama pekee.

Pia sio kila mtu anaweza kuwa Mufilisi, sheria ya makampuni imewataja watu wawili, either awe Wakili au Auditor na watateuliwa na Mahakama hata kama ni involuntary liquidation lazima upeleke jina la mtu mnayependekeza awe liquidator au kama ni involuntary basi walioomba hiyo liquidation watapewa kulingana na mtu aliyependekezwa na kama Mahakama itaridhika nae.

Sasa ukisema Musiba ni mifilisi naona umejichanganya lakini kama ulimaanisha amekuwa bankrupt, hiyo haina tatizo Ila ni mpaka wanaomdai wakiamua kuomba Mahakama itoe amri ya kumfilisi ili alipe hayo madeni yake na sio lazima alipe yote Ila ukiacha madeni ya kisheria ambayo kwanza ni Kodi then anajilipa Mufilisi halafu wengine ndio wanaendelea. Hapo akina Membe wakiwahi kimfilisi ndio watakuwa wamecheza bingo.

However, kama amefilisika, bado wanaweza kuamua kupeleka maombi Mahakamani kutaka musiba afungwe hela kama Civil Prisoner na hii watu wengi huwa hawajui kwamba deni linaweza kukufunga miezi sita sita mpaka utakapolipa Ila anayekuweka ndani anapaswa kukuhudumia tu. Hii situation ilimkuta Marehemu mchungaji Mtikila alikuwa anadaiwa milioni nane akawa anasumbua kulipa mdai akapeleka kesi Mtikila awekwe jela as a civil prisoner, alipoona hivyo ikabidi alipe tu maana alikuwa anataka kuleta janja janja.

So, kwa Musiba the saga is not over, wanaweza kuamua kumkomesha tu kama walitaka, naona awahi aombe radhi atafute watu wazima awalilie shida wamtafute mzee Membe na Fatma wayamalize.

Sponsor huwa anakufa jamani.
 
Mahakama ikimpa nafas ya kujitetea basi anaweza kusema naomba nihurumiwe maana kitu pekee nilicho baki nacho ni chupi tu
 
Kampuni zote za Musiba zilishafilisika hata mishahara hawezi kulipa, na anadaiwa na watumishi wake kitambo.

Hivyo hizi amri za kulipa aliowac hafua pesa hazitekelezeki sababu kampuni zake lilishaishiwa pesa.

My take; Tusikenue meno tukadhania amepatikana kumbe hakuna chochote atakachopoteza.
Hana uwezo wa kulipa ila ana uwezo wa kufungwa
 
Jifunze kuandika halafu ukajifunze sheria. Huyo jaji aliyetoa hiyo hukumu ni mwehu?
Jaji kazi yake ni kutoa hukumu. Namna ya kuitekelza hiyo hukumu ni kazi ya watu wengini. Kama mtu amefilisika (hana kitu) huwezi kupata chochote.

Kwa vile hiyo ni civil case, Musiba hawezi kwenda jela. Ndiyo maana wakati mwingine kabla hujatumia pesa nyingi kwenye kesi ya madai, angalia kama kuna uwezekano wa ku"collect".

Otherwise, utawalipa mawakili na hutapata chochote toka mdai, kwa sababu hana kitu.
 
Kampuni zote za Musiba zilishafilisika hata mishahara hawezi kulipa, na anadaiwa na watumishi wake kitambo.

Hivyo hizi amri za kulipa aliowac hafua pesa hazitekelezeki sababu kampuni zake lilishaishiwa pesa.

My take; Tusikenue meno tukadhania amepatikana kumbe hakuna chochote atakachopoteza.
Tutamfunga miezi sita sita mpaka atapoweza kulipa akishindwa tunakazia hapohapo ..akitoka tunafunga tena miezi sita ,akitoka tumafunga tena miezi sita mpaka aseme aliyekuwa ana MPA kiburi anacheo gani mbinguni au kama yupo akhera atutahadharishe mapema tuokoke. Maana bora kumkuta shetani kule kuliko huyu aliyetutoka.

Screenshot_20211029-035234.png
 
Hata asipolipa Ila wote waliomsujudia magufuli Sasa wanapata somo la ASIEFUNZWA NA MAMA YAKE; UBAYA WA KUMTEGEMEA SPONSA NK HAWA WATU SABAYA MSIBA POLEPOLE BASHIRU WAMEFANYIKA SOMO KWA JAMII YA WATANZANIA KWAMBA UKIPATA DHAMANA KUWA MNYENYEKEVU.
 
Jaji kazi yake ni kutoa hukumu. Namna ya kuitekelza hiyo hukumu ni kazi ya watu wengini. Kama mtu amefilisika (hana kitu) huwezi kupata chochote.

Kwa vile hiyo ni civil case, Musiba hawezi kwenda jela. Ndiyo maana wakati mwingine kabla hujatumia pesa nyingi kwenye kesi ya madai, angalia kama kuna uwezekano wa ku"collect".

Otherwise, utawalipa mawakili na hutapata chochote toka mdai, kwa sababu hana kitu.
Ficha ujinga basi sheria ya wapi hiyo
 
Kampuni zote za Musiba zilishafilisika hata mishahara hawezi kulipa, na anadaiwa na watumishi wake kitambo.

Hivyo hizi amri za kulipa aliowac hafua pesa hazitekelezeki sababu kampuni zake lilishaishiwa pesa.

My take; Tusikenue meno tukadhania amepatikana kumbe hakuna chochote atakachopoteza.
Anadaiwa Musiba siyo kampuni zake, Musiba naye ni muajiriwa wa hizo kampuni kwani naye analipwa mshahara. Waliofungua kesi walimshitaki Musiba na hawakuhusisha mashitaka kwenye magazeti isipokuwa ushahidi upo kwenye magazeti, Musiba anazo mali binafsi na ana mke na watoto.
 
Kampuni zote za Musiba zilishafilisika hata mishahara hawezi kulipa, na anadaiwa na watumishi wake kitambo.

Hivyo hizi amri za kulipa aliowac hafua pesa hazitekelezeki sababu kampuni zake lilishaishiwa pesa.

My take; Tusikenue meno tukadhania amepatikana kumbe hakuna chochote atakachopoteza.
unajua sheria ya kufirisika? au kushindwa tu kulipa mishahara ndio kufirisika?
 
Back
Top Bottom