Uchaguzi 2020 Musoma yarindima Lissu akilakiwa kwa Shangwe kubwa, fomu za dhamana zajazwa

Uchaguzi 2020 Musoma yarindima Lissu akilakiwa kwa Shangwe kubwa, fomu za dhamana zajazwa

ANAESTHESIOLOGIST

Senior Member
Joined
Dec 29, 2019
Posts
158
Reaction score
266
Hali ya hewa siyo rafiki Musoma Mjini Kuna mvua inanyesha tangu saa moja asubuhi. Huwezi amini watu wamefika na mvua hiyo, na Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hajafika, bado yuko Mwanza.


IMG-20200812-WA0007.jpg
IMG-20200812-WA0005.jpg

Haijapata kutokea!

Mgombea Urais kupitia Chadema Tundu Lissu ameingia Musoma kwa Shangwe kubwa huku mji ukiwa umesimama kupisha ujio wake.

Lissu ambaye Yuko katika ziara ya kusaka wadhamini ameingia mjini Musoma kwa kishindo kikubwa.

Akiwasalimu maelfu kwa maaelfu waliojitokeza kumlaki Lissu ameendelea kumwaga sera kadhaa mojawapo inayovutia wananchi Ni ile ya kutoa Uhuru wa watu kuzungumza, vyama kufanya shughuli za kisiasa na vyombo vya Habari kuwa huru.Pia kufanyia marekebisho makubwa Idara ya Habari Maelezo, TCRA na TRA.

Wachambuzi wa kisiasa hapa Musoma wamesema haijawahi kutokea mwanasiasa akalakiwa na umati mkubwa hivyo katika mji huo tangia nchi ipate Uhuru

Lissu ameueleza umati huo kuwa kwa Sasa anatafuta tu wadhamini na kipindi Cha kampeni ndiyo ataeleza rasmi mustakabali wa nchi yetu .

#Niyeye2020
1597239499152.png
1597239510347.png

 
Mbona kama sijaelewa unataka kusema nini? kama unaweza dadavua zaidi na zaidi
 
Hali ya hewa siyo rafiki Musoma Mjini Kuna mvua inanyesha tangu saa moja asubuhi.Huwezi amini watu wamefika na mvua hiyo,na Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hajafika bado yuko Mwanza
Yani kama CHADEMA haikuchukua nchi wakati wa Lowassa sidhani kama itaweza mara hii kwa maana Lowassa alikuwa na nyomi la kufa mtu, Serikali ndiyo ile ile, NEC ndiyo ile ile, Polisi ndiyo wale wale
 
Katika kosa la kimataifa litakalo fanywa na viongozi wa ngazi za juu wa ccm ni kutumia kigezo Cha walioshinda Kura za maoni za madiwani na ubunge kupitishwa kupeperusha bendera ya CCM mwaka 2020.Walioshika nafasi zote za juu Kura za maoni ni kundi lililokubalika kwa wajumbe wachache ndani ya CCM kupitia kutoa rushwa na kushinda kura za maoni ,wakipitishwa kugombea na upinzani litakuwa kosa la kihistoria katika uchaguzi mkuu ujao ndani ya CCM.
 
Katika kosa la kimataifa litakalo fanywa na viongozi wa ngazi za juu wa ccm ni kutumia kigezo Cha walioshinda Kura za maoni za madiwani na ubunge kupitishwa kupeperusha bendera ya CCM mwaka 2020.Walioshika nafasi zote za juu Kura za maoni ni kundi lililokubalika kwa wajumbe wachache ndani ya CCM kupitia kutoa rushwa na kushinda kura za maoni ,wakipitishwa kugombea na upinzani litakuwa kosa la kihistoria katika uchaguzi mkuu ujao ndani ya CCM.
Hali ya hewa siyo rafiki Musoma Mjini Kuna mvua inanyesha tangu saa moja asubuhi.Huwezi amini watu wamefika na mvua hiyo,na Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hajafika bado yuko Mwanza
 
Yani kama CHADEMA haikuchukua nchi wakati wa Lowassa sidhani kama itaweza mara hii kwa maana Lowassa alikuwa na nyomi la kufa mtu, Serikali ndiyo ile ile, NEC ndiyo ile ile, Polisi ndiyo wale wale
Yule mzee alishinda kura ila zilikuwa zinabadilishwa tu za kwake anapewa Magufuli za Magufuli anapewa Lowasa.

Jimbo la Tunduma Lowassa alipata kura 32 ila zilitangazwa Elfu 6 tu mpaka alipolalamika ndiyo yakafanyika marekebisho.

Imagine jimbo la Bumbuli za urais zilikuwa inabidi idadi ya wapiga kura wote. Kumbu kumbu zangu January Makamba alipata kura 28 Elfu halafu Magufuli akapewa 42elfu.

Mikoa ya kusini Lowassa alimpita Magufuli kwa kura nyingi sana ila zilizotangazwa walikuwa toe to toe.
 
Yule mzee alishinda kura ila zilikuwa zinabadilishwa tu za kwake anapewa Magufuli za Magufuli anapewa Lowasa.

Jimbo la Tunduma Lowassa alipata kura 32 ila zilitangazwa Elfu 6 tu mpaka alipolalamika ndiyo yakafanyika marekebisho.

Imagine jimbo la Bumbuli za urais zilikuwa inabidi idadi ya wapiga kura wote. Kumbu kumbu zangu January Makamba alipata kura 28 Elfu halafu Magufuli akapewa 42elfu.

Mikoa ya kusini Lowassa alimpita Magufuli kwa kura nyingi sana ila zilizotangazwa walikuwa toe to toe.
NEC ni wale wale, Polisi ni ile ile, CCM ni wale wale na huenda now wamekaza zaidi, Nyomi la Lissu sina hakika kama linashinda la lowassa. Ndiyo maana nikasema kama Lowassa hakutangazwa mshindi sidhani kama CHADEMA itashindwa kiti cha uraisi mwaka huu. Nothing has changed.
 
Yani kama CHADEMA haikuchukua nchi wakati wa Lowassa sidhani kama itaweza mara hii kwa maana Lowassa alikuwa na nyomi la kufa mtu, Serikali ndiyo ile ile, NEC ndiyo ile ile, Polisi ndiyo wale wale
Sisi tuna njaa. Hakuna wa kutuzuia. Likianzishwa tu, mtajua bora kifo cha gaddaf kuliko kitakacho mkuta mtu
 
Back
Top Bottom