Muswada wa Marekebisho Sheria-2020: Unajua watu hawataweza kudai haki kwa niaba ya Wanyonge? Viongozi wa juu Serikalini hawatashtakiwa moja kwa moja!

 
Naomba kujuzwa hapa sijapaelewa kabisa au sijui kichwa changu cha panzi au la,mwenye uelewa wa suala hili atujuze
 
sijaelewa kutoka chini ya sakafu ya moyo wangu juu ya jambo hili kwa nini haya yapo zaidi katika awamu hii ya 5
 
Mange kimambi aliyasema haya tukamdharau na sasa hivi amekaa kimya mpambane wenyewe
 
Kwa kifupi sheria inahamasisha ufisadi,sheria ya kinga ilikuwa inamfaa Baba wa Taifa tu
 
Yaani inashangaza majitu ya ccm inapiga makofi
 
Malaika muungwana asiyekuwa na mipango ya kufanya matendo ya kishetani hahitaji kinga ili abakie mbinguni.

Mbinguni ndiyo makao yao waungwana isipokuwa njia pekee ya kubakia mbinguni baada ya kutenda matendo ya kiibilisi Ni kuibadili katiba ya mbinguni.

Jpm akijipa Kinga ya kisheria ya kutoshitakiwa atakuwa amefanya kosa la kuigharimu taifa kwa sababu atakuwa amejiweka juu ya sheria. Tanzania inahitaji mtu msafi asiyeogopa sheria kwa sababu hofu ya sheria Ni evidence ya uchafu wa matendo.

Hata Kama ana mazuri elfu moja lakini kitendo Cha kujiwekea Kinga ya kisheria kinaonyesha yale mazuri Yana harufu ya unafiki na ghilba ndani yake isipokuwa tumefichwa ukweli na tunapigwa propaganda ili tusielewe uhalifu unaoendelea.
 
Mbona kuweka kinga?..unaogopa nini iwapo unafuata haki,taratibu na sheria?.

Sijui wengine mnanonaje ila mhh this looks like a Red Flag!
 
Hiyo ni moja ya dalili kuwa watawala hawataki kutoka madarakani na wanapanga kufanya maovu zaidi na hasa wakati huu wa uchaguzi mkuu. Wajuzi wa mambo tupenì mwongozo tufanye nini ili tudai katiba mpya kabla ya uchaguzi wa October?

Je tunaweza kusaini fomu maalum na kwamba tukifika idadi kadhaa basi lazima serikali ifanye mchakato wa katiba mpya kabla ya uchaguzi?
 
Hapa ndio pale tunasema hii nchi imeshakuwa ya Kidikteta. Halafu inasema inatetea Wanyonge
Inasikitisha kwamba toka 1985 wakati Rais wa kwanza amestaafu hadi hivi leo, hatuna rekodi inayo onyesha, Spika, Naibu,Jaji mkuu,Waziri mkuu ,makamu wa Rais na Rais wote walio staafu kama waliwahi au mmojawao aliwahi shitakiwa kwa makosa aliyotenda akiwa madarakani.

Sasa kama hiyo haijawahi kutokea ,hawa wakubwa zetu wa sasa, wamefanya nini/wanatarajia kufanya nini ambacho wana shaka nacho kwamba kinaweza kuwafikisha mahakamani wakisha staafu nyadhifa zao?

Hivi tulipo nanga inapaa, serikali kaa la moto,mahakamani hakueleweki,bungeni watu wanaingia bila hata udhamini wa vyama! Wakijiwekea uzio hii nchi tutaendeshwa kwa kasi gani?
 
Mabadiliko haya yakipitishwa yatazuia raia wengine kufungua mashtaka kwa maslahi ya umma wanapohisi kuna uvunjifu wa Katiba.

Hutaruhisiwa kumtetea raia mwenzako hata kama hana uwezo wa kujitetea, hutaruhusiwa kutetea nchi yako kupitia mahakama isipokuwa pale tu unapokuwa umenyanyaswa moja kwa moja, na hutaweza kutoa mchango wako kuilinda KatibaYetu. Hii inaondoa uzalendo.

Kutoruhusu mtu au taasisi kufungua mashtaka bila kuathirika moja kwa moja inakulazimisha kujitegemea na kujitetea unapokutwa na unyimwaji wa haki zako unaohitaji mahakama kuingilia.

Mabadiliko haya yatawaathiri sana wasiokuwa na uwezo na ujasiri wa kujisimamia wenyewe kisheria kama vile walemavu, watoto, wajane na makundi mengine mengi ya kijamii ambayo yamekuwa yakisaidiwa na watetezi wa haki za binadamu kwa maslahi ya umma.
 
Hii itasaidia kupunguza wateja kulizwa pesa ndefu na mawakili
 
Sheria za namna hii ni kwa faida ya nani? kwa karne hii ningesikia kua wenye nia ya kufungua kesi kwa faida ya Umma wangepewa usaidizi wa kisheria na serikali.
 
Hii nchi Ina watawala wa ajabu sana ,naona watatawala milele ,Mungu atupe uzime tuje tuwaone wanavyopandishwa the hague na vilevile Mungu asiwaue mapema mpaka wapande ndege kwenda the hague.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…