Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba: Download na pitia uone kilichomo na usambaze

Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba: Download na pitia uone kilichomo na usambaze

Tittle za thread zenu ni bora zingeendana na hicho unacho kitoa.
mna creat confussion.
 
Tanzania ni nchi huru na ina mahitaji yake kulingana na wakati tulionao,wananchi wake wana mtazamo na fikra endelevu hivyo hawahitaji kukopi chochote kutoka kwa wengine,kama Kenya wameendelea ni kwa sababu ya kufanya mambo ambayo wanadhani kwao ni ya faida kwa wakati waliopo,tukikopi inamaanisha ndio tutaendelea kuwa nyuma maana hakuna jipya ambalo tutakuwa nalo katika kuamua maendeleo yetu.
Katiba yetu itokane na mawazo na fikra zetu,kwa mazingira yetu na mahitaji yetu na si utashi wa watu wengine wala kuangalia wengine wanafanya nini.
 
:bored:

Chijana hii ni JF na sio global publishers...heading za ku-attract attention na haziendani na topic ni upuuzi, yes i mean so
 
Kama kweli tunataka kuwa na katiba mpya ambayo itaweza kulinufaisha Taifa letu na kuwa na Tanzania ambayo itakuwa njema kwa kila mmoja wetu ingefaa tukaiga wenzetu hawa hebu soma uone na ndio maana wanaendelea Kuliko sisi .

tafadhali chukua muda kidogo soma utanufaika na mengi na hata ukitaka kutoa maoni unaweza kupata mambo ya kuongezea.
kama kuna kitu cha kujifunza kutoka Kenya ni kutambua hatua walizopitia hadi kufikia hayo mafanikio..

Ifahamike tu kwamba Kenya hawakuipata katiba mpya wakati Moi na KANU wapo madarakani na ilikuwa mshike mshike na usanii mkubwa hadi Wakenya wenyewe walipojipanga na vyama vya Upinzani na kuwapa kura za ushindi kuiondoa KANU madarakani ndipo mwanga kamili ulipoanza kujitokeza..

Kwa hiyo tambueni katiba mpya haiwezi kupatikana chini ya CCM kwa sababu katiba mnayoitaka ni kitanzi cha chama.. CCM hawapo tayari kujinyonga wala kumkabidhi mtu panga...

Hivyo ondoeni kabisa fikra za kudhania ama kuamini kwamba CCM na JK watakubali katiba mpya kirahisi pasipo kupigana hadi dakika ya mwisho..

Ni maamuzi yenu wananchi kuchagua aidha kukubali ya JK au chukueni jukumu hilo wenyewe kwa kuwapa kura na support zenu vyama vya Upinzani na hasa Chadema..

Bado naamini kwamba vyama vya Upinzani haviwezi kumshinda CCM pasipo kushirikiana kwa sababu nguvu yao itaunganisha wananchi wengi dhidi ya chama tawala.. Laa sivyo CCM itaendelea kutumia fursa mnayowapa ya kuwagombanisha wananchi kupitia vyama na kuvunja nguvu ya umoja wa wananchi..
 
Kikwete siyo tatizo, Makamba siyo Tatizo, Pinda siyo Tatizo, Werema siyo tatizo, Kombani siyo tatizo, wengi siyo tatizo!!:
TATIZO NI MFUMO WALIORITHI KUTOKA KWA WAKOLONI. TATIZO NI NYERERE ALIYEAMUA KUKUBALI KURITHI KATIBA YA MKOLONI KISHA KUBAKI AKITUMIA BUSARA ZAKE BADALA YA SHERIA MAMA. NYERERE ALIAMINI MA-RAIS WOTE WATAKAOMRITHI WATAMUDU KUTUMIA BUSARA ZAO KUONGOZA TAIFA PASIPO KUWA NA KATIBA IMARA. Matokeo yake warithi wake wote wametumia hiyo katiba kujenga usultani.
Misingi ya katiba ya Mkoloni ilikuwa ni kutugawa na kututawala. baada ya uhuru tuliweka misingi ya kuungana lakini tukashindwa kuweka misingi hiyo kwenye katiba yaani mkuu wetu akaongelea kuungana ilhali sheria mama ina misingi ya kutugawa!!!
THEREFORE: in order to get the best constitution originated from our desire for unity, we need a Leader with desire to make history not a Leader desired by history!! CCM is a Leader desired by History!!
 
Nimejitahidi kuyatafsiri hayo uliyoyanukuu kwa kiingereza, pengine yatatusaidia kufahamu zaidi kwa lugha yetu ya Taifa ya kiswahili. Nairudia ya Kiingereza na Tafsiri yake ipo chini hapo ni kama ifuatavyo:
“(2) In the implementation of subsection (1), the Commission shall adhere to national values and ethos and shall, in that respect, observe inviolability and sanctity of the following matters:
“(2) Katika utekelezaji wa kifungu kidogo cha kwanza (1), Tume itakuwa ikizingatia imani, maadili na itikadi ya taifa, na kwa matilaba hayo, itahakikisha inaheshimu kutokuwepo utenguaji na utakatifu wa mambo yafuatayo:
(a) the Union of Tanganyika and Zanzibar;
(a) Muungano wa Tanganyika na Zanzibar;
(b) the existence of the Executive, Legislature and the Judicature;
(b) kuwepo wa Serikali, Bunge na Mahkama;
(c) the Presidency;
(c) Urais (inakusudiwa Raisi na madaraka ya Uraisi)
(d) the existence of the Revolutionary Government of Zanzibar;
(d) kuwepo kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar;
(e) national unity cohesion and peace;
(e) mshikamano wa umoja wa kitaifa na amani;
(f) periodic democratic election based on universal suffrage:
(f) uchaguzi wa kidemokrasia kwa kuzingatia dhima ya Haki ya lazima ya upigaji kura kwa mwanadamu:
(g) the promotion and protection of human rights;
(g) ya kuendeleza na kulinda haki za binadamu;
(h) human dignity, equality before the law and due process of law;
(h) utu, usawa mbele ya sheria na taratibu zote za haki za Kisheria;
(i) the secular nature of the United Republic; and
(i) kutofungamana na udini kwa Jamhuri ya Muungano, na
(j) the independence of the Judiciary.”
(j) uhuru wa Mahakama. ”
Suala kubwa hapa kutojadiliwa na kutenguliwa muungano wenyewe kama kifungu (a) kinavyotaka kwahiyo majadiliano hayo ya katiba yatatufikisha wapiiiii? Jee katika mjadala wa katiba tukagundua muungano hautufai, si watatubana hawa kwa hadidu rejea za makubaliano juu ya mjadala wa katiba utavyoendeshwaa? Kwahiyo ni sawa sawa kwa WaZanzibari kukaa na msimamo wa kukataa kujadili muungano kwa masharti kama haya.
Ati muungano usijadiliwe hadi kutenguliwa kwa utakatifu wake. Hivi muungano huu wa kijizi jizi una utakatifu gani? Labda kwa Tanganyika lakini sio kwa Wazanzibari.amahani hapa wasomaji kwa jazba. Inaudhi sana mara nyengine kusoma maandiko yao hawa wataalamu wa Janjanyika. Labda wawaeleze wadanganyika tu.
Au kifungu (c) kinachosema Uraisi hivi Uraisi na hasa huu wa Kitanzania una ukamilifu gani na utakatifu gani hata uwe usiguswe katika kujadiliwa katiba?
Kifungu (d) kuwepo kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Jee tukiamuwa sio “Serikali ya Mapinduzi” tena badala yake ni “Serikali ya Zanzibar” tu, na hilo iwe tumeliamuwa sisi wenyewe WaZanzibari wenyewe tutakuwa hatuna haki? Pengo la fikra hilo katika utungaji wao.
Kwa vifungu e,f,g, h, na i utaona wameyaandika maelezo vizuri sana. Lakini uzowefu wetu wa miaka 47 unatuonesha hakuna hata moja katika haya wanaloliheshimu sawa sawa kama inavyotakikana hasa kwa upande wa Zanzibar. Sasa sijui utukufu wake upi huo tuulinde katika kuijadili Tanzania na mambo hayo. Chaguzi sio za kidemokrasia na za uwazi kama inavyotakiwa ni wizi wa kura tu na vurugu. Amani na utulivu na umoja ndio unazidi kuyoyoma kila siku zikienda. Huko Tanganyika ndio hawatambuani na udini. Sisi Zanzibar wamejitahidi kutuletea fitna za umajimbo, tushukuru Mungu tumeamka sasa. Ni wao Tanganyika ndio wakipalilia tafauti za Wazanzibari. Sasa sijui wana utukufu gani katika hili la kuwa waheshimike.
Tanzania hakuna utu kwa kiwango cha kusifiwa duniani. Ujambazi uliotopea na Polisi ndio washiriki wakubwa, Mazeruzeru wanauliwa ovyo ovyo n.k n.k. Sasa heshima ya utu na haki za binaadamu hizo zenye utukufu ziko wapi za kulindwa?
Tanzania tunaambiwa nchi haina dini. Nenda Tanganyika utizame Udini unavyoingizwa kwenye mambo ya Serikali dhahiri dhahiri. Ati uhuru wa Mahkama. Hivi kweli Mahkama ziko huru kama inavyotakiwa?
Sasa inaposemwa katika kujadili katiba tuhakikishe kutotengua na kuucha utukufu uliopo, ni utukufu upi na lipi ambalo tusilitengue kutokana na uzuri wake. Yote yanatengulika na kufanywa upya kutokana na uoza uliopo.
Nawakilisha hoja
SOSI: MZALENDO.NET
 
amendimenti ndio inayofanyika, Zenji wameshtuka wamechana muswada mbele ya Samwel Sitta.
 
Inawezekana Rweye. Inauma sana jinsi mambo yanavyofanyika. Unajiuliza, ni kwa manufaa ya nani? Wanamfurahisha nani? Wanataka kufanikisha nini? Kwa niaba ya nani? Majibu yote yanaacha maswali mengi zaidi.

Haya maswali ni kila mtanzania ajiulize, mimi huwa najiuliza sana na majibu yake huwa sipati... Swali lingine ni hili hivi hao wanaCCM haswa wabunge wao wanapoyafanya haya haswa ya kuipitisha miswada isiyokuwa na mbele wala nyuma(mingine imerudi na kuwatenda) wanapitisha kwa kuikomoa CHADEMA na wapinzani au wananchi?

Naamini kuwa katiba mpya madhubuti na ya wananchi yenye kukidhi mahitaji ya kikatiba ya sasa na yajayo mpaka miaka 50-100 ijayo ndio majibu yangu.
 
The Consitutional Review Bill that is being currently debated should be scrapped without delay and a new Bill laying out procedures for collecting peoples' view be published for peoples' views before being sent to Parliamnt.

After referendum, a Bill for a New Constitution, based on the views of the majority, should be drafted, published and sent to parliament for passing or refusal
 
We request you to post the Bill in PDF so that we may also read it. This will help us to understand it well.
 
Hii inajidhihirisha ni namna gani huko kujivua gamba kunakosemwa na CCM ni danganya toto tu. Haiwezekani wakaamua kujisafisha halafu matendo yao kubaki ya kigandamizaji namna hiyo. Chimbuko la wazo la kutoa Muswada wa namna hii ni kukomaa kwa fikra kwamba, wananchi bado tu wajinga na hivyo wana-CCM wana fursa ya kuendelea kutumia mtaji huo wa ujinga wetu kujinufaisha wenyewe.

Haiingii akilini, kwamba, pamoja na kupigiwa kelele na wananchi leo karibia miaka 15 kuhusu kuandikwa kwa Katiba Mpya wao wanaibuka na Waraka dhaifu namna hiyo. Yaani hata hawakuelewa nini wimbo wetu juu ya agenda hii ya Katiba Mpya. Na kwa kuogopa kivuli cha Katiba hiyo mpya, wameamua kufunika hoja kwa Muswada huu ambapo, kama wananchi hatutakuwa makini, tunaweza tukaliwa kilahisi sana. Nawasihi wananchi tuwe makini kama ambavyo tumekuwa makini katika kudai kuwepo kwa Katiba Mpya kwa kipindi kirefu sasa. Tusiwape mwanya wa kutugandamiza hata kidogo.
 
kwa pamoja tunaweza tumechoka na hao wanaojivua magamba kama nyoka[CCM]
 
tatizo wanajifanya viziwi yaani hawasikii wananchi wanayoyoyataka na vipofu hawaoni wanainhi wanayoyaitaji sasa ngoja si wanadhani watatawala karne na karne muda si mrefu yatawatokea puani
 
Inawezekana Rweye. Inauma sana jinsi mambo yanavyofanyika. Unajiuliza, ni kwa manufaa ya nani? Wanamfurahisha nani? Wanataka kufanikisha nini? Kwa niaba ya nani? Majibu yote yanaacha maswali mengi zaidi.
Jibu ni rahisi: Huu muswada ni kwa manufaa ya makupe yenye kudhani kwamba wananchi bado hawana uwezo wa kufikiri ila wao tu ndo shule walizosoma zinafundisha critical thinking and reasoning! Lengo lao hapa ni kulinda maslahi egemezi ya upande wao na familia zao. Anyway, nadhani picha halisi ya mawazo huru wameshaiona!
 
Shime shime vijana hii nchi ya kwetu na wala sio ya hao wanakomaa na madaraka na kutunyonya....
 
Back
Top Bottom