Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kula Tano man 👊Hata nidaiwe vp, nikutane na magumu kiasi gani, siwezi kufikiria kujiua. Haiwezekani na kamwe haitatokea eti siku moja nitingwe na mawazo mpaka kufikia hatua ya kukatisha uhai wangu.
AseeAngesubiri kidogo angalau ajue hata mwenye kiti wa CCM ni nani?
Kwani Marehemu Alikuwa Anasemaje?Muuguzi wa Hospitali ya Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, David Mtaita (30) amejinyonga hadi kufa kwa kutumia kamba ikiwa ni baada ya kujichoma sindano ya kutuliza maumivu.
Akizungumza leo Alhamisi Aprili 29, 2021 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kubainisha kuwa katika uchunguzi wa awali wamebaini muuguzi huyo alijinyonga juzi saa 12 jioni kutokana na msongo wa mawazo uliosababishwa na madeni.
Amesema kabla ya kujinyonga alijichoma sindano ya kutuliza maumivu kwa kuwa ilikutwa pembeni ya mwili wake.
“Alifanya kitendo hicho katika nyumba aliyokuwa anaishi eneo la Singisi wilayani Arumeru,” amesema na kubainisha kuwa uchunguzi bado unaendelea.
Chanzo: Mwananchi
Acha kabisa😬😬Kwa umri wake usikute alikua anajitolea tu na kulipwa kidogo jambo lililopelekea kuwa na madeni mengi. Yaani unafahamika kama dotor halafu unaishi kwa mlo mmoja.
Dah umeandika ukweli kabisaHaya maisha hatari sana. Asubuhi unaenda kazini unarudi jioni. Ndugu zako wakikuomba hata 10, 000 hauna unafikiri umewanyima hela.
Kila siku unatengeneza matatizo tu unaona bora ufe ili uondoe lawama kbsa.