Muujiza wa Kwanza alioufanya Yesu ni kubadili maji kuwa divai. Kwanini Makanisa mengi yanahubiri kuwa pombe ni dhambi?

Hapa kwenye hili suala kila mtu atatetea upande wake unaomvutia kwa kigezo cha mistari ya biblia na kuna watakaosema baadhi ya mistari ya biblia ni fumbo

Cha msingi kila kitu kina kiasi chake

Unaetumia usiwakere wasiotumia na usiotumia pia usiwakere watumiaji

IMANI YAKO ITAKUPONYA
 
Tunaangamia kwa kukosa Maarifa

Mithali23
29 Ni nani apigaye, Yowe? Ni nani aliaye, Ole?
Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye mguno?
Ni nani aliye na jeraha zisizo na sababu?
Ni nani aliye na macho mekundu?
30Ni wale wakaao sana kwenye mvinyo;
Waendao kutafuta divai iliyochanganyika.
31Usiitazame mvinyo iwapo ni nyekundu;
Iitiapo bilauri rangi yake, ishukapo taratibu;
32Mwisho wake huuma kama nyoka;
Huchoma kama fira.
33Macho yako yataona mambo mageni;
Na moyo wako utatoa yaliyopotoka.
34Naam, utakuwa kama alalaye katikati ya bahari;
Au kama yeye asinziaye juu ya mlingoti.
35 Utasema, Wamenichapa wala sikuumia;
Wamenipiga wala sina habari;
Nitaamka lini, nitazidi kuitafuta tena.
 
-Ujue Mvinyo hutengenezwa kwa kukamua maji ya mzabibu kisha hutokea juisi divai
-Divai inaweza kuwa juisi isiyolewesha na divai inaweza kuwa pombe iliyokaa mda mrefu na hii huitwa mvinyo.
-Yesu alitengeneza juisi ya mzabibu na sio pombe, angefanya hivyo angekinzana na maandoko mengi katika biblia na hivyo leo hii tungesema Yesu hakuwa mtii kwa maandiko.

31 Usiitazame mvinyo iwapo ni nyekundu; Iitiapo bilauri rangi yake, ishukapo taratibu;
32 Mwisho wake huuma kama nyoka; Huchoma kama fira. (Mithali 23:31-32)
 
11 "Ole wao waamkao asubuhi na mapema, wapate kufuata kileo; wakishinda sana hata usiku wa manane mpaka mvinyo imewaka kama moto ndani yao! " Isaya 5:11


"Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;"Waefeso 5:18
 
Mleta mada unataka kusema YESU ALIKUWA CHAPOMBE?
 
Unataka kusema YESU ALIKUWA CHAPOMBE?
 
Aya ya 9.
Muwe mnasoma maandiko yenu jamani.
 
Kwanini Yesu muujiza wake wa kwanza uwe kubadili maji kuwa divai? Alitaka kutufundisha nini?
 
Unajua divai/wine ni pombe fulani yenye kilevi kidogo tu just kuchangamsha,, lkn kupitia andiko hili wachaga(sio wote) hapa ndio wanahalalisha double kiki, k vant, gongo etc.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…