Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Muundo wa Muungano: Tanganyika tunataka 'Serikali moja, nchi moja, taifa moja'!

Tunataka serikali moja tu

Serikali ya watu wa TANGANYIKA

Hao wengine hatutaki kuwasikia, waende kupika urojo huko kwao

Ni wakati umefika Ng'ombe akatae kunyonywa na kupe mlalamishi.

Hivi kwanza wana faida gani kwa bara hawa wazenji zaidi ya kelele na udini?

Watu wote MIOYONI mwetu TUNATAMANI kuona Tanganyika kivyake na Zanzibar Kivyake. Shida ni huyo wa kusema na IWE hivyo.

Viongozi wangependa kuona kero za muungano Zimefika MWISHO. Wananchi tuko wazi kabisa kuwa kero hazitokani na kero bali kero hizi zinatokana na MUUNGANO wenyewe. Tusingeungana tungekuwa huru sana kuliko huu UTUMWA wa sasa.

Siungi mkono nchi moja maana hapo zitazaliwa kero mpya kabisa. Kwamba Zenj yenye Rais wake sasa iwe mkoa na Shain awe RC ni kichekesho! Huko tusiende.

Suruhu yetu ni moja tu kuwa tuwe kama ilivyokuwa March 1964. Tanganyika huru na Zanzibar huru kila mtu amtakie heri mwenzake.
 
je wazanzibari wanataka serikali tatu ?

Isaac JK

Kama ulifuatilia utoaji wa maoni kuhusu Katiba mpya hawa watu walisema "waachiwe wapumue".

Kwa sababu hadidu rejea alizopewa Warioba na Tume anayoingoza ni kuwa "Muungano ujadiliwe kwa nia ya kuuboresha tu" na sio uwepo wake au kutokuwepo kwake. Wazanzibari waliuona mtego wa JK na walibuni kitu walichokiita "Muungano wa Mkataba".
Walipendekeza mamlaka kamili kwa Zanzibar , mamlaka kamili kwa Tanganyika na Muungano wa mkataba.

Tume ya Warioba wamekuja na rasimu ambayo haizingatii maoni hayo na walitoa angalizo kuwa Tume itakuja na mapendekezo ya Rasimu ya Katiba mpya inayoangalia masilahi ya taifa na sio inayotokana na maoni ya wananchi.

Katika upokeaji wa maoni kutoka kwa wananchi, Tume ya Warioba ilipata wakati mgumu ilipofanya kazi zake kule Zanzibar na Wajumbe wa Tume walionekana kukerwa na maoni yaliyodai Zanzibar huru,Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa,kufufuliwa kwa Tanganyika na muungano wa mkataba.

Kama Tume ingeyafanyia kazi maoni yaliyotolewa na wazanzibari (kitakwimu inasemwa ni asilimia 66) basi Tume ya Warioba ingekuja na mapendekezo ya kuifufua katiba ya Tanganyika na serikali ya Tanganyika na bila ya kupoteza muda, mchakato wa kuandika katiba mpya ya Tanganyika ungeanzishwa.

Tunawalazimisha wazanzibari wawe ndani ya muungano lakini hawautaki muungano, hawataki serikali tatu,mbili au moja. Wameshasema sana wanataka nchi yao na uhuru kamili wa kujiamulia mambo yao.

Tunalazimisha serikali tatu lakini kama ni muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar tu, hautadumu. Kama nchi za Malawi, Zambia, Burundi, Rwanda zitaruhusiwa kujiunga, huenda Zanzibar watajifunza kitu na kutamani kubakia katika muungano.

Wakati watu wanajadili "usanii" wa Tume ya Katiba mpya, CCM wanacheka sana, wanachekelea sana. Muda wa kuandika Katiba ya Tanganyika na kuiunda na kuisimika serikali ya Tanganyika utafanya uchaguzi mkuu usogezwe mbele au itatumika katiba ya 1977.

Kwa kweli kinachoendela ni kituko/maigizo tu. Kama Tume imetoa pendekezo la kuanzisha serikali tatu. Hatua ya kwanza ilikuwa ni kuandika katiba ya Tanganyika na kuunda serikali ya Tanganyika. Baadae serikali ya Tanganyika ikae mezani na serikali ya Zanzibar kujadili Muungano kama vile wabia hawa wa muungano walivyofanya 1964.

Tunatengeneza utata na maumivu tu ya muungano badala ya kuamua kulishughulikia tatizo la muungano na mfumo/muundo wake lililopo mbele yetu kwa ujasiri na kwa kujiamini. Tunateketeza fedha za kodi za walalahoi na pia tunatengeneza matatizo mingine mapya na mazito zaidi.

Tanzania ni nchi ya mazingaombwe!
 
Serikali moja tu

Ndio, serikali moja tu ,ya Shirikisho la Afrika Mashariki.

Link https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...;-sema-ndiyo-serikali-moja-3.html#post6510457

Hatuhitaji kuwa na serikali ya Tanganyika , ya Zanzibar au ya muungano. Tukasimishe mamlaka ya serikali zetu kwa Serikali ya Shirikisho la Afrika Mashariki. Tuharakishe mchakato ili Muungano wa Kikanda na Afrika ufanikiwe kwa haraka.

Kama umepitia hiyo link utaona jinsi ambavyo tumeshachelewa kidogo kufuata ratiba ya kuunda shirikisho la kisiasa la Afrika Mashariki.

Umoja ni nguvu.
 
Nyerere aliukataa muundo wa serikari tatu tena Miaka ile ya Analogia iweje kipindi cha hiki cha Digtal tusiyaenzi maoni ya Nyerere ?

Hukumwelewa Mwalimu.

Mwalimu hakupenda kuiona Zanzibar ikiwa nje ya aina ya Muungano, inaonekana Mwalimu alikuwa na hofu fulani kama Zanzibar itakuwa ni nchi huru, nchi yenye mamlaka yake kamili. Lakini aliridhia kwa kusema ikiwa nchi za Afrika Mashariki zitaazimia kuungana(Shirikisho la Afrika Mashariki) basi itakuwa rahisi Tanganyika na Zanzibar kujiunga huko kama washiriki tofauti.

Angalia hapa link https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...;-sema-ndiyo-serikali-moja-3.html#post6510457
 
Nonda;6517850]Isaac JK Kama ulifuatilia utoaji wa maoni kuhusu Katiba mpya hawa watu walisema "waachiwe wapumue".
Kwani walifanya jaribio lipi la maana na akili ambalo tunaweza kusema waliamua wapumue?
Je, waliwahi kumwita makamu wa rais arudi kutoka bara, waliwahi kupeleka mswada bungeni au BWL, waliwahi kuzuia wabunge wao kuja Dodoma, waliwahi kuwaita viongozi katika utumishi wa JMT? Jibu ni hakuna.

Pili hao viongozi wanaofanyakazi katika JMT na wale waishio Tanganyika ambao ni wengi kuliko walioko znz, wao siyo wznz na je hawakuona umuhimu wa kupumua.
Kuruka ruka barabarani hovyo siyo njia ya kupumua, ilikuwa ni movement isiyojua inakwenda wapi
]Kwa sababu hadidu rejea alizopewa Warioba na Tume anayoingoza ni kuwa "Muungano ujadiliwe kwa nia ya kuuboresha tu" na sio uwepo wake au kutokuwepo kwake. Wazanzibari waliuona mtego wa JK na walibuni kitu walichokiita "Muungano wa Mkataba".Walipendekeza mamlaka kamili kwa Zanzibar , mamlaka kamili kwa Tanganyika na Muungano wa mkataba
Nonda si kweli! Wazanzibar hawakuwa naakili hiyo.
Wangekuwa nayo basi wasingeweka jitihada, akili na fikra zao katika kutafuta wajumbe kwa uwiano. S
isi tuliona hilo tukaonya kuwa kuna tatizo tukapaza sauti

Kuhusu kupendekeza mamlaka kamili, huwezi kuwa na malaka ukiwa huna vyombo vya ulinzi na usalama.
Hakuna mamlaka kamili kwasababu unamkumbuka Mliberali alikamatwa kama mwizi wa kuku na kusweka ndani.

Unakumbuka mwingine aliitwa na kuambiwa stop,Unakumbuka yule aliyetishia kurudi na ASP kutoka Dodoma alipotoka nje ya ukumbi kuanzia mlinzi wake hadi makanda wa polisi wamehamishwa.

Kuanzia hapo hatujamsikia tena! kwanza lazima uwe na ulizi na usalama kitu ambacho znz haitaki kwasababu haijawahi kuwa na bajeti toka mwaka 1964 na uchumi haurusu. Ndizo sababu za mkataba.
Katika mambo ya mkataba hutamsikia mzanzibar akizungumzia ulinzi na usalama, in fact wanasema wazi wanafaidika na hilo
Katika upokeaji wa maoni kutoka kwa wananchi, Tume ya Warioba ilipata wakati mgumu ilipofanya kazi zake kule Zanzibar na Wajumbe wa Tume walionekana kukerwa na maoni yaliyodai Zanzibar huru,Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa,kufufuliwa kwa Tanganyika na muungano wa mkataba
Katika wajumbe 30, 15 wanatoka znz, sasa unaposema walikereka ina maana hata wajumbe wa znz walikereka.
Wakati mgumu uliletwa na vurugu za wanamapinduzi na waliberali kuchapana makonde si tume.
Hukufuatilia au unapotosha
Kama Tume ingeyafanyia kazi maoni yaliyotolewa na wazanzibari (kitakwimu inasemwa ni asilimia 66) basi Tume ya Warioba ingekuja na mapendekezo ya kuifufua katiba ya Tanganyika na serikali ya Tanganyika na bila ya kupoteza muda, mchakato wa kuandika katiba mpya ya Tanganyika ungeanzishwa
Ndiyo maana tulisimama na kusema tume ilianzia mahali ambapo sipo.

Wazanzibar walikuwa bize wakitaka 50/50. Hao unaosema walitaka Tanganyika ndio hao hao wanaikataa serikali 3 akiwemo muasisi wa serikali 3 Seif Sharif. Asilimia 66 ni bendera fuata upepeo
Tunawalazimisha wazanzibari wawe ndani ya muungano lakini hawautaki muungano, hawataki serikali tatu,mbili au moja. Wameshasema sana wanataka nchi yao na uhuru kamili wa kujiamulia mambo yao.
Mkataba wanataka wa nini?
Seif aliulizwa binafasi na Warioba kwanini tusikutane EAC, akasema muungano wetu ni mzuri kuliko wa EAC. Seif ambaye amebeba akili za wznz anasema muungano ni bora hakusema hataki muungano,sasa mznz gani aliyebaki.
Mansour,Moyo, Jusa walisimama na kusema wanataka muungano, mznz aliyekataa ni yupi tena
Tunalazimisha serikali tatu lakini kama ni muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar tu, hautadumu. Kama nchi za Malawi, Zambia, Burundi, Rwanda zitaruhusiwa kujiunga, huenda Zanzibar watajifunza kitu na kutamani kubakia katika muungano.
Unajichanganya, hapo juu umesema wznz walitaka serikali ya Tanganyika kwa maana walitaka serikali 3.
Chama cha CUF sera yao ni serikali 3 sasa leo kipi cha kuwatetea kuwa waliona zaidi.

Walichokiona ni wajumbe 50/50.Tuliwaambia tusimame pamoja kukataa tume, wao akiwemo mpiga debe mkuu wa znz kupitia BBC Ali Swalehe akakimblia masufuru na 50/50.

Akili ya kuona kilichokuwa kinakuja haikuwepo. Akaingia mliberai huyo ndiye akatumbukiza nyongo kabisa akidai mkataba. Tukasikia kama wa Uswiss, Hong Kong, Bemuda na Nigeria n.k Leo mseme hamtaki muungano, acheni uongo asiyetaka muungano ni Mtanganyika anayewaambia nendeni kwenu hatuwahitaji.
Ikiwana nusu ya znz ipo Tanganyika nguvu ya kukataa muungano ni ya akina Uamsho, wznz wenyewe hawana jeuri hiyo.
Wakati watu wanajadili "usanii" wa Tume ya Katiba mpya, CCM wanacheka sana, wanachekelea sana. Muda wa kuandika Katiba ya Tanganyika na kuiunda na kuisimika serikali ya Tanganyika utafanya uchaguzi mkuu usogezwe mbele au itatumika katiba ya 1977.
Wenzetu mlitaka 50/50 kwamaneno mengi quantity siyo quality
Kwa kweli kinachoendela ni kituko/maigizo tu. Kama Tume imetoa pendekezo la kuanzisha serikali tatu. Hatua ya kwanza ilikuwa ni kuandika katiba ya Tanganyika na kuunda serikali ya Tanganyika. Baadae serikali ya Tanganyika ikae mezani na serikali ya Zanzibar kujadili Muungano kama vile wabia hawa wa muungano walivyofanya 1964
Tuliyoona haya tulisema tume itaingiza watu mkenge, wenzetu mkaendelea na hadithi za Seif na uwiano. Hapo ndipo tatizo lilipoanziaHatukuwa na true partner

Tunatengeneza utata na maumivu tu ya muungano badala ya kuamua kulishughulikia tatizo la muungano na mfumo/muundo wake lililopo mbele yetu kwa ujasiri na kwa kujiamini. Tunateketeza fedha za kodi za walalahoi na pia tunatengeneza matatizo mingine mapya na mazito zaidi.
Hasa rasimu hii inammaliza mznz kabisa. Hakuna mamlaka kamili na utegemezi unafikia kikomo ingawa bado tutabeba zigo la kuendesha serikali. Waambie wznz hii ni fursa pekee kwao kukataa rasimu na muungano. Baada ya hapo ni maumivu. Kama walifanya makosa huko mwanzo warekebishe sasa, tutawasadia sana katika kupata mamlaka lakini lazima wao kwanza watake. Sisi hautingii SMZ,BLW au BLM. Tunawapa mawazo tu, wale walioko Dodoma walete mswaada hilo una uwezo nalo kuwasadia. Knyume chake maumivu makali yanaisubiri znz hasa Tanganyika inaporudi.
 
........... wenzetu mkaendelea na hadithi za Seif na uwiano. Hapo ndipo tatizo lilipoanzia.Hatukuwa na true partner

Hasa rasimu hii inammaliza mznz kabisa
. .....maumivu makali yanaisubiri znz hasa Tanganyika inaporudi.

Maalim Pacha wa Mzee

Sehemu kubwa ya waraka wako ni hadithi na mipasho. Ungefaa zaidi kuwemo katika bunge hili linaloongozwa na Mwali Makinda. Just for a lough, mkuu.

Ukiondoa hiyo hadithi refu na kauli za uliberali na ninyi,sisi, nililoliona la maana katika waraka wako ni hayo niliyoweka wino mwekundu.

Nafikiri wazanzibari wataichambua hiyo Rasimu iliyotolewa na wakiona haina masilahi kwao wataikataa kwa kuipigia kura ya HAPANA. Lakini kwanza wataitolea mapendekezo kupitia mabaraza ya katiba na Mtaalamu Warioba na Tume yake watakaposhindwa, watakapokataa kuifanyia ukarabati Rasimu hiyo ni wazi itapewa kura ya HAPANA.

Hayo hawatafanya wazanzibari peke yao. Hata sisi watanganyika tutafanya uchambuzi wa rasimu,tutatoa mapendekezo tuyatakayo na tutakapoiona haiendani na masilahi yetu tutaikataa.

Mchakato haujamalizika bado, Maalim Nguruvi3.

Rasimu ya Katiba iliyotolewa ni janga la kitaifa!

Mkuu nini ambacho unapendekeza kiingizwe au kiondolewe katika Rasimu iliyotolewa?
 
Ritz, tena kawa Mzanzibar? mimi siwezi kushikiwa akili mtu anaishi Marekani aniamlishe eti sema hapana serikali tatu, sema ndiyo serikali moja kwa kumfurahisha yeye.

Mimi natumia akili yangu napima mambo kama wewe na wenzako mnashikiwa akili siyo mimi.

Kila mmoja ana haki yake tusipangiane mambo.

Siku hizi unatumia akili zako si za Lumumba?
 
Maalim Pacha wa Mzee

Sehemu kubwa ya waraka wako ni hadithi na mipasho. Ungefaa zaidi kuwemo katika bunge hili linaloongozwa na Mwali Makinda. Just for a lough, mkuu.

Ukiondoa hiyo hadithi refu na kauli za uliberali na ninyi,sisi, nililoliona la maana katika waraka wako ni hayo niliyoweka wino mwekundu.

Nafikiri wazanzibari wataichambua hiyo Rasimu iliyotolewa na wakiona haina masilahi kwao wataikataa kwa kuipigia kura ya HAPANA. Lakini kwanza wataitolea mapendekezo kupitia mabaraza ya katiba na Mtaalamu Warioba na Tume yake watakaposhindwa, watakapokataa kuifanyia ukarabati Rasimu hiyo ni wazi itapewa kura ya HAPANA.

Hayo hawatafanya wazanzibari peke yao. Hata sisi watanganyika tutafanya uchambuzi wa rasimu,tutatoa mapendekezo tuyatakayo na tutakapoiona haiendani na masilahi yetu tutaikataa.

Mchakato haujamalizika bado, Maalim Nguruvi3.

Rasimu ya Katiba iliyotolewa ni janga la kitaifa!

Mkuu nini ambacho unapendekeza kiingizwe au kiondolewe katika Rasimu iliyotolewa?
Ha ha ha ha! unanipeleka kwa mwali! huko sikuwezi maana unatakiwa uwe kidogo na tatizo la kichwa! just for lough

Nikisema napendekeza au naondoa nini napata taabu sana. Kwakweli kilichotakiwa ni kuanza mchakato kwa kutumia mkutano wa kitaifa halafu ndipo maoni na kisha rasimu. Sasa hivi naona vurugu tupu.
Najifariji kuwa japo nilikataa.

Naangalia mambo mengi sana
1. Kwanini kuwe na serikali ya muungano kuubwa kiasia hicho
2. Mbona uendeshaji wa hiyo serikali haukusemwa au ndio tunategemeawafadhili
3. Kuna vifungu ambavyo vinahusu watu wanne, pindi mola akiwachukua havina kazi
4. Kinga ya rais iondolewe ili tuwe na rais anayeogopa kazi yake
5. Kwanini tuwe na wabunge wa jinsia mbili
6. Kuna tech writting iliyokosewa makusudi kwa makusudi yao na si wananchi
7. Kura ya maoni ilitakiwa itangulie rasimu siyo rasimu na sasa ni kama kura ya maoni
8. Baraza la usalama la taifa halina maana iliyokusudiwa
9. Sula la muungano lilitakiwa lipatiwe ufumbuzi mapema kabisa
10. Mtanganyika na serikali yake watabeba mzigo mkubwa sana, wa serikali yao na ya muungano pengine na mshirika
........100
 
NIMEANZA KUFUMBUKA MACHOO BAADA YA KUONA KUWA MADHUMUNI YA WAZUNGU YAMEANZA KUTIMIA 'divide and rule' FREEMASON WANAISHARA YA 3 NA TANZANIA INATAKA SERIKAR TATU WHAT DO YOU MEAN? NIYA YA WAZUNGU NI KUONDOA UMOJA ILI WATUCHONGANISHE NA KUTUTAWALA, KATAA SERIKAR TU.
 
............
Kuhusu kupendekeza mamlaka kamili, huwezi kuwa na malaka ukiwa huna vyombo vya ulinzi na usalama.
Hakuna mamlaka kamili kwasababu unamkumbuka Mliberali alikamatwa kama mwizi wa kuku na kusweka ndani.

Unakumbuka mwingine aliitwa na kuambiwa stop,Unakumbuka yule aliyetishia kurudi na ASP kutoka Dodoma alipotoka nje ya ukumbi kuanzia mlinzi wake hadi makanda wa polisi wamehamishwa.

Kuanzia hapo hatujamsikia tena! kwanza lazima uwe na ulizi na usalama kitu ambacho znz haitaki kwasababu haijawahi kuwa na bajeti toka mwaka 1964 na uchumi haurusu. ...........

Mkuu Nguruvi3

Ingawaje umeandika ukiwa na dhamira ya kuonesha kitu kingine kabisa lakini kauli hizi ulizoandika hapa zinathibitisha kuwa ni "Watanzania bara/ Watanganyika ndio tunaolazimisha Muungano.

Hili jambo wamelisemea sana wazanzibari kuwa wanaburuzwa,wanalazimishwa kubaki katika Muungano au utaamua kuzikana kauli hizo hapo juu uliziandika katika hadithi yako?

Kwa nini Maalim Nguruvi3, sisi wadanganyika ndio tunaung'ang'ania muungano huku tunalalamika kuwa unatutia hasara tu, hauna faida kwetu?
 
Ha ha ha ha! unanipeleka kwa mwali! huko sikuwezi maana unatakiwa uwe kidogo na tatizo la kichwa! just for lough

Nikisema napendekeza au naondoa nini napata taabu sana. Kwakweli kilichotakiwa ni kuanza mchakato kwa kutumia mkutano wa kitaifa halafu ndipo maoni na kisha rasimu. Sasa hivi naona vurugu tupu.
Najifariji kuwa japo nilikataa.

Naangalia mambo mengi sana
1. Kwanini kuwe na serikali ya muungano kuubwa kiasia hicho
2. Mbona uendeshaji wa hiyo serikali haukusemwa au ndio tunategemeawafadhili
3. Kuna vifungu ambavyo vinahusu watu wanne, pindi mola akiwachukua havina kazi
4. Kinga ya rais iondolewe ili tuwe na rais anayeogopa kazi yake
5. Kwanini tuwe na wabunge wa jinsia mbili
6. Kuna tech writting iliyokosewa makusudi kwa makusudi yao na si wananchi
7. Kura ya maoni ilitakiwa itangulie rasimu siyo rasimu na sasa ni kama kura ya maoni
8. Baraza la usalama la taifa halina maana iliyokusudiwa
9. Sula la muungano lilitakiwa lipatiwe ufumbuzi mapema kabisa
10. Mtanganyika na serikali yake watabeba mzigo mkubwa sana, wa serikali yao na ya muungano pengine na mshirika
........100

Unaona Maalim, mambo inavyokuwa mzuri unapoacha madoido na yale mambo wanafanya katika mjengo wa Mwali.
Upunguze aina ya uandishi wa riwaya. Hapa ujumbe unaeleweka kwa urahisi na wepesi.

Umesoma hapa? https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...;-sema-ndiyo-serikali-moja-3.html#post6510457
 
Yes! This would be a good starting point. Mimi sitaki muungano. Nataka Tanganyika. Hivi kweli nani aliwahi kuiona ile instrument ya muungano wa 1964? Hawa wazee walikuwa na hoja gani za msingi?


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
.
Kweli mi-AFRICA ni nusu wanyama nusu wanadamu, hivi katika karne ya sasa ambayo hata wale wenye nguvu kubwa za kiuchumi, kiteknologia na kijeshi wanaangalia jinsi ya kuungana!! sisi masokwe tunaangalia jinsi ya kuvunja kile ambacho kilishawahi kuundwa!!!!!!!!!!! migogoro baina ya watu/ vyama/nchi zilizoungana ni vitu vya kawaida na ndio maana mazungumzo yanaruhusiwa kujadili mapungufu according to time. wazo la kuuvunja muungano ni wazo dhaifu, toka katika akili dhaifu zinazowaza kidhaifudhaifu... changamoto katika mahusiano ni vitu vya kawaida mazeee
 
Sema hapana Serikali "Tatu", Sema ndiyo "Serikali moja". Nchi moja, Taifa Moja, Watu wamoja - nje ya hapo Hapana!!! Tumeshatengeneza ulaji na ukiritimba wa kutosha kwenye serikali mbili halafu tunataka kuongeza serikali ya tatu? Mizigo miwili midogo imetushinda (tunahangaika nayo) halafu magenius wetu wanataka kutupa mizigo mitatu mikubwa!? Kwanini tusiamue kutengeneza mzigo mmoja tu tukaubeba!?

Pamoja na jaribio dhaifu la Tume ya Warioba kupendekeza kuikataa majimbo, pendekezo lao la Katiba Mpya kimsingi linatengeneza majimbo yale yale (States) ambapo kutakuwa na majimbo mawili - Tanganyika na Zanzibar! Kwa sababu kama nchi mbili zimeungana na kuunda 'Shirikisho" basi zile zilizoungana haziwezi kuendelea kuwa nchi tena; zinahamisha hakimiya (sovereignty) yake kwenda kwenye federal government isipokuwa kama kilichoundwa (Shirikisho) siyo nchi!

Kwa kuanzisha mfumo wa Majimbo - Jimbo la Tanganyika litakuwa na nguvu kubwa sana kuliko jimbo la Zanzibar. Lakini kama wakiamua kufanya hali ya sawa katika kuendesha serikali ya Jamhuri ya Muungano Zanzibar itaonewa kwani ikitakiwa kuchangia nusu ya gharama za kuiendesha serikali ya Muungano italalamika mno na sidhani kama Wazanzibari watatakiwa kukubali mfumo huo.

Kwa sababu hiyo njia ya kuimarisha "Muungano" kama lengo ndio hilo basi ni kuingia Serikali Moja ya Kitaifa na Nchi Moja - siyo serikali tatu za kitaifa. Chini ya serikali hiyo moja ya kitaifa (federal government) kutakuwa na serikali za Majimbo (States) ambapo Zanzibar itabakia kama ilivyo (Visiwa vya Mafia, Bagamoyo, Pangani vinaweza kuongezwa huko... I know.. I know.. au ikagawanywa Unguja ikawa kivyake na Pemba kivyake!.) halafu Tanganyika igawanywe kwa States saba hivi ambazo zitaunda 'Regional Governments). Chini ya Regional Governments kutakuwa na "Local Governments" za Miji, Majiji, Vijiji na mifumo mingine ya kujitegemea.

Na maneno mengine mengi....

In short.. Tusikubali serikali tatu za nchi; bali serikali moja, nchi moja, taifa moja na watu wamoja.. Mapendekezo ya Tume ya Warioba kuwabebesha Watanzania mizigo hii ni ya kupingwa, kukataliwa na kupuuzwa.

kama wazanzibar hawawezi kukubali kuvunjwa muungano ya kuwa na serikali moja ni sahihi kuwa na serikali tatu.
 
Sijui kwa nini bado tuna “flip flop” na suala la Muungano. Wote tunajua kuwa huu Muungano ni kikwazo kikubwa sana katika ku-design a good, an effective and a responsible governing system.

Kama siyo huu muungano wala tusingekuwa na system, au kujaribu hata kupendekeza system, ya utawala isiyoeleweka, even kufikia extent ya kupendekeza kuwa na ceremonial president.

Watanzania wapewe haki ya kujiamualia through a referendum. Waulizwe kama bado wanapenda kuendelea kuwepo kwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Kama hawapendi, basi na Muungano uvunjwe, kila mtu achukue times zake. Kama bado wanapenda Muungano uwepo, basi waulizwe wanapendelea Muungano wa aina gani.

Personally, kuendelea kupendekeza kuwepo Muungano wa serikali tatu, tena with a ceremonial president, ni kukwepa ku-address the core problems za Muungano wa sasa na kuendelea kuendeleza kiini macho cha Muungano.

Najaribu kufikiria idea ya kuwa na ceremonial president kwenye nchi ambayo viongozi wake waliochaguliwa kuwa accountable kwa wananchi, lakini wanafanya kazi zao in a ceremonial way. Sasa itakuwaje kama wakipewa full title ya kuwa ceremonial leaders?

Kwa nchi kama Tanzania, we need a responsible and accountable President, not a ceremonial president. Hatutaki kuwa na Rais ambaye kazi yake itakuwa ni kutembea na mikasi mfukoni kwa ajili kukata utepe kama anavyofanya Makamu wa Rais.

Kama vipi na tusiwe na rais wa aina hiyo kabisa. We aren’t that rich to pay for someone simply for doing nothing.

...well said mkuu!
Hivi hawais it possible kuwa walioko huko juu hawalioni hili?au wanafanya makusudi 2!?
Manaake najaribu kufikiria vichwa vyote hivyo vimeshindwa kweli kuliona hili?
Kweli nimeamini serikali ya ccm haiwezi kufanya kitu kwa maslahi ya taifa/wananchi unless 10% kwanza ndo mengine yaendelee!
 
Mwanakijiji.

Vipi bwa mkubwa umekurupushwa usingizini nini?

Mbona wakti wa kutoa maoni umeshapita na wewe ukukumbuka kusema hayo?

Ok kuna nafasi nyingine labda yapenyeze kwenye mabaraza ya Katiba tuone kama yatapita.

Sisi msimamo wetu ule ule LET TANGANYIKA COME TO FREE ZANZIBAR. Na zaidi tunasisitiza Uzanzibari kwanza, Utanzania baadae.

Unakumbuka shuka wakti kumeshakuchwa.

Pole sana
 
kwa nchi ndogo kama tz kuwa na serikali 3 ni kunyonya nguvu za wanyonge na kuwanufaisha wachache,coz serikali zote hz zitahitaji mawazir ambao watakuwa wanalipwa pesa nying bila kufanya kaz na pia umaana wa muungano pia utakuwa umetoweka kabsaa!!!!
 
Ha ha ha badirisha title kama unataka tuchangie huwezi kuita uhuni maoni ya wananchi vinginevyo kachangie na familia yako huwezi kuleta thread ya matusi hapa umeumia jangiri la tembo
 
Ha ha ha badirisha title kama unataka tuchangie huwezi kuita uhuni maoni ya wananchi vinginevyo kachangie na familia yako huwezi kuleta thread ya matusi hapa umeumia jangiri la tembo

kwan lazima uchangie, au mada kuchangiwa ni credit nini mkuu!
 
Kweli kabisa ni uhuni

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Serikali tatu sio uhuni ni fumbo kubwa sana,binafsi hii hoja kupitishwa na tume naiona kama vile ni hatua kubwa sana ya kipimo cha uzalendo.Hapa naona hesabu hii rahisi wamewachia watanzania wenyewe waamue nini cha kufanya kwani hesabu hiyo ni je
a). 1+1=2?
b). 1+1=3?
c). 1+1=1?
d).Kwanini jibu ni "a" , "b" au "c"?
d).Nini muundo wake kama jibu ni "a" ,"b" au ,"c"?

My take: 1+1=1 (mistari miwili iliyo sambamba kamwe haikutani na unapojaribu kuikutanisha kutoka umbali uliopo kati yao unapata mstari mmoja mmyoofu).Hii inawezekana tu iwapo vikwazo vyote vitabashiriwa kama havipo.
 
Back
Top Bottom