Muungano bado una shida nyingi tusidanganyane

Muungano bado una shida nyingi tusidanganyane

ya nini yote hayo ?????

kwa nini tusiachane nao jumla ???

nchi moja, nchi mbili, serikali tatu, serikali mbili.... za nini cha mno ???????


Zanzibar wana kitu gani cha mno tunachokihitaji cha kutupa stress hii ya Muungano ???
Wanasema usalama,, kwamba maadui wakikichukua hicho kisiwa tutakuwa na hatari ya kushambuliwa au kuhujumiwa
 
Mikwara ya nyerere hiyo, sio lazima tuwe wamoja, tungetaka hivyo basi bara zima au dunia zima tungekuwa taifa moja.
Acha kila mtu ashike chake, nao wakiparaganyika waparaganyike tu, ya nini kushikilia makali unaumia wewe tu, sisi kama tanganyika tuma faida gani haswa na huu muungano mpaka tuung'ang'anie!? Je tuna faida kulilo hasara!?
Hujui kitu were, hii amani Na utulivu wa. Tanganyika Na Zanzibar tunaojivunia nao sasa una mchango mkubwa wa muungano huu.
Watanganyika zamu yetu sasa kulalamika kuhusu huu Muungano, kelele za upande wa pili hazisikiki sana kipindi hiki.
Tanganyika wako zaidi ya watu 59m wakati Zanzibar wako 1+m tu, tanganyika kwavyovyote vile haiwezi kulizwa na zanzibar hata kidogo, ila kero za muungano ni nyingi sana na zisizokuwa na majibu na hazitapata majibu hata siku moja na milele. Kama Tanganyika na Zanzibar ziliwezekana kuongozwa zote na wazanzibar kwa wakati mmoja, basi siku sio nyingi mtanganyika/watanganyika pia wataziongoza tanganyka na zanzibar kwa wakati mmoja.
 
Kama kuna vitu nyerere alibugi basi mojawapo ni huu muungano.
Ajira za Tanzania ni za wote bara na visiwani lakini za visiwani ni ya wazanzibar peke yao, ardhi ya Zanzibar huruhusiwi mtu wa bara kuimiliki lakini wazanzibar wanamiliki ardhi ya Tanganyika.
Halafu sisi watanganyika ndiyo tunaulazimisha sijui tunaumwa nini,
Wazanzibar watu wazima hawazidi 500,000 tu, kumiliki ardhi bara ndio mtego wenyewe huo waliotegewa na Nyerere, maana ardhi ina maana kubwa kuliko thamani ya ukoo mzima. Ukikosa ardhi umekwisha kabisa na ukiipata ardhi hutataka kuiachia. Israel walikosa ardhi wakaja Palestine kutafuta ardhi na sasa wanapigana na wapalestine na wako tayari kufa kuliko kuondoka. Visiwa vile ni vidogo sana na wanazaana sana, kuna
wazanzibar wengi sana wamezaliwa bara, wameolewa bara, wameoa bara, wamezaa na wabara, wanafanyakazi bara, wamejenga bara, wana biashara bara, wana mashamba na mifugo bara. Zanzibar litakuwa jina na mtaa tu wa Tanzania some years later. Hakuna mzanzibar ambae yuko bara atakubali kuacha kila kitu chake ili arudi kwao zanzibar, haiwezekani na haitawezekana. Sisi ni wamoja tayari (inseparable), kaka yangu kaoa wazanzibar 2 na ana watoto 11 na dada yangu ameolewa na mzanzibar ana watoto 4 wote hawa wana nyumba na ardhi zanzibar na tanganyika. Wanajeshi wengi wako Zanzibar na wanazaa ovyo na wazanzibar ili kazi iendelee. Hebu ona Rais Mwinyi shangazi zake wote ni watu wa bara mkoa wa Pwani lakini sasa hivi ni Rais wa Zanzibar, kazi iendelee, yajayo yanafurahisha, Nyerere alikuwa na akili nyingi sana kuliko unavyodhani wewe, hakuna haraka.
 
Wazanzibar watu wazima hawazidi 500,000 tu, kumiliki ardhi bara ndio mtego wenyewe huo waliotegewa na Nyerere,

maana ardhi ina maana kubwa kuliko thamani ya ukoo mzima. Ukikosa ardhi umekwisha kabisa na ukiipata ardhi hutataka kuiachia.

Israel walikosa ardhi wakaja Palestine kutafuta ardhi na sasa wanapigana na wapalestine na wako tayari kufa kuliko kuondoka.

Visiwa vile ni vidogo sana na wanazaana sana, kuna
wazanzibar wengi sana wamezaliwa bara, wameolewa bara, wameoa bara, wamezaa na wabara, wanafanyakazi bara, wamejenga bara, wana biashara bara, wana mashamba na mifugo bara. Zanzibar litakuwa jina na mtaa tu wa Tanzania some years later.

Hakuna mzanzibar ambae yuko bara atakubali kuacha kila kitu chake ili arudi kwao zanzibar, haiwezekani na haitawezekana. Sisi ni wamoja tayari (inseparable),

kaka yangu kaoa wazanzibar 2 na ana watoto 11 na dada yangu ameolewa na mzanzibar ana watoto 4 wote hawa wana nyumba na ardhi zanzibar na tanganyika. Wanajeshi wengi wako Zanzibar na wanazaa ovyo na wazanzibar ili kazi iendelee.

Hebu ona Rais Mwinyi shangazi zake wote ni watu wa bara mkoa wa Pwani lakini sasa hivi ni Rais wa Zanzibar,

Nyerere alikuwa na akili nyingi sana kuliko unavyodhani wewe, hakuna haraka.
 
Back
Top Bottom