Mkandara,
Ninaelewa adha ya kipengere cha usultani. Nilipomlinganisha na Banana nilikuwa natafuta figure ya kuonyesha kuwa alikuwa ni ceremonial, na wala hakuwa commander in chief. Najua kabisa kuwa position ya Banana na ya Sultani zilikuwa tofauti kabisa, lakini zote zilikuwa ceremonial.
Naelekwa kuwa katika mapambano ya uhuru ASP walikuwa na front mbili: kuondoa ukoloni wa mwingereza na kuondoa usultani, wakati ZNP walikuwa na lengo moja la kuondoa mwingereza tu na labda kuimarisha usultani. Kwa upande wake ZPPP ilikuwa na lengo moja tu la kuomwondoa mwingereza na kuiweka serikali mikononi mwa wazanzibari; swala la usultani halikuwamo kwenye ajenda yao: kwepo au kutokuwepo kwa sultani ilikuwa siyo tatizo kwao. Ndiyo maana Shamte alikuwa ASP na baada ya kuondoka na kuanzisha chama chake aliweza kuungana na ZNP.
Jamshid alikuwa raia wa Zanzibar kwa vile baba yake alizaliwa Zanzibar na yeye mwenyewe alizaliwa na kukulia Zanzibar. Ni kama Kennedy aliyezaliwa Marekani na baba yake pia alizaliwa Marekani lakini Babu yake alitoka Ireland.
Tukiachana na huo mlolongo wa koo za sultani, ninalotaka lieleweke ni kuwa mapinduzi yale yawe ni ya kumng'oa sultani au ya kuindoa serikali ya Shamte kutoka madarakani, hayakuwa halali.
Ni kweli usultani ulikuwa hauhitajikin tena katika Zanzibar huru, hata hivyo njia zilizotumiwa na ASP zilikuwa za kinyama sana na za kupinga demokrasi. Nimeifutilia historia ya harakati za uhuru wa Zanzibar kwa makini sana na kugundua kuwa kilichosababisha kifungu cha Sultani kubaki kwenye katiba ni failure ya ASP yenyewe kwenye mazungumzo yale ya katiba. Wangeweza kabisa kudai sultani uondolewe lakini madai yao yalikuwa vague sana, wao waling'ang'ania kutaka uchaguzi urudiwe tena na tena bila kweka madai ya msingi kama kugawanya majimbo ya ucahguzi kufuatana na idadi ya watu, na kuondokana na mamlaka ya usultani.