Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
Wanaotakiwa kudai serikali ya Tanganyika ni Watanganyika wenyewe na si Wazanzibar.

Wazanzibar wana haki ya kudai mambo mengine yote, hili la kudai serikali ya Tanganyika si lao wala hawatakiwi kuwa na uchungu nalo.

Mimi kama Mtanzania kutoka ilokuwa Tanganyika sijawahi kumwomba hata mzanzibari mmoja kunisemea ili kudai serikali ya Tanganyika.

Hoja hii ya baadhi ya Wazanzibari ni hoja ya kukemewa vikali, kwa sababu lengo lake ni kurudisha nyuma hoja nzima ya kujadiri kero za muungano ambazo wote tunajua zipo na kamwe hazitakaa ziondoke mpaka sisi Watanzania wenyewe tuweke makalio yetu chini na kuzijadiri kwa kina na kuzitolea ufumbuzi wa kisheria.

Wote tumechoka kukoromewa na watu wanaojifanya kutetea muungano kwa misuli yao bila kuweka akili zao katika utetezi.
Lakini hatuwezi vumilia vitendo vya kuvuruga mambo na kuingilia haki za watu wengine na kuleta madai ambayo kisheria wasemaji hawana uwezo wa kuajadiri.

Kama hoja ya kudai Zanzibar hruru isiyokuwa mshiriki wa Muungano wa Tanzania haiwezi simama kwa miguu yake yenyewe mpaka hoja ya kudai Tanganyika iwekwe mezani, basi hoja ya kudai Zanzibar haina nguvu na pengine itakufa kwa kujikaba yenyewe kuliko kuuawa na watu.

Labda tu kama kuna maana nyingine ambayo mtoa hoja anaweza kuianisha, Sivyo "Shut Up and Drive".


Kama tungekuwa na tabia ya mtu kujiamulia jambo linalomuhusu basi tungekuwa Wastaarabu lakini hili halipo na ndio maana Wazanzibari wnaamuwa kuwalisheni dawa ile ile mnayoitumia nyie YA KUINGILIA MAMBO YASIYOWAHUSU>
 
Wanaotakiwa kudai serikali ya Tanganyika ni Watanganyika wenyewe na si Wazanzibar.

Wazanzibar wana haki ya kudai mambo mengine yote, hili la kudai serikali ya Tanganyika si lao wala hawatakiwi kuwa na uchungu nalo.

Mimi kama Mtanzania kutoka ilokuwa Tanganyika sijawahi kumwomba hata mzanzibari mmoja kunisemea ili kudai serikali ya Tanganyika.

Hoja hii ya baadhi ya Wazanzibari ni hoja ya kukemewa vikali, kwa sababu lengo lake ni kurudisha nyuma hoja nzima ya kujadiri kero za muungano ambazo wote tunajua zipo na kamwe hazitakaa ziondoke mpaka sisi Watanzania wenyewe tuweke makalio yetu chini na kuzijadiri kwa kina na kuzitolea ufumbuzi wa kisheria.

Wote tumechoka kukoromewa na watu wanaojifanya kutetea muungano kwa misuli yao bila kuweka akili zao katika utetezi.
Lakini hatuwezi vumilia vitendo vya kuvuruga mambo na kuingilia haki za watu wengine na kuleta madai ambayo kisheria wasemaji hawana uwezo wa kuajadiri.

Kama hoja ya kudai Zanzibar hruru isiyokuwa mshiriki wa Muungano wa Tanzania haiwezi simama kwa miguu yake yenyewe mpaka hoja ya kudai Tanganyika iwekwe mezani, basi hoja ya kudai Zanzibar haina nguvu na pengine itakufa kwa kujikaba yenyewe kuliko kuuawa na watu.

Labda tu kama kuna maana nyingine ambayo mtoa hoja anaweza kuianisha, Sivyo "Shut Up and Drive".


Kama tungekuwa na tabia ya mtu kujiamulia jambo linalomuhusu basi tungekuwa Wastaarabu lakini hili halipo na ndio maana Wazanzibari wnaamuwa kuwalisheni dawa ile ile mnayoitumia nyie YA KUINGILIA MAMBO YASIYOWAHUSU>
 
Tee..hee.. hii yanikumbusha kwenye ndoa - hivi nani anatakiwa afungashe na kuondoka ? Anayeona hapendwi (anaonewa, hathaminiwi) au yule ambaye bado anapenda. Nafikiri hapa hakuna cha kuondoka mtu bali kuna wivu tu wa kutaka apendwe zaidi - wivu wa kike ? Nani tena huyu anataka kulitia doa penzi kati ya Tanganyika na kisiwa cha karafuu ?


Kwa utamaduni wa sasa kuna aina tatu za ndowa , mke na mume, dume na dume na mke na mke. Sijui ndowa hiyo ni aina gani kati ya hizi tatu?
 
Binafsi huwa sioni faida za hii ndoa, bora ivunjike tu, kwanza mizigo wanatubebesha, kaeneo kadogo kama mkoa mmoja wa bara, lakini kila kitu kanataka mgawo kama nchi kamili!

Ingekuwa mie talaka tatu ningetoa mara moja!


Unajuwa tatizo ni nini? Watu wa huko kwahala wamezowea kulisha na wanawake na ndio wanangangania.
 
Mkuu Madela Wa- Madilu hapa umemaliza. Ni ajabu Wazanzibar kudai bara wawe na Serikali inawahusu nini? Wenyewe tumeridhika na Serikali ya muungano kama nao wanatamani si wavunje SMZ ili tuwe na Serikali moja tu?


AT last mmekubali ukweli kuwa hakuna Serikali ya Muungano.
 
MOJA WAPO YA matatizo makubwa kule Zenj ni uvivu ulio kithiri.
Hawalimi maana wanasema si jadi yao ni ya WATWANA kulima.Kila aliyepo anataka kufanya biashara ya kununu bidhaa nje na kwenda KUUZA BARA.
Ardhi ya Zanzibar na Pemba , hasa Pemba ni nzuri mno kwa kilimo.Katika miaka ya 80 Mzee Kawawa alipo watembelea kule Pemba risala ilisomwa kuwa wanasikitika kuwa ski hizi(siku hizo) wanyamwezi hawaruhusiwi au wamepungua kuingia Zanzibar. Hivyo kilimo kimeathirika.Mzee Kwawa alishangaa sana na kuwa uliza kuwa , hivi nyinyi hamli mpaka mlimiwe.
Hiki ni kielelezo cha utegemezi kwa upande wa bara ambako vile vile kuna umaskini wa kutisha.Sasa ukimtegemea mtu/taifa jingine wakati wewe mwenyewe hujifanyii maendeleo yoyote ndio mwanzao wa kudai talaka kwa ajili ya kukosa matunzo.
Suala la kutenga na Zanzibar linaweza kuwa si suluisho la kudumu kwa matatizo ya Zanzibar maana baada ya matatizo haya ya reja reja bado kunatatizo kubwa sana la tofauti kubwa ya Zanzibar(mainisland) na Pemba.
Mimi nejihakikishia kuwa muungano ukivunjika leo wawili hawa hawaivi chungu kimoja.



Wabara je si Wavivu? Kwani kinachokuhamisheni vijijini na kujijaza mijini nini?
Huo uhodari wenu wa Kilimo mpaka sasa haujakutoweni katika kufa kwa njaa. Mko ndani ya Basi moja na Zanzibar angalau wao wana sababu kuwa hawapewi uhuru wa kufanya kazi zinazostahiki. Hivyo dhana yako kuwa maendeleo ya nchi zote yataletwa kwa kilimo? Hata hivyo kuna wakati Zanzibar iliwasaidia majirani wake kwa Fedha iliyotokana na Kilimo na sio kitu chengine.
 
Taabu kubwa Visiwani ni watu wavivu ktk kazi!!!

Kubwa Visiwani wanalojua ni Kulalamika tu na kuomba msaada!!!

Hivyo huo uvivu wao ndio uwafanye kuhama kwenu kwa makundi na kwenda kuweka kambi huko kwa kazi za vibaruwa na umachinga?
 
Jana usiku niliona yule waziri Khatibu akitoa maelezo kuhusu mafanikio ya muungano na jinsi walivyotatua kero za muungano katika channel ya TBC1. Ni mzanzibari huyu ambaye anasema kuna mafanikio makubwa katika kuuimarisha muungano. Wenzie wanasema uvunjike. Ni vurugu mechi tu maana wazanzibar hawautaki huu muungano. Nakubaliana na wanaosema ni muungano unaolazimishwa na viongozi wetu kwa maslahi yao. Ndiyo sababu kamwe wananchi hatutaruhusiwa kuamua kama tunauhitaji au vipi, au pia kama uboreshwe vipi?

WASALITI WAPO KILA PAHALA. Kweli una manufaa kwake na ndio maana hangatuki lakini safari hii itabidi ateuliwe maana jimboni hawako pamoja nae.
 

Hata Wabara hatuutaki, wanaong'ang'ania ni Viongozi ambao hawana vision hawataki kusikiliza maoni ya Wananchi na wanaung'ang'ania ili kulinda maslahi yao. Hakuna chochote ambacho Wabara tunafaidika kutokana na Muungano huo.


...Nakubaliana na wanaosema ni muungano unaolazimishwa na viongozi wetu kwa maslahi yao. Ndiyo sababu kamwe wananchi hatutaruhusiwa kuamua kama tunauhitaji au vipi, au pia kama uboreshwe vipi?

Mchukia Fisadi, Bubu Ataka Kusema, n.k.,

Mimi sioni ni vipi kiongozi wa Tanzania Bara, fisadi and such, anaweza kunufaika binafsi na Muungano. Kwa mfano kivipi, hebu nipeni nadharia moja. Nionavyo mimi, kama wewe ni kiongozi wa Tanzania bara, ungetaka huu muungano ufe, sababu moja ikiwa ni kwamba Wazanzibari wanamaliza Oxygen ya uongozi huku kwetu.

Wazanzibari tumewapa ki affirmative action fulani hivi, wanatengewa nafasi za uongozi lukuki wakati wanatoka kwenye kiwilaya kimoja tu, I mean, Unguja, Pemba zote (1660 sq. km) zinamezwa na Masasi (8,940 sq. km). zaidi ya mara tano. Lakini tunawapa V.P. wa muungano, mawaziri kibao, yani ni bwena, na wabunge lukuki wakati wanawakilisha watu kiduchu. Can't believe it, I mean, there are more Mtwarans than Zanzibaris. Sasa ni kwa nini waachwe wamalize Oxygen ya uongozi huku kwetu bara?


175px-Tanzania_Mtwara.png

 
Kama tungekuwa na tabia ya mtu kujiamulia jambo linalomuhusu basi tungekuwa Wastaarabu lakini hili halipo na ndio maana Wazanzibari wnaamuwa kuwalisheni dawa ile ile mnayoitumia nyie YA KUINGILIA MAMBO YASIYOWAHUSU>


Dawa mmetuandalia ili mtunyweshe sisi, lakini bahati mbaya mmeamua kuonja wenyewe kabla hamjatunywesha sasa mnapata maumivu ya bure. Tunywesheni basi hiyo ilobaki nasi tupate maumivu ili yatupe nguvu ya kudai Tanganyika.
 
kazi zenyewe zipo? nyinyi mkiletwa huku kuja kupiga kura na chama chenu cha Mafisadi hamrudi makwenu mnahamia kila pahala mnajipachika tu...........aaaaagh.

Kwani hakuna wazanzibari bara? wangapi wamehamia bara? na chama chetu cha mafisadi nyie mnaongozwa na chama gani? si mkitoe madarakani.
 
hivi vimkoa vidogo vinavyoongozwa na waziri asiye na wizara maalum, tabu tupu, vyeo wamepewa, hela wanapewa lakini basi tu...vurugumavi tu, kila saa...sijui wanataka nini sasa...mimi nadhani its time katiba katiba and lets call a spade a spade na karume awe mkuu wa mkoa etc, kama wao wanavyokula umeme wa bara (bila kulipa), basi mafuta yao nao yetu wote...hamna arguments hapo,
 
Kulingana na matangazo ya moja kwa moja ITV ya sherehe za Muungano uwanja wa Uhuru Jijini Dar Es Salaam. Hadi sasa sherehe hazijaanza rasmi. Watu wanakula Burdani ya Muziki wa wana Msondongoma. Rais kashindwa kuja Uwanjani wakimsubiri Rais wa Zanzibar aje Dar tokea Zanzibar.

Hali ya Hewa imezuia Ndege iloenda kumchukua kushindwa kutua DIA.

Sijui itakuwaje kama hiyo hali ya hewa ikisusa kuruhusu hiyo ndege kutua.

Helikopta inaonekana ikikatisha kucheki hali ya hewa.

Hii ya leo kali

Naomba kuwakilikisha
 
Hali ya Hewa imezuia Ndege iloenda kumchukua kushindwa kutua DIA.


Helikopta inaonekana ikikatisha kucheki hali ya hewa.

Hii ya leo kali

Naomba kuwakilikisha

Kwa hiyo helikopta inakagua hali ya hewa eeh? Na DIA ndege haiwezi kutua kwa kuwa hali ya hewa mbaya?

Mkuu, Unawakilisha, au unawasilisha? Unawakilisha nini au nani?
 
Wee pata ujumbe tu wa hali halisi ya maendeleo ya sherehe za Muungano, ukianzisha lugha za ubishi utabishana mwenyewe
 
Sasa keshaingia uwanjani makamu wa Rais, na anaesubiriwa ni Rais Kikwete. Bila shaka Rais Karume karudi Zanzibar juu kwa juu
 
ukweli uliopo, jamaa wa CUF, wamewawin CCM kwa hili, lakini agenda ya CUF siku zote ni ubaguzi tu japokuwa wanauficha, lengo na madhumuni makubwa ya wana CUF ni kuchukua Pemba na kisha kujirudisha kwa sultan wao wa Oman, kwani sidhani kabisa kwamba hawa jamaa wanajiona ni waswahili, na ni ukweli usiofichika kama hawa jamaa wakijitenga hata mwaka haufiki Pemba na Unguja nazo zitajitenga
 
Tayari Rais Kikwete kaingia uwanjani. Mshereheshaji hajaeleza bado kilichosibu hadi viogozi hawa wakuu wa juu kuamua kuendelea na hii shughuli bila ya Mwenzao wa Zanzibar kuwepo.
 
Back
Top Bottom