Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
Naam sasa haya maneno, Salim A. salim kawafumbua macho!
Hakuna kibaraka mkubwa wa CCM kama huyo Salimu japo alipigwa na chini katika kuutaka uraisi lakini bado ni mwandamizi katika safu ya CCM hana jipya ,huyo katika mauaji yaliofanywa dhidi ya jamaa zake kule Pemba hakusema hata kwinn'yoo na mpaka hii leo hata hajagusia ,sasa awache kujikomba baada ya kuona kuwa kuna mambo yameanza kuingia sura abakie huko huko kwa wanyarugusu wenzake ,huyo hafai kabisa tena hana msaada wa aina yeyote yeye yupo tu kulinda maslahi binafsi na si ya waTz ,hivi muulizeni aliifanyia nini Tz alipokuwa kiongozi pale UN na hata AU ,hana hata moja muoneneni hivyo hivyo ,hutatua mambo kwa nguvu za wengine.Unajua kuna watu wana bahati au wanabahatika basi yeye ni mmoja wao.
 
Hakuna kibaraka mkubwa wa CCM kama huyo Salimu japo alipigwa na chini katika kuutaka uraisi lakini bado ni mwandamizi katika safu ya CCM hana jipya ,huyo katika mauaji yaliofanywa dhidi ya jamaa zake kule Pemba hakusema hata kwinn'yoo na mpaka hii leo hata hajagusia ,sasa awache kujikomba baada ya kuona kuwa kuna mambo yameanza kuingia sura abakie huko huko kwa wanyarugusu wenzake ,huyo hafai kabisa tena hana msaada wa aina yeyote yeye yupo tu kulinda maslahi binafsi na si ya waTz ,hivi muulizeni aliifanyia nini Tz alipokuwa kiongozi pale UN na hata AU ,hana hata moja muoneneni hivyo hivyo ,hutatua mambo kwa nguvu za wengine.Unajua kuna watu wana bahati au wanabahatika basi yeye ni mmoja wao.
Ulitaka awafanyie nini? wewe, yeye alikuwa UN amefanya kazi nzuri huko UN kwa mujibu na misingi ya UN hiyo inatosha na tunajivunia hilo watanzania wote acha upuuzi wewe.
 
Huu ni mchezo munatuchezea. Sisi wazanzibari hatuutmbui MUungano wa Karume na Nyerere maana ilikuwa ni muungano wa kuburuzana na mpaka sasa munaendelea kuiburuza Zanzibar. Tunachokitaka ni UHURU wetu. Ukoloni wa waingereza umefuatiwa na ukoloni wa MUAFRIKA. Ukoloni wa Muafrika ni mbaya zaidi. Iko haja mutuachie nchi yetu. Hakuna sababu za muungano.
 
I was born a Tanzania and I hope to die a Tanzanian one day. I hope our union can survive. But I also believe that our brothers and sisters have a right to choose which path they want to take. Kama watu mnataka kusolve matatizo ya muungano tuyasolve kama watu hamtaki kuya tatua matatizo na maneno yenu ya kwanza ni tutengane then so be it. Maana naona sasa huku kutishiana kutengana kimekua kamchezo watu wanacho tumia kujipatia wanacho taka. Nchi isiendeshwe kitoto, mambo ya kubembelezana ya nini? You either want the union or not.
 
Wengi wa Wazanzibari wasio taka Muungano ni wale ambao kwa namna moja au nyingine wanamakazi nje ya Visiwa hivyo au ndugu au jamaa zao wanamakazi ya kudumu nje. Kundi hilo hujiona kama wazanzibari wa daraja la kwanza.

Lakini kwa wazanzibar walio wengi ambao ni akina sisi tunaoitwa 'magolo'; 'chogo'; wamrima nk, maisha yetu na future yetu haina wingu zito kwa sababu ya kuwepo kwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Laiti kama Muungano unavunjika leo hii basi wingu zito litatanda juu ya hatma yetu ya baadae. Kimsingi wengi wa wazanzibar asili yao ni nchi za bara kwahiyo kuwa na Muungano ni jambo jema kwani linatuunganisha na ndugu zetu wa damu, hatuna haja ya kuchukiana.

Halafu mimi huwa ninajiuliza hivi kama hatutaki muungano huko bara tunakokwenda kila baada ya nusu saa tunafuata nini?

Kama hatutaki Muungano hayo maduka na biashara zingiine tunazozifungua kula kukicha huko bara ni za nini?

Muungano hatuupendi lakini bara tunakupenda, ya kweli hayo?
Kila kona ukienda ya bara wazanzibari wamejaa na wala hatuulizwi tumefutata nini, tunafanya mabiashara mengi mengi tu.

Ah, wasiotaka Muungano hawatutakii mema sisi wananchi wa kawaida, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni muungana wa watu wenyewe ni lazima uendelee kudumu na kuimarishwa zaidi na zaidi.
 
Wana JF, wapi naweza kupata huo mkataba wa mungano, kati ya Tanganyika na unguja ?
 
Mwezi wa nne kulikuwapo na mjadara wa suala la muungano katika TBC1. Juma Duni peke yake ndiye alionekana kupingana na wenzake na kusema tume nyingi zimeundwa bila kuzaa matunda yoyote ya maana. Akina prof. Rwaitama (ambaye sikuona uprof wake) walimbeza sana. Khatibu pamoja na kutaka kumpinga alijikuta akikubali bila kujua kwa kutaja tume nyingi zilizoundwa na hakuonyesha matokeo ya tume hizo.
Mama mmoja mwanasheria alijikanyaga sana baada ya kuanza vizuri; nadhani aliogopa waliomzunguka.
Sasa kama huu ndio msimamo wa wawakilishi wa wananchi wote wa zanzibar bila kujali uvyama wao, (maana wanawakilisha mawazo ya wananchi) je Prof. Rwaitama na mwenzio Khatibu mnasimama wapi?
Siku nyingine mkiitwa kwenye mijadara muwe wakweli kama Duni, muache unafiki!

"Re: Karume amekacha sherehe za Muungano?

--------------------------------------------------------------------------------

Niliangalia majadiliano juu ya Muungano yaliyorushwa TBC. Inaonekana kama Duni asingekuwapo, mjadala usingekuwepo pia, maana wote kwa upofu wao walionekana kumshupalia yeye.
Yule mama mwanasheria alinza vizuri baadae akaonyesha woga na kushindwa kutetea hoja zake za awali akabaki kuchekacheka tu.
Hoja aliyoizungumza mwanzo kwamba- kuwe na bajeti tatu: Bajeti ya Zanzibar, Bajeti ya Seriakali ya Muungano kwa mambo ya Muungano, na bajeti ya serikali ya muungano kwa mambo yasiyokuwa ya muungano. Yaani serikali ya muungano iwe na bajeti mbili kwa kuwa inatekeleza mambo ya muungano na yasiyokuwa ya muungano (ya Tanganyika).
Hii ilikuwa approach nzuri, lakini baadae akawa mwoga tu.
Profesa Lwaitama alikuwa kama kituko fulani hivi, alibalia kucheka tu akidhani anazungumza hoja kumbe upuuzi mtupu."

--------------------------------------------------------------------------------
 
Last edited:
Tunaomba ukumbushe jamvini. Ni maoni gani hayo unayoyaita wewe kuwa yana hekima- kuhusiana na mada hii ya Muungano na mustakbala wa Zanzibar na Wazanzibari wake.
1.Maoni ya Mh. Aboud Jumbe Mwinyi, Rais mtaafu wa heshima Zanzibar, ambaye yy alishuhudia mchakato mzima wa kuundwa muungano huu kifisadi fisadi, na anaujuwa nje ndani kuliko mtu yeyote yule kwa kuwa yy alikuwa mshauri No.1 wa Mzee Karume wakati muungano huo ulipo asisiwa.
2. Maoni ya tume mbalimbali zilizoundwa kwa gharama na fedha za wavuja jasho mfano hasa tume ya Jaji R. Kisanga ya " white paper" akaambiwa na Mh.Mkapa(fisadi,Muuwaji) kuwa "mambo ya serikali tatu hayamuhusu (kisanga)"
3. Maoni ya wananchi na makundi mbalimbali ya kijamii, hapa nitai refer ile G55, kwa kuwa walikuwa ni wabunge wa wananchi wa Tanganyika hivyo waliwakilisha maoni na maono ya wananchi wao n.k
 
kwa mana hiyo Mheshimiwa Khatib anasema watoto wa wakwezi na wakulima hawana serekali hapa zanzibar ,serekali ni ile iliyopokule TZbara akiwa yeye binafsi waziri wa mungano kwa tafsi nyingine ya hapa kwetu visiwani wanaotuongoza ni sawa na wapiga DUMBAKI hawa washi na wala hawazimi ,lakini juu ya yote hayo naimani kaka zetu SMZ watamjibu Mh Khatibu .
 
Hivi hawa wazenji wanatafuta nini hasa na hizi chokochoko za muungano? Mi binafsi sioni cha maana tunachovumilia kwa wenzetu wa visiwa labda watoto wazuri wa kiarabu na kimakunduchi....najua fitna zote hizi kuna mkono wa kisiasa kutoka upande wa pili maana njia pekee ya kuitawala zenji ni kwa kuing'oa CCM ambayo msingi wake mkuu ni huku Bara.

Mi namshauri Maalim na chama chake wafanye petition kujua ni wazenji wangapi hawautaki muungano na wangapi wanauta halafu tuanzie hapo badala kuwasemea watu wazima kwa kofia ya uanasiasa. Inasikitisha ukienda visiwani humo na ukajulikana wewe ni unatoka Bara yaani unaweza hata usipewe maji ya kunywa jinsi utakavyobaguliwa. Sasa kuna faida gani kama watu wenyewe wanafikia hatua hii. WAPENI WANACHOTAKA BWANA KWANINI KUNA NINI...eboooo!!
 
Hivi hawa wazenji wanatafuta nini hasa na hizi chokochoko za muungano? Mi binafsi sioni cha maana tunachovumilia kwa wenzetu wa visiwa labda watoto wazuri wa kiarabu na kimakunduchi...
Poa moto kaka. Kwa watoto tu. Hata sisi tumemwaga manyanga kwa watoto wazuri wa Kichaga. Kina -Mwaya wa kule Tanga, Wale wa Buharamulo (shingo kuliko Twiga) bila ya kusahau vitoto vya kimachinga, hujaja Kwa - Wa-Rangi wala hujapitia Mbeya na Iringa hapo !!. Kwa watoto tu tunahitajiana Kaka. Na nafikiri kwa hilo Muungano udumu.
 
Poa moto kaka. Kwa watoto tu. Hata sisi tumemwaga manyanga kwa watoto wazuri wa Kichaga. Kina -Mwaya wa kule Tanga, Wale wa Buharamulo (shingo kuliko Twiga) bila ya kusahau vitoto vya kimachinga, hujaja Kwa - Wa-Rangi wala hujapitia Mbeya na Iringa hapo !!. Kwa watoto tu tunahitajiana Kaka. Na nafikiri kwa hilo Muungano udumu.

Kaka tatizo nyie mnabana kuliko siye huku...mimi mwenyewe nimepigwa chini kupewa mke wa kiarabu pale pemba eti kisa mi Mbara...bora ningekuwa wa huko. Hebu uona mwenyewe uonevu huu. Mtu unapenda tena uzuri watoto wa huko bwana wengi bado wapya, hapa nchi kavu kumkuta mtoto bikra ni zaidi ya kuokota lulu bwawani....sasa harahara tuvumiliane na kwingine jamani eeheee
 
1.Maoni ya Mh. Aboud Jumbe Mwinyi, Rais mtaafu wa heshima Zanzibar, ambaye yy alishuhudia mchakato mzima wa kuundwa muungano huu kifisadi fisadi, na anaujuwa nje ndani kuliko mtu yeyote yule kwa kuwa yy alikuwa mshauri No.1 wa Mzee Karume wakati muungano huo ulipo asisiwa.
2. Maoni ya tume mbalimbali zilizoundwa kwa gharama na fedha za wavuja jasho mfano hasa tume ya Jaji R. Kisanga ya " white paper" akaambiwa na Mh.Mkapa(fisadi,Muuwaji) kuwa "mambo ya serikali tatu hayamuhusu (kisanga)"
3. Maoni ya wananchi na makundi mbalimbali ya kijamii, hapa nitai refer ile G55, kwa kuwa walikuwa ni wabunge wa wananchi wa Tanganyika hivyo waliwakilisha maoni na maono ya wananchi wao n.k
Tatizo lenu Wazanzibari hamueleweki ni nini hasa mnahitaji katika Muungano. nafikiri inabidi mujipange na kutoka na msimamo mmoja. Junius ndugu yangu Serikali zinaweza zikawa tatu. Ikawepo na ya Tanganyika. Lakini katika hali ya sasa hiyo ya Tanganyika inaweza kuimeza ya Tanzania na SMZ ikabaki pale pale (underdog). Huo mdidimizo mnaofanyiwa hivi sasa si utaendelea tu. Fikirini vizuri wa Zenj. Daini la msingi badala ya kukakatiza tatu tu.
 
Inasikitisha ukienda visiwani humo na ukajulikana wewe ni unatoka Bara yaani unaweza hata usipewe maji ya kunywa jinsi utakavyobaguliwa. Sasa kuna faida gani kama watu wenyewe wanafikia hatua hii. WAPENI WANACHOTAKA BWANA KWANINI KUNA NINI...eboooo!!
Ukitaka kumjuwa mtu aliekosa malezi ya baba yake na mama yake kama wewe(nahakika unamalezi ya gengini au pwani kwa wabeba mizigo kama hutokea Namamnga au Unyaturuni) utamjuwa kwa kauli zake za kiutovu wa adabu na kukosa heshima kwa watu waungwana na wastaarabu.
Huo uwongo wako na unafiki,ukome kuusemea hapa JF penye watu wastaarabu na waungwana, Zanzibar haina historia ya kuwa na watu wenye roho mbaya za kufika kumnyima mgeni yeyote chakula seuze maji yanayopatikana bure(siku hizi CCM ndo wanayauza),sifa ya ukarimu na huruma ya watu wa visiwani si suala la mjadala, hiyo ni sehemu ya utajiri katika historia ya watu wa visiwani waliolelewa ktika maadili ya dini ya Kiislamu wanayoamini kuwa kumkarimu mtu si sifa bali ni thawabu na unapata fungu kwa Mw'mungu. Na ndo maana watu kutoka mataifa mbalimbali wanawapenda watu wa visiwani kwa sifa yao ya ukarimu bila ya kudai malipo, na kadhalika ndo pakasemwa kuwa ZANZIBAR NI NYEMA ATAKAYE AJE.na nyinyi wabara ndo mkaja kujazana tele huku eti mnauza nyungo, kahawa na njugu, mbaya zaidi baadhi yenu mnakuja kuharibu utamaduni wa kukarimiana kwa kutuletea mambo ya utapeli,ujambazi na umalaya.
 
seuze maji yanayopatikana bure(siku hizi CCM ndo wanayauza)
Junius CCM hawayauzi Ndugu yangu. Acha hiyo. Kuna sera tu ya kuchangia gharama za maji safi, elimu, afya. Kwani wakati ule wa Ukoloni Wazee wetu si walikuwa wakilipa Shilingi Tatu (fixed rate) kwa ajili ya maji Mjini Zanzibar?
 
Tatizo lenu Wazanzibari hamueleweki ni nini hasa mnahitaji katika Muungano. nafikiri inabidi mujipange na kutoka na msimamo mmoja. Junius ndugu yangu Serikali zinaweza zikawa tatu. Ikawepo na ya Tanganyika. Lakini katika hali ya sasa hiyo ya Tanganyika inaweza kuimeza ya Tanzania na SMZ ikabaki pale pale (underdog). Huo mdidimizo mnaofanyiwa hivi sasa si utaendelea tu. Fikirini vizuri wa Zenj. Daini la msingi badala ya kukakatiza tatu tu.
Nafikiri walichokieleza waheshimiwa wabunge kipo wazi(japo wabunge wa CCM zanzibar, wamesema kiwogawoga,lakini wamesema) na msimamo wa Wazanzibar unaeleweka kuwa Muungano wa serikali mbili hautufai na moja hatuitaki, zilizobakia zinawezekena tukikubaliana.
kama ndo lazima tuungane basi tuungane katika muungano muafaka na si wa mashaka.Bado si rule out workability ya muungano wa serikali tatu(shirikisho)muundo ambao unafanya kazi vuzuri katika mataifa kadhaa duniani.
 
Pakacha si mtu wa Zanzibar inawezekana umepata uraia kwa kuja kuisaidia kura CCM ,siku hizi hata wamasai ni Wazanzibari ,mmesahau ule msemo wa .All Zanzibarians are Tanzanian but not all Tanzanianz are Zanzibariz.
Where are Tanganyikans ? Nimegundua wanaona aibu kuitwa mTanganyika, mi huku Ulaya nikiulizwa nasema ni Mzanzibar ,hakuna chogo aneulizwa akasema mi ni Mtanganyika ila sio ajabu maana hata baazi ya Wapemba wanaona tabu kusema wanatoka Pemba ila mimi najua kama mi sikubali nasema natokea natokea Pemba ,Chanja-n'jawiri 😀
 
Nafikiri walichokieleza waheshimiwa wabunge kipo wazi(japo wabunge wa CCM zanzibar, wamesema kiwogawoga,lakini wamesema) na msimamo wa Wazanzibar unaeleweka kuwa Muungano wa serikali mbili hautufai na moja hatuitaki, zilizobakia zinawezekena tukikubaliana.
kama ndo lazima tuungane basi tuungane katika muungano muafaka na si wa mashaka.Bado si rule out workability ya muungano wa serikali tatu(shirikisho)muundo ambao unafanya kazi vuzuri katika mataifa kadhaa duniani.
Tatizo unaweza kuambiwa Zanzibar una Serikali yako. Junius utaridhika almradi tu zipo tatu- na Tanganyika wanayo yao. Hapana? Junius kama tunasema Zanzibar ina Serikali yake- basi hiyo Serikali iwe kweli Serikali- iwe na meno Ndugu yangu , isibanwe, Iwe huria. Ijitanue- kwa mujibu wa Katiba na sakafa za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Junius haya ndio ya kupigania. Na haya hayapo hivi sasa. Tunapuyanga tu.
 
Back
Top Bottom