Wote tu ndugu yangu, huyo Kikwete na Pinda aliyekuwa mbele hajulikani. Nchi yetu kwa sasa ina pengo kubwa sana la viongozi na sijui kama tutaweza kulirekebisha hili katika uchaguzi ujao 2010.

Si rahisi kulirekebisha hili kwani viongozi tulionao ndio kioo cha Wtz tulivyo yeyote atayekuja hali itakuwa hivi hivi kwa vile tunavuna tulichopanda.
 
 
Uhaini hauwezi kufanyika lakini Mapinduzi nina hakika yanawezekana kabisa kufanyika ,na kama atatokea mtu kusema Uhaini na mapinduzi ni kitu kimoja basi hawa wahafidhina wote na Chama Chao ni Wahaini kwani Serikali waliyoipindua sio ya Muarabu ni Serikali ya Wazalendo waliopata Uhuru na kumbukumbu zipo sherehe zipo.
Ila sikubali kabisa kama Zanzibar kwa hapa tulipo inaweza kujiita Nchi , nafahamu kuwa Zanzibar wanae Raisi na bendera yake na wimbo wake wa Taifa ,la kujiuliza ni lini na ni wapi Raisi wao alifanya ziara ,hilo moja jingine kama aliwahi kufanya ziara je huko alikofikia alipokelewa kama nani ? Tatu Je alipigiwa wimbo wa Taifa ,Nne Je gari aliyoipanda ilipachikwa nembo ya Raisi wa Zanzibar ,weka kando yote hayo Je ilibandikwa bendera ya Tanzania ? Sasa kama yote hayo hayakufanyika kuna tofauti gani na Mkuu wa Mkoa anaekwenda kuztembea Ulaya ?
Zanzibar ni mkoa unaojitawala wenyewe Ndani ya Utawala wa mkoloni Tanganyika so far Wapemba wameanza kudai uhuru upya.
 
Nimetahayari na kufedheheshwa sana na haya Matamshi yako.

Unajua mtu mzima dawa lakini wengine wanaweza kuwa maradhi na ndivyo tunavyowaona wazee wa CCM au Wahafidhina wa Unguja jinsi wanavyodhalilishwa na purukushani hizi zote ujue wamebanwa sasa wanaanzisha uzushi ili wawatishe waTanganyika ,sijui kuna jambo gani ila ukiona hivi basi karibu watatoa kauli yao ya basi turudishieni ASP yetu ,kwa taarifa yenu tu Kikwete atawabinya mpaka mseme mmekoma ,si mnajidai ujuba basi ndio kwanza dawa yenu inachemshwa na ASP hamrudishiwi n'ngo , kama mna mbavu zaidi ya WaPemba basi tuwasikie na nyie hapo Unguja mnadai ASP kwa sauti na sio mdai bali muamke na kusema CCM haipo tena Unguja iliyokuwepo ni ASP imerudi upya CCM mwisho Chumbe ,WaPemba wameonyesha uanaume na wametamka mchana kweupe kama ukiritimba wa Wahafidhina hautakomeshwa basi CCM na wahafidhina wao mwisho Nungwi.
 
Kuna thread imewekwa hapa leo ambapo Pinda alikuwa akitoa ufafanuzi kuhusu kauri yake ile. Isomeni muone kama kweli alikosea katika kauli yake?
 
Mimi nafikiri hapa watu (Mh.Pinda na huyo mwanasheria) wanajaribu kutikisa mbawa tu bila sababu za msingi.

Zanzibar ilikuwa ni koloni la Muingereza. Mzungu akaona awashauri Hayati Mwalimu na Hayati Abedi Karume RIP (kwa sababu zake muingereza) kwamba itakuwa ni vema kama Zanzibar itakuwa sehemu ya Tanganyika kiutawala.

Sasa naomba nigusie kidoogo kuhusu mfano wa Scotland ambao mkuu Mkandara umegusia pia.

Scotland au Kingdom of Scotland kabla ya kuungana na United Kingodm ilikuwa ni "state" inayojitegemea ikiwa inajiendeshea mambo yake.

Kwa ushauri wa utawala wa kiingereza (kingdom of England) wakaona waungane kisiasa na ndio ikazaliwa United kingdom of Great Britain. Lakini nao pia waliweka "Treaty" au mkataba wa Muungano na baadae wakaufanya sheria au "Acts of Union" (sisi twaita Articles of Union) na ukapitishwa na mabunge ya sehemu zote Scotland na Great Britain.

Ila kwa upande wa Sotland walipinga sana jambo hili lakini likapitishwa. Scotland inafuata sheria zake zinazotungwa na wa-Scotish wenyewe na ni tofauti kabisa na sheria za Uingereza, Wales na Northern Ireland. Pia wana mfumo wao wa elimu,utamaduni na utaifa (identity).

Lakini Scotland sio "sovereign state" na iko chini ya United Kingdom of Great Britain , Wales na Northen Ireland na wameweka hata katika pasi yao ya kusafiria.

Lakini point yangu hapa ni pale kwamba "Articles" au "Acts" za muungano wa Scotland na Uingereza zilipitishwa na mabunge na sio watu wachache kujadili na kutia saini kama ambavyo mzozo huu wa Zanzibar unavyokuja.

Kwa hio basi naona kwamba Waziri Mkuu Pinda hajakosea kwa kusema kwamba sawa, Zanzibar ni nchi (country) ndani ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Na Zanzibar sio "sovereign state" kwani itakuwa ni nje ya "Articles of Union".

Muungano wa Zanzibar na Tanganyika ulipaswa kujadiliwa upya bungeni kama mkoloni alivyofanya huko kwake na watu wote wakubali kwamba kuwe na muunganio au usiwepo, na kama ukiwepo ni kwa faida ya nani, kiusalama, kiutamaduni,kisheria au nini?

Naomba kutoa hoja.
 
Ndugu wana taaluma wa JF, nilikua natafakari kwa muda mrefu na pia hasa wakati huu ambapo kuna malumbano kama Zanzibar ni Nchi au sio Nchi. Leo hii Sijapata ufumbuzi wowote kuhusu swala hili, naombeni michango yenu ya dhati ili mwisho wa siku kila mmoja wetu tuelewe ni nani yuko sahihi kisheria, kisiasa na pia kiuchumi. Je Zanzibar ni Nchi au Sio Nchi?

Kuna utatata wa hali ya juu, kwa mfano mtu anaposema sio nchi je inakuwaje kuna serekali ambayo inaongozwa na Rais (Serikali ya Mapinduzi ya Zanziba), je kuna sehemu yeyote duniani ina serikali lakini sio Nchi? Kuna bunge la Mapinduzi, kuna budget yake peke yake, kuna maamuzi yake peke yake, kuna kukusanywa kodi, Je hivi vyote na vingezo vinginevyo vinaweza kutupa dira kua Zanzibar sio nchi?

Naomba Kutoa hoja
 
Nionavyo mimi huu Muungano wetu ni muungano wa kukidhi haja iliyokuwepo Baada ya Mapinduzi ya Zanzibar. Waasisi wa Muungano huu walifanya Muungano kwa malengo mawili tofauti. Kwa upande wa Karume alikubali Muungano kwa kutaka usalama wa Dola yake na Nyerere alitaka Muungano akitekeleza ndoto yake ya Kuunganisha Afrika. Kilichotokea ni kuwa hawakuwa makini na namna ya Muungano huo na ndio kinachosababisha matatizo ya sasa hivi.
Laiti kungekuwepo na mfumo unaotambulika wa muungano basi matatizo haya yasingekuwepo. Kinachofanyika sasa ni kusukumana na kutoleana vitisho na kejeli. Iwapo chombo kama Baraza la Wawakilishi kinaonyesha kutoridhishwa na kauli ya Waziri Mkuu hii si dalili tosha kuwa hapa yapo matatizo. Kwa bahati nzuri waasisi hawa hawakusahau kufikiria kutokea tatizo kama hili la sasa na wakaweka utaratibu wa kupatikana ufumbuz na utaratibu huo ndio njia muafaka ya kutatua utata huu.
Iwapo kinachodaiwa na Zanzibar ni uendeleaji wa mfumo ambao Karume na Nyerere waliutekeleza na upande wa pili hautaki kuukubali kwa maneno lakini wanauachilia kuendelea hapa lipo tatizo. Tangu wakati wa Karume Zanzibar ilikuwa na kila kitu chake na ikijitegemea kwa kila hali hata kuwa na Central Bank yake, bendera yake , Rais wake na Katiba yake(Katiba ambayo hivi sasa Waziri Mkuu anasema inawakanganya Wazanzibari) kulishawahi kuhukumiwa watu kwa kesi ya Uhaini na Waliohukumiwa vifo wakanyongwa na waliotumikia vifungo walifanya hivyo(Suala la kukataliwa uhaini limekuwa kigezo kukosekana kwa sifa ya nchi hivi sasa), Viongozi wa nchi za kigeni wakipigiwa Mizinga ya kukaribishwa na kuagwa iwapo wanamalizia ziara zao Zanzibar na juu ya hilo Zanzibar ilishawahi kutowa misaada kwenda nchi za nje (mfano Kenya) wakati Zanzibar ilipokuwa tajiri.
Haya yote yakitendeka wakati Nyerere akiwa madarakani na hakuwahi kutowa kauli ya kuyapinga na mengi kati ya haya yanaendelea kufanyika, sasa tatizo nini? Lazima tukubali kuwa Muungano wetu ni mfano kwa uzuri na pia kwa mkanganyiko. Ni mazowea yetu ya kujifanyia mambo yetu kitofauti na mifumo inayoeleweka na kuwa na taratibu zake na ndio maana hat ujamaa wetu ulikuwa wa mfano wa kipekee duniani.
Kilichobaki tukae chini kindugu na tuujadili namna ya utaratibu mzuri wa Muungano wetu kutumia mabavu kwa ajili ya ukubwa na utajiri si suluhisho. Binaadamu atafanya kila liwalo apate haki yake na tuone Mifano ya Russia,Canada,na wa karibuni huu wa Belgium(hatukutegemea mambo kama haya kutokea nchi kama Belgium.
VIVA MUUNGANO NA SIO UTAWALA WA TAIFA MOJA KWA JENGINE
 

Muungano wowote ule wa hiyari wa pande tofauti ni kwa ajili ya kukidhi haja, matakwa na malengo ya kuzinufaisha pande hizo. Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hauna tofauti yoyote.


Kelele na maneno ya kejeli kutoka pande zote na hususani visiwani ndivyo vinavyosababisha mpaka Watanganyika waanze kuujadili na kuufikiria huu muungano. Watanganyika wengi wanaona kama vile wanalazimisha ndoa/penzi au kama vile wanakuwa "mabuzi" katika muungano huu.

Mimi kama Mtanganyika ningependa kujua hasa kwanini nchi hii ina serikali zaidi ya moja hususani ukizingatia ya kwamba serikali nyingine ni kwa ajili ya eneo ambalo ni sehemu ya nchi iitwayo Tanzania.Hiki ni kipengele kimoja cha terms za muungano chenye kuhitaji ufafanuzi wa hali ya juu kwangu mimi binafsi.
 
Nipo Zanzibar, hivi punde nimetoka kwenye mkutano wa hadhara uliohutubiwa na katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Dharif Hamad. Ajenda kuu ilikuwa kauli iliyozua mjadala ya Pinda kuwa Zanzibar si nchi.
Maalim amemtaka Pinda awaombe radhi wazanzibari hadharani kwa kauli hiyo ambayo imewahuzunisha, kuwakwaza na kuwafadgaisha wazanznibari wote.
Lakini kikubwa, Maalim ameitumia kauli hiyo ya Pinda kuonyesha kuwa muungano wa sasa unaendeshwa kwa hila za kutaka kuiua Zanzibar. Anasema hili lilianza tangu awali na lilianzishwa na Nyerere ambaye alionyesha kuichukia Zanzibar tangu mwanzo.
Amesema Nyerere alitumia ghilba kumshawishi Karume (Original) akubali Muungano na alipokataa alimtishia kuwa ataondoa askari wake.
Kwa kuwa nchi ilikuwa changa (siku chache baada ya mapinduzi) karume alikubali lakini kwa sharti kwua Zanzibar iendelee kuwa nchi.
Maalim Seif anasema lakini hila za kuiua Zanzibar zilianza wakati huo na ndio maala masuala ya Muungano yameongezeka kutoka 11 ya awali hadi 23 hivi sasa.
Anasema kuongezeka kwa masuala ya muungano kunamaanisha kupungua kwa madaraka ya Zanzibar na hilo haliwezi kukubalika.
Amemtaka Shamsi Vuai kutangaza katika Baraza la Wawakilishi kuwa Zanzibar ni nchi na hiyo itasababisha kuwepo kwa mgororo wa kikatiba. Ameitaka SMZ itangaze mgogoro huo wa kikatiba na CUF itaiunga mkono.
 
Narudia Maalimu Seif hana tofauti na Marehemu. Jonas Savimbi... Jambo kama hili linahitaji subira... litnahitaji kutatuliwa kwa utaratibu sio la kuleta hamasa kubwa kutoka kwa wananchi lazima ajue wananchi wana uelewa tofauti.

Haya imeshakuwa ajenda ya uchaguzi wa mwaka 2010 ya CUF hiyo,
 
Nafikiri muda si mrefu tutakaa pazuri. mafisadi bado linapamba moto sasa la zanzibar laja, kwani siku zote walikuwa hawajui kuwa si nchi mbona wanakuja kuanza sasa?
 

Mimi nasema na kusisitiza kuwa Zanzibar ni nchi kwa sababu zifuatazo:

1. Ina Raisi
2. Ina baraza la wawakilishi
3. Inayo mahakama
4. Siyo mkoa bali ina mikoa na watendaji wake huteuliwa na raisi wake
5. Ina kiongozi wa serikali ndani ya baraza
6. Uchaguzi mkuu wa raisi na wawakilishi hufanyika kila baada ya miaka mitano na kuapishwa kama katiba yake inavyoelezea.
7. Inayo wimbo wake wa Taifa

Sana kama hayo yote hayatoshi kuitwa nchi, nchi ni nini.
 

Kelele za vyura bwawani. Kila mtu changu, changu! Iwe nchi, iwe taifa, iwe nini. Cha msingi ni mamlaka gani unayo kwa muundo upi. Wilaya yenye mamlaka na muundo mzuri wa kuleta maendeleo ni ya maana zaidi kuliko nchi au taifa lisilo kuwa na mamlaka yoyote na muundo kiini macho. Hapa dawa ni Wazanzibar tupewe Zanzibar yetu, wadanganyika wapewa Tanganyika yao halafu tukutane katikati kwenye shirikisho la Tanzania. Kama CCM hamtaki na bazara letu na mapinduzi na kamati kuu yenu basi tuunde Shirikisho la MAJIMBO tu hapo.

Asha
 
Nadhani Zanzibar ni kama zile US wanaita states ambazo zina utawala wao chini ya magavana, zinatunga hata sheria zao, zinakusanya hata kodi, na bado si nchi. Ziko katika muungano.
Muungano wetu wakuu umeshathibitishwa kuwa na mapungufu mengi katika kuu practice na viongozi wetu walishalikili hili.
Ndio sababu muungwana kaunda mara wizara mara kamati na kadhalika ili kuona ana mend shida iliyopo. Hata hivyo matatizo ni mengi kiasi kwamba iko wazi tunaitaji KATIBA MPYA.
 

Umeona jinsi swala zima lilivyo la kifalsafa.Hakuna mtu mwenye Zanzibar yake. Mtu aleyezaliwa na kukulia Sumbawanga ana haki sawa na ardhi ya Zanzibar kama mtu aliyezaliwa na kukulia Micheweni and vice versa i also true.Hiyo ndio maana ya taifa.
Sasa ukitaka kuigawa yule wa sumbawanga atakwambia mbona unaipunguza nchi yangu na wa Micheweni pia.Utawajibu nini hapo?
 
sisi wengine kula kulala hata wakisema tanzania ni wilaya,hakuna ubaya ilimuradi sembe haikosekani dukani kwetu mambo ni bambam
 
Na maalim Seif kahoji baada ya kusema Zanzibar si nchi, mbona hawajasema kama Zanzibar ni wilaya, jimbo au mkoa? Duni Haji kaongezea haitoshi kusema Zanzibar ni sehemu ya Muungano kwa sababu hata Mtwara ni sehemu ya muunganio na inajulikana kuwa ni mkoa
 
Wapewe tu nchi yao kama yetu mafisadi wamemaliza basi afadhali wachukue yao mapema kabla haijaingiliwa kisha wakaanza kutuambia siri za usalama wa taifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…