Leo wanawambia wavae suruali kesho watwambia wav..suruali,hii ni kashfa nzito sana hailingani na mabo ya ngombe,hapa tunaambiwa Watanganyika tunakwenda uchi,hivi mnatazama mambo kwa karibu,hapa akipigwa mmoja tunapigwa sote na tatizo ni baadhi yetu kulinganisha na ng'ombe,ipo wapi thamani ya ng'ombe na thamani ya Utanganyika,kila anaedharau chake basi huyo atakuwa amepotoka,siwezi kukubali kudharauliwa kwa Mtanganyika yeyote kwani dharau hiyo inanigusa na mimi moja kwa moja,nilikwenda kupigana Uganda si kwa sababu Nduli amechukua sehemu ya Kagera bali nilikwenda kupigana kwa sababu amechukua sehemu ya Tanganyika,Ngoja nitoke nje kidogo kama unayo software ya Google earth jaribu kuangalia sehemu za kusini mwa Tanzania tunapopakana na malawi utaona kuna RED Boarder ambayo imeliweka lile ziwa Nyasa au ziwa malawi kuwa au kuonekana ni sehemu ya Malawi sijui unakumbuka ile nyimbo inayosema Banda wa Malawi katuvalia ngozi ya Chui akafikiri atatustisha..hivi unaikumbuka uliza sababu ya nyimbo ile,ok nilipouliza habari ya mstari au mpaka mwekundu katika sehemu ile nikaambiwa sehemu ile ina matatizo au kuna tatizo la mpaka baina ya Tanzania na Malawi,sasa kama Mwanakijiji yupo na atasoma hii thread anifikishie hili suali kwa Waziri wa mambo ya ndani na ya inje kuulizia ni kwa nini kuna red line pale Je Tanzania ina miliki au haimiliki sehemu ya ziwa lile na kwanini hakuna mpaka unaokatiza katikati ya ziwa...damu inanichemka halafu anatokea mtu anasema anajali ubinadamu,hapa pana Utanganyika tu wanasema usicheze na mali cheza na mwenye mali,Utamaduni na mila ni mali ya kila mtanganyika kudharauliwa au kunyanyaswa mimi binafsi sitokubaliana nako hata akiwa anaebamizwa kwa utamaduni wake ni mmasai,halafu unaleta ya kuleta eti ng'ombe hivi hujawahi kuona mmasai kuuza ng'ombe,jiulize sasa kwa nini anamuuza au ndio unataka kutwambia kwamba anafanya utapeli,hizo habari za vibarazani sina nafasi nazo,kilichofanywa na serikali ya Zanzibar ni udhalilishaji wa hali ya juu kwa Mtanganyika,kama haitoshiutawasikia wakisema hii ni mipango ya serikali ya Muungano au serikali ya Bara kama wanavyoiita kuwajaza waTanganyika huko kwao visiwani,haya kama si matusi ni kitu gani jamani hebu yatazameni haya mambo kwa undani,sio mnakulupuka na jazba ya yule mfalme alietoka nje bila ya nguo mpaka mtoto mdogo akasema mfalme yupo uchiii,huku ni kutukanwa kwa watanganyika wote,bado sijaona sababu za msingi juu ya faida za Muungano labda labda kuna kundi tunalo ndani yetu kundi hili linafaidika katika mambo ya siasa inapofika wakati wa kumchagua Mgombea Uraisi wa Tanzania,hapo natumai kila mmoja anaweza kuona ndio sababu kuu lakini hakuna sababu nyengine zaidi ya hiyo,na naamini kabisa siku kundi hili kutoka Zanzibar likija kuangushwa na CUF ndio mwisho wa Muungano huu kwani sasa itakuwa waliokamata serikali kule visiwani watu wasiotaka mambo ya kuoneana haya kila kitu kitazungumzwa,tunalijua hilo kuwa hawa CUF watakuja na mambo mapya kutaka kuuzungumza Muungano katika ngazi za kimataifa ili uonekane ni muungano wa kweli na sio huu wa kulindana hata ikifikia hapo basi nitafarijika kwani itabidi tuheshimiane kikweli la wakiteleza kidogo tu tumemewawacha mkono.