Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
Under Age,
Malalamiko sasa 40 yrs tumezoea -je uko hapo? Ngonjera ile ile! May be mpiga ngoma tu ni tofauti!
Comoro wako wenyewe so long- ni instalility tu na kutoaminiana- Zenj ni sehemu ya Muungano kisiasa- Mke wako amekuzalia watoto wazuri- huwezi kumfukuza kwa sababu wewe unazozitoa! Watoto wako waende wapi? Na wewe unakuwa baba au mama wa namna au heshima gani?
 
Under Age,
Malalamiko sasa 40 yrs tumezoea -je uko hapo? Ngonjera ile ile! May be mpiga ngoma tu ni tofauti!
Comoro wako wenyewe so long- ni instalility tu na kutoaminiana- Zenj ni sehemu ya Muungano kisiasa- Mke wako amekuzalia watoto wazuri- huwezi kumfukuza kwa sababu wewe unazozitoa! Watoto wako waende wapi? Na wewe unakuwa baba au mama wa namna au heshima gani?
mzalendo.
lile jibu nililotoa lilikuwa ni la kumkata makali mwiba na kejeli zake za kwamba anahisi muungano ukivunjika labda wazanzibari tutakufa njaa. nadhani msimamo wangu kuhusu muungano nilikupa katika post ya nyuma.kisiasa ni serikali tatu, kibinafsi ni kumhukumu mtu kwa anavyonichukulia (individually).siamini sana mipaka ya kijiografia,kwani haina zaidi ya kuleta fitna.
 
Zanzibar ni sehemu ya Tanzania na Raisi hawezi kuwa na maamuzi ya kugawa nchi. Huyo mtu anayefikiria Zanzibar ni nchi tofauti anaota ndoto za mchana. Kunawakati wa nyuma ilikuwa nchi pekee lakini sasa Zanzibar si nchi ni kitongoji cha Tanzania kilicho pewa uhuru kidogo.
 
Zanzibar ni sehemu ya Tanzania na Raisi hawezi kuwa na maamuzi ya kugawa nchi. Huyo mtu anayefikiria Zanzibar ni nchi tofauti anaota ndoto za mchana. Kunawakati wa nyuma ilikuwa nchi pekee lakini sasa Zanzibar si nchi ni kitongoji cha Tanzania kilicho pewa uhuru kidogo.
Tatizo sio Zanzibar ni Nchi au si Nchi,wewe unasema hivyo lakini wao wanasema ni nchi na wana Raisi na vikosi na usalama na mahakama ,hilo liweke kando hatutafuti uhalali wa Zanzibar ni nchi au ni mkoa.Kinachotakiwa tunafaidika na kitu gani kuwa na Muungano na watu hawa,wakati wao ndio wanaopiga makelele kila kona kudai tunawameza,tumeweka mirija mpaka kwao(TRA) kwa nia na madhumuni ya kuwamaliza kiuchumi,hivi hamukumbuki ni juzi tu walifika Kenya sijui umoja wa mataifa kuushitaki Muungano huu au mmekwisha kusahau jinsi walivyo tudhalilisha hadi kufikia eti waonyweshwe mkataba wa Muungano na kama haupo basi hakuna uhalali wa kuwepo kwa nchi inaitwa Tanzania,hapo ndio wanaposema tunatumia nguvu kuuweka muungano huu,jamani kipi kikubwa kinachotufanya tutumie nguvu kuulinda Muungano hii ni hasara kwa Tanganyika.
 
Tatizo sio Zanzibar ni Nchi au si Nchi,wewe unasema hivyo lakini wao wanasema ni nchi na wana Raisi na vikosi na usalama na mahakama ,hilo liweke kando hatutafuti uhalali wa Zanzibar ni nchi au ni mkoa.Kinachotakiwa tunafaidika na kitu gani kuwa na Muungano na watu hawa,wakati wao ndio wanaopiga makelele kila kona kudai tunawameza,tumeweka mirija mpaka kwao(TRA) kwa nia na madhumuni ya kuwamaliza kiuchumi,hivi hamukumbuki ni juzi tu walifika Kenya sijui umoja wa mataifa kuushitaki Muungano huu au mmekwisha kusahau jinsi walivyo tudhalilisha hadi kufikia eti waonyweshwe mkataba wa Muungano na kama haupo basi hakuna uhalali wa kuwepo kwa nchi inaitwa Tanzania,hapo ndio wanaposema tunatumia nguvu kuuweka muungano huu,jamani kipi kikubwa kinachotufanya tutumie nguvu kuulinda Muungano hii ni hasara kwa Tanganyika.

Mwiba:

Unadanganya sasa. Umezaliwa wakati muungano tayari na faida ya kuishi kama mtanganyika ukuiona wewe. Tanganyika ilikuwa nchi kwa kipindi cha miaka 44. Na katika kipindi hicho ni miaka 3 tu Tanganyika ilikuwa nchi ya huru. Na kipindi kilichobaki cha miaka 41, Tanganyika ilikuwa chini ya ukoloni.

Faida ya Tanganyika ilikuwa mzawa kupigwa viboko kulipa kodi ya maendeleo na sikushangahi mtu kama wewe kutumia stamp ya Malikia wa Uingereza, mtawala wa Jumuia ya Afrika mashariki kama icon yako. Mvivu kama wewe siku zote unapenda makombo ya ukoloni.

Mambo mengi unayotaja hapa ni matatizo ya kiuchumi. Zaidi ya asilimia 50 ya bajeti ya nchi yako ni misaada kutoka nje. Fanya kazi na acha kutegemea misaada.
 
Mwiba:

Unadanganya sasa. Umezaliwa wakati muungano tayari na faida ya kuishi kama mtanganyika ukuiona wewe. Tanganyika ilikuwa nchi kwa kipindi cha miaka 44. Na katika kipindi hicho ni miaka 3 tu Tanganyika ilikuwa nchi ya huru. Na kipindi kilichobaki cha miaka 41, Tanganyika ilikuwa chini ya ukoloni.

Faida ya Tanganyika ilikuwa mzawa kupigwa viboko kulipa kodi ya maendeleo na sikushangahi mtu kama wewe kutumia stamp ya Malikia wa Uingereza, mtawala wa Jumuia ya Afrika mashariki kama icon yako. Mvivu kama wewe siku zote unapenda makombo ya ukoloni.

Mambo mengi unayotaja hapa ni matatizo ya kiuchumi. Zaidi ya asilimia 50 ya bajeti ya nchi yako ni misaada kutoka nje. Fanya kazi na acha kutegemea misaada.


vijana ahsanteni, hivi ndivyo tunavyokwenda asifahamu hadi kwa fimbo afahamishwe hivyo hivyo.

ndugu yangu mzanzibari mwenzangu under age hongera sana kwa kazi njema unayoifanya Allahu yujziiyka kulla kheyr
 
ZEC Zanzibar yakamilisha mapendekezo

2007-11-18 10:43:21
Na Mwinyi Sadallah, Zanzibar


Tume ya Uchaguzi Zanzibar, (ZEC), imekamilisha mapendekezo ya muundo mpya wa Sekretariat ya Tume hiyo, kama ilivyopendekezwa na Tume ya Rais ya pamoja ya utekelezaji Muafaka wa CCM na CUF.

Hayo yamo katika ripoti ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar, iliyokabidhiwa kwa Rais Amani Abeid Karume na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Bw. Masauni Yussuf Masauni.

Mfumo huo wa Sekretariat ya Tume ya Uchaguzi umetokana na ushauri wa wataalamu kutoka ndani na nje ya nchi, akiwemo Bw. Ron Gould kutoka Canada na Profesa Chris Peter kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Ripoti hiyo ilisema wataalamu hao ndio waliotayarisha mapendekezo ya muundo wa Sekretariat ya Tume hiyo na majukumu ya utendaji katika chombo
hicho.

Ilielezwa kuwa baada ya kupokea mapendekezo hayo, Tume imeyafanyia kazi kwa kuzingatia mazingira ya utendaji kazi ya Zanzibar na kufanya marekebisho, ikiwemo kuondoa nafasi ya Naibu Mkurugenzi wa Uchaguzi na Wasaidizi wa Wakurugenzi Uchaguzi.

``Muundo wa Sekretariat ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar ulikubalika kuwa na divisheni sita?, ilisema ripoti hiyo.

Ilisema divisheni ya kwanza ni ofisi ndogo ya uchaguzi Pemba itakayosimamia shughuli za kiutawala, fedha na shughuli nyengine zote za uchaguzi, ikiwemo kumshauri Mkurugenzi wa Tume hiyo.

Divisheni ya pili ni ya uchaguzi ambayo itakuwa ikimshauri Mkurugenzi kuandaa utekelezaji wa taratibu za uandikishaji wapiga kura, uteuzi wa wagombea, kampeni za uchaguzi, upigaji kura, kuhesabu na kutangazwa kwa matokeo.

Aidha, ripoti hiyo imependekeza kuwepo divisheni ya utawala na uendeshaji itakayosimamia shughuli za mafunzo kwa wafanyakazi, uajiri na haki za wafanyakazi kwa kuzingatia kanuni za utumishi.

Wataalamu hao wamependekeza kuwepo divisheni ya habari na uhusiano itakayokuwa na majukumu ya kujenga uhusiano kati ya vyombo vya habari na
Tume na utoaji wa elimu kwa wananchi.

Divisheni nyingine ni ya fedha, ukaguzi na bajeti itakayokuwa na majukumu ya kuandaa bajeti ya fedha na malipo yanayofanyika kuhakikisha yanakidhi mahitaji yote ya upatikanaji na utumiaji wa fedha.

Wataalamu hao pia wamependekeza kuwepo divisheni ya sheria itakayofanyakazi ya kumshauri Mkurugenzi wa Uchaguzi masuala yote ya sheria za uchaguzi na
kuwa Mwakilishi wa Tume ya Uchaguzi mahakamani wakati inapohitajika kutoa au kujibu hoja kuhusu masuala yote ya uchaguzi yanayotokana na Katiba ya
Zanzibar, Sheria ya Uchaguzi na Kanuni zinazotungwa.

Ripoti hiyo imesema Tume ya Uchaguzi inatarajiwa kuwa na ofisi zake katika kila Wilaya ili kuendeleza zoezi la uandikishaji wapiga kura watakaokuwa wamefikisha umri unaotakiwa kisheria.

Ilisema kwamba ofisi hizo pia zitakuwa na kazi ya kuangalia watu waliohama katika maeneo na kuingia katika maeneo mengine, ili kuhakikisha wanashiriki
katika uchaguzi bila matatizo yoyote.

Tume ya Uchaguzi Zanzibar ilikabidhi ripoti yake kwa Rais wa Zanzibar baada ya kumaliza muda wake.

Tume hiyo Mwenyekiti wake alikuwa Masauni Yussuf, Makamo Jaji Augostino Ramadhani na Makamisha wake walikuwa Khatib Mwinyichande. Ussi Khamis Haji,
Nassor Seif Amour, Mosi K.
Mshamte na Halima Tawakal Khairalla.

SOURCE: Nipashe
 
natumai hamjambo kwa ujumla wenu.nakutakieni kheri na fanaka katika siku hii ya leo.

Kwa hakika nimechelewa kuuona huu mjadala na nimeosoma kwa pupa sana kwa hivyo nitajibu kwa ufupi tu.

Hoja ya muungano bila ya shaka wazanzibari wengi kama kutaitishwa kura ya maoni watesema hatutuutaki muungano wa tanganyika na zanzibar na hilo nalisema nikiwa mie ni mmoja wao.

Lakini wakati huo huo mfahamu kwamba suala la muungano linajadilika lakini kuuvunja sio kitu kinachowezekana hata siku moja. kinachotakiwa na wazanzibari au na wabara ni kuurekebisha kwa maana muungano huo umeasisiwa na watu wawili Nyerere na Karume bila ya kuwashirikisha watanzania.

Suala la kuwafukuza masheikh wa bara nitalijibu kwa mujibu wa uwezo wangu. masheikh waliofukuzwa waliingia zanzibar na kuhubiri dini ya kiislamu lakini kama mnakumbuka mashaikh hawa wamekuja kwa sura kama ile walikuja nao masheikh wa wakati ule ambao walijulikana kama akina mazinge masheikh hawa wanahubiri ubaya wa dini nyengine ambayo sio uislamu na waliitwa na serikali yaani ofisi ya mufti kwa ajili ya kukatazwa kuwahubiria watu yaani kuwataka kuoina dini ya kikristo ni mbaya. kw ahivyo walitakiwa wahubiri dini ya uislamu na sio kutia doa dini nyengine au kutoa kauli za kashfa dhidi ya dini nyengine lakini baada ya kuitwa kwa kuandikiwa barua hawakwenda wakatumiwa njia nyengine kupitia vyombo vya serikali vya radio na televisheni pia walikataa kwenda na waliitwa kw alengo la kukatazwa kutoa maneno ya hamasa dhidi ya dini ya ukiristo, serikali imeamua kuwafukuza kwa sababu wamekataa kutii amri hiyo.

suala la imani ni kubwa sana na lina gharama zake amani ikitoweka kupitia imani ya dini ni machafuko na sio kitu chengine. na zanzibar lazima mfahamu licha ya kuwa na waislamu asilimia 95 basi wanaishi vizuri sana sana na wakiristo na dini nyengine kama hindu nk. lakini maneno ya watu kuwa kanisa limevunjwa, wakristo wanaonewa ni mambo ya wana siasa tu ambao wanatumia njia hiyo kuwatoa imani wananchi.

mimi tokea udogo wangu nimelelewa zanzibar na nilikuwa nasoma na marafiki zangu wa kikristo hata siku moja sijawahi kuwoana wakibaguliwa kwetu wala mie sijawahi kugabuliwa kwao wakati wa krismas mimi nakwend akula kwao na wakati wa idd el fitri wao wanakuja kula kwetu na hilo mtu yoyote aliyekuwa mzanzibari atakuthibitishia yaani hakuna ubaguzi wa dini.

sheikh kurwa ni kwelia lifukuzwa unguja na kupelekwa bara kwa madai anatoa kauli za kadhfa dhidi ya viongozi wa serikali lakini tukumbuke kuwa sheikh kurwa sio mtu wa bara ni mtu wa pemba na anaitwa kurwa na mwenzake ambaye ni pacha wake anaitwa doto hadi leo tupo huko huko pemba anaishi dk salmini alimfukuzwa na kutumia njia hiyo lakini kurwa na mpemba na sio mbara hiyo ilikuwa ni siasa na watu walimpigania mpaka wakachoka lakini wapi wakubwa wakishaamua...

turudi kwenye suala letu la muungano kwa hakika kila mmoja wetu ambaye anaijua vizuri zanzibar na akitaka kuzungumzia ukweli sio jazba za kisiasa wala kidini atakubaliana nami kwamba tanzania bara imenufaika sana na inaendelea kunufaika sana na zanzibar kwa mambo mengi tu hasa ya kiuchumi. na hilo alityekuwa anabisha basi ajaribu kuwauliza wataalamu wa uchumi na watu wenye kuijua zanzibar miaka ya nyuma.

kuhusu wapemba waliokuwa wanafanya biashara huko dar au katika mikoa ya tanzania bara hilo naomba mfahamu kwamba wapemba sipendi kuita wapemba bora niseme wazanzibari wanaofanyabishara wanalipa kodi nyingi kwa sababu wana bishara zao kubwa kubwa kwa hivyo wanaingiza pato kwa nchi tofauti na wabara waliopo huku wengi wao wanauza mifagio na mikanda yaani bishara ndogo ndogo sisemi hivyo kwa kuwadharau la hasha naeleza ukweli.

jambo jengine watu wa bara siku hizi wapo wnegi sana na wanatumiwa kwa namna nyingi wengine wamekuja wenyewe kwa kutafuta kazi ambao kabila la wamasai tu wapo zaidi ya elfu moja kw amujibu wa takwimu walizotoa wenyewe juzi katika kikao chao walichofanya huko Nungwi mkoa wa kaskazini unguja.
wengine wanaotoka bara takriban hoteli zote za kitalii zina wafanyakazi kutoka mikoa ya tanzania bara. mbali ya vijana wanaokuja kufanya kazi za maofisini na majumbani, mbali ya wale vijana waliokwisha kata tamaa ambao huchukuliwa wakati wa uchaguzi na wana CCM ili wawapigie kura baadae hawaondoki tena kwa maana ya kuahidiwa kupewa makaazi na kupatiwa ajira vijana wa aina hiyo wapo wengi sana na kama huamini ukimalzia uchaguzi tu wanavamia ofisi wa waandishi wa habari na kutoa siri hiyo kwa kudai wamedhulumiwa hawajalipwa haki zao walizoahidiwa.

mbali na wanaokuja kwa ajili ya kufanyakazi za wakandarasi wa barabara ni wengi sana sana kwa hakika siku hizi ukizungumzia suala la kuvunjwa muungano unaweza ukachekwa kwa sababu watu wa bara wengi wameshaowa na kuolewa huku na kuzaa na wazanzibari wameshaowa na kuolewa na wabara kwa hivyo hilo ni gumu sana labda mie naweza kusema suala la muungano lipitiwe upya katika muundo wake kwa sababu article of union original ni 11 lakini sasa zimeongezwa na kufikia 23. ni tatizo yaani zimeongezwa kinyemela.
asante sana
 
Sasa nimewasmoke out na mnawaona hapo wanatoka ndani ya mashimo , Mtanganyika Tetea Utanganyika wako wacha kujikomba usikotakiwa nitarudi naenda kupata maji ya bendera ya Tanganyika...Eti tumenufaika sana loh aibu gani hii.
 
Stone Town,
Mbona ulipotea Yahee!

Mchango wako umefafanua mengi- you are a realist! Mimi natoka Bara- na huja mara nyingi Zenj haswa Weekend kupata upepo mzuri, kupata vyakula safi vya Kizanzibari pale Forodhani usiku (ile juice ya miwa napenda sana), pia huenda Prinson Island kuogelea kule- na kuwaona wale tortoise! Watu pia wakarimu zaidi- ni napenda sana kila unayekutana naye Atakusalimia- ni tofauti na kupigana vikumbo tulivyovizoea Dar!

Mimi nimetokea sana kupenda huko Zenj- pia Pemba (Wete na Chake) nimefika. Nikisikia hisia za kuuvunja Muungano- huwa najisikia vibaya!

Kuna mambo ya kurekebisha- kwa kukaa pamoja na kuongea ila sii kuvunja Muungano!
 
Hoja ya muungano bila ya shaka wazanzibari wengi kama kutaitishwa kura ya maoni watesema hatutuutaki muungano wa tanganyika na zanzibar na hilo nalisema nikiwa mie ni mmoja wao.asante sana
1) Ili kuweka sawa ni sababu zipi zingekufanya upige kura ya kuumaliza Muungano katika kura ya maoni ambayo wengi wenu ndio mnaona ndio kujikomboa kutoka katika makucha ya Muungano ambao munauwita jinamizi lililoilalia Zanzibar.
2) Kama unajadilika unafikiri tutachukua miaka mingapi kuujadili kumbuka Muungano umezaliwa 1964.
3)Karume alifariki Apr. 17, 1972 na Nyerere 14 October 1999,umesema Muungano umeasisiwa na wawili hao bila ya kuushirikisha umma sijui unamaanisha nini.Ila kipindi walichofariki wawili hao ni kikubwa kama kurekebishwa kumefanywa au kungefanyika kwa wale wanaoona wamenyimwa haki kama nyinyi.
4) Kusema kuuvunja sio kitu kinachowezekana hivi unaweza kutoa misingi ya kutowezekana kwa tendo hilo.
5)Unamfukuza Mtanzania katika nchi yake,unamfukuza aende wapi ? Umesema kama waliitwa tena na serikali hivi serikali ilishindwa kuwafungulia mashitaka na kuona ni bora iwafukuze,hilo haliwezi kuingia akilini ila mlilokuwa nalo ni ubaguzi wa huyu Mtanganyika na huyu mzanzibar hakuna Utanzania hapo na zaidi ulipogusia shee kurwa kuwa yeye ni mpemba huoni kama inaonyesha yanayosemwa na CUF ni kweli kuwa serikali iliyokuwepo madarakani huko Zanzibar ni ya kibaguzi inawabagua watu ?
6) Unasema huwezi kuwaita Wapemba,wabara zaidi utatumia Wazanzibar,waTanzania lakini ulipowafukuza uliwaona ni nani ? Kwa nini usiwahukumu kama ni Wazanzibar na badala yake uliwatenga kwa uzalendo wao !
7) Hapa ndio patamu zaidi unaposema Tanganyika inafaidika,inamaana Zanzibar haifadiki na Muungano,hapo ndipo mnaposema tunawanyonya,hebu jaribu kwa muono wako Tanganyika tunafaidka vipi kiuchumi,kitu gani tukikosa tutalala na njaa hata ukathubutu kusema tuna mirija huko imekita.
8) Kuwepo kwa watanganyika huko ndiko kunakowavuruga vichwa vyenu ni juzi tu mmesema tumewaingizia ukimwi na wazanzibar huwacha wake zao kwa machangu doa kutoka Tanganyika,unafikiri ni mtanganyika gani atakubali tusi hilo.
Vijana waliokwisha kata tamaa,tusi hilo kwa Mtanganyika.Sasa msiwe mnapiga makelele kwa sababu zisizo na msingi hao wanaokuja huko hufanya kazi maofisini mahoteli ni waajiriwa kihalali kabisa,kama wapiga kura mnawachukuwa wenyewe,inakuwaje mnasema mnajaziwa watu kutoka Tanganyika.
 
vijana ahsanteni, hivi ndivyo tunavyokwenda asifahamu hadi kwa fimbo afahamishwe hivyo hivyo.

ndugu yangu mzanzibari mwenzangu under age hongera sana kwa kazi njema unayoifanya Allahu yujziiyka kulla kheyr
rabbi takqabbal duaa inshallah. pia namwomba mungu atuunganishe wazanzibari ili tuepukane na dharau tunazodharauliwa na watu kama kina mwiba na kejeli wanazotufanyia kwa kisa tu kwamba tumeungana.
 
Stone Town,
Mbona ulipotea Yahee!

Mchango wako umefafanua mengi- you are a realist! Mimi natoka Bara- na huja mara nyingi Zenj haswa Weekend kupata upepo mzuri, kupata vyakula safi vya Kizanzibari pale Forodhani usiku (ile juice ya miwa napenda sana), pia huenda Prinson Island kuogelea kule- na kuwaona wale tortoise! Watu pia wakarimu zaidi- ni napenda sana kila unayekutana naye Atakusalimia- ni tofauti na kupigana vikumbo tulivyovizoea Dar!

Mimi nimetokea sana kupenda huko Zenj- pia Pemba (Wete na Chake) nimefika. Nikisikia hisia za kuuvunja Muungano- huwa najisikia vibaya!

Kuna mambo ya kurekebisha- kwa kukaa pamoja na kuongea ila sii kuvunja Muungano!

mzalendohalisi. naweza kujenga imani kwamba ukigombea urais wa muungano nitakupa kura yangu. kwani umejaa kila aina ya hisia katika maongezi yako.masuali mengi tunayojadili hapa hayahitaji usomi bali yanahitaji common sense ,ili tupendane zaidi basi hatuna budi muungano huu ufanyiwe marekebisho.nimekaa na watanganyika watatu zanzibar kwa kiasi cha miaka 5 au zaidi na walikuwa ni marafiki zangu sana tu na mpaka leo wao wananiona mie ni ndugu yao nami nawachukulia kama ni kaka zangu,wao ni wakristo na mimi ni muislam lakini hatujawahi kukwaruzana,walikuwa na hisia sana kuhusu zanzibar ,mpaka walifika wakati wakaniambia kama wazanzibari wangeungana wakawa kitu kimoja na muungano ukaipa nafasi huru zanzibar ya kujiendeleza kiuchumi basi naamini zanzibar ingekuwa mbali sana kimaendeleo,nami nikawajibu kama tanzania ingekuwa na watu wenye hisia kama nyinyi basi hakuna ambae angelalamika kuhusu muungano huu.mzalendo,nakubaliana na wewe, kinachohitajika ni marekebisho,na inshallah kwa uwezo wa mungu basi yatakuja ,japo kama sisi tushafariki ila kizazi kijacho kinaweza kikafanya mabadiliko.
 
mzalendohalisi. naweza kujenga imani kwamba ukigombea urais wa muungano nitakupa kura yangu. kwani umejaa kila aina ya hisia katika maongezi yako.masuali mengi tunayojadili hapa hayahitaji usomi bali yanahitaji common sense ,ili tupendane zaidi basi hatuna budi muungano huu ufanyiwe marekebisho.nimekaa na watanganyika watatu zanzibar kwa kiasi cha miaka 5 au zaidi na walikuwa ni marafiki zangu sana tu na mpaka leo wao wananiona mie ni ndugu yao nami nawachukulia kama ni kaka zangu,wao ni wakristo na mimi ni muislam lakini hatujawahi kukwaruzana,walikuwa na hisia sana kuhusu zanzibar ,mpaka walifika wakati wakaniambia kama wazanzibari wangeungana wakawa kitu kimoja na muungano ukaipa nafasi huru zanzibar ya kujiendeleza kiuchumi basi naamini zanzibar ingekuwa mbali sana kimaendeleo,nami nikawajibu kama tanzania ingekuwa na watu wenye hisia kama nyinyi basi hakuna ambae angelalamika kuhusu muungano huu.mzalendo,nakubaliana na wewe, kinachohitajika ni marekebisho,na inshallah kwa uwezo wa mungu basi yatakuja ,japo kama sisi tushafariki ila kizazi kijacho kinaweza kikafanya mabadiliko.

Under-age,
Unajua Mwiba sijaona na kuelewa hoja yake hadi sasa hata husema Muungano uvunjwe!
Unakumbuka hii hoja ya mapungufu ya Muungano tuliijadili sana hapo nyuma na Mkandala, Kichuguu na wewe na wengine kwa kina. One of central conclusions from such arguments was a consensus that kuna maeneo ya kurekebisha ili kuimarisha Muungano! Haikutokea a polarized view kama ya Mwiba over sababu za kimsingi kuvinja Muungano!
Well tu watu wamoja, tumevumiliana kwa miaka 40, tumeoleana, na kozoena! Hivyo nikiona hoja ya kuvunja Muungano huwa nashidwa kuelewa!
 
kuna mtu anasema ati zanzibar tunawafukuza watanganyika na kutoa mfan sheikh kurwa.

jee Tanganyika mlisahau mlipomfukuza Sh Hassan Bin Ameir? huyu hakuwa mtanzania? au kwa ni mzanzibari.

kila nchi inayo haki kumtimua anaehatarisha usalama wa upande na kumrejesha alipotoka.
tushawafukuza waliokuwa wakiendesha umalaya na wengine na tuliwa fukuza kwa mujibu wa sheria tulizokubaliana na halikuwa tatizo hilo si tatizo la muungano.

matatizo tuliyaainisha na yanaendelea na tutaendelea nnaamini kwa uwezo wa mungu tutafika pazuri tutakuwa na muungano wa kiungwana sio huu wa kiguberi.


wazanzibar ni watu wa pole na wakarimu ila " be ware with the fury of patient man"
 
kuna mtu anasema ati zanzibar tunawafukuza watanganyika na kutoa mfan sheikh kurwa.

jee Tanganyika mlisahau mlipomfukuza Sh Hassan Bin Ameir? huyu hakuwa mtanzania? au kwa ni mzanzibari.

kila nchi inayo haki kumtimua anaehatarisha usalama wa upande na kumrejesha alipotoka.
tushawafukuza waliokuwa wakiendesha umalaya na wengine na tuliwa fukuza kwa mujibu wa sheria tulizokubaliana na halikuwa tatizo hilo si tatizo la muungano.

matatizo tuliyaainisha na yanaendelea na tutaendelea nnaamini kwa uwezo wa mungu tutafika pazuri tutakuwa na muungano wa kiungwana sio huu wa kiguberi.


wazanzibar ni watu wa pole na wakarimu ila " be ware with the fury of patient man"
Unaona hapo ndio inapatikana ile TIT for TAT ,kama mnalipa kisasi wakati mlitakiwa muondokane na hizo za kumfukuza mtu uliemtaja anaeitwa Hasani ili kuonyesha hamrudii kosa,lakini leo baada ya miaka 44 mnatenda kosa lile lile hii ni kuonyesha hamna nia ya kutengeza zaidi ya kuharibu.
Tokea 1964 kunajadiliwa kitu gani mapungufu gani hayo yanayompa tabu binadamu kuamua kama si ukorofi wa wa Zanzibar kudai wanaonewa wanamezwa na watu hawa wameshaona kuwa wanadhulumiwa basi hakuna chochote kitakachoamuliwa isipokuwa wataona bado hawajatendewa haki na watakuja na lingine jipya kuna madai wanadai eti walipwe tokea walipounganisha benki kuna hisa zao hawalipwi wao ukiwatajia kuwa hamlipi umeme wa kidatu wanapanda mori.
 
wakuu mbona kimya?

haya amapendekezo yanaweza kuondosha manung'uniko ya pande zpote hasa CUF kule zanzibar?

au inaonekana ni geresha tu?
 
Mwiba,
Zenj ni visiwa vidogo vya watu 1 milion- wakati bara ni 37 m. It is logical Zenj kulalamila wanaonewa au wanahisi wanmezwa na Bara- wewe ungependa Bara walalamile kuwa wanamezwa na Zenj?
 
Watanzania wenzangu nafikiri tuwe na mawanzo ya kujenga na sio kubomowa.Sikweli kama wengi mavyofikiria kuwa Zanzibar itashindwa kujiendeleza wenyewe bila kuitegema Bara. Zanzibar inaitegemea Bara kwa vile ndio inavyotakiwa iwe hivyo. Zanzibar wakati wa Abeid Karume ilikuwa mbali kimaendeleo kwa vile iliachiwa kujiendeleza haikubanwa kama sasa hivi. Hivi sasa wapo watu wasiotaka kuiona ikiendelea kama ilivyokuwa hapo mwanzo. Ni kuionea kwa maneno ya kejeli wakati haipewi nafasi inayostahiki.
Kwa wale wanaodhani kuwa Zanzibar haiwezi kuendelea na wajiulize ilikuwa vipi kabla ya kupata utegemezi wa Bara. Zanzibar itabaki kuwa sehemu ya muungano kwasababu tuliuungana cha kufanya ni kutatua kero zinzoeleweka wazi kwa nia ya ndugu mmoja juu ya ndugu mwenziwe. Tukumbuke Watanzania wenzangu hivi karibuni tu tuliungana sote kupinga shirikisho na nini zilikuwa sababu zetu?
 
Watanzania wenzangu nafikiri tuwe na mawanzo ya kujenga na sio kubomowa.Sikweli kama wengi mavyofikiria kuwa Zanzibar itashindwa kujiendeleza wenyewe bila kuitegema Bara. Zanzibar inaitegemea Bara kwa vile ndio inavyotakiwa iwe hivyo. Zanzibar wakati wa Abeid Karume ilikuwa mbali kimaendeleo kwa vile iliachiwa kujiendeleza haikubanwa kama sasa hivi. Hivi sasa wapo watu wasiotaka kuiona ikiendelea kama ilivyokuwa hapo mwanzo. Ni kuionea kwa maneno ya kejeli wakati haipewi nafasi inayostahiki.
Kwa wale wanaodhani kuwa Zanzibar haiwezi kuendelea na wajiulize ilikuwa vipi kabla ya kupata utegemezi wa Bara. Zanzibar itabaki kuwa sehemu ya muungano kwasababu tuliuungana cha kufanya ni kutatua kero zinzoeleweka wazi kwa nia ya ndugu mmoja juu ya ndugu mwenziwe. Tukumbuke Watanzania wenzangu hivi karibuni tu tuliungana sote kupinga shirikisho na nini zilikuwa sababu zetu?
WaTanganyika tupo huyu kidogo amejaribu ametoa joto na ukweli halisi upo katika maneno niliyoyakazia wino;-
Watanganyika tunaikandamiza bara tunauwa uchumi wao ndo wakapata sentensi hiyo.Hatutaki kuiona ikiendelea tunalitumia bunge kuweka mipaka ya kazi zao.Maamuzi yote wanayofanya inabidi yapate baraka zetu,wanasema tunawachagulia Raisi na ushahidi wanao,ukisoma kwa kina hiyo habari hapo juu utayaona yote.
Mimi sikubaliani na yote hayo aliyoyaandika kinachonipa moyo ni kuwa hawa wanataka kutubebesha hata uzembe wao,kila wanapokwama husema Bara ndio kikwazo,wanajidai kuutaka muungano ila kuna vijikero kidogo visawazishwe,hivi tuwaambie basi tufanyeni raisi mmoja kama hawajaluka !!!
Sasa someni gazeti hili ambalo nimeliweka na kulihifadhi kama baadhi ya ushahidi wa watu hawa..
0) Inawezekana kabisa Muungano wa Zanzibar na Tanganyika ni muungano wa pumbazo la kisiasa la kuharibu na kunyonya upande mmoja ambao ni Zanzibar

1) Zanzibar tunataka kuanzisha kampuni ya simu (ZANTEL) ambayo itatoa huduma Zanzibar bado nayo tunatiliwa ngumu eti TTCL itakosa mapato.

2)Zanzibar ni nchi yenye asilimia 99% ya Waislamu kati ya wananchi wote wa Zanzibar. Cha kushangaza serikali ya Jamhuri ya Muungano imeizuia Zanzibar kujiunga na umoja wa nchi za Kiislamu (OIC) kwa sababu zisizoeleweka.

3)Zanzibar inashindwa kutetea nguvu za umeme wa kutumia taka kutoka Malaysia ambao ilitarajiwa kuwekeza hapa Zanzibar. Hii ni kutokana na serikali ya Jamhuri ya Muungano kutounga mkono na shinikizo toka nje.
Zanzibar tunategemea umeme kutoka bara, hii ni kutufanya tuwe tegemezi katika nyanja muhimu ili tutawaliwe kisiasa na kiuchumi na ndivyo ilivyo. Sababu mojawapo ya kuzuia uwekezaji ule wa umeme wa taka ni kwmba eti TANESCO itakosa mapato kutoka Zanzibar
4)Kama kweli Tanzania ni muungano wa nchi mbili zenye Marais yaani Zanzibar na Tanganyika, mbona mgawanyo wa taasisi na vyuo vya elimu haupo sawa? Tanzania bara kwa mfano kuna vyuo vya biashara kama vile College of Business Education (CBE), DSA, Vyuo vya Ufundi, SIDO n.k. ambavyo vimetapakaa karibu mikoa yote ya bara na hakuna hata kimoja Zanzibar.
5)Sasa hivi tuna msuguano mwingine wa Zanzibar kuwa "Free Port" bado tunatiliwa ngumu na serikali ya Jamhuri eti serikali itakosa mapato, mapato gani hayo? Kama kweli Muungano wetu ni wa kheri kwanini tuvutane au tuwekeane ngumu kwa kuona wivu kuwa Zanzibar itanufaika.
Hitimisho lao:
Mlioliona kwa serikali ya Jamhuri kukosa mapato ni kwa Zanzibar kuwa "Free Port" tu? Vipi ndege za Kikristo zinaingia na kutoka Tanzania kwenye viwanja vyao bila kupekuliwa hamuoni kama serikali inakosa mapato? Mali inayoingizwa au kutolewa kwenye "Air Strips" za Wakristo kusiko na polisi wala Afisa "Custom" kwa ndege za Kikristo mnazijua? Ila Zanzibar tu kuwa "Free Port" huu ni udini ulio dhahiri.

Ili kujinasua na hali hii serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Wazanzibari wote kwa ujumla bila kujali tofauti za kisiasa tushikamane ili tuweze kujitegemea katika njia zote kuu za uchumi na ulinzi. La sivyo, tukubali Zanzibari kuwa mkoa na siyo nchi yenye Rais.


Halafu anakuja mzanzibari hapa sijui hiki sijui kile wazandiki wakubwa,nyie mna lenu tu ,hizi ndizo faida tunazopata kwa Wazanzibar sijui wakienda nchi za nje wanazusha uzushi gani.
 
Back
Top Bottom