Faida za muungano kwa mujibu wa Prof Shivji ambaye kanunuliwa na chama cha magamba. Ile hotuba yake ya upotoshaji imejaa unafiki. Hakuna suala la hasara na faida kabla hatuja-establish muungano nini? Yale maandishi yenye sign ya Mwl Nyerere ya ku-forge? Nina hoja na Shivji angalau nitoe yangu kama ifuatavyo. Tanganyika ni mzimu unaowafanya CCM na ma-darling wao waweweseke kama wana majini. Shivji anajaribu kucheza na jargon za kinadharia tu na kwa aina ya vijana wale wenye upeo finyu wa kuutafuta UKWELI kama ilivyo ndani ya CCM, sioni kwa nini wasiungane naye.
Shivji kama mabarakala wenzake wanaiogopa sana Tanganyika kwa sababu wanazozijua wao. Tanganyika ni kuleta uwazi ndio maana wahafidhina wote wanaiogopa. Wakati shivji Anahalalisha Uzanzibar eti upo karne mbili za akina Seyyed Said na ukoo wake na kwamba Utanganyika ni ukoloni. Hivi huyu Shivji ndiye yule wa dialectical materialism au amegeuka wa dialectical idealism (Hegelian?). Ni wazi kama unaukubali uzanzibar wenye asili ya ukoloni wa Waarabu sharti ukubali Utanganyika japo ni wa ukoloni wa kingereza. Unaogopa nini kuukubali ukweli huu.
Serikali tatu Shivji anasema inaamsha na kushawishi hisia za Utanganyika, na, pili, kufanya watu wa Tanzania Bara wawachukie wenzao wa Zanzibar.(kifungu hiki kilikuwemo kwenye hotuba ya JK Dodoma, nadhani kuna ubia kati ya JK na Shivji). This is obvious huwezi kufuta awareness ya Watanganyika kwa kuficha ukweli wa historia kwamba Tanganyika ilikuwepo na itaendelea kuwemo kwenye historia. Eti kuwepo hadharani kwa Tanganyika inahatarisha muungano badala ya kuuimarisha. Ni ajabu prof anashindwa kuelewa muungano wa watanganyika na wazanzibar haukuanza 1964 kwa Articles of Union. Hivi Karume, Mwinyi, Moyo, Kisasi, Mfaranyaki, Mwakanjuki, nk. ni wenyeji wa wapi? Hao na wengine wengi wana asili ya Tanganyika na historia inatueleza hivyo. Shivji mwenyewe ana asili ya Zanzibar akahamia Morogoro (kama ilivyo kwa Wahindi na Wazanzibar wengi ambao wako Tanganyika) kabla ya 1964. Watu hao bila kujali articles of union za 1964 wanaendelea kuhusiana kijamii, kibiashara, kiuchumi, kuoana nk. Huu ndio muungano wa kweli ambao hauhitaji serikali mbili, moja, tatu, au nne. Na Shivji ansema muungano wowote hauwezi kudumu, au kudumu kwa amani, kama hauna mizizi katika watu na hisia zao. Nani kamwambia shivji eti Watanganyika na Wazanzibar hawana hisia za kushirikiana? Kinachoendelea Dodoma ni ya wanasiasa na kwa kuwatumia vibaraka wao kama akina shivji na wenzao kama visemeo(ndio maana Shivji anamnukuu Kikwete au Kinyume chake) - eti Tanganyika itaamsha nationalist tendencies, kwani Zanzibar hakuna nationalist tendencies? Kwa nini kwa Tanganyika iwe dhambi kuonyesha utaifa wao?
Shivji anawatisha vijana eti Na Utanganyika wenu hautadumu kwa sababu mtaanza kudai sasa Jamhuri ya Makonde na Jamhuri ya Sukuma! Mtakuwa vipande vipande. Shivji usitishe na kudanganya vijana hao. Hivi ni vitisho; Mmakonde kaolewa Moshi, msukuma kaoa Tanga, Mmatengo kaolewa Musoma, Mmasai kaolewa Mbamba Bay, Mwera kaolewa Mbeyya nk. Mhehe anaishi Kilwa, Mkaguru anaishi Kigoma nk. Suala la jamhuri hizi za Shivji za kufikirika ni alinacha za prof. za mchana. Kutumiwa ni kubaya, unaweza kuhadhirika na heshima yako kama prof wangu anavyojidhalilisha. Shivji anatoa mifano hai mbele yetu ya Somalia imesabaratika, Libya pia, Sudan, Afrika ya Kati, na nchi nyingine nje ya Afrika – Afghanistan, Pakistan, Syria, Iraq bila kutaja nchi za Ulaya. Hapo tunazungumzia muungano wa Tanzania, lakini mifano ya Shivji haihakisi context na historical conditions za Tanzania. Anaficha ukweli kwamba anachoshabikia yeye ndicho kilichofanya nchi hizo zisambaratike. Yaani kutumia gilba kulinda utaifa, kutumia udikteta katika kufanya maamuzi ya kitaifa kama CCM wanavyofanya, kukataa kusikiliza hoja za walalahoi (ambao kwa kipindi kirefu Shivji amekuwa mtetezi wao).
With due respect najua prof bado yeye kama mwanazuoni anapenda kuchochea mijadala ya kitaaluma ambayo kimsingi haiwezi ku-address practical problems za muungano. Na mwanasiasa atakayechukua ushauri aupeleke kufanyiwa kazi ajihakikishie anatumbukiza taifa katika mtafaruku. Na ndoto ya kupata katiba mpya haitakuwa kweli. Napenda kuungana na Mzee Msekwa aliyesema kuwepo kwa idadi yeyote ya serikali sio hoja maana muungano utakuwa imara ilimradi kuna political will. Je hawa wanasiasa (JK na CCM type) Shivji anawatetea anawajua wana nia gani? Kama Shivji anataka mfano hai akamwulize Prof. Mihanjo na Mukama na dossier la pendekezo lao la CCM kujivua gamba limeishia wapi. Chezea wanasiasa wa CCM wewe!