Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?

Muungano upo ICU haihitajiki Elimu ya juu kutambua Hilo hata wa darasa la pili anajua Kuwa Tanganyika anachunwa Kama buzi huku Zanzibar wakijiimarisha kwa kila nyaja kisha watimukie kwa waarabu.
 
Mimi ni mtanzania wa hali ya kawaida sana . Ninakerwa na Viongozi wanao ogopa Kumfunga paka Kengele. Kikwete kasema Muungano yeye hauvunji labda atoke madarakani ndiyo watu waje kuuvunja. Inaonyesha CCM wanaogopa kubeba hiyo Dhambi ambayo kwenye Biblia wala Quran haipo. SASA MIMI NAJITOLEA KUBEBA HIYO LAWAMA KWA HISTORI YA VIZAZI VYOTE VITAKAVYOKUJA MBELE YETU. Nipeni Urais wa Mkataba wa Mwaka Mmmoja nifanye yafuatayo.

1. Siku ya pili baada ya kuapishwa Nitatangaza Nchi ya Tanganyika; hivyo nitatoa Mwezi MMOJA Wazanzibar wote popote pale walipo huku Tanganyika warudi kwao. Watakao taka kurudi Bara Wafuate taratibu za Uhamiaji.
2. Wanajeshi wote Kutoka Tanzania Bara watarudishwa Tanganyika. Hii ikiwa na kubeba Silaha zote zilizokuwa huko Visiwani.
3.Nitaimarisha ulinzi Mkali kwenye Mwambao wote wa Bahari ya Hindi Kuanzia Tanga hadi Mtwara.
4. Watanganyika Nitawapa Mwezi MMOJA waamue Jina la nchi yao. Je libaki kuwa TANZANIA au lirudi TANGANYIKA.
5.Vyama vya siasa Vitaamua vyenyewe kubadirisha majina au Kutumia hayohayo ya Mwanzo.
6. Mwisho Nitaitisha Uchaguzi mkuu Muwachague viongozi wenu mtakao wataka Wanchi yetu TANGANYIKA ambao hawatakuwa wamebeba hii lawama.
Asanteni sana. SITANII NIKO SERIOUS.

Ha ha ha mkuu nimefurahi sana
 
Wakati wa Chama kushika hatamu ulipita zamaaani! Sasa hivi Watanzania wameelimika na wanajua nini ni nini mambo ya kupeana miongozo hayapo tena. Suala la Katiba ni la watu binafsi na siyo la kivyama. Kila mtu atatoa mawazo yake binafsi. Kama lingekuwa la vyama basi wangekusanya vyama vya siasa na kwenda kupata maoni.
Nyerere aliacha - Muungano serikali moja nchi mbili, tumefiakaje kwenye muungano serikali mbili na nchi mbili? halafu sasa hata rasimu za katiba ziko mbili, moja ya maoni ya wananchi, nyingine maoni ya vyama. Kufika sijui?
 
BAVICHA NA NDOTO ZA ALINACHA.......
niliwaambia humu Kuwa serikali Tatu hazitakuwepo hata msujudu uchi.
Hii nchi haiwezi kuendeshwa na mawazo ya KI-MBWA
Siyo kila anayepingana na CCM ni BAVICHA.
 
Ni wakati wa kuwa na Tanganyika yetu ndo tuungane nao. Huu unafiki wa serikali mbili ni dhambi kubwa ya taifa!

Mkuu, hii thread ni ya miaka kibao nyuma!!!!


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
faida za muungano zipo nyingi sana kuliko hasara.siku zote umoja ni nguvu. Lakini hatuwezi kuona faida kubwa za muungano hadi kwa bahati mbaya tutengane, wajerumani ukiwauliza leo watakwambia faida nyingi sana za muungano .sikatai kuna baadhi ya viongozi wetu hawasimamii ipasavyo mambo ya muungano na baadhi ya vipengele vya muungano vyahitaji kurekebishwa.haya ni mawazo yangu binafsi.
Mkuu tunaomba utaje hizo faida nyingi angalau kwa uchache tu.
 
Mkuu ngongo .. heshima mbele.... hili bandiko limeshiba ukweli na uhalisia ....asante sana .... umenichosha ama kunifurahisha hapo kwenye red .... utanitendea haki pamoja na wengine wanaofuatilia mada hii ukitoa angalau ufafanuzi kidogo tu kuhusu sentensi hii

wakimbizi hawatajuwa wengi ksma sukosei sensa iliyopita zanibaru hajafika hat milioni 3 na kea muonekano a sa sa nafikiri nusu yao wako ilala magomeni na temeke
 
Naomba kuelewa hasara ni nani muungano huo wa Tanganyika na Zanzibar ukivunijka ?

Je kuna maslahi yoyote ya kuwa katika muungano huu.
 
Wanasiasa wengi wamekuwa wakisifia sana muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kwamba wale wote wanaokosoa muungano ni watu wasiotakia mema nchi.lakini nimekuwa nashangazwa na haohao linapokuja suala la muungano wa E.africa.watakuja na hoja zilezile zinazotumiwa na wazenji dhidi ya Tanganyika mara ooh hatutaki wachukue ardhi mara vile.SASA NAJIULIZA KAMA MUUNGANO NI KITU KIZURI MBONA SISI TUNAOKWAMISHA MUUNGANO WA AFRIKA MASHARIKI.NA KAMA NI KITU KIBAYA KWANINI TUNAING'ANG'ANIA ZANZIBAR.nawasilisha.
 
Wanasiasa wengi wamekuwa wakisifia sana muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kwamba wale wote wanaokosoa muungano ni watu wasiotakia mema nchi.lakini nimekuwa nashangazwa na haohao linapokuja suala la muungano wa E.africa.watakuja na hoja zilezile zinazotumiwa na wazenji dhidi ya Tanganyika mara ooh hatutaki wachukue ardhi mara vile.SASA NAJIULIZA KAMA MUUNGANO NI KITU KIZURI MBONA SISI TUNAOKWAMISHA MUUNGANO WA AFRIKA MASHARIKI.NA KAMA NI KITU KIBAYA KWANINI TUNAING'ANG'ANIA ZANZIBAR.nawasilisha.

Amini nakuambia Zanzibar ikijitenga mwaka hauishi watakuja kuomba hifadhi Tanganyika maana mapinduzi yapo nje nje kama kule Sudani. Kama unabisha weka jiwe mimi nakuahidi laki moja.
 
faida za muungano zipo nyingi sana kuliko hasara.siku zote umoja ni nguvu. Lakini hatuwezi kuona faida kubwa za muungano hadi kwa bahati mbaya tutengane, wajerumani ukiwauliza leo watakwambia faida nyingi sana za muungano .sikatai kuna baadhi ya viongozi wetu hawasimamii ipasavyo mambo ya muungano na baadhi ya vipengele vya muungano vyahitaji kurekebishwa.haya ni mawazo yangu binafsi.

Mkuu acha kumung'unya maneno taja hizo faida za muungano ili wananchi wazielewe kusema ziko nyingi haitoshi:focus:
 
BAVICHA NA NDOTO ZA ALINACHA.......
niliwaambia humu Kuwa serikali Tatu hazitakuwepo hata msujudu uchi.
Hii nchi haiwezi kuendeshwa na mawazo ya KI-MBWA

Inaonyesha jinsi ulivyo na upeo mdogo wa kufikiri jenga hoja za kutetea msimamo wako sio kutukana eleewa wenye
msimamo tofauti na wako wana haki ya kutoa mawazo yao sio kuwa wewe na kundi lako ndio mna mawazo mazuri
kushinda wengine matusi ni dalili ya kutokomaa kifkra na kukosa hoja za msingi:thinking:
 
Watu wengi, hasa hawa wa kizazi cha dijitali, wamekuwa wakijiuliza kuhusu faida za muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar. Muungano una faida nyingi za kiuchumi na kimaendeleo.

Zifuatazo ni baadhi tu ya faida za muungano:

1. Wazanzibar (wapemba) wengi wamepata fursa za kiuchumi nchini Tanganyika. Idadi kubwa ya wapemba wanamiliki ardhi, nyumba, na biashara kubwa nchini Tanganyika, jambo ambalo lisingewezekana nje ya muungano.

2. Kuoleana: Wananchi wa nchi hizi mbili wamekuwa wakioleana tangu kale na wameendelea kufanya hivyo hata baada ya muungano.

3. Muungano ni wa kihistoria. Kuulinda ni sawa na kudumisha historia. Nyerere na Karume hawakuwa machizi walipoamua kuunganisha nchi hizi.

4. Visiwa vya Zanzibar ni vidogo na havitanuki. Kuungana kumewezesha baadhi ya wazanzibar kuhamia bara na kupunguza msongamano visiwani.

5. Kihistoria, wakazh wa Zanzibar walitokea Tanganyika. Muungano umewaunganisha na ndugu zao wa asili.

6. Bila muungano, waarabu watahamia Zanzibar na kuishambulia Tanganyika.
 
Hizo zote umetoa hoja dhaifu sana,pili umeonyesha faida ziko kwa wazanzibari,je watanganyika wanafaidika nini na muungano?

Kwa akili yako chochote alichokisema au kukifanya Nyerere hakitakiwi kuhojiwa?au ni kosa kukihoji.

Unaleta hoja ya kuoleana?hata watanzania wanaoishi mipakani wameoana sana na wenzao wa upande wa pili,je tuungane nao pia?

Hoja namba 6 ni hoja dhaifu kuliko zote,kwa hiyo tunaungana kwa kuhofia waarabu?
 
Unatoa hoja kama jk? Ina maana tukioa mwingereza ndo tuungane nao, hoja dhaifu kama mwenyekiti wa ccm taifa
 
Hizo zote umetoa hoja dhaifu sana,pili umeonyesha faida ziko kwa wazanzibari,je watanganyika wanafaidika nini na muungano?

Kwa akili yako chochote alichokisema au kukifanya Nyerere hakitakiwi kuhojiwa?au ni kosa kukihoji.

Unaleta hoja ya kuoleana?hata watanzania wanaoishi mipakani wameoana sana na wenzao wa upande wa pili,je tuungane nao pia?

Hoja namba 6 ni hoja dhaifu kuliko zote,kwa hiyo tunaungana kwa kuhofia waarabu?

Faida kuu kuliko zote ni usalama wa nchi yetu!
 
Back
Top Bottom