Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?

zanziberi ni koloni la TANGANYIKA chini ya mwamvuli wa muungano! I hate this union shit thing...
Tungewaacha wazanzibar waendelee na nchi yao maybe sasa hivi ingekuwa kama singapore/dubai hivyo tungekuwa tunaagiza bidhaa with low cost. Infact huu muungano unatucost wote tanganyika na z'bar
 
Maadui wa Muungano sio sisi tunaoitetea na kuilinda hadhi ya Zanzibar katika Muungano bali wale ambao kwa makusudi wamekuwa wakitumia hadaa na hujuma kuizima na kuifisidi hadhi ya Zanzibar, uwepo wake na historia yake.

Wakati sisi tukimpa heshima zote Rais wa Jamhuri ya Muungano, wengine wamekuwa wakiidhihaki na kuidogosha heshima ya Rais wa Zanzibar hadharani, wakiidhalilisha hadhi ya Zanzibar kama nchi yenye nasab na historia yake na kuwadogosha wananchi wa Zanzibar kwa makusudi bila ya Serikali ya Jamhuri kukemea udhalilishaji unaofanywa dhidi ya mamlaka ya Zanzibar.

#Nani_Sababu Anaechangia mmomonyoko wa Muungano ni SMT yenyewe hasa uongozi wa juu unaoonekana kufurahia na kuchangia hii dhana potofu ya uwepo wa Zanzibar kama nchi ni kosa la jinai na uadui dhidi ya Muungano.

SMT ndio sababu kuu ya wananchi wa Zanzibar kuanza kuuchukia na kuujutia Muungano kwa vile kila tukisonga mbele katika uwazi wa nia ya kuungana kunaonekana ishara na dalili zinazojenga dhana ya kuwa Muungano ni kuifuta Zanzibar katika ramani ya Ulimwengu na kwa hilo halistahamiliki abadan.

[HASHTAG]#MpenziDhati[/HASHTAG] Wapenzi wa kweli wa Muungano ndio wanaodai kuundwa kwa Mahakama ya Katiba kama ambavyo Katiba ya Muungano inavyoeleza kuwa ndio chombo pekee cha juu cha kuondosha utata dhidi ya hizi shengesha za kidhalili za Muungano. Hebu fikiri kama Waziri wa Zanzibar akamsema Rais wa Muungano katika lugha kama ya Kabudi dhidi ya hadhi ya Rais wa Zanzibar ingelikuwaje?

Jiulize katika hali ya utata kama huu kweli ni maslahi ya nani yanayolindwa hata kusiitishwe mahakama maalum ya Katiba tukatatua kero hizi kisheria na kikatiba? [HASHTAG]#WalinziMuungano[/HASHTAG] Wazanzibari ndio walinzi wa kweli na wapenzi wa uhakika wa Muungano kama ulivyoasisiwa kwa nia ya kuungana kwa yenye maslahi ya pamoja sio nia ya kummeza mdogo au kumfuta mmoja kwa sababu dhaifu kama wingi wa waislam au uchache wa wananchi wake. Hivi ni nchi gani ilioungana kama sisi ikafanyiwa dharau za namna hii kwa Mkuu wake wa nchi halafu ikakubali kwa miaka zaidi ya hamsini kubaki katika Mkurogano kama huu?

Tuseme ukweli mpenzi wa Muungano ni Zanzibar na adui wa Muungano ni hawa wachache wanaofikiri kauli za kejeli zitaodogosha hadhi ya Zanzibar kama nchi. [HASHTAG]#MchawiNani[/HASHTAG] Msimtafute mchawi, si wazanzibari waliokubali kuendelea na haya yanayofanyika tokea siri mpaka dhahiri katika dunia hii ya leo ya teknolojia na kizazi hichi cha utandawazi. Ni kweli Zanzibar tunamgawanyiko wetu wenyewe wa kiitikadi lakini si sababu ya kufikiri hatustahili kuwepo na nchi yetu, uongozi wetu na hadhi yetu.

Kutunyoshea vidole kama maadui wa Muungano kwa kudai haki na hadhi yetu katika Muungano wa khiyari ni ukosefu wa insaf na kupotosha nia, ajenda na sababu za kuungana. Zanzibar si nchi pekee ilio na athari ya mvutano wa kiitikadi na ukitazama kwa undani mgawanyiko wa kiitikadi ni fursa kubwa ya msukumo wa maendeleo kwa anaejitambua. [HASHTAG]#Zanzibar[/HASHTAG] Tokea unaasisiwa Muungano huu kwa mkataba wa Muungano hatukuwahi kukubali kufuta uwepo wa nchi yetu na kujiongoza wenyewe kama nchi kamili.

Tuliungana tukiwa na nia ya kushirikiana pamoja kwa yale yatayoweza kusukuma maendeleo, kutulinda pamoja na kujenga msingi imara wa udugu wa asili tulio nao. Na ndio tulikuwa na mambo 11 tu ya msingi huu sio kutusukuma katika lindi litalofuta nyayo za historia na urithi wetu kama nchi iliostahili heshima zote za kuitwa nchi. #Moja_Abadan Msema kweli mpenzi wa Mungu, serikali moja abadan haikukubalika awali na haitakubalika milele. Na hii dhana kwamba inawezekana kuigeuza Serikali ya Zanzibar kuwa sawa na ya jimbo ndio itayozaa kaburi la Muungano.

Mifano sahihi ipo, Singapore na Malaysia ziliungana kwa nia njema lakini Muungano wao ulikufa kwa dhana hizi za mkubwa kufikiri ana hadhi zaidi ya mdogo. Singapore ilifukuzwa na Malaysia kwa sababu kama hizi tunazopewa sasa, leo iko wapi? Unajuwa kuwa Rais wa Singapore alilia hadharani baada ya Malaysia kuifukuza Singapore katika Muungano huo? Leo iko wapi? Na unajuwa ni Singapore iliokuwa ikitazamwa kama adui wa Muungano? #Khiyari_Haki Sisi ni wapenzi madhubuti wa Muungano tukiamini kuwa ukiwa utaendeshwa kwa misingi ya khiyari, uwazi, ukweli na nia thabit za usawa, haki na heshima basi tutajenga taifa madhubuti linalothamini uwepo wa nchi mbili huru zinazojiongoza zenyewe na kuongozana pamoja kwa yale yaliokubalika pamoja.

Mzee Warioba ni shahidi wa nia zetu maana katika waliopokea kwa furaha mabadiliko ya kweli ya Muungano ni wazanzibari kwa sababu ya mapenzi kwa Muungano usio na shaka dhidi ya uwepo wa nchi yao sio huu wa sasa wa Waziri tu tena wa kuteuliwa kumfananisha Rais wa nchi mdau wa Muungano kuwa sawa nae katika porojo ya mwaka ya dhihaka ya ajabu. #Jenga_Bomoa Hivi tunapata nini kuidhalilisha hadhi ya Zanzibar kiasi hiki? Tuseme kweli haya ya kina Pinda na Profesa Kabudi yanajenga au kuvunja Muungano?

Hivi haki kutuwekea mawaziri wawili na Naibu mmoja katika baraza la zaidi ya Mawaziri Hamsini lakini tukiwa tumepoteza zaidi ya mambo 30 katika Muungano? Yaani unatupora mamlaka kirahisi rahisi na kutunyima fursa alau ya kuwa na muwakilishi hata yule “Symbolic” tu wa kuonyesha thamani ya kuyapoteza mamlaka hayo? Hivi hatusomi katika maandishi ya mwenye kondoo 99 dhidi ya kondoo mmoja na mwisho wake? Hebu hasa niulize kulazimisha lisilotendeka kuna jenga au kuna vunja?
 
CUF ya Maalim ni chama kinachopata pesa toka kwa Sultani aliepinduliwa. (Maalim anakutanishwa na Sultani Jemshid Qatar, na Karume anajua) Kwanini tunachezea shilingi chooni? Pia kinaitwa Hizbu kama chama asilia ya Sultani yaani kwa kiswahili ndio chama cha wananchi. Chama kichafu hichi kwa amani na mustakabali wa nchi yetu. Chama kifutwe mara moja. Migogoro mingine sio ya lazima, tuachwe tufanye kazi, hawa wanaotamani uarabu kama suluhu ya matatizo ya kiuchumi waone Siria, Somalia na Yemen wakigombania kula mizoga ya mbwa na watu. Futeni chama chenye ndoto ya piga ua kuigawa Tanzania.
 
Mkuu Maalim Seif sio mwarabu,Maalim Seif ana asili ya Kishirazi,si unakumbuka Afro Shirazi Party(ASP),chama kilichoongozwa na Karume,Chama kiilichompindua Sultan wa Zanzibar,halafu chama hicho kikaungana na TANU mwaka wa 1977 halafu kikazaliwa CCM

Sasa hizi propaganda za Hizbu zimetokea wapi,kwanza unajua maana ya Hizbu,Hizbu ni neno la Kiarabu linalomaanisha "chama",kwahiyo ukisema "Hizbu" lazima uweke neno jengine mbele yake mfano:"Hizbu alwatan" au "Hizbu llah" nakadhalika

Aliekuwa Sutani wa Zanzibar Jemshid hayuko arabuni yuko Portland Uingereza,Wa Oman walimkataa kumchukua baada ya kupinduliwa kwasababu waliona sio mwanarabu sio Muomani,ni Mzanzibari...Jemshid yuko Uk anaishi kama mkimbizi hana tafauti na wasomali au mkimbizi yoyote yule.

Mkuu propanganda kama hizi zimepitwa na wakati,"zilipendwa",lete propaganda ambazo zitaleta maendeleo Zanzibar,sizo ambazo zitawagawa wazanzibar.....

Hamna mtu anaetamani uarabu,wazanzibar wanatamani wajitawale wenyewe,walimuondoa Sultan ili wawe na nchi ya Jamuhuri,sasa wanaona wanatawaliwa,wanaona hakuna faida yoyote ya huu mungano...

Zanzibar haiwezi kukopa ili ijipatie maendeleo,Zanzibar haiwezi kucheza michezo ya kimataifa,Zanzibar haiwezi kujiendeleza kiuchumi,Kwa jina la Muungano unazidi Zanzibar kila kukicha...

Kwahali ilivyo sifikirii kama kuna mzanzibari anaweza kuzisikiliza propaganda kama hizi....
 
Kaka sijui kama unajua unachokiongea,Katiba ya Zanzibar imebadiliswa wakati wa utawala wa Kikwete,makubaliano ya maridhiano baina ya CUF na CCM Zanzibar ilikuwa wakati wa utawala wa Kikwete..UAMSHO wakati wa Kikwete...

Meli imekuja juzi wakati wa utawala wa huyu Unko yako Magu,sasa haya mambo yamehusiana na nini...
jaribu kuweka wazi Mkuu
 

Mkuu unaonekanwa Unakerwa kweli na waarabu. Hebu twambie wamekufanya nini ?
 
Amani iwe nanyi wana jamvi.

Awali ya yote ni watakie makaribisho mema kusubiria siku ya Maazimisho ya Muungano 26.04.2018 Mungu awape nguvu nyote ili siku hiyo itukute tukiwa hai.

Tangu nilipo anza kujitambua na kuufahamu vyema Muungano wa Tanganyika na Zanzibar sikuwahi ona faida zake bali ni hasara tu.

Mifano kadhaa ya hasara:

1.Ajira- kuna wa Zanzibar wengi wameajiriwa ktk sekta mbalimbali ambazo tungeweza kuajiri vijana wetu wanao tangatanga mitaani na vibahasha kutafta ajira.

2.Bunge wawakirishi- hizi gharama zinazolipwa hawa wabunge zingeweza kusaidia kutatua matatizo mengi yanayotukabili kama taifa.

3.Biashara- hatuna mawasiliano katika biashara, Mfano mwaka Jana mwezi wa 11 nilinunua screen "32" (TV) kutoka Zanzibar kwa sh 295,000 nilipofika bandari ya DSM TRA walikokotoa kodi ya 278'500 Muungano una faida gani?

Tuambiwe nini faida za Muungano kama hazipo tuwaache Wa Zanzibar waamue msitakabari wa Taifa lao.
Na wa Tanganyika tuendelee na maisha yetu.
 
Point ya pili na ya tatu zina mashiko kiasi chake. Kuhusu point ya kwanza naona unakosea kwasababu kuna wa bara nao pia wameajiriwa huko visiwani.
 
Rekebisha namba 1. Wabara wapo zenji wengi tu wameajiriwa.
Nadhani upande wa ajira hakuna tatizo, ni kama vile kwenda kufanya kazi nje ya nchi
 
Point ya pili na ya tatu zina mashiko kiasi chake. Kuhusu point ya kwanza naona unakosea kwasababu kuna wa bara nao pia wameajiriwa huko visiwani.
Wa bara walio ajiriwa visiwani ni wachache lakini wa visiwani ni wengi sana kuliko sisi
Huku wamejenga lakini mtu wa bara kupata ardhi visiwani ni ngumu na Zanzibar wana ubaguzi sana kwetu wa bara.
 
Rekebisha namba 1. Wabara wapo zenji wengi tu wameajiriwa.
Nadhani upande wa ajira hakuna tatizo, ni kama vile kwenda kufanya kazi nje ya nchi
Mkuu ukiangalia mgawanyo wa ajira kwa bara na Zanzibar ni Zanzibar wanafaidika kuliko sisi na kuna ubaguzi sana wanabagua sana wa Bara
 
Faida ya muungano ni pamoja na naibu raisi kutoka zenji

Samaki wa pwani ya bara na wale wa zenji kuwa na uhuru wa kuzaliana na kutembeleana...kuliko hata binadamu wamiliki wa muungano huo
 
Ilikuwa desturi ya Wazanzibar kutumia lugha ya hekma na busara. Wapo waliosema wanataka Serikali tatu, wako waliotaka kufanyike kura ya maoni, wapo wanaotaka waachiwe wapumue, wapo wanaodai mamlaka kamili pia wapo wanao nung’unika midomi na wengine rohoni. Uhalisia nikuwa wote hawa wanabeba ujumbe mmoja kuwa hawautaki muungano huu wa Zanzibar na Tanganyika.

Kila linapojadiliwa suala la muungano wa Zanzibar na Tanganyika, ni Wazanzibar bila kutafuna maneno wanosema wamechoshwa na hawautaki muungano huu wa Zanzibar na Tanganyika. Tumesema sana, na tutazidi kuendelea kusema kuwa Wazanzibar wamechoshwa na muungano, watafurahi wakiachiwa uhuru wao, watafute sehemu nyengine ya kujiunga.

Kawaida ya miungano ni kweli huleta faida, ila miungano mingi ni yenye hasara kama huu wetu na mengine mingi iliyotangulia na mwisho ikawa ni kugawanyika. Mfano, tuangalie kila nchi inakimbilia kujiunga na United Nation (UN) kwamba kule kuna maslahi. Inapotokea nchi moja kusimamishwa au kufukuzwa uanachama nchi hiyo italalamika sana, kuomba radhi na mwisho kutaka irudishwe.

Tuangalie muungano wa USSR ulivyovunjika, hakukuwa na nchi iliyotaka kurudi, zote zilikhiari kutunza uhuru wao. Wakati ulipofika wakajiunga na muungano wa Ulaya. Hapo ilionyesha kuwa muungano wa USSR haukuwa na faida kwao.

Zanzibar nayo haitaki tena muungano na Tanganyika kwa vile hauna faida yoyote upande wake. Zanzibar inahitaji na inatafuta muungano wenye manufaa na maslihi juu yake. Leo hii mtoto wa miaka 15 wa Zanzibar ukimuuliza faida na hasara za kuungana na Tanganyika, atakutajia hasara nyingi sana na atakwammbia hajaona faida yoyote.

Wala hapana haja ya kuorodhesha hasara za muungano huu kwenye andiko hili, kubwa ni kusema kuwa Wazanzibar hawana hamu wala hawataki kuusikia muungano wa kikoloni wenye dhamira ya kuitawala na kuikalia Zanzibar kiujanja.
Baada ya Kisiwa cha Mombasa kukabidhiwa Kenya, na Tanganyika nayo chini ya Julius Kambarage Nyerere wakati huo alipeleka maombi yake kuwa akabidhiwe Zanzibar na eneo lake lote liliobakia. Hivyo huu ulikuwa mpango wa kugawanywa Zanzibar kwa nchi mbili hizi; Kenya na Tanganyika. Kenya walikabidhiwa kwa ujanja wa mkata wa lease (kukodishwa) wa muda mrefu. Zanzibar ikakubalika akabadhiwe Tanganyika kwa mkataba wa muungano.

Sasa Tanganyika inaongoza Zanzibar bila kujali kuwa Zanzibar ni nchi, kuna mkataba wa muungano, na Tanganyika nayo inamipaka yake. Leo hii ikiwa Sheria ya Tanganyika ndio yenye nguvu, Waziri wa Sheria anasema sheria zao zina mamlaka yote, kwa mambo yote na wao (Tanganyika) ndio Amiri Jeshi Mkuu, huo mkataba wa muungano upo wapi hapo.

Ikiwa Watanganyika hawathamini kuwepo nchi ya Zanzibar wanakwambia nchi moja unategemea kuona kuwa na muungano hapo au ukoloni na kutawaliwa tena Zanzibar.

Wazanzibar bila kuchoka wala kukata tamaa wataendelea kuupinga muungano huu hadi pale watakapopata uhuru wao. Wazanzibar wako wazi wanasema hawataki tena kutawaliwa na Tanganyika.
 
Nyerere alimpindua Sultani mwenyewe ili awasaidie wa Africa wa Zanzibar wapate haki sawa kama binadamu wengine. Kwa kuwa ilibidi atumie zile silaha alizochukua Algeria baada kufanikisha kuwaunganisha maadui wakubwa wa siasa visiwani wakati huo yaani African Association na Shiraz Association na hatimae akisaidiana na Waingereza na Kanisa katoliki alifanikisha kuunda ASP na kumpa Karume uenyekiti.

(Sheikh Ali Muhsin Barwani na Mke wa Karume YouTube ) ila wa Africa wa Zanzibar waliogopa kubaki peke yao baada ya Mapinduzi, walijua waliopokonywa kwa nguvu lazima wajipange, ndio wakaomba kuchanganyana kabisa na ndugu zao wa African mainland.
 
Ni jambo la heshima sana Muungano wa Tanfanyika na Zanzibar kufikisha miaka 54 ukiwa imara na ambao ni wa mfano duniani.

Faida za Muungano huu zipo nyingi za ktk nyanja za kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiulinzi.

Hongereni watanzania wote kwa maadhimisho ya miaka 54 ya Muungano wetu yatakayofanyika tarehe 26 kesho makao makuu Dodoma.

Tujihadhari na maadui wa ndani na nje wanasioutakia mema Muungano wetu tulioachiwa na waasisi wa taifa letu.

Chilonwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…