Mkuu, maswali yako ni murua kabisa!!! Ndio maswali tunayotakiwa kujiuliza na kupata majawabu.
1. Waasisi wa mawazo mengi Afrika, Lumumba, Nyerere, Nkrumah nk walikuwa na maono ya uhuru na umoja. Na walifanya mengi kuleta umoja afrika. Kizazi cha viongozi kilichofuata kilikuwa ni utajiri, madaraka na ubinafsi. (kuvunjika kwa Sudan, mapinduzi ya kijeshi, vita vya wenyewe kwa wenyewe nk).
2. Ndicho kinachofanyika. Hakuna mtu anataka kuwa ndiye wa "kulaumiwa" na historia. Kila mtu anampitishia mwenzake. Mabadiliko ya kwanza yalikuwa ni 1984 kwa upande wa Zanzibar. Toka kipindi hicho kasi ya mabadiliko kwenye muungano ilishika kasi na kusiwe na hata mamlaka ya kuhoji. Hakuna aliyetaka kutoa maelezo, hata wale waliokuwa sahihi nao walinyamaza!! Nao pia hawakutaka kuwa historia, kila mtu alikuwa mwoga. Maoni ya Kamati ya SMZ imesema kwa Warioba kuwa wanataka dola kamili mbili lakini je umekwishasikia CCM kutoka Zanzibar wakisema hilo kwa mdomo?? Je umeelewa sasa kwanini hakuna makubaliano kwenye kamati za bunge ambako misimamo hasa ya CCM Zanzibar hatupati kuyasikia lakini changes kwenye rasimu zinashindwa kupitishwa kwa kukosa au theluth mbili upande wa Zanzibar au na Tanzania Bara pia?? The truth is nobody wants to take responsibility. Hata Kinana anasema "tujilaumu wenyewe kwa katiba ya Zanzibar 2010". Kwani CCM au JMT hawakujua na kuona katiba hiyo mpya kabla haijapitishwa?? We are reactive and not proactive!!
3. Nasema tena, hakuna faida za kiuchumi au kisiasa wala kiusalama kwa Tanganyika. Kama ni swala la usalama, Kenya has the longest porous border with Tanzania. Threat zingetoka zaidi huko kuliko Zanzibar. Kuna mwingiliano wa kijamii na Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi, Kenya na Msumbiji kuliko uliopo na Zanzibar. Faida pekee ni ya kisiasa ambayo ilianza kwa kuunganisha TANU na ASP. So kwa CCM wanaogopa kuharibu historia yao ya kisiasa. Wanaogopa kupoteza ideologies zao na wanaogopa kupoteza madaraka na influence katika sehemu moja coz kwa mifano ya UNIP Zambia, KANU Kenya, inamaanisha kuwa inaweza kuwa ndio mwisho wa CCM kama chama baada ya muda mchache!! Kwa CCM, it is a survival battle and they will fight to the last drop of their blood. This fact is understandable!!! Toka Uchaguzi wa kwanza wa 1995, seats za CCM katika uwakilishi wa mawazo ya wananchi katika mabunge na serikali za mitaa zimekuwa zikipungua progressively. CCM has been notified and they want to put a halt to the downfall.