How?Wakuu kiusalama muungano unaumhimu sana tuulinde sote kwa nguvu zote.
Muungano unalinda usalama kivipi?
Mmetukaribishaje wakati haturuhusiwi kumiliki ardhi Zanzibar kisheria?Wazanzibar tumewakaribisha Watanganyika tokea enzi zilee
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
How?Wakuu kiusalama muungano unaumhimu sana tuulinde sote kwa nguvu zote.
Mmetukaribishaje wakati haturuhusiwi kumiliki ardhi Zanzibar kisheria?Wazanzibar tumewakaribisha Watanganyika tokea enzi zilee
Tuwe na serikali tatu na tuwe na nia ya kuwa na muungano sio kulaghaiana!
TheMonthlyJob.com Earn 10$ for every 30 second Task. Internet Job jionee wabunge wanavyo kula hela
Huu si uhuru bali ni pango! Hivyo tutaishi sisi na vizazi vyetu katika kupangishwa? Uhuru ni uhuru wa kujitegemea na kuamuwa kwa matakwa yako bila kuingiliwa na mtu. Huoni kuwa hili sisi na wao litaendelea daima sasa na vizazi vijazo? Ni bora tuanze mwanzo kwa ugumu lakini tukiwa na uhakika kuwa tunafanya tufanyayo bila kuja mtu akatusimbulia. Watanganyika mna roho za kutokumkubali mtu yoyote asie nyie. Hadi leo Wapemba mnawaita Wapemba ingawa wapo Dar miaka mingi kuliko wengi wenu mliotoka mikoani. Mpaka leo bado kuna WEaarabu na Wahindi na akikosa kidogo ananza kutajiwa kabila yake. Jee unafikiri ungekuwa wewe ni Mzanzibari ungekubali kuishi katika hali hiyo?
hoja yako inadhihirisha hoffu na woga uliotawala fikira zako, ila mbaya zaidi umeonesha kama kwamb Wazanzibar ndio walinzi ama wavunjaji wakuu wa Muungano huu, na kuwafanya Watanganyika wawe watiifu na kuwapigia magoti Wazanzibar ili kuunisuru Muungano, wazo ambalo sio sahihi...!!
Muungano huu utalindwa pale utaposimamia misingi ya usawa na hakki baina ya pande mbili, bila ya kujali ukubwa ama population ya nchi washirika,
Hivyo kuuenzi Muungano sio Zanzibar kusarenda
mambo yake kwa Tanganyika bali kufuata misingi ya hakkki na usawa ktk Muungano huu!!
maganjwa,mimi nimetoa kitu kitakachokea ila faida ya muungano utaiona siku muungano ukivunjika kama wewe wazenji watapata ndio wataopata shida zaidi itakuwa kama urusi na jimbo la cremia kutaka kujiuunga na urusi maana angalia ukubwa wa tanganyika na zanzibar kibiashara wataathirika sana sidhani kama chakula watajiweza wasije tanganyika mpakani lazima watozwe sawasawa.
Mimi ninachkuambia ni kutokana na historia ya huu muungano mpaka tumefikia hatua hii ya kuandika katiba mpya tanganyika haijawahi kulalamika isipokuwa zenji na mimi ninakuambia muungano umefika mwisho wake kwa maana mtaka fitina hakosi sababu na zanzibar kama katiba mpya waliyoandika haiatabadilishwa hakuna muungana maana iko juu ya serikali ya muungano je nani atkubali ujinga huo?
inayokusumbua wewe ni hofu tu, hakuna kingine. Kuna ushahidi japo c wakisayansi kuwa makaburi ya watu waoga huwa yanadidimia hali inayofanya watu wanaoamini uchawi kusema wachawi wamefukua maiti.
Angalia na wewe kaburi lako lisije didimia. Ni rahisi tu kuepuka hili, just "ACHA WOGA USIO NA KICHWA WALA MIGUU"
maganjwa,
Kwani ukivunjika muungano Zanzibar haitaweza kufanya uhusiano na mataifa mengine au haitaweza kujinunulia chakula chake? Zanzibar kabla Muungano ilikuwa ni miongoni mwa nchi tajiri duniani. Kylikuwa na supermarkets za serikali vyakula vilikuwa rahisi tu. Kenyan products including vyakula kama sembe la packets na mafuta ya kupikia siagi, vitunguu na hata vitu vya na sanitary kama sabuni za kuogea na.dawa za meno zilitoka Kenya, UK, India na China.
Nakuona uko katika majanga ya ufaham mdogo wangu majangwa. Nahisi Tanganyika itapata tabu kiuchumi, maana kila upande majirani wanaangalia kwa jicho la waswasi, Kaskazini (Kenya & Uganda) Magharibi Ruwanda na Kusini Malawi. Hawa wote ndio wa kufanya zaidi biashara na Tanganyika. Zanzibar population ya watu milioni 1 wakiagiza tani alfu 20 za mchele kutoka India au Thailand inatosha chakula cha miaka miwili.
Vitunguu vya India ni rahisi sana na juu ya gharama za usafirishaji kuliko vya Iringa.
Zanzibar ikitangaza kuwa bandari huru inatosha kwani haya yalifanywa huko nyuma wakati waingereza nq wajerumani walipotaka kuikwamiza Zanzibae kiuchumi.
Kuna, vyombo vingi vya kushiriki zanzibar kujiendelza kiuchumi. Kuna kama Indian Ocean Rim, SADEC, OIC, ASEAN, etc.
Badili ya Kudai Tanganyika nayo ikawa na mamlaka yake ili iingiane mikataba ya haki na usawa katika muungano mnashika kuking'ang'ania kanchi kadogo kwa nguvu mkitawale. Kwa mantiki gani na nini hasa mnachokitafuta Zanzibar?
Hebu boresheni utawala katika majimbo ya Tanganyika hasa ya Kusini amabako Mungu amejaalia kuna rasilmali za kutosha kuinyanyua nchi badala ya juendesja siasa chafu za kikoloni.
Ritz, gombesugu, THE BIG SHOW, mfumo
Zanzibar
Tunapoteza muda hapa wa bure zanzibar hawataki muungano tena herufi kubwa.Dullyhami;
Hivi kweli unayoyasema yanatoka moyoni au akili yako tuu ulivyo uelewa huo Muungano na chokochoko zake? Mbona unawakingia kifua hao Wazenj kuwa sio wao walio anzisha chokochoko?
Wamejiandikia katiba yao ilokuwa imepotezwa na Muasisi wa huo Muungano, kama hilo halitoshi wakajitungia wimbo wa Taifa huru, ka hilo halitoshi wakajiundia majeshi yao na Mkuu wao wa Majeshi. Weye upo hapo? Ka hiyo haitoshi, wakasema, Twataka Dola yetu, Benki Kuu yetu na Sarafu yetu. Ni nchi moja tu duniani inatumia Fedha yake yenyewe ila ina value 2 tofauti. Tanzania. Umeona wapi, Fedha halali ya JMT na Fedha halali ya BMZ. Jamani, mambo mengine tuyaangalie. Haya yoote yanatendeka, Rais wa JMT yupo hai tena anasema yupo Ikulu ya JMT.
Kivumbi ni pale bunge lilipo mpindua Rais wa JMT na kumfanya sawa na rais wa BMZ. Ati, akitaka kufanya lolote, awasiliane na huyo wa BMZ. Na yule wa Tanganyika yupo wapi hapo???? Wazenj, kubalini msikubali, hakuna Muungano. Hata hiyo katiba mpya inayo andikwa, sijui Zanziba wanakaa na wanani. Kwa nini wajiandikie katiba mbili???? Kama haki ipo hiyo unayoisema, waanze kwanza kuiunda Tanganyika kwani Zanziba ipo, kwa nembo zao kuu walizojianzishia kama Taifa.
Hivyo Zanziba wamesha onesha wazi kuwa, Hawajajiunga na ushirika wowote ila wapo watu wanaojibalagaza kuwataka ushirika nao hao Wazenj hawawajui hao watu wanaojiita Tanzania Bara. Hilo ni Taifa gani? Tanzania Bara???!!! Ni wanani hao?
Nasema, Wajumbe wa hilo Bunge la katiba kama wana moyo mzuri na Taifa hili, waache kuendelea na hiyo Katiba. Ni kama Mama kwenda labour Ward na kulala huko akingojea mtoto kuzaliwa huku hamjui mume wala hana ujauzito. Ni maajab haya duniani. Wanajadili Katiba Mpya ya nchi gani?
Zanzibar waliuvunja muungano tangu 2010 walipoandika katiba yao.
Tanganyika haiwezi kulalamika kwavile imebadili jina na kujiita Tanzania. Ukiangalia kiundani utaona Tanganyika inaikoloni Zanzinzibar.
Sent from my GT-I9192 using Tapatalk
Maganjwa ndugu yangu kuna mengi nyuma ya Pazia la falsafa ya Muungano wetu wa Tanganyika na Zanzibar mm nahisi sio matakwa binafsi ya waasisi wetu wa muungano tu nahisi pia kulikuwa na shinikizo la Mataifa ya nje.Yaap umekuja kenye point. na suala muhim sana ilikuwa kuuliza watu je tuwe na muungano au tusiwe na muungano. hilo swali ni uhaini na kitu cha kuhioji ni je muungano uwe wa aina gani? umeona?
Binafsi sioni faida ya Muungano.Nitakuwa wa Mwisho kuutetea.
Natamani uvunjike hata leo.
Dullyhami;
Hivi kweli unayoyasema yanatoka moyoni au akili yako tuu ulivyo uelewa huo Muungano na chokochoko zake? Mbona unawakingia kifua hao Wazenj kuwa sio wao walio anzisha chokochoko?
Wamejiandikia katiba yao ilokuwa imepotezwa na Muasisi wa huo Muungano, kama hilo halitoshi wakajitungia wimbo wa Taifa huru, ka hilo halitoshi wakajiundia majeshi yao na Mkuu wao wa Majeshi. Weye upo hapo? Ka hiyo haitoshi, wakasema, Twataka Dola yetu, Benki Kuu yetu na Sarafu yetu. Ni nchi moja tu duniani inatumia Fedha yake yenyewe ila ina value 2 tofauti. Tanzania. Umeona wapi, Fedha halali ya JMT na Fedha halali ya BMZ. Jamani, mambo mengine tuyaangalie. Haya yoote yanatendeka, Rais wa JMT yupo hai tena anasema yupo Ikulu ya JMT.
Kivumbi ni pale bunge lilipo mpindua Rais wa JMT na kumfanya sawa na rais wa BMZ. Ati, akitaka kufanya lolote, awasiliane na huyo wa BMZ. Na yule wa Tanganyika yupo wapi hapo???? Wazenj, kubalini msikubali, hakuna Muungano. Hata hiyo katiba mpya inayo andikwa, sijui Zanziba wanakaa na wanani. Kwa nini wajiandikie katiba mbili???? Kama haki ipo hiyo unayoisema, waanze kwanza kuiunda Tanganyika kwani Zanziba ipo, kwa nembo zao kuu walizojianzishia kama Taifa.
Hivyo Zanziba wamesha onesha wazi kuwa, Hawajajiunga na ushirika wowote ila wapo watu wanaojibalagaza kuwataka ushirika nao hao Wazenj hawawajui hao watu wanaojiita Tanzania Bara. Hilo ni Taifa gani? Tanzania Bara???!!! Ni wanani hao?
Nasema, Wajumbe wa hilo Bunge la katiba kama wana moyo mzuri na Taifa hili, waache kuendelea na hiyo Katiba. Ni kama Mama kwenda labour Ward na kulala huko akingojea mtoto kuzaliwa huku hamjui mume wala hana ujauzito. Ni maajab haya duniani. Wanajadili Katiba Mpya ya nchi gani?
Zanzibar waliuvunja muungano tangu 2010 walipoandika katiba yao.
Hicho chakula munatugaiya bure ? Mbona hoja za kitoto ? Nyie wenyewe munakufa na njaamimi nimetoa kitu kitakachokea ila faida ya muungano utaiona siku muungano ukivunjika kama wewe wazenji watapata ndio wataopata shida zaidi itakuwa kama urusi na jimbo la cremia kutaka kujiuunga na urusi maana angalia ukubwa wa tanganyika na zanzibar kibiashara wataathirika sana sidhani kama chakula watajiweza wasije tanganyika mpakani lazima watozwe sawasawa.
Binafsi sioni faida ya Muungano.Nitakuwa wa Mwisho kuutetea.
Natamani uvunjike hata leo.