Sina hakika unayapata wapi haya uliyoyaandika. Kwamba ni illusions tu? Umeandika kwa kirefu, nitakujibu vivyo hivyo:
1. Hapana hiyo si thinking yangu. Ni jambo la kushangaza sana hata Ile kuwa na wazo tu. Kulikoni kunibashiria thinking zako ndugu?
"Sijui kwa nini mna makasiriko hivi?"
Kufanana kwa Wanaowanyanyapaa kina Mwabukusi na visa vya Yesu
Nini tofauti yenu na ya kisa cha kaka wa mwana mpotevu?
2. Unajielekeza kusiko. Maneno ya hekima haya yanaweza kukuhusu sana ndugu:
View attachment 2776334
Si busara hata kidogo kuwafikiria wengine namna ambayo kumbe yaweza kuwa inakuhusu wewe. Uswahilini wakisema nyani haoni k*ndule.
3. Kwani una maana hivi vyama vilivyopo kuna wenye hati miliki? Nani anataka kusajili vyama vingine? Kulikoni kujikita kwenye yasiyokuwapo?
Kama mkristo ninaweza kusali kwa Mzee wa upako, Rashid, kwa Mwamposa hadi TEC huko na nikapata upako vile vile.
"Hivi huwa hata mnasoma au hata kufuatilia au kujitahidi kuelewa lolote? Wekeni makasiriko pembeni ndugu, mtaweza kuona vizuri.
Agenda zake kasema ni hizi hapa;
1. Katiba mpya ni sasa.
2. Hakuna katiba mpya, hakuna uchaguzi.
3. Bandari haziko sokoni.
"Kwani wewe hutaki katiba mpya? Kwani wewe ni dalali wa DP world?"
4. Hili ni jambo jingine la kushangaza mno. Wewe si Mwabukusi. Unaweza vipi hata kufikiria kuwa yeye?
Ushauri wa bure kwako:
"Wewe si uutumie huo ushauri wako mzuri, Ili ukafanye vyema zaidi? Tukikuelewa utatuona tu wala hutatuita."
"Mwabukusi hajatuita bali tumemwona kwenye tunayosimama nayo tukamwelewa."
Zingatia uzi huu ni wa Machi 21, 2023:
Uchaguzi 2024/25 wa nini kama hakuna Katiba Mpya?
Kumbe basi, nani anamwunga mkono nani? Kumwunga mkono mtu ni haki ya mtu yeyote.
Tushindane kwa hoja. Hoja haipingwi jwa rungu
Wapi kawa rival na Chadema? Ushahidi uko wapi? Wengine sisi hatu advocate rivalry:
"Hatuna adui wa kudumu wala rafiki.'
Habari ndiyo hiyo.