Mwaka 1989 ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kutapeliwa jijini Dar es Salaam

Mwaka 1989 ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kutapeliwa jijini Dar es Salaam

Mkuu hiyo 1989 form 4 ilikuwepo? Maana Babu yangu aliishia Darasa la 4na kuandika na kusoma Kiingereza anajua, alisema alivyo itimu Darasa la 4 aka ajiriwa Serikalini.
Babu yako alianza shule na kumaliza hilo la 4 mwaka gani mkuu?
 
Hapana mkuu maana alisena 1989 alitumwa Dukani ina maana kwa ukadilia alikuwa na umria kuanzia miaka 10, huyo atakuwa kazaliwa si chini ya 1975
Nilikuwa na 7 mkuu, ila nakumbuka mengi yaliotokea miaka hiyo. Japo kwa umri huo ilikuwa ngumu kujua zuri na baya.
 
Mbali na wale wanaonipigia simu na kuhitaji msaada sidhani kama nilishatapeliwa physically
Una bahati sana pengine umekulia katika kipindi hiki ambacho kila kitu sasa kinajulikana. Ni tofauti na sisi wakati huo utapeli nahisi ndo ulikuwa unazaliwa.

Lakin pia na udogo ulichangia. Mtoto wa miaka 7-8-9 hadi 10 ilikuwa ngumu sana kujua swala la kutapeliwa haswa muhusika anapoonesha kukujua wew, ndugu zako na wazazi wako.
 
Ndugu nadhan huo ulikuwa ndo utapeli wa kipind hicho Dar,na mimi nilitapeliwa kwa namna hiyo mwaka 1992 bado nikiwa hata darasa la kwanza sijaanza,mimi nilitumwa na mama,kipindi hiko mzee yupo Arusha.

Nilitumwa na mama dukan nakumbuka nilipewa elf kumi ile ya blue,ile nmetoka kununua kitu cha kwanza ilikuwa nyama natoka buchani niende kwenye kununua vitu vingine nikiwa nimeshikilia chenji,kuna jamaa akaniita akaniamba wewe si una baba yako yupo arusha,nikamjibu ndiyo akaniambia kuna mzigo kanipa niulete kwenu kwa vile nimekuona ngoja nikupe uende nao,na mimi kwavile nilikuwa bado mdogo nikamwamini kwel anamjua mzee.

Basi bana akaniambia lete hizo hela na ile nyama ili anishikie ili nisije kuangusha then akaniambia niende umbali wa mita 300 kuwa kuna mwembe kuna mtu utamkuta atakupa huo mzigo then uje hapa uchukue vitu vyako uendelee na manunuzi mengine ya vitu vilivyobaki.

Nimeenda mpka kwenye ule mwembe sioni mtu,kuulizia watu pemben wanasema hawaelew kinachoendelea,ile kurudi mpka sehemu nilipomwacha jamaa sikumkuta,jamaa alishayeya

Kurudi hom na kilio kumwambia maza haelew,aliyeniokoa nisipate bakora za maza ni bibi aliyekuwa katutembelea,ila jamaa nilikuja kumuona tena.miaka ya 2000 nikiwa sekondari

Huu utapeli walipigwa sana wauza mayayi na koni miaka hiyo 90s. Wanajifanya waganga wanakusugua utosini unatoka moshi au unatema nywele wanakuambia umelogwa , wanakuambia acha vitu vyako vyote pesa,mayai au koni halafu nenda kachote mchanga kule uje nao ili tukutibu. Ukianza kwenda tu jamaa wanasepa na vitu vyako vyote 🤣 🤣.
 
Huu utapeli walipigwa sana wauza mayayi na koni miaka hiyo 90s. Wanajifanya waganga wanakusugua utosini unatoka moshi au unatema nywele wanakuambia umelogwa , wanakuambia acha vitu vyako vyote pesa,mayai au koni halafu nenda kachote mchanga kule uje nao ili tukutibu. Ukianza kwenda tu jamaa wanasepa na vitu vyako vyote 🤣 🤣.
Yah huu utapeli unaosema hapa ulikuja baadae miaka ya 95 to 2000.

Kuna jirani yetu mtu mzima na akili zake alitapeliwa baskeli K'koo baada ya kukutana na jamaa aliejifanya mganga wa kienyeji anataka kumsaidia 😂😂😂
 
Yah huu utapeli unaosema hapa ulikuja baadae miaka ya 95 to 2000.

Kuna jirani yetu mtu mzima na akili zake alitapeliwa baskeli K'koo baada ya kukutana na jamaa aliejifanya mganga wa kienyeji anataka kumsaidia 😂😂😂

Utapeli wa baiskeli wa aina hii ulikuwa Common sana. Hata wale wa koni walitapeliwa pesa, koni na baiskeli.
 
Utapeli wa baiskeli wa aina hii ulikuwa Common sana. Hata wale wa koni walitapeliwa pesa, koni na baiskeli.
Inawezekana hata gari pengine kuna watu walitapeliwa, sema hatukuwahi kushuhudia au kupata story zao 😂😂
 
Back
Top Bottom