Mwaka 1989 ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kutapeliwa jijini Dar es Salaam

Mkuu hiyo 1989 form 4 ilikuwepo? Maana Babu yangu aliishia Darasa la 4na kuandika na kusoma Kiingereza anajua, alisema alivyo itimu Darasa la 4 aka ajiriwa Serikalini.
Babu yako alianza shule na kumaliza hilo la 4 mwaka gani mkuu?
 
Hapana mkuu maana alisena 1989 alitumwa Dukani ina maana kwa ukadilia alikuwa na umria kuanzia miaka 10, huyo atakuwa kazaliwa si chini ya 1975
Nilikuwa na 7 mkuu, ila nakumbuka mengi yaliotokea miaka hiyo. Japo kwa umri huo ilikuwa ngumu kujua zuri na baya.
 
Mbali na wale wanaonipigia simu na kuhitaji msaada sidhani kama nilishatapeliwa physically
Una bahati sana pengine umekulia katika kipindi hiki ambacho kila kitu sasa kinajulikana. Ni tofauti na sisi wakati huo utapeli nahisi ndo ulikuwa unazaliwa.

Lakin pia na udogo ulichangia. Mtoto wa miaka 7-8-9 hadi 10 ilikuwa ngumu sana kujua swala la kutapeliwa haswa muhusika anapoonesha kukujua wew, ndugu zako na wazazi wako.
 

Huu utapeli walipigwa sana wauza mayayi na koni miaka hiyo 90s. Wanajifanya waganga wanakusugua utosini unatoka moshi au unatema nywele wanakuambia umelogwa , wanakuambia acha vitu vyako vyote pesa,mayai au koni halafu nenda kachote mchanga kule uje nao ili tukutibu. Ukianza kwenda tu jamaa wanasepa na vitu vyako vyote 🀣 🀣.
 
Yah huu utapeli unaosema hapa ulikuja baadae miaka ya 95 to 2000.

Kuna jirani yetu mtu mzima na akili zake alitapeliwa baskeli K'koo baada ya kukutana na jamaa aliejifanya mganga wa kienyeji anataka kumsaidia πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Yah huu utapeli unaosema hapa ulikuja baadae miaka ya 95 to 2000.

Kuna jirani yetu mtu mzima na akili zake alitapeliwa baskeli K'koo baada ya kukutana na jamaa aliejifanya mganga wa kienyeji anataka kumsaidia πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Utapeli wa baiskeli wa aina hii ulikuwa Common sana. Hata wale wa koni walitapeliwa pesa, koni na baiskeli.
 
Utapeli wa baiskeli wa aina hii ulikuwa Common sana. Hata wale wa koni walitapeliwa pesa, koni na baiskeli.
Inawezekana hata gari pengine kuna watu walitapeliwa, sema hatukuwahi kushuhudia au kupata story zao πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…