Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya Sekondari ya Serikali. Waliobahatika walijulikana kata nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya Sekondari ya Serikali. Waliobahatika walijulikana kata nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

Sasa hivi C mbili na D moja unaingia advance
Tena unaweza kuta C za civics na nutrition, D ya Bible/Islamic knowledge

Chuo E mbili

Akitoka hapo hataki kazi za bodaboda, eti anataka kazi za hadhi yake, hivi wana hadhi gani hawa mbwa!!!!
Umesikitisha Sana kuita watu mbwa....

Kuna watu wanafaulu Sana makaratasi alaf maisha Yana wapiga knot out.....

Mungu ameumba watu tofaut tofauti....Kuna jamaa chuo Kikuu nilikua na mwacha mbali kweny matokeo GPA....
Ila mm binafsi nilikua namkubali Sana tulikua tuna mwita Kitivo.... A.k.a profesa...
kweny content yupo vizuri sanaa....Ila ndio ivyo Ni mkali Ila GPA 2.O

Usiite watu mbwa bwanaaaa!!
 
Enzi zetu kwa Dar shule zilikuwa nne tu basi yaani Pugu,Minaki,Tambaza,Azania hakukuwapo na Benjamini Mkapa.
Mtoto wa kiume unatakiwa ukaze ili uende angalau hata Aza Boy.

Ila binafsi nilichaguliwa Ilboru kata nzima nilikuwa mwenyewe ila DsM nzima tulikuwa watatu tu.

Advance tukatupwa mzumbe pale kwa DsM tulikuwa wa tano mkoa mzima.
Forodhani na kibasila umezisahau
 
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi..
1970s kulikuwa na shule za binafsi? Wapi hiyo?

Wilayani kwetu mimi early 1990s kulikuwa na shule ya wazazi tu kama mbadala huku ‘wanaochaguliwa’ kwenda Secondary za Serikali kutoka kila shule hamzidi watu 8. Yaani the battle was cut-throat.

Nakumbuka vichwa vingi kadhaa ilibidi viachwe tu maana hapakuwa na namna nyingine
 
Mimi mwaka niliomaliza STD 7 hapo dar shule zilikuwa Ni hizi tu

Azania
Benjamin William mkapa
Dar es salaam sec
Kambangwa
Kisutu
Kibasila
Zanaki
Jangwani
Kiluvya
Chang'ombe
Forodhani
Tambaza ( a level tu)

Ukikosa hizi we umeshafeli [emoji1787][emoji1787]

Otherwise uende kipaji maalumu
Pugu umesahau
 
Sasa hivi C mbili na D moja unaingia advance
Tena unaweza kuta C za civics na nutrition, D ya Bible/Islamic knowledge

Chuo E mbili

Akitoka hapo hataki kazi za bodaboda, eti anataka kazi za hadhi yake, hivi wana hadhi gani hawa mbwa!!!!
Chuo kipi E mbili, acha uongo
 
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi tofauti na hivi sasa ambapo wanafunzi wa private ndio wanaheshimika.

Je, kauli hii ina ukweli wowote ndani yake?
Kumbe we bado dogo Sana.

Ni kweli tuliochaguliwa gov. Schools tulionekana Tofauti, lakini form Two na form Four tuliwaacha wengi
 
Kwa miaka ya hivi karibuni, hata mimi nilistaajabishwa na jinsi wizara ya elimu wanavyojitahidi kuwapangia wanafunzi shule, kutokana na ufaulu wao. Hapa naongelea matokeo ya kidato cha nne. Kulikuwa na vijana mbalimbali, wewe mikondo mbalimbali na ufaulu tofauti tofauti, kuanzia daraja la kwanza mpaka la tatu.

Nikashuhudia waliochaguliwa katika mkupuo wa kwanza, walipelekewa kidato cha tano, wengine chuoni, muda ukapita wengine wa daraja la tatu na nne wakiwa mtaani. Mara uchaguzi mkupuo wa pili ukaja, hapa waliochaguliwa kwa kuzingatia kile mtu alichofaulu, mfano mtu alifeli hesabu, uhasibu, biashara, jiografia, ila akawa na ahueni katika Kiswahili, Kiingereza na Historia. Basi akapelekwa kidato cha tano HKL.
Serikali imejitahidi sana kwa kweli...
 
Uzi umenikumbusha mbali sana, Tanga mjini miaka ya 2002 kurudi nyuma shule za secondary zilikua nne tu , Usagara Sec, Tanga school (hii ilichukua vipaji) Galanos na Mkwakwani. Yaani hapo ilikua ukichaguliwa ujue we mwanaume hasa. Shule nyingi za primary zilikua na wanafunzi wanaomaliza la 7 zaidi 100 lkn wanaochaguliwa kwenda sekondari hawazidi 20. Hivyo kujihakikishia nafasi lazima uhakikishe upo ndani ya top 10 darasani

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
USS
FB_IMG_1601732912269.jpg
 
Ukweli ni kuwa hapo zamani watu wengi wamekosa nafasi ya kusoma secondary school sio kwa sababu ya kutofaulu bali sababu ya uchache wa shule za sekondari.

Unakuta wilaya nzima kuna shule moja ya sekondari halafu shule za msingi zaidi ya120.Ilikuwa jambo la kawaida kukuta shule yote haijatoa hata mwanafunzi mmoja wa kujiunga kidato cha kwanza.

Kwa kweli aliyeleta shule za kata alifanya jambo la maana sana pamoja na changamoto zake. Kujivunia ule uzamani ambao uliwanyima wenzetu nafasi za kusoma na sababu kubwa ikiwa ni ukosefu wa shule za sekondari unakuwa sio uzalendo
Umenena kiutuuzima sana. Nadhani bila ya uwepo wa shule za Private katika nyakati zile wengi wetu tungelikosa fursa ya kupata elimu, ambayo kwa kiasi kikubwa imekuwa na maana sana katika maisha yetu katika nyakati za sasa.
 
Uzi umenikumbusha mbali sana, Tanga mjini miaka ya 2002 kurudi nyuma shule za secondary zilikua nne tu , Usagara Sec, Tanga school (hii ilichukua vipaji) Galanos na Mkwakwani. Yaani hapo ilikua ukichaguliwa ujue we mwanaume hasa.
Kuna jamaa yangu alisomaga hapo Galanos Advanced Level...
 
Back
Top Bottom