Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,892
- 16,476
- Thread starter
- #241
Mkuu, kumbe mimi ni mkubwa sana kwakoNasubiri picha ya shule yangu Ndanda boys ingawa mimi sikumaliza 1999 kurudi nyuma!!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu, kumbe mimi ni mkubwa sana kwakoNasubiri picha ya shule yangu Ndanda boys ingawa mimi sikumaliza 1999 kurudi nyuma!!
Hahahahahaaaaa, soda ya VINTO zamani sana hii mkuuNakumbuka bi mkubwa alipika pilau na soda vimto. Mtoto kapasi
1992 mkuu wakati huo vijana wa kiume wanavaa kaptula mpk form sixHahahahahaaaaa, soda ya VINTO zamani sana hii mkuu
Mkuu, umekosea sana kuwaita binadamu wenzio MBWASasa hivi C mbili na D moja unaingia advance
Tena unaweza kuta C za civics na nutrition, D ya Bible/Islamic knowledge
Chuo E mbili
Akitoka hapo hataki kazi za bodaboda, eti anataka kazi za hadhi yake, hivi wana hadhi gani hawa mbwa!!!!
Daaah, zamani ilikuwa ni shiiiida mkuutulitoka Burka primary school tukaenda Arusha secondary school, tulikuwa saba tu kati ya watoto mia tatu ila tulivyunja rekodi
shida tupu, shule zilikuwa chache mno hivyo ili uchaguliwe yakupasa ufanye vizuri kweli, tena hususana masomo mazuri kama hisabati na sayansi kwa ujumla wake, ni mazuri na ni matamu ,sio magumuDaaah, zamani ilikuwa ni shiiiida mkuu
Kumbe na wewe umepashtukia Mwl.Lugalo Secondary , mwaka gani hiyo boss?
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa JamiiForums.
Ndugu zangu watanzania;
Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya secondary ya serikali. Wachache waliobahatika walijulikana kata/tarafa nzima. Je, wewe ni mmoja wao?
TABORA BOYS SECONDARY SCHOOL
View attachment 1661676
Juzi kuna mtoto wa jirani yangu alinifuata akaniambia brother ninaomba uniangalizie matokeo yangu ya darasa la saba. Mimi bila hiyana na smartphone yangu hii nikaingia katika website ya necta nikamuangalizia fresh tu. Dogo bwana alipata C flat masomo yoooote.
Nikajua ndio basi tena. Baada ya selection ya shule kutoka nikasikia huyu dogo amepangiwa shule moja ya kata mwendo kama wa dakika 20 kutoka hapa tunapokaa, ndio nikajisemea kimoyomoyo hakika dunia imebadilika kwa kasi sana.
Yaaani mtu anapata C flat bado anaenda secondary? Ninakumbuka dada yangu aliyeniachia ziwa, sasa hivi ni engineer, yeye ni moja kati ya wanafunzi 4 waliofaulu kwenda secondary shule ya serikali. Kumbuka enzi hizo kuchaguliwa tulikuwa tunaita kufaulu.
Yaaani wewe ukichaguliwa unaonekana umefaulu na wale ambao hawakuchaguliwa wanaonekana wamefeli ingawa kiuhalisia hawakuwa wamefeli ila shule zilikuwa ni chache mnoooo kiasi kwamba ni ngumu ku-accomodate wanafunzi wooote waliofaulu.
View attachment 1661678
Dada yangu alifaulu wakati huo baba anafanya kazi Wilaya ya ******* Mkoa wa Mbeya. Watu walifurahi familia nzima, lilipikwa pilau kana kwamba kuna sherehe ya kipaimara. Ndugu waliokuwa wanaishi karibu walikuja kumpa pongezi dada utadhani labda amejifungua mtoto.
Dada alikuwa maarufu sana kwa maana akiwa anaenda shuleni basi ni yeye tu ndiye aliyekua anaonekana asubuhi amevaa sare wakati huo wenzake aliomaliza nao darasa la saba bado wamelala au wameenda shambani.
Mgeni aliyekuwa hapafahamu nyumbani akiwa anaulizia kwa mama fulani wenyeji wanaanza kudadisi kwa kuambiana "au yule mama mjaluo ambaye mwanae anasoma secondary". Kwenda secodary ya serikali ilikuwa ni umaarufu kama dereva kwa maana enzi zile hakuna gari ya automatic transmission.
Gari zote ni manual na anayeweza kuendesha ni mzee mmoja au wawili tu mtaa mzima. Wanafunzi wa secondary walikuwa maarufu kama madereva kutokana na uchache wao.
View attachment 1661682
Matokeo yalikuwa yanasubiriwa kwa hamu na shauku kubwa sana kwa maana matokeo na selection zilikuwa zinakuja kwa pamoja tofauti na sasa hivi ambapo matokeo yanaanza kutoka na mwanafunzi au mzazi wake anaingia katika internet kisha baada ya mwezi mmoja mbele ndio selection inatangazwa.
Je, wewe ni mmoja ya wanafunzi wachache waliobahatika miaka ya 1990?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Daah, nililia sana nilipokosa kwenda Tabora Boys na badala yake kuchaguliwa Iyunga. Ila nilipofika, nikasema Mungu mkubwa kwani booonge ya shule kumbe. Early 1990's hiyo.
Siku hizi secondary bwerere sana mpaka rahaHiyo iko poa kama ulivyo wasilisha.
Wakongwe hua wanasema hayo yote.
Kwa sisi ambao tuko bado shule kama tunavyo ingia sekondari sana ilichaguliwa shule ya serikali kawaida ila waliopo shule binafsi ndio wanajiona wao ndio wao
Safi sana mkuu...Tulipasua vibaya saana....nakumbuka wilaya nzima tulikiwa 15 tu tulijulikana!! Moshi Tech, Bihawana, Msalato, Weruweru; Tabora Boyz / Girls....
Wakati huo elimu under Mwalimu ilikuwa na hadhi...ukiwa form one ukirudi likizo kwenye msiba kijijini basi unakaa na wazee wa heshima eee wazee wastaafu na walimu na watumishi wa Serikali kama katibu kata / tarafa; Mratibu wa Elimu etc
Sawa baba....nitarudi.
Vice versanikweli kabisa....wale wanoenda private tuliwaita wamefail..sie wa serikali tumefaulu...lkn kwa sasa kibao kimegeuka.
Hongera mkuu1980 Njombe secondary nilienda peke yangu kwenye wilaya niliotoka
Siku hizi tofauti kidogoNi zaidi ya ukweli, ulikuwa huwezi kuwakalisha pamoja mwanafunzi wa Geita sekondari na wa Sengerema secondary.
Kabisa nasikia walikua wanaweza kuchaguliwa watu kumi tu wilaya nzima mzee wangu alisoma tabora boys na kumaliza mwaka 1979WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi tofauti na hivi sasa ambapo wanafunzi wa private ndio wanaheshimika.
Je, kauli hii ina ukweli wowote ndani yake?
Mkuu usiwaite Mbwa ,siyo poaKwa chuo kwa sasa lazima uwe na D mbili na kuendelea
Amemaanisha A- level.Hizo bado zilikuwa na O level tuJangwani na Zanaki,kisutu na Forodhani,Kibasila hazikua Secondary?,naanza kupata wasiwasi na wewe