Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya Sekondari ya Serikali. Waliobahatika walijulikana kata nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

Ni kweli, mimi ni mmojawapo ingawa si miaka ya 90, ilikuwa miaka ya 2000 enzi za tano kwanza ya Mkwere.

Nilibahatika kuwa mwanafunzi pekee kuchaguliwa shule ya Bweni huko Rock City. Baada ya matokeo kutoka na kupewa habari nilipigwa na butwaa kwa kujawa na furaha isiyokuwa na kifani. Kwani ndio ndoto yangu ya kwenda kulifahamu jiji la Mwanza ndio ilikuwa inaenda kutimia. Mara zote nilikuwa naisikia tu Mwanza redioni kupitia Redio Free Africa(RFA) hasa katika vipindi vyake maarufu wakati huo vya SITASAHAU(kila jumapili), DARUBINI, JE WAJUA? N.K

Cha kushangaza sasa baada ya kufika jijini na kuishi huko kwa kipindi chote cha Masomo sikuwahi kufika RFA[emoji23][emoji23][emoji23]
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mkuu umenionesha bweni langu la Kimweri hapa Tabora boys kwa chini huku uwanjani kuna choo kinanuka ukitaka kuingia lazima uvue nguo zote nje ndio uingie vinginevyo ukitoka wenzako wanakukimbia
Hata shule niliyosoma mimi pia kulikuwa na choo kinachonuka maana kilikuwa kikongwe sana.

Protocols ya kuingia pale ilikuwa ni lazima uvue nguo zote na kuziacha nje.
 
Wakati huo kupangiwa shule kama 'uboyzini' ilibidi uwe 'kipanga' kama CCNP Engineer
Naam Naam... Form one ukifika unakutana na wenzio waliongoza mkoa/wilaya walizotoka.
Wote vichwa. Mimi niliongozaga mkoa wa Shinyanga. Mshikaji nilikua nashindana nae alikua wa pili kimkoa, akaenda Kibaha.
Tuliendeleza ligi watu wakawa wanasubiri NECTA ya form four waone nani atamkimbiza mwenzie.
 
Reactions: Pep
Ilikua ni kufaulu au lugha nyingine ku pass. Mimi tulikua watatu tu darasa zima. Hata hivyo wapo baadhi waliofeli tukawaacha kijijini wana maisha bora sana,na tena wana amani kupita mfano. Tofauti na mimi ambaye leo nikisikia Jaffo anakuja nahisi tumbo la kuhara. Ujiko wote kwamba nina akili kuliko tarafa nzima haujanisaidia chochote.
 
Walipoanza kuleta mamitihani ya OMR ya kuzungushia jibu ndio wakaharibu kabisa

Mwanafunzi anaweza piga hata ana ana dooh!! Na akapata jibu[emoji1]

Matokeo makubwa Sasa (Big results Now[emoji1])

Advocate wake akiwa yule waziri wa Tanzania=Tanganyika+Zambia[emoji1787][emoji1787]
 
Halafu wanafunzi Wa kipindi hicho tulikuwa na Akili sana tofauti kabisa na hawa Wa sasa
 
Tanzania imetoka mbali sana mkuu
 
Jangwani na Zanaki,kisutu na Forodhani,Kibasila hazikua Secondary?,naanza kupata wasiwasi na wewe
Jangwani, Zanaki, Kisutu ilikuwa ni Wasichana tu.

Maza wangu alibukua Zanaki
 
Siku iz unakuta kidato kimoja lima students 637 πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
ule woote ulikuwa umasikini tu....shule tunapima uelewa na sio kutaulu mitihani..mashule yapaswa kufundisha uelewa na kupima uelewa zaidi..

Hii na ile stayle ya watu kufanya mtihani mmoja kuandika waliyokalili ni kama kupiga ramli tu
 
Baada ya kumaliza darasa la Saba wakati ninasubiri matokeo mzee alinipeleka sehemu nijifunze kushona suti, mwalimu wangu alikuwa katili mno vibao vya nguvu vilitua kwenye shavu langu pindi nilipoangalia kwingine tofauti na kumuangalia anavyoshona. Hali hii iliniathili kisaikolojia kila wakati sikuwa na amani, matokea yalivyotoka nilikuwa nimechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza Kijiji kizima nilianza kuonekana kama mtu special hata yule mwalimu wangu wa kushona suti alianza kuniheshimu. Wazazi wangu walianza kuhofia kuwa huenda mwanao atalogwa maana shule nzima wamechaguliwa wanafunzi watatu tu, siku hizi cha kushangaza hata wasiojua kusoma na kuandika wanafaulu kwenda sekondari.
 
Kwahiyo kufaulu wachache na kufaulu wengi kipi bora?. Yani kipi bora wachache waelimike au jamii nzima ielimike?. Acheni husda ngoja maisha yawanyooshe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…