Zero Hours
JF-Expert Member
- Apr 1, 2011
- 12,942
- 18,669
Safi Sana, naona ulikuwa njema sana Boss, hongera zako
Hahah DsM ndio walikuwa wanatoka wengi mikoa mingine mmoja au wawili au hakuna.Watano mkoa mzima sio mchezo mkuu. Na hapo ni Dar tu mkoa wa serikali, vp hiyo mikoa mingine? Si unakuta anatoka mmoja tu wa kwenda huko Mzumbe?
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi tofauti na hivi sasa ambapo wanafunzi wa private ndio wanaheshimika.
Je, kauli hii ina ukweli wowote ndani yake?
Simu enzi hizo zilikuwa zile za posta na simu,zile za mezani ikiita mnakimbilia atakae wahi kulipokea,na ukipokea lazima uanze kwa kusema Halooo,shikamoo,nani mwenzangu,sasa ole wako uulize we nani? Utagombezwa mpaka ujute.Unakuta sanduku la posta hilo moja linatumiwa na watu kibao mpaka ndugu yake na rafiki yako wa kazini...
Juzi kuna. Denti nimeonana nae ni mtoto wa jirani yangu nikamuuliza kuhusu matokeo akanijibu wamefauli darasa zima kasoro mmoja nikasema kazi ipo
2003 nipo chuo dogo ,Arusha sec ya headmaster Don king, ilboru nilipafaidi A level kipindi hicho Arusha sec hamna AdvanceMwaka gani hiyo mkuu?me 2003 ndiyo nimeanza form 1 hapo arusha secondary school nikitokea Naura primary school.Enzi hizo Arusha kuna shule tano tu za secondary ambazo ni Arusha sec,Arusha day,Kaloleni,Sinoni na Ilboru(hii ilikuwa ya vipaji maalumu)
[emoji33]1980 Njombe secondary nilienda peke yangu kwenye wilaya niliotoka
Ni kweli, wakati ule tuliokuwa tunasoma shule za serikali tuliheshimika Sana wale waliokuwa wanasoma shule za binafsi walihesabika kuwa walifeli ndo maana wakaenda kusoma private.WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi tofauti na hivi sasa ambapo wanafunzi wa private ndio wanaheshimika.
Je, kauli hii ina ukweli wowote ndani yake?
Unashangaa nini kijana wangu[emoji33]
Ndio mimi ni mmoja wao. Kati ya wanafunzi 90 tuliomaliza shule ya msingi Magereza Moshi tulichaguliwa wawili (2) tuu kwenda Form I Mawenzi Secondary School.Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa JamiiForums.
Ndugu zangu watanzania;
Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya secondary ya serikali. Wachache waliobahatika walijulikana kata/tarafa nzima. Je, wewe ni mmoja wao?
TABORA BOYS SECONDARY SCHOOL
View attachment 1661676
Juzi kuna mtoto wa jirani yangu alinifuata akaniambia brother ninaomba uniangalizie matokeo yangu ya darasa la saba. Mimi bila hiyana na smartphone yangu hii nikaingia katika website ya necta nikamuangalizia fresh tu. Dogo bwana alipata C flat masomo yoooote.
Nikajua ndio basi tena. Baada ya selection ya shule kutoka nikasikia huyu dogo amepangiwa shule moja ya kata mwendo kama wa dakika 20 kutoka hapa tunapokaa, ndio nikajisemea kimoyomoyo hakika dunia imebadilika kwa kasi sana.
Yaaani mtu anapata C flat bado anaenda secondary? Ninakumbuka dada yangu aliyeniachia ziwa, sasa hivi ni engineer, yeye ni moja kati ya wanafunzi 4 waliofaulu kwenda secondary shule ya serikali. Kumbuka enzi hizo kuchaguliwa tulikuwa tunaita kufaulu.
Yaaani wewe ukichaguliwa unaonekana umefaulu na wale ambao hawakuchaguliwa wanaonekana wamefeli ingawa kiuhalisia hawakuwa wamefeli ila shule zilikuwa ni chache mnoooo kiasi kwamba ni ngumu ku-accomodate wanafunzi wooote waliofaulu.
View attachment 1661678
Dada yangu alifaulu wakati huo baba anafanya kazi Wilaya ya ******* Mkoa wa Mbeya. Watu walifurahi familia nzima, lilipikwa pilau kana kwamba kuna sherehe ya kipaimara. Ndugu waliokuwa wanaishi karibu walikuja kumpa pongezi dada utadhani labda amejifungua mtoto.
Dada alikuwa maarufu sana kwa maana akiwa anaenda shuleni basi ni yeye tu ndiye aliyekua anaonekana asubuhi amevaa sare wakati huo wenzake aliomaliza nao darasa la saba bado wamelala au wameenda shambani.
Mgeni aliyekuwa hapafahamu nyumbani akiwa anaulizia kwa mama fulani wenyeji wanaanza kudadisi kwa kuambiana "au yule mama mjaluo ambaye mwanae anasoma secondary". Kwenda secodary ya serikali ilikuwa ni umaarufu kama dereva kwa maana enzi zile hakuna gari ya automatic transmission.
Gari zote ni manual na anayeweza kuendesha ni mzee mmoja au wawili tu mtaa mzima. Wanafunzi wa secondary walikuwa maarufu kama madereva kutokana na uchache wao.
View attachment 1661682
Matokeo yalikuwa yanasubiriwa kwa hamu na shauku kubwa sana kwa maana matokeo na selection zilikuwa zinakuja kwa pamoja tofauti na sasa hivi ambapo matokeo yanaanza kutoka na mwanafunzi au mzazi wake anaingia katika internet kisha baada ya mwezi mmoja mbele ndio selection inatangazwa.
Je, wewe ni mmoja ya wanafunzi wachache waliobahatika miaka ya 1990?
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Mkuu member wengi wa JF Wana angalau elimu ya secondary.Aisee, kwenye huu uzi kila mtu anasema alifaulu.
Jf raha sana, ukianzisha mada ya magari basi kila mtu atasema analo.
siyo elimu tu wanaufahamu kuliko hao viongozi wenu serikaliniMkuu member wengi wa JF Wana angalau elimu ya secondary.
Usifikiri wana ongopa.
Vipi wee mbna umeandila kwa jazba sana? [emoji23][emoji23][emoji23]Sasa hivi C mbili na D moja unaingia advance
Tena unaweza kuta C za civics na nutrition, D ya Bible/Islamic knowledge
Chuo E mbili
Akitoka hapo hataki kazi za bodaboda, eti anataka kazi za hadhi yake, hivi wana hadhi gani hawa mbwa!!!!