Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya Sekondari ya Serikali. Waliobahatika walijulikana kata nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya Sekondari ya Serikali. Waliobahatika walijulikana kata nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

Hata iyo c flat kabebwa tu. Matoto ya sikuizi yanamakiza secondary hata hayajui kusoma na kuandika mengine
 
Natafhimini ya ufaulu miaka hiyo unaulizwa shule yenu mwaka Jana imefaulisha wangapi unajibu 20 na we we unashika wa ngapi unajibu kumi bora utafauli ila ukijibu 40 utafeli
 
Safi Sana, naona ulikuwa njema sana Boss, hongera zako

Watano mkoa mzima sio mchezo mkuu. Na hapo ni Dar tu mkoa wa serikali, vp hiyo mikoa mingine? Si unakuta anatoka mmoja tu wa kwenda huko Mzumbe?
Hahah DsM ndio walikuwa wanatoka wengi mikoa mingine mmoja au wawili au hakuna.

Harafu wanafunzi wote mnafahamiana mpk wale wa shule zingine na mikoa mingine maana kila mtu anatoka ameongoza kijiji au wilaya au mkoa.
Unakuta mtu yupo Mzumbe form 4 lakini anawajua wanafunzi wote wa form 4 Ilboru au Tabora huko noma sana wee hacha tu.

Ushindani ulikuwa wa hali ya juu watu special school ukimaliza bila kuwa kichaa shukuru Mungu tu maana unalogwa na kijiji kizima😂😂😂😂
 
Ni kweli
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi tofauti na hivi sasa ambapo wanafunzi wa private ndio wanaheshimika.

Je, kauli hii ina ukweli wowote ndani yake?
 
Unakuta sanduku la posta hilo moja linatumiwa na watu kibao mpaka ndugu yake na rafiki yako wa kazini...
Simu enzi hizo zilikuwa zile za posta na simu,zile za mezani ikiita mnakimbilia atakae wahi kulipokea,na ukipokea lazima uanze kwa kusema Halooo,shikamoo,nani mwenzangu,sasa ole wako uulize we nani? Utagombezwa mpaka ujute.
WHEN LIFE WAS LIFE.
 
Juzi kuna. Denti nimeonana nae ni mtoto wa jirani yangu nikamuuliza kuhusu matokeo akanijibu wamefauli darasa zima kasoro mmoja nikasema kazi ipo

Hahahaha! Eti kazi ipo, labda mitihani ya siku hizi ni mtelezo.
 
Mwaka gani hiyo mkuu?me 2003 ndiyo nimeanza form 1 hapo arusha secondary school nikitokea Naura primary school.Enzi hizo Arusha kuna shule tano tu za secondary ambazo ni Arusha sec,Arusha day,Kaloleni,Sinoni na Ilboru(hii ilikuwa ya vipaji maalumu)
2003 nipo chuo dogo ,Arusha sec ya headmaster Don king, ilboru nilipafaidi A level kipindi hicho Arusha sec hamna Advance
 
Sera za Elimu zinabadirika.
Kwa sasa "elimu ya msingi" ni mpaka kidato cha nne.
 
1609307065953.png

1609307082464.png


1609307134160.png
1609307082464.png
 
Hao Jamaa walio soma enzi hizo waliofanikiwa kujuinga olevel walikua vichwa sana
 
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi tofauti na hivi sasa ambapo wanafunzi wa private ndio wanaheshimika.

Je, kauli hii ina ukweli wowote ndani yake?
Ni kweli, wakati ule tuliokuwa tunasoma shule za serikali tuliheshimika Sana wale waliokuwa wanasoma shule za binafsi walihesabika kuwa walifeli ndo maana wakaenda kusoma private.
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa JamiiForums.

Ndugu zangu watanzania;

Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya secondary ya serikali. Wachache waliobahatika walijulikana kata/tarafa nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

TABORA BOYS SECONDARY SCHOOL
View attachment 1661676

Juzi kuna mtoto wa jirani yangu alinifuata akaniambia brother ninaomba uniangalizie matokeo yangu ya darasa la saba. Mimi bila hiyana na smartphone yangu hii nikaingia katika website ya necta nikamuangalizia fresh tu. Dogo bwana alipata C flat masomo yoooote.

Nikajua ndio basi tena. Baada ya selection ya shule kutoka nikasikia huyu dogo amepangiwa shule moja ya kata mwendo kama wa dakika 20 kutoka hapa tunapokaa, ndio nikajisemea kimoyomoyo hakika dunia imebadilika kwa kasi sana.

Yaaani mtu anapata C flat bado anaenda secondary? Ninakumbuka dada yangu aliyeniachia ziwa, sasa hivi ni engineer, yeye ni moja kati ya wanafunzi 4 waliofaulu kwenda secondary shule ya serikali. Kumbuka enzi hizo kuchaguliwa tulikuwa tunaita kufaulu.

Yaaani wewe ukichaguliwa unaonekana umefaulu na wale ambao hawakuchaguliwa wanaonekana wamefeli ingawa kiuhalisia hawakuwa wamefeli ila shule zilikuwa ni chache mnoooo kiasi kwamba ni ngumu ku-accomodate wanafunzi wooote waliofaulu.

View attachment 1661678

Dada yangu alifaulu wakati huo baba anafanya kazi Wilaya ya ******* Mkoa wa Mbeya. Watu walifurahi familia nzima, lilipikwa pilau kana kwamba kuna sherehe ya kipaimara. Ndugu waliokuwa wanaishi karibu walikuja kumpa pongezi dada utadhani labda amejifungua mtoto.

Dada alikuwa maarufu sana kwa maana akiwa anaenda shuleni basi ni yeye tu ndiye aliyekua anaonekana asubuhi amevaa sare wakati huo wenzake aliomaliza nao darasa la saba bado wamelala au wameenda shambani.

Mgeni aliyekuwa hapafahamu nyumbani akiwa anaulizia kwa mama fulani wenyeji wanaanza kudadisi kwa kuambiana "au yule mama mjaluo ambaye mwanae anasoma secondary". Kwenda secodary ya serikali ilikuwa ni umaarufu kama dereva kwa maana enzi zile hakuna gari ya automatic transmission.

Gari zote ni manual na anayeweza kuendesha ni mzee mmoja au wawili tu mtaa mzima. Wanafunzi wa secondary walikuwa maarufu kama madereva kutokana na uchache wao.

View attachment 1661682

Matokeo yalikuwa yanasubiriwa kwa hamu na shauku kubwa sana kwa maana matokeo na selection zilikuwa zinakuja kwa pamoja tofauti na sasa hivi ambapo matokeo yanaanza kutoka na mwanafunzi au mzazi wake anaingia katika internet kisha baada ya mwezi mmoja mbele ndio selection inatangazwa.

Je, wewe ni mmoja ya wanafunzi wachache waliobahatika miaka ya 1990?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Ndio mimi ni mmoja wao. Kati ya wanafunzi 90 tuliomaliza shule ya msingi Magereza Moshi tulichaguliwa wawili (2) tuu kwenda Form I Mawenzi Secondary School.

Najivunia sana elimu ya wakati ule kwani sijabebana na lundo la vitabu wala kuchoshwa na Tuition; walimu walijuma na kutupa NOTES na majaribio yaliyotuwezesha kuwa mahiri.

Elimu ya sasa hivi mtoto wa CLASS II anaandikia vitabu zaidi ya nane, daftari la Class work na Homework anakuwa na mzigo uliozidi umri wake; sijui hawa walimu huwa wanaokotwa wapi maana badala ya kuwapa watoto notes na homework, watoto wanatumia vitabu kama ndio notes.
 
Aisee, kwenye huu uzi kila mtu anasema alifaulu.
Jf raha sana, ukianzisha mada ya magari basi kila mtu atasema analo.
Mkuu member wengi wa JF Wana angalau elimu ya secondary.
Usifikiri wana ongopa.
 
Nilipomaliza darasa la saba, mkoa mzima (yaani na wilaya zake zote) kulikuwa na nafasi 10 tu za kwenda Umenyeni...
 
Sasa hivi C mbili na D moja unaingia advance
Tena unaweza kuta C za civics na nutrition, D ya Bible/Islamic knowledge

Chuo E mbili

Akitoka hapo hataki kazi za bodaboda, eti anataka kazi za hadhi yake, hivi wana hadhi gani hawa mbwa!!!!
Vipi wee mbna umeandila kwa jazba sana? [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom