Mwaka 2022 kaa mbali, wapinge na wadharau watu wote wenye tabia za ki-antsocial

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Watu wenye tabia za ki-antsocial huwa na tabia zifuatazo.

1.Hawajali haki za wengine.
2. Huwa ni wenye hila(Manipulative). Wanafanyafanya ujanja ili wakutake advantage.
3. Waongo. Ni watu waongo waongo ili wafanikishe mambo yao au kucover uovu wao. Uingo wa kujirudiarudia
4. Hawajutii makosa yao. Watu antsocial huwa hawajutii kabisa, wala nafsi zao huwa haziwasuti kwa mambo wanayotenda. Na zaidi ni kuwa hawana huruma kwa wengine.
5. Hawaheshimu wengine.
6. Huwa wagomvi.
7. Kujikweza na kujiona bora.
8. Kukosa uwajibikaji kifedha, kazini na kwenye mahusiano.

Wapinge, waepuke na wadharau watu wa namna hiyo. Kwa upande wa pili, hii ni shida ya kisaikolojia, pengine anaweza angalia namna ya kuwasaidia.
 
Pole mkuu
 
Safi.
Umetumia ubungo vizuri kung'amua sifa hizi za kubumba.

Mleta uzi hajui alichotupia humu ili mradi liende tu!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kilayman ni sawa, lakini kisaikolojia antsocial ni mtu mwenye sifa nilizotaja. Antsocial akikomaa anakuwa psychopath.
 
Tabia ya kutojihusisha na watu (na mambo yao), antisocial, ninavyoijua ni kuwa, kweli mtu hanajali kujihusisha na yeyote, sio kwa jema wala baya.
Sasa kama kuna wenye tabia ulizoainisha hapo juu, huyo ni tapeli na sio antisocial.
 
Acha Majungu wewe ...kila Mtu kaumbwa na kaliba yake ....
 
Kilayman ni sawa, lakini kisaikolojia antsocial ni mtu mwenye sifa nilizotaja. Antsocial akikomaa anakuwa psychopath.
Anti social to Psychopath?? [emoji2955][emoji2955][emoji2955][emoji2955] Psychology ya kijijini kwenu au?
 
Tabia ya kutojihusisha na watu (na mambo yao), antisocial, ninavyoijua ni kuwa, kweli mtu hanajali kujihusisha na yeyote, sio kwa jema wala baya.
Sasa kama kuna wenye tabia ulizoainisha hapo juu, huyo ni tapeli na sio antisocial.
Huyo ndiyo antsocial sasa. Wewe hiyo defination yako siyo rasmi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…