Mwaka wa kumi huu au zaidi umeajiriwa (unatumwa tumwa tu); je, ni kitu gani kinakufanya usijiajiri?

Mwaka wa kumi huu au zaidi umeajiriwa (unatumwa tumwa tu); je, ni kitu gani kinakufanya usijiajiri?

Mkuu Equation,
Sidhani kama upo uhusiano wa mtu kupendwa kuajiriwa sababu tu ni nature au vinywaji.

Kitu kikubwa mkuu wengi hatupendi kutoka katika “Comfort zone”

Kutoka katika hali ya kustarehe au sehemu tuliyoizoea huwa ni mtiti sana, ndio maana kuna kuwa hakuna mabadiliko.
Huenda inasabishwa na kuogopa sehemu nyingine,
Kupenda kuajiriwa by nature nafikkri ni mazingira ya mtoto anapokulia na nini anCholishwa akilini mwake tangu udogo mpaka ukubwa wake.

Familia nyingi watoto wazazi waliokulia katika biashara lazima wataangukia humo, kadhalika mtoto atakayekulia kumuona baba ni mjeshi, mama ni mjeshi kuna asilimia kubwa mtoto akaangukia humo japo si wote.
Kwa hoja yako hii, inathibitisha mazingira tunayoyaishi ndio yanayotuathiri
 
Uko sahihi, mfano; watoto waliotoka kwenye familia zenye viwanda, huwa hawaajiriwi, wataenda nje watapata elimu, na baadaye wanakuja kusimamia viwanda vilivyoanzishwa na watangulizi wao.
Hawaajiriwi au wanaajiriwa kwenye viwanda vyao au biashara zao? Biashara ikiwa kubwa na professionally run hata mmiliki unakuwa mwajiriwa wa biashara yako.
 
Ratiba ya watumishi wa Tz
Kuingia kazini 8:00-9:00
Breakfast 8:30-10:00
Lunch. 1300-check if the boss is present, if not, go home
Kwa yule mwenye viashiria vya kuona mbali, kwa mazingira hayo, kwake ni rahisi kujiajiri kwa sababu anapata muda wa kufanya mambo yake katika ajira mpya ya kujiajiri
 
Tunaamini elimu tunayoipata huko vyuoni na mashuleni, inatupa uhuru wa kufanya maamuzi sahihi katika uzalishaji mali pamoja na kujitegemea.

Tulitegemea ujuzi na elimu ulioipata huko duniani n.k iwe chachu ya wewe kujijenga na kuanzisha na kumiliki kampuni, taasisi, au kiwanda ili pia iweze kutoa ajira kwa wengine.

Mtaji kwako sio tatizo, kwa sababu umeshaajiriwa kwa miaka mingi na una sifa zote za kukopa; Swali, kwanini unashindwa kujiajiri?

Tatizo ni nini?​
Mshahara ni sumu anayopewa mtu asahau ndoto zake
 
Population ya waliojiariji ni 2/10 wanaotoboa

Tofauti na watumishi 6/10 wanaotoboa


MTumishi anaoption ya kufanya biashara,kukopa kirahisi huku mfanyabiasha anaoption moja tu biashara na kupata mkopo lazma biashara iwe imara

Japo mfanyabiashara free will yake ni kubwa kuliko mtumishi...

N:B..kuhusu kutake risk bussnesman🙌🙌🙌🙌
 
Tunaamini elimu tunayoipata huko vyuoni na mashuleni, inatupa uhuru wa kufanya maamuzi sahihi katika uzalishaji mali pamoja na kujitegemea.

Tulitegemea ujuzi na elimu ulioipata huko duniani n.k iwe chachu ya wewe kujijenga na kuanzisha na kumiliki kampuni, taasisi, au kiwanda ili pia iweze kutoa ajira kwa wengine.

Mtaji kwako sio tatizo, kwa sababu umeshaajiriwa kwa miaka mingi na una sifa zote za kukopa; Swali, kwanini unashindwa kujiajiri?

Tatizo ni nini?​
Kitu ambacho hujui... Hata wewe uliye jiajiri ni mtumwa KWa mteja wako....
 
Back
Top Bottom