Mwakyembe awatega wabunge CHADEMA, awaambia wakitaka ukweli warudishe hoja ya Richmond Bungeni

Mwakyembe awatega wabunge CHADEMA, awaambia wakitaka ukweli warudishe hoja ya Richmond Bungeni

Eti naye ni Dr.....aiseee...ukweli gani atakaoutoa SAA hiz...wakat aliuficha ukweli kipindi kile....anatafuta kiki za kupuuz kabisa....okay najua anataka aseme uongo ili awasafishie watu flan njia 2020....
 
Fumbo mfumbie mjinga mwerevu hung'amua.

Baadhi ya makamanda wa CHADEMA (hasa CHADEMA asilia) hawaitaki ndoa ya kisiasa kati ya Mbowe na Lowasa, sasa watoke vipi ni jinsi ya kuirudisha suala RICHMOND bungeni.

Mwakyembe naye kawatega waingie vichwa vichwa. Likiachwa kurudishwa bungeni, basi yatosha CHADEMA kuthibitishiwa kuwa waliyekuwa wakimtuhumu, kwenye majukwaa kuwa ni fisadi, kweli ni fisadi.

Hivyo hoja yao, ya kila siku kila akitajwa kuhusika na ufisadi, ati mwenye ushahidi atoe afikishwe mahakamani, haitakuwa na nguvu tena. Kwanza, kwa yeye kujiuzuru Uwaziri Mkuu, ilikuwa adhabu tosha kwa mtu mwenye uchu wa madaraka, kama yeye.
Siasa majitaka
 
Usipende kuweka mawazo yako kwenye mawazo ya wengine.

Ukiniuliza kuhusu Urais nitakujibu hivi,Siyo JPM wala Lowassa wenye uwezo wa kutuongoza.Kama kukosa CDM pamoja na CCM mliingia mkenge.Ni bora CCM wangemweka Chikawe au Judge Ramadhani lakini kwa JPM hamna kitu kuanzia Uongozi mpaka kicwani kwani anafikiria kwa Chuki,visasi na ubaguzi. Hope umenielewa.

Kama ufisadi Lowassa na JPM wote ni mafisadi wametajirika kutumia madeal na wizi wa pesa za Serikali hakuna msafi hapo.
Ufisadi wa jpm unaojaribu kutuaminisha hapa ni porojo ambazo ukiambiwa uthibitishe hutaweza, lakini kwa lowasa ni tofauti.......kamati teule ya bunge ilimwaga ushahidi wote ya ufisadi wake!
 
..Wabunge wa upinzani wanataka Mwakyembe ashughulikie suala la Makonda kwa mtindo uleule alioutumia kushughulikia kashfa ya Richmond.

..kama Mwakyembe aliweza kuhitimisha suala lile bila kumhoji Lowassa kwanini anashindwa kuhitimisha suala la kuvamiwa clouds bila kumhoji Makonda?

..hoja haipaswi kuwa Lowassa alionewa or not. Kwa maoni yangu hakuonewa.

..hoja ni kwamba Mwakyembe alitengeneza precedence ya kutoa hukumu bila kulazimika kumhoji mtuhumiwa namba moja. Precedence hiyo ndiyo wabunge wanataka Mwakyembe aitumie kwenye shauri la Makonda vs Clouds ambapo kuna ushahidi wa video.

..lingine ni kwamba Mwakyembe alikuwa waziri wa sheria. Sasa nini kilimzuia kipindi hicho kumfungulia mashtaka Edward Lowassa?

..tena Mwakyembe alikuwa akijitapa wakati wa kampeni kwamba jinai haifutiki. Kwamba Lowassa alitenda jinai hivyo ana kesi inamsubiri.

..kwa hiyo MWAKYEMBE kudai suala la richmond lirudi bungeni ni ULAGHAI tu. Suala hilo lilishamalizika bungeni na linapaswa kwenda Mahakamani.
It's obvious ...Mwakyembe hawezi kufanya lolote ....kama Waziri aliyekuwepo katimuliwa kwa kuunda tu tume mnategemea huyu achukue hatua gani kama si upinzani kukosa mbinu ya namna ya kumlazimisha mamlaka ya uteuzi kuchukua hatua ....unaibuaje hoja kama hii kwa mgongo wa issue ya aibu kama Richmond ambayo sasa inaleta ukakasi hata huko Chadema? ....
 
Mwakyembe sema ukweli , tunazo taarifa zote kuhusu safari yako ya Marekani , tunawafahamu hata waliokuwa wanakutembeza , walipogundua uongo wako wakakushiti , ulitumwa kufunika kombe , UNABISHA , NIFUKUE MAKABURI ? tena aliyekuwa anakuzungusha ni mlokole mmoja mwenye asili ya kiafrica , natoa wito kwa wabunge wa Chadema kuirudisha bungeni hoja hii , Mwakyembe atakimbia .
Fukua makaburi kijana
 
Mkuu kuna kitu sikielewi hivi ina maana serikali inashindwa yenyewe binafsi kumburuza lowassa mahakamani mpaka upinzani eti wairudishe bungeni?? Kma lowasa ana machafu kafanya basi sheria ichukue mkondo wake ssa hivi vitisho toka 2015 mara ooh mahakama ya mafisadi sijui fisadi papa huku mahakama na polisi ni yenu ssa kumkamata mnaogopa nni???
Chadema ina ushahidi wa ufisadi wa Lowassa
 
Ni kweli hakuhojiwa hata ujio wake ukawa pia hakuhojiwa ila tumwache mzee apumzike mbona aliyekula nae kapumzika!
 
Waziri wa habari Harrison Mwakyembe amewambia wabunge wa chadema kama wanataka ukweli wa ufisadi wa Richmond warudishe hoja hiyo bungeni.

Haya sasa karibuni kukanyagana maana hii hoja ni mwiba ambao watu wengine hawatakaki hata kuuona!

Wanyakyusa ni kati ya watu wakweli sana, huyu Mwakyembe sijui ni wa aina gani! Ati naye ana Ph.D Kweli mtu akiingia siasa ukoo umtenge kwanza, siku akiacha siasa arejeshwe kwenye ukoo.Kumbe siasa inaendeshwa kwa unafiki na uongo.
 
Namshangaa sana Waziri Mwakyembe eti hakumhoji Mh.Lowassa Kwa kuwa ushahidi dhidi yake ulikamilika.Kama ndio hivyo mbina Ushahidi dhidi ya Paulo Makonda nao ulikamilika? Bw.Mwakyembe wewe ni mwana Sheria kumhoji mtuhumiwa ni haki kisheria kutomhoji Mh.Lowassa ulikosea huo ndio ukweli je kwanini suala la Makonda unataka ahojiwe? Mbona nao ulikamilika? Kumbuka watanzania hatudanganyiki tumesoma kama we we Sheria tunaijua mkuu
 
Namshangaa sana Waziri Mwakyembe eti hakumhoji Mh.Lowassa Kwa kuwa ushahidi dhidi yake ulikamilika.Kama ndio hivyo mbina Ushahidi dhidi ya Paulo Makonda nao ulikamilika? Bw.Mwakyembe wewe ni mwana Sheria kumhoji mtuhumiwa ni haki kisheria kutomhoji Mh.Lowassa ulikosea huo ndio ukweli je kwanini suala la Makonda unataka ahojiwe? Mbona nao ulikamilika? Kumbuka watanzania hatudanganyiki tumesoma kama we we Sheria tunaijua mkuu
Ushahidi dhidi ya Lowasa ulikamilika ndiyo maana alitimuliwa kwenye Uwaziri Mkuu. Makonda bado Rc Mkoa wa Dsm, huoni tofauti hiyo?
 
Kwa hiyo kama kuna ufisadi mahali na serikali inaujua, na wahusika inawajua mpaka isubiri upinzani ulete hoja ndo ishughulikie? Kwa maana hiyo Mwakyembe anatwambia serikali haina uchungu na fedha za nchi hii na kama kuna mwenye uchungu ajitokeze? Sioni alichowatega CHADEMA zaidi ya yeye kujionyesha alivyo dhaifu katika Maamuzi kiasi cha kusubiri wenzie waanzishe jambo ndo adandie. Kwani tumesahau kwamba yeye ndiye alikuwa Mwenyekiti wa kamati ya Bunge iliyochunguza suala hili na kuhitimisha kwa kusema angeweka wazi ukweli wote nchi ingetikisika? Kwa maana hiyo ukweli bado anao, na naamini akiuweka wazi sasa hivi haitatikisika maana walioko madarakani ni wengine japo chama ni kilekile. Au bado nchi itatikisika kwa vile mhusika si mmoja tu toka ndani ya chama hicho? Tunakumbuka pia wakati wa kampeni aliahidi kumuumbua Lowasa kwa kuweka wazi ushiriki wake kwenye Richmond lakini mpaka kampeni zinaisha hakusema lolote zaidi ya yale aliyosema February, 2008 bungeni, au anataka tuamini kampeni bado zinaendelea na sasa yuko tayari kuhtimisha kampeni? Mwakyembe ukweli wa suala hili unaujua wote na wewe ndo wa kuuweka wazi vinginevyo ukae kimya maana burden of proof ya jambo hili iko kwako na si mtu mwingine maana wewe ndo tulikulipa hela yetu utuletee ukweli wote lakini ukasema umeweka nusu na kibakiza akiba. Basi tunaomba utumalizie nusu uliyobakiza vinginevyo tutaendelea kukudài UKWELI wetu uliobakiza.
 
Hivi huyu mzee alimaliza dozi ya kutoa sumu mwililini?
naona kabisa ambavyo sumu inazid kuathiri ubongo wake.
 
Back
Top Bottom