Mwakyembe awatega wabunge CHADEMA, awaambia wakitaka ukweli warudishe hoja ya Richmond Bungeni

Mwakyembe awatega wabunge CHADEMA, awaambia wakitaka ukweli warudishe hoja ya Richmond Bungeni

kwani richmond na Escrow ipi kubwa coz wabunge wa upinzani huwa ni upande wa wananchi na wabunge wa ccm ni upande qa serikali
 
Kha! Ndo mnamuita Dr huyo, mbona hoja zake hazina mashiko na hazistahili kuongelewa na mtu mwenye hadhi-cheti cha PHD achilia mbali nafasi aliyonayo ya uwaziri.

My take: Atumwe India kwa matibabu haraka sana, mana naona ile sumu imekula kaubongo kaliko kabakia kazima kale daaah

Elimu yako ya kawambwa
 
mahakama ya mafisadi hivi imeshafunguliwa au bado maana hapo ilipo hapapitiki
 
Hii serikali ijiuzulu tu.

Yaani wao ndio wameshika dola na wao ndio waliofunga huo mjadala Bungeni alafu leo ndio wanaowataka wapinzani waibue swala hilo badala ya kutekeleza maazimio ya Bunge au kufungua kesi Mahakamani.

Pathetic!
Mbunge ana uhuru wa kupeleka hoja ya kureview hoja kama hakuridhika kufungwa haimaanishi haiwezi kurudishwa kwa hoja binafsi.
 
Mwakyembe amezeeka vibaya. Anasahau yeye alisema mwenyewe kwamba ni kweli alikataa kumpa Lowasa nafasi ya kujitetea? Amesahau alisema na dunia nzima ikamsikia kwamba kuna mambo mengi mazito hakutaka kuyaweka wazi maana angefanya hivyo serikali ingeanguka? Apeleke mambo yake huko. Kwanza amjibu Nasari. Kwa nini alipeleka ripoti ya Richmond bungeni bila kumhoji Lowasa lakini sasa anashindwa kutoa ripoti iliyoandaliwa na Nape kwa sababu eti kuna mtu hajapewa nafasi ya kuhojiwa? Tangu atamke hayo mbona hajamhoji mhusika? Tafadhali Mzee Mwakyembe kama unataka uendelee kubaki na ka heshima hata kadogo usiwe unafikiri sisi umesahau uliyofanya
 
Kiukweli wenye Mamlaka ya kuurudisha mjadala Wa Richmond Bungeni ni Ccm maana wako wengi !

Lakini Watanzania hawajasahau kipindi kile wapinzani walileta hoja ya kurejesha Upya bungeni Lakini Ccm wakagoma !

Hata kama MTU alikuwa na makosa lakini ulituthibitishia baadhi ya watu muhimu hawakusikilizwa akiwemo Mh Lowassa!

Kwa maoni yangu Nitaiombea sana Nchi yangu , lakini sitaruhusu mtu acheze na akili yangu mpaka 2020 nitakapotumbukiza kura yangu .
Tume haikumuhukumu lowassa bali ilitoa mapendekezo ajiuzuru au ahojiwe na wabunge akaamua kujiuzuru. Kamati ile haikufanya kazi ya mahakama ambayo ni lazima itoe haki ya kila mtu kusikilizwa bali ilifanya kazi ya uchunguzi bunge lilimpa nafasi ya kumhoji akakataa na kuamua kujiuzuru.
 
Hebu shirikisheni kidogo mbongo zenu. Mbali ya Lowassa kujiuzulu ni mapendekezo mangapi ya Kamati ile teuli ya bunge yalitekelezwa. Hata bila ya hoja kurudishwa Bungeni yeye Mwakyembe aseme ni nini walitekeleza kwenye mapendekezo ya kamati ile teule ambayo yeye alikuwa Mwenyekiti?
Anayetakiwa kutekeleza mapendekezo ya kamati ya bunge ni serikali sio kamati yenyewe. Wakati wa kamati mwakyembe hakuwa madarakani.
 
INATUAMINISHA SISI KUWA MHUSIKA NAMBA MOJA NI YULE ALIYEKIMBIA BAADA YA KUTOSWA URAISI.....FULL STOP
 
Angetuambia awali hyo 2009 anakuja kusema leo huo ni upotevu wa vi2 tunavyofikiria kwa sasa
 
Wanaipelekaje Bungeni. Wanaipeleka kama hoja mpya ama kama hoya ile ile ya zamani. Kwani hiyo Richmond bado ipo? Mitambo yake iliuzwa kwa Dowans na Serikali ikachukua kodi, na Dowans nao wakawauzia Symbion na serikali ikachukua kodi na mitambo hiyo inatumika kuwauzia TANESCO umeme na serikali inachokua kodi na tozo mbali mbali!!
Kumbukumbu zote zipo. Kureview jambo sio lazima vitu vyote viwepo linajadiliwa tendo la ufisadi katika mchakato wa kuipa tender richmond sio uwezo wa mitambo ya richmond.
 
Kha! Ndo mnamuita Dr huyo, mbona hoja zake hazina mashiko na hazistahili kuongelewa na mtu mwenye hadhi-cheti cha PHD achilia mbali nafasi aliyonayo ya uwaziri.

My take: Atumwe India kwa matibabu haraka sana, mana naona ile sumu imekula kaubongo kaliko kabakia kazima kale daaah
Warudishe ile hoja bungeni tutajua mwenye ugonjwa, mwenye PHD na mwenye Bachelor Degree ya kucheza ngoma jukwaani na manyanga miguuni. Wekeni mziki acheni maneno...
 
Sishangai lugha hiyo kutoka kwenye akili yako, kwa kuwa hiyo lugha tumeizoea na kesho utasema kinyume chake - kula matapishi.

Kukuamini itabidi nikapimwe akili, kama hayo anayoyaandika Daudi Mchambuzi, kila siku, ni ya mtu hai kweli au maiti (nakunuu).
Usipanic sasa [emoji16][emoji16][emoji16]
 
Back
Top Bottom