Mwami Theresa Ntare VI wa Heru - Chifu wa kwanza mwanamke

Mwami Theresa Ntare VI wa Heru - Chifu wa kwanza mwanamke

Rubaman,
Sijui umekusudia nini kusema, ''kipolitics,'' na ''informative.''
Noamba ufafanuzi.

Unasema hii ndiyo sababu ''hatujui,'' na ''hatutayajua baadhi ya mambo.
Umetoa mfano kwa dhana ya ''resistance,'' ya babu zetu kuwa inafundishwa.

Binadamu hafundishwi kuwa huru hili ningependa ulizingatie hakuna shule
inafundisha mtu kutaka kuwa huru katika nchi yake mwenyewe.

Ninachokiona kwako ni kuwa na uniwie radhi, hujui historia ya uhuru wa
Tanganyika.

Imetokea kuwa huyu anayeandika hapa ameandika kitabu cha historia ya
TANU uhuru wa Tanganyika, ''The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924
- 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in
Tanganyika,'' (London 1989) na ameshiriki katika kuandika historia ya Zanzibar
akiwa Mtafiti Msaidizi wa Dr. Harith Ghassany mwandishi wa kitabu ''Kwaheri
Ukoloni Kwaheri Uhuru.''

Hakuna kisichojulikana nakushauri usome vitabu hivi.

i9kvYbC_3fn_BXtQxXIyX0UZoQV7vqncU7quS_2FzgIMGpJF-fKs-fXesFw7KSoKJqAOkYDmICWbSlhGrkJ_Pqc8eg7PntQuaDtF8REpoL6KsRz65g68mdfQnArVHhy9ewxzxZkJqd08wIArKhhJm3n7dQfZKxX_Q8a6NEtgUE91yn37GHf6GmSJOdvRgdsRZdQmdC1gT5tbb4ahknBWn90nSPtQYfrAc-pMrIQRBUtH6wh3EgSjzb_IXB4R3ExkacEHEku8Y6S1Qdn_LHSp-FHM1OLyOTlT1yscBrhKNYcgbCEfTRvospKYKMbOHA-TuzqLH8r3QbZnM_oOnOAYl0JcYBAkbrLsG6MqcncLGZ0K12lIrbaZpOOZQWoLxHS7iLZE1S1-rok5EAOF8ejPkjPft8tUywKjhgZz2_qHB7WlMb4dtbeNuE1qyq8j4ZP0YEqeQZAlIgKUs8JzeTxQQ88fUiAwLO9IId5Cbl1UFH-gsJVyK3i-XphkJxQHKlg9VxdbnyMHMAr9Y3MymmYDpyzvxWGpY_CcpMAnvQ_6dXJhI44KdnMT37fMIryDn1JOjtfSDpARZkaVV4k1E49LV27PC2fjggeIh6PnG7w=w855-h632-no


Unaweza kusoma muhtasari wa historia hii hapo chini:
Mohamed Said: WALIFIKAJE TAREHE 7 MWEZI WA SABA 1954 NA KUASISI TANU?
Ni kweli sijui mengi juu ya uhuru wa Tanganyika zaidi ya kile nilichofundishwa Primary na siwezi kuja kudai kwamba najua mengi. Watanzania wengi (keyword Tanzania) hatujui mengi jinsi ya uhuru wa nchi hizi mbili ulivyopatikana sababu moja ni jinsi tulivyofundishwa. Tumefundishwa kipolitics zaidi kwamba tunajua yale yanayosifia na yanayotukuza upande mmoja bila kujali pande nyingine. Uhuru wa Tanganyika kwa asilimia kubwa tulifundishwa uanzilishaji wa TAA then TANU na Nyerere, Nyerere, Nyerere, Nyerere up to independence. Ndio maana nasema kipolitics. Wangetufundisha vitu vyote hata vile vilivyokuwa negative from Team TAA/TANU/Nyerere katika post zangu unaweza kuona nimesema focus nyingi ilikuwa kwa Nyerere bila kujali mchango wa wengine. Hawa kina Sykes na wengine hawajapewa focus ya mchango wao ndio maana wengi hatuwajui. Nina uhakika wewe pia kuna mengi (harakati za uhuru) ambayo hujawahi kuyasikia huyajui na hutoyajua.
Nimeuliza awali je palikuwa na vyama vyingine zaidi ya TAA/TANU vilivyoshiriki katika harakati? Kuna watu ambao walikuwa na mawazo tofauti na kina Nyerere katika harakati hizi? Je unayajua haya Mr. Mohamed? Kama unayajua naomba utuletee. Tusiendelee kudanganywa kwamba watanganyika wote walikuwa wanakubaliana na lengo moja na msimamo mmoja. Hata katika hii story ya Mwami Thereza Ntare amesema hata Enzi zake palikuwa na vibaraka. Napenda kujua kama challenges hizi zilikuwamo ndani ya TANU. Napenda kujua watu Nyerere aliokwaruzana nao katika harakati. Vyote hivi ni part ya historia ya uhuru. Haya ndo nayasema as Informative. Tusikubali kuambiwa yale yanayopendeza tu wakati palikuwa na mengine yaliyo negative. Fikiria (hypothetical) hivi endapo CCM isambaratike kesho, keshokutwa baada ya miaka 50 wakija kuandika historia ya CCM wataandika yale mazuri tu ya CCM haya mabovu, maovu yafanywayo na CCM na watu wake hutayasikia. Hii pia inaweza kusemwa juu ya vyama vyingine pia not just CCM only.
 
Our system of education wasn't designed to produced thinkers. And what's worse is our independence didn't entail individual liberty which guarantee your right to question authority and be critical.
Yeah hilo ndilo tatizo. Ndio maana wengi tunapishana kuelewa humu. Elimu imedizainiwa kukwambia ukariri unachofundishwa sio ku-analyze na ku-question unachofundishwa.
 
Ni kweli sijui mengi juu ya uhuru wa Tanganyika zaidi ya kile nilichofundishwa Primary na siwezi kuja kudai kwamba najua mengi. Watanzania wengi (keyword Tanzania) hatujui mengi jinsi ya uhuru wa nchi hizi mbili ulivyopatikana sababu moja ni jinsi tulivyofundishwa. Tumefundishwa kipolitics zaidi kwamba tunajua yale yanayosifia na yanayotukuza upande mmoja bila kujali pande nyingine. Uhuru wa Tanganyika kwa asilimia kubwa tulifundishwa uanzilishaji wa TAA then TANU na Nyerere, Nyerere, Nyerere, Nyerere up to independence. Ndio maana nasema kipolitics. Wangetufundisha vitu vyote hata vile vilivyokuwa negative from Team TAA/TANU/Nyerere katika post zangu unaweza kuona nimesema focus nyingi ilikuwa kwa Nyerere bila kujali mchango wa wengine. Hawa kina Sykes na wengine hawajapewa focus ya mchango wao ndio maana wengi hatuwajui. Nina uhakika wewe pia kuna mengi (harakati za uhuru) ambayo hujawahi kuyasikia huyajui na hutoyajua.
Nimeuliza awali je palikuwa na vyama vyingine zaidi ya TAA/TANU vilivyoshiriki katika harakati? Kuna watu ambao walikuwa na mawazo tofauti na kina Nyerere katika harakati hizi? Je unayajua haya Mr. Mohamed? Kama unayajua naomba utuletee. Tusiendelee kudanganywa kwamba watanganyika wote walikuwa wanakubaliana na lengo moja na msimamo mmoja. Hata katika hii story ya Mwami Thereza Ntare amesema hata Enzi zake palikuwa na vibaraka. Napenda kujua kama challenges hizi zilikuwamo ndani ya TANU. Napenda kujua watu Nyerere aliokwaruzana nao katika harakati. Vyote hivi ni part ya historia ya uhuru. Haya ndo nayasema as Informative. Tusikubali kuambiwa yale yanayopendeza tu wakati palikuwa na mengine yaliyo negative. Fikiria (hypothetical) hivi endapo CCM isambaratike kesho, keshokutwa baada ya miaka 50 wakija kuandika historia ya CCM wataandika yale mazuri tu ya CCM haya mabovu, maovu yafanywayo na CCM na watu wake hutayasikia. Hii pia inaweza kusemwa juu ya vyama vyingine pia not just CCM only.
Rubaman,
Yote ninayoyajua nimeandika katika kitabu cha Abdul Sykes.

Mengine nimayaandika katika papers nilizotoa katika mikutano
mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Na mengine mengi yamo katika www. mohammedsaid.com
na katika mitandao tofauti ya kijamii.

Ngoja In Shaa Allah niingie Maktaba nikutafutie kitu fulani
umekigusa hapo
juu.
 
Rubaman,
Yote ninayoyajua nimeandika katika kitabu cha Abdul Sykes.

Mengine nimayaandika katika papers nilizotoa katika mikutano
mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Na mengine mengi yamo katika www. mohammedsaid.com
na katika mitandao tofauti ya kijamii.

Ngoja In Shaa Allah niingie Maktaba nikutafutie kitu fulani
umekigusa hapo
juu.

Re: Tanganyika(TANU) imetoka mbali waasisi wake wengi wao wametangulia
mbele ya haki

By Gagnija

Alikuwa kipenzi cha wa-Tanganyika. Picha uliyoiweka ni ya Zanzibar kwenye
mazishi ya Karume aliyeuwawa kwa risasi, ulitegemea aende huko kama anakwenda
harusini? Labda kama alivyosema Jaji Werema, sisi wengine mambo ya huko hatuyajui
na hayatuhusu. Tuwaachie wenyewe.

Turudi kwenye mada, wale wazee waliompokea Nyerere Dar walisukumwa na kitu gani
hasa hadi kumchagua kuwaongoza mtu toka kijijini bara asiyejua hata kula chapati?

Gagnija,
Nakuomba upunguze hamaki.

Maswali unayouliza ni mazuri na yanaweza kunogesha sana mnakasha huu
ukawa wenye tija na vilevile kustarehesha wasikilizaji na wachangiaji ila
kwa sharti kuwa tuondoe hamaki zetu.

Tujiepushe na lugha, kwa kutumia lugha ya Bunge la Tanzania, tujiepushe
na lugha za ''maudhi.''

Vyakula kama chapati huendana na utamaduni wa watu.
Mie binafsi nikipata tabu sana na wenzangu tukisafiri.

Wanataka tukale chakula kwenye baa na wanaagiza pombe, ugali na nyama
ya kuchoma.

Nikitaabika sana la kwanza huo ugali na kisha kula chakula baa.

Lakini ndiyo maisha kila mtu ana mazoea aliyotokanayo kwao kwa hiyo kwa
sasa tuachane na hayo masuala ya ''chapati.''

Turudi kwenye mada.
Ukweli ni kuwa TAA ilikuwa imefika mahali haiendei mbele wala hairudi nyuma.

Walikuwa hawajaitisha ''delegates conference'' kwa miaka 4 toka ule uchaguzi
wa 1950 uliomtia madarakani Abdul Sykes na Dk. Vedasto Kyaruzi.

Lakini katika hii miaka 4 TAA ilikuwa imefanya mambo makubwa katika uwanja
wa siasa kiasi cha serikali kutoa onyo kupitia Government Circular No. 5 na 6
ya 1953.

Sasa haya ninayoeleza hapa chini ni katika mazungumzo yangu na Tewa Said
Tewa tulikyokuwa tukifanya mara kwa mara.

Tewa anasema Abdul ndiye aliyekuwa akizuia kuitishwa kwa hiyo ''delegates
conference,'' na mimi natumia neno lilelile alilokuwa akipenda kutumia Mzee
Tewa, ''delegates conference.''

Nilimuuliza Mzee Tewa, ''Vipi mtu mmoja anaweza kuzuia msiitishe mkutano
kwa miaka 4?''

Jibu alonipa lilikuwa, ‘’TAA ilikuwa haina fedha zake yenyewe na sisi katika
masuala ya fedha tukimtegemea sana Abdul.''

Katika majibu haya mimi nikafanya, ''deduction,'' kutoka taarifa nyingine
ambazo nilizokuwanazo kuhusu siasa katika kipindi kile.

Kipindi hiki cha 1950 - 1953 ndicho kipindi ambacho Abdul alikuwa na vikao
visivyokwisha nyumbani kwake na Chief David Kidaha Makwaia wa Shinyanga
kuhusu yeye kujitoa kwa Waingereza na kuja kuongoza TAA ili waunde TANU.

Wakati ule Chief Kidaha alikuwa katika Legico.

Mzee Tewa hili la kumleta Chief Kidaha TAA akilijua na alinieleza lakini yeye
hakuunganisha kama moja ya sababu ya Abdul kuchelewesha kuitisha kwa
wakati ''delegates conference,'' kwa kumsubiri Chief Kidaha.

Kwa nini Abdul alihangaika sana na Chief Kidaha?
Hili swali ni mojawapo ya maswali ambayo mie binafsi yakinitaabisha sana.

Jibu nililipata katika Nyaraka za Sykes.

Katika nyaraka hizi nimmesoma Dk. Wilbard Mwanjisi akiandika mwaka 1951
akisema maneno hayo hapo chini katika italics:

The conflict between TAGSA and the government was not to end there.
In his inaugural speech to TAGSA members upon his election as president,
Dr Mwanjisi attacked the British and called them ‘uncivilised’, emphasizing
in his speech the fact that human intelligence has nothing to do with race
or skin pigmentation; and that all human beings were born equal and therefore
subject to the same limitations.

Dr Mwanjisi called upon the government to allow civil servants to take part
in politics with the following words:

‘’In recent session of the Legico, Honorable Chief Kidaha Makwaia, advised
the Government to consider the question of allowing civil servants to take
part in open politics, I completely and fully support that young chief, the
greatest African politician of our day in this territory. There are many great
brains of his calibre but sorry, they are being wasted just because they are
civil servants.’’ [1] (
‘Doctor Mwanjisi Speaks to TAGSA’ 22 nd December,

1951. Sykes' Papers).

Chief Kidaha alipowakatalia TAA ndiyo sasa 1952 hapo akatokea Nyerere na
kisomo cha hali ya juu pamoja na Hamza Mwapachu kumueleza Abdul bila
kuuma maneno kuwa yeye anamjua vyema Nyerere na anaweza akakisaidia
chama pakubwa.

Kwa ufahamu wangu hali ilikuwa hivi na ndivyo Nyerere alivyoingia TAA pale
Makao Makuu ya TAA, New Street.

Ilikuwa baada ya hapa na Nyerere kuchukua uongozi kama rais wa TAA 1953
ndipo sasa alipojulishwa kwa Sheikh Hassan bin Amir na kwa wazee wengine.

Tatizo linalowakumba wengi ni huku kutojua hali halisi ya siasa za wakati ule
na ‘’advantage,’’ kubwa niliyokuwanayo mie dhidi ya wengi hapa jamvini ni
kuwa mimi ninazo taarifa ambazo hata hawa viongozi wa leo katika CCM
hawana na waliokuwanazo weshatangulia mbele ya haki

Bila ya taarifa hizi mtu atakuwa anapigiapigia pembeni tu hana mbele wala
nyuma.

Kilichojenga TANU si ule mkutano wa Julai 7, 1954.
Historia ya TANU ilijengwa kabla ya saba saba.

Kwa kumalizia na katika mojawapo ya maswali ambayo sijapata majibu hadi
hii leo ni kuwa Dk. Mwanjisi na Chief Kidaha walikuja kuwa maadui wakubwa
na Nyerere baada ya uhuru na wote wawili wakakimbia nchi na kwenda kuishi
Kenya.
 
Nini kilisababisha Dr Mwanjisi na Chief Kidaha wawe maadui wakubwa wa Nyerere baada ya uhuru mpaka wakimbilie Kenya?
Karibu ndugu Mohamed Said.
 
Nini kilisababisha Dr Mwanjisi na Chief Kidaha wawe maadui wakubwa wa Nyerere baada ya uhuru mpaka wakimbilie Kenya?
Karibu ndugu Mohamed Said.
Gwamahala,
Hili somo linataka utafiti zaidi kuweza kupata majibu.
 
Gwamahala,
Hili somo linataka utafiti zaidi kuweza kupata majibu.
Inasadikika kuwa Nyerere alikuwa hapatani sana na independent thinkers, kwasababu alipenda sana fikra zake zidumu. Watu dizaini ya Kawawa aliwapenda sana.
 
Sahihi,hats Mzee wangu alinisimilia vivi hivi!alipofariki,alisema kwenye kaburi lake upande wa kichwani,ulipandwa mti uitwao" umurinzi!"sikimbuki vizuri kama jinahili ni sahihi!
 
Zito Kabwe siyo Mwami wa Heru kwani kwao Mwandiga hapastahili kuwa na Mwami? Tafadhali sana, usiwatukane Wanyaheru(Buha) kwa kuwavika sifa bandia wanasiasa. Wanyaheru ndiyo Waha halisi na HERU JUU ndiyo BUHA, wengine wote ni RUNDI
huu ni uongo. inawezekaje kijiji kimoja tu ndio kiwe na waha katika mkoa mzima wa kigoma, waliobakia wawe warundi?
Huu ni uongo mkubwa kabisa
 
Nimevutiwa sana kujua Historia ya mwanamke shupavu ambaye alikuwa ni mtawala wa kutoka katika kabila la waha wa Jamii ya kitutsi, ukanda wa Kasulu sehemu za Heru Juu.

View attachment 338139
Mwami Theresa Ntare (1922 - 1999)​

Ambapo zama zile jamii nyingi za Kiafrika zilitajwa kuwaweka nyuma wanawake, Mwanamama huyu aliweza kuwa Kiongozi wa Jamii ya Heru huko Kasulu. Hakuishia hapo, mama huyu aliweza kushika wadhifa mkubwa ambapo alikuwa ni mkuu wa machifu akipokea kijiti kutoka kwa Chifu Petro Itosi Marealle mwaka 1958.Makabidhiano yalifanyikia shule ya Mzumbe, na mpaka sasa Mzumbe kuna bweni linaitwa Ntare.

Mwami Theresa Ntare alikuwa ni mmoja ya Wabunge wachache wa Baraza la Kutunga Sheria la Tanganyika kabla hata ya Uhuru wa Tanganyika.

Sina details nyingi za huyu mama, WanaJF kama kuna anayefahamu zaidi kuhusu huyu mama shupavu basi atupe historia yake.

*Mwami ZITTO KABWE sasa hivi ndiye Chifu wa Heru.


------- Nyongeza kutoka kwa wadau--------

IAmShedeOne, anasema

Alipata nafasi ya kwenda kusoma Ulaya enzi ukoloni nafasi maalum za watoto wa machifu.Alihitimu mafunzo ya ya sheria.Alikuwa msaada mkubwa sana wa kisheria wakati wa kudai Uhuru,hasa kwenye mikataba ya kimataifa.
Mengi hayajulikani katika historia ya utoto wa Mwami Theresa Ntare, lakini inaaminika alikuwa mtoto wa kike pekee wa Chifu Ntare. Inaelezwa kwamba Mwami Thereza Ntare alitawazwa uchifu baada baba yake Mwami Ntare kukosa mtoto wa kiume. Baada kutawazwa uchifu ilibidi atafutiwe mchumba kutoka ukoo wa Chifu Lusimbi wa Kalinzi hivyo akawa ameolewa na kijana wa kitutsi kutoka Kalinzi akiitwa Bw. George Shinganya.

Kulingana na mila za Kiha, Mwami haolewi. Akiolewa inabidi ahame milki yake ya Uchifu ili akawe mke wa huyo muoaji. Hivyo basi, Mwami Ntare hakuolewa na Bw. George Shinganya. Bali familia ya Mwami ndiyo iliyolipa mahari kwa familia ya Bw. George Shinganya. Hivyo, Jina la Shinganya likaondolewa na akaitwa George Ntare.

Baadaye ndoa ya Mwami Theresa Ntare na George ilivunjika na Mwami Theresa Ntare akaoana na Mwami Louis Dantes Ngua wa Ufipa(Huyu ana asili ya uchifu wa Ufipa). Kuna nadharia zinazoeleza pia kuwa Mwami Theresa Ntare alipata pia kuwa mke wa Chifu Makwaia wa Usukuma. Lakini hakuna ushahidi wowote juu ya hilo.

Wakati wa zama hizo jamii nyingi za Kiafrika zilitajwa kuwaweka nyuma wanawake hasa katika masuala ya Uongozi. Hilo halikumfanya Mwanamama Mwami Theresa Ntare asiweze kuongoza vizuri na kishupavu jamii yake ya Waha wa Heru huko Kasulu.

Hakuishia hapo, mama huyu aliweza kushika wadhifa mkubwa ambapo alikuwa ni Mkuu wa machifu wote Tanganyika akipokea kijiti kutoka kwa Chifu Petro Itosi Marealle mwaka 1958. Makabidhiano yalifanyika shule ya sekondari ya Mzumbe, na mpaka sasa Mzumbe kuna bweni linaitwa Ntare.

Mwani Theresa Ntare aliheshimika kama chifu wa Kasulu yote na sio tu Heru alisimamia vyema msimamo wa Baraza la Machifu mwaka 1958 na kuunga mkono juhudi za TANU katika kudai uhuru.

Mwami Theresa Ntare alikuwa ni mmoja ya Wabunge wachache wa Baraza la Kutunga Sheria la Tanganyika kabla hata ya Uhuru wa Tanganyika.

Aliendelea kuwa Mbunge mpaka miaka ya 1980, lakini kabla ya hapo aliachia uchifu Disemba 9, 1962, Katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es salaam nchini Tanganyika. Hapo alikaribishwa kama Malkia wa Heru kwa Ngoma Maalumu kutoka Ngome ya Malkia wa Heru kwa heshima kubwa.

Inaelezwa alifariki miaka ya 1990 na mara ya mwisho alikuwa akiishi maeneo ya karibu na barabara inayoelekea Munyegera - Kati ya ilipo shule ya msingi na Kahaga Dispensary (kulikuwa na soko hapo kati miaka ya 1985).

Kwa sasa Mwami wa Heru ni Costa Shinganya au Ntare ambaye ni mtoto wa kwanza wa Mwani Theresa Ntare.

Kuna wanaosema Mbunge wa Kigoma mjini, ndugu Zitto Ruyagwa Kabwe ndiye hasa Mwami wa Waha wote. Lakini hili ieleweke yeye amepewa heshima tu ya Mwami Mpole aliyejulikana kama Ruyagwa.

Huyu ndiye Mwami Theresa Ntare VI, Malkia wa Heru kuanzia 16 Aprili, 1946 mpaka 9 Novemba, 1962.
Matukio mawili yaliyowatokea yeye na Baba wa Taifa ni:
Walizaliwa mwaka mmoja 1922,wamefariki mwaka mmoja1999.

--------------

Mohamed Said, anasema

Tuliyohadithiwa na Wazee wetu Paramount Chief Dantes Ngua na Mkewe Mwami, Theresa Ntare

Ilikuwa mnamo mwezi wa Novemba 1992, mida ya adhuhuri katika mizuguko ya kuwatembelea wakogwe walioshiriki katika harakati za ukombozi wa Tanganyika kutoka ukoloni wa Waingerza.

Safari yetu ilitufikisha nyumbani kwa Alhajj Chief Abdallah Saidi Fundikira eneo la Magomeni Mikumi, Dar es salaam. Tulipata bahati kubwa kwakuwa tulimkuta Chief Fundikira akiwa na rafiki zake Chief Dantes Ngua na Mhe. Joseph Kasella Bantu pamoja na watu wengine wawili, wakiwa katika mazungumzo ya kawaida. Baada ya kuwasalimia, tulikaribishwa tukaketi.

Mohamed Said hakupoteza muda. Aliwachokoza na maswali yahusuyo mambo muhimu wanayoyakumbuka sana katika enzi za harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika. Wote walitabasamu huku kila mmoja wao akimuangalia Chief Fundikira kana kwamba wakitaka Mzee Fundikira aanze yeye. Mzee Fundikira akasema kuwa yapo mengi ya kuzungumzwa ila muda ule haukuwa wa kutosha kwa sababu alikuwa ameshauriwa asikae muda mwingi pasipo kupumzika. Masharti hayo alipewa na daktari baada ya kutoka katika mtikisiko wa homa. Na hapo tukatambua kuwa wale wazee walienda kumjulia hali baada ya kupata taarifa ya kuumwa kwake.

Hata hivyo, Mzee Fundikira akanyanyuka huku akisema; “Mohammed, ngoja nikuletee zawadi…” Alipanda ghorofani na kurudi na kitabu kidogo cha kurasa 55 kiitwacho, Ukombozi wa Tanganyika kilichoandikwa na Simon Ngh’waya; na kuchapwa na Chief Printer, CCM Printing Press, Dodoma, 1991. Mzee Fundikira akasema, “huyu mwandishi aliniletea mimi hiki kitabu. Nimekipitia na ninaona kitakufaa.” Mzee akaongeza kusema, “Ni vyema watu waandike watakavyoweza kuandika juu ya yale yaliyotokea wakati wa enzi za kudai uhuru.”

Baada ya hapo yakafuatia mazungumzo machache tena, ya kuagana tu. Mzee Dantes Ngua akatuambia, “karibuni nyumbani, siyo mbali ni hapo jirani huku akituelekeza na kumalizia njooni, mtanikuta.” Mzee Kasella Bantu yeye alituaga akisema yeye atakuwa tayari kwa mazungumzo siku yoyote tutakayopanga na kwamba tukipita kwa Mzee Fundikira itakuwa rahisi kujua alipo na namna ya kuwasiliana nae.

Hivyo wazee wale walipoondoka nasi hatukuwa na haja ya kumchosha Mzee Fundikira ingawa hakuonyesha dalili ya kutaka tuondoke kwa haraka. Tukamuaga na kuelekea kwa Chief Dantes Ngua.

Wakati tukiwa kwa Chief Fundikira, Mohamed Said alimfahamisha Mzee Ngua kwamba alikuwa akiwafahamu baadhi ya vijana wake ambao baadhi yao wakati ule wakiongoza kampuni ya kuingiza magari kupitia Bandari ya Dar es Salaam. Hiyo ilituongezea ukaribu kwa Mzee Ngua.

Mazungumzo yetu kwa Mzee Ngua hayakuchukuwa muda kuanza. Mzee alianza kwa kutufahamisha kuwa yeye kimila ni Paramount Chief wa Ufipa ambako makabila ya Wafipa wakati huo yalienea kutoka maeneo ya Rukwa hadi kaskazini mwa Zambia ambako wakijulikana pia kama Wawemba. Hivyo yeye alikuwa ni Chief Mkuu (Paramount Chief) wa machifu wadogo, wajumbe na wazee wa koo mbalimbali, wakiongoza katika maenneo yao. Alitujulisha pia kuwa na Mkewe Bibi Theresa Ntare alikuwa Mwami, yaani Chief Mkuu wa kabila la Waha wote waliokuwepo maeneo ya Kigoma hadi katika maeneo ya Burundi. Makao yake makuu kiutawala yalikuwa Kasulu.

Jinsi Dantes Ngua na Julius Nyerere Walivyokutana kwa Mara ya Kwanza

Chief Dantes Ngua alituhadithia jinsi walivyokutana na Mwlalimu Julius Nyerere kwa mara ya kwanza.

Chief Dantes alisema:

''Wakati huo nilikuwa Mwanafunzi Tabora School mwaka wa pili. Ilikuwa kipindi cha kupokea wanafunzi wapya. Wakati huo pale palikuwa na utaratibu wa kuwathamini watoto wa machifu. Waliorodheshwa na kupewa Head Prefect kiranja wao. Pale shuleni pia wanafunzi walikuwa wakipewa vyakula vya kurutubisha afya; karanga na maziwa. Watoto wa Machfu pia walikuwa wakipata ration (mgao) huo; ila kwao ulikuwa mkubwa kiasi. Hivyo mimi nilikuwa Head Prefect wa wanafunzi ambao ni watoto wa Machifu.

Siku moja wakati wanafunzi wapya wakipokewa pale shule, niliitwa ofisi ya Head Master. Nilipofika nikawakuta wanafunzi wapya wawili. Head Master akaniambia, ‘Hawa ni wanafunzi. Ni watoto wa Machifu.’ Kisha akanitajia majina yao. Mmoja alikuwa ni Julius Nyerere na mwengine Wilbert Chagula.''

Chief Dantes alituambia kuwa yapo matukio mengine muhimu ya kipindi cha mapambano ya kudai uhuru na katika muelekeo wa kupatikana uhuru. Matukio yaliyojaa visa vya wakoloni na vituko vya Nyerere. Mama Theresa alikuwepo pale sebuleni katika yale mazungumzu, bahati mbaya hakuwa akijisikia vizuri. Lakini alikuwa na shauku ya kuzungumza mengi kuhusu jinsi alivyoshiriki mapambano yale ya kudai uhuru wa Tanganyika.

Aliyotuhadithia Mwami Theresa Ntare Jinsi Alivyoipa Nguvu TANU Buha

Mzee Dantes alitushauri tumsikilize Mama Theresa kisha tumpe nafasi akapumzike. “Mama yenu msimuone hivyo, ana mengi sana,” alisema Chief Ngua, na kuongeza, “Tena yeye uhuru ulipopatikana alipewa uwaziri.” Kwa maneno hayo ya sentensi ya mwisho ya Mzee Dantes Ngua, Mwami Theresa akaitikia; “Ah, nikikumbuka yale niliyokumbana nayo katika mapambano ya kudai uhuru wetu na kitendo nilichofanyiwa na kuondolewa uwaziri, ah, basi tu.”

Mwami Theresa hakutaka kuzungumzia kilichomtoa katika uwaziri. Aliamua kutuhadithia kisa cha mpambano wake na maafisa Wazungu wa serikali ya kikoloni kwa ajili ya kuipa nguvu TANU ili nchi hii iwe huru:

''Serikali ya kikoloni haikutaka sisi machifu tuwe katika siasa hasa kuisaidia TANU. Hata hivyo tukiwa wananchi na viongozi wa wanchi wanaotaabika chini ya utawala wa kikoloni, tuliiamua kushiriki siasa kwa siri na kuipa nguvu Tanu ili tujitawale. Kuna wakati taarifa zilinifikia kwamba ujumbe wa Umoja wa Mataifa ulikuwa unakuja kusikiliza maoni ya kudai uhuru. Utaratibu wa kikoloni ni kuwa chama japo ni cha kitaifa, kilitakiwa kipate pia usajili katika kila jimbo. Hivyo TANU ikidai kuwa inawakilisha wananchi wote, watawala wa mikoa walikuwa wajiandaa kukisuta kuwa si kweli na kuonesha sehemu ambako hakikuwa na wanachama. Moja ya sehemu hizo wakoloni waligundua ni katika himaya ya utawala wangu wa Buha. Waligundua TANU haipo kwa Waha. Taarifa za siri zikanifika kwa wakoloni wataiambia tume hiyo ya UNO juu ya hilo. Nikaamua kuchukua hatua kwa siri na kwa haraka.

Nilitoa pesa zangu binafsi na kuagiza haraka kadi za TANU elfu tatu. Zikaletwa kwenye vikapu. Nikaweka mkakati wa siri na watu wangu jinsi ya kuzigawa kadi hizo kwa haraka kwa wananchi wa maeneo ya Buha. Majira ya saa tatu za usiku lilipigwa baragumu la wito wa dharura watu waje kwa Mwami. Wito ulifikishwa kwa haraka kila eneo. Wananchi wakamiminika. Eneo la makazi yangu lilikuwa na uwanja mkubwa sana. Niliwapanga watu wangu katika lango la kuingilia wakiwa na vikapo vilivyokuwa na kadi za TANU na karatasi zake za risiti.

Kila mtu alipoingia alipewa kadi na risiti isiyoandikwa. Kisha akaambiwa aifikiche kadi na hiyo risiti pasipo kuichana. Na asiongee chochote hadi afike lango la nyuma ambalo ni la kutokea. Hapo palikuwepo watu wamejipanga katika meza. Walipofika hapo walimpa huyo aliyekuwepo katika meza hiyo kadi na risiti kisha kumtajia majina yake, anakoishi nk.

Yule karani aliiiandika ile kadi na risiti kwa tarehe za miezi ya nyuma, meza nyingine ilipiga muhuri. Mwisho mwenye kadi aliambiwa kuwamba ameisha kuwa mwanachama wa TANU wa muda mrefu. Akiulizwa atoe kadi na aitetee TANU pasipo kumtaja Mwami wala kilichotokea usiku ule; kwake hicho ni kiapo cha utiifu kwa Mwami. Aliruhusiwa na kusisitizwa kuitunza hiyo kadi na risiti yake.''

Mwami Theresa alitufahamisha kuwa zoezi lile lilikamilika mnamo saa tisa za usiku. Meza zikaondolewa na wafanyakazi wakatawanyika na kwenda kulala. Mzee Ngua akasema, “Sisi machifu tulikuwa na utiifu mkubwa toka kwa wananchi. Hata hili tatizo la Ukimwi, kama ingelikuwa enzi zile, tungetoa tamko la muongozo wa kuacha zinaa, Ukimwi ungeishatokomezwa.”

Mwami akaendelea kutuhadithia:

''Ilipofika alfajiri karibu ya saa kumi na mbili za asubuhi, nikaambiwa kuna msafara wa magari ya polisi unaelekea kwenye makazi yangu. Niliyategemea hayo, maana vibaraka wapelelezi walikuwepo enzi hizo. Hata hivyo, kwa tukio lile walikuwa wameshachelewa. Mimi siku ile sikuwa nimelala wala kupata usingizi. Nilikuwa katika nguo zangu za kawaida. Nilipoletewa taarifa ile, nikaingia chumbani na kuwaambia walinzi wangu kuwa wakifika, kwanza kuweni imara kuhusu siri ya kilichotokea usiku.

Pili waambieni kuwa Mwami hajamka. Ngoja tukamwamshe. Kisha mje kunigongea. Na kwamba nitakapotoka na kufokeana nao, nyiye onesheni utiifu kwangu na kuwakasirikia wao; wala msioneshe kuwahofu. Mkakati huo ukaeleweka.''

Mwami Theresa akatueleza kuwa wakaingia maofisa wa polisi akiwemo mmoja Mzungu na DC (District Commissioner) Mzungu pia. Wakauliza kama Mwami yupo. Wakaambiwa amelala, na kwamba wanaenda kumuamsha. Walinzi wa Mwami wakaenda kungonga mlango wake. Baada ya muda akaitikia na kuuliza kwa sauti ya juu, “kunanini mnanigongea usiku huu?” wakamjibu, “kuna Bwana DC na mkubwa wa polisi.” Mwami akajibu kwa sauti kali, “wanataka nini wakati hakujakucha ngoja nije.”

Akatuambia kuwa alijiandaa kwa kuvaa “night dress” akatimua nywele zake kisha akajiviringisha shuka na blanketi akatoka akiwa ameshikilia na alipofika sebuleni na kuwaona hakuwa salimia wala kusubiri salam zao. Alianza kwa kuwafokea kwa lugha ya Kiingereza:

“How dare you wake me up at this time of the hour? Can you do this to the Queen of the UK? Don’t you know I am the the Queen of Buha? Is it because I’m an African that’s why you are doing this to me? I will file my complaints and report you to the Governor for this.”

Mwami akatuhadithia kuwa wale maofisa wa kikoloni walichanganyikiwa na kuanza kujitetea kuwa walipata taarifa kwamba alikuwa akigawa kadi za TANU usiku. Akawajibu, “Je, mmkuja na ‘’search warrant?” Kisha akaongeza kwa kuwaambia, “Nyiye askari wanaume watupu pamoja na DC mmekuja kunipekua mimi mwanamke? Nitamlalamikia Gavana.

Hawakuwa na ‘’search warrant.’’ Mwami akawageukia walinzi wake na kuwataka wawaambie wale DC na mapolisi wake watoke mara moja au wapige baragumu kuashiria Mwami amevamiwa ili waje wamhami. Yule DC na watu wake waliomba radhi haraka na kuondoka.''

Baada ya kutuhadithia kisa hicho Mwami Theresa Ntare alituambia bora turudi pale siku ya Jumamosi iliyofuata kwa mazungumzo na mahojiano zaidi. “Jumamosi mtapata mengi. Maana kuna waandishi Wamarekani watakuja kunihoji kuhusu harakati za wanawake kuhusu kupigania uhuru wa Tanganyika.” Bahati mbaya hatukuweza kupata fursa ya kwenda siku hiyo. Mwami akasafiri. Na hatukuonana nae tena.

Unakuta mtu anajiita chief tu mtaani hapa. Hajui hata historia ya uchief.
 
Mimi mwenyewe nimejaribu kuitafuta historia ya huyu mama ila sijafanikiwa, tusubili wenye kuifahamwatujuze
Mkuu nakusudia kuandika Historian ya Hawa mashujaa wetu.Lakini Kuna ufinyu wa Taarifa sahihi zinazowahusu.Nilitaka kuanza na Mwanamalundi lakini historian yake ina mkangayiko Sana.
 
Mkuu nakusudia kuandika Historian ya Hawa mashujaa wetu.Lakini Kuna ufinyu wa Taarifa sahihi zinazowahusu.Nilitaka kuanza na Mwanamalundi lakini historian yake ina mkangayiko Sana.
Njoo Bujola utapata msaada unaohitaji.
 
Unanikumbusha heru-ushingo, hili eneo hatari sana kwa ujambazi na ulozi kadiri ya masimulizi ya wenyeji.
 
Uso wake nao pia unaongea kitu kingine kizuri cha ziada kuhusu yeye; atakuwa alikuwa ni mama bora sana nyumbani hasa kwenye familia yake
 
HAPO zamani za kale jamii nyingi za Kiafrika zilitajwa kuwaweka nyuma wanawake, ni wanawake wachache tu wanapatikana katika kurasa muhimu za Historia ya Tanzania. Kama vile Bibi Titi Mohamed, Binti Namabengo na Mkomanile au Nkomanile (Mwanamke shujaa wa vita vya majimaji).

Mjadala mkubwa umeibuka mitandaoni baada ya Rais Samia Suluhu Hassan mwamba wa Tanzania huyu kusimikwa kuwa mkuu wa machifu wote Tanzania huku machifu wa Kisukuma wakimpa jina la HANGANYA maana yake, ‘NYOTA INAYONG’AA’, mitandaoni wanadai haijawahi kutokea chifu akawa mwanamke.

Sasa kwa taarifa yako nikwambie tu kwamba, Theresa Ntare ni mwanamke shupavu ambaye alikuwa ni Mtawala (Chifu) kutoka katika kabila la Waha jamii ya Kitusi, Ukanda wa Kasulu sehemu za Heru juu. Huyu ni mwami Theresa Ntare VI, Malkia wa Heru kuanzia April 16, 1946 mpaka November 9, 1962. Mwanamama huyu aliweza kuwa Kiongozi wa Jamii ya Heru huko Kasulu.

Unapajua Heru?
Heru ni eneo ambalo lipo katika wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma. Eneo la Heru limegawanyika katika sehemu mbili (Heru juu na Heru chini). Heru Chini inaundwa na vijiji vya Nyansha, Mgandazi, Ntare, Bugaga, Nyumbigwa, Nkundutsi, Zeze na vijiji vyote vya maeneo ya Kasulu ya chini. Heru juu inaundwa na vijiji vya Munyegera,Heru na Buha pamoja na vijiji vya ukanda wote wa juu kuelekea Buhigwe.

Kihistoria Wanyaheru (Buha) ndio hasa Waha asilia na Kiha cha Heru (Buha) kina tofauti ya kimatamshi na jamii zingine za Waha. NGOMA ZA BWAMI ambazo ni maarufu kwenye kabila la Waha zinaelezwa kushamiri eneo la Heru zaidi kuliko maeneo mengine.

Bibi-Titi-Mohamed-3.jpg

Mwami Theresa Ntare alikuwa ni mmoja ya Wabunge wachache wa Baraza la Kutunga Sheria la Tanganyika kabla hata ya Uhuru wa Tanganyika. Sina details nyingi za huyu mama, WanaJF kama kuna anayefahamu zaidi kuhusu huyu mama shupavu basi atupe historia yake.

Alipata nafasi ya kwenda kusoma Ulaya enzi ukoloni nafasi maalum za watoto wa machifu. Alihitimu mafunzo ya ya sheria akawa msaada mkubwa sana wa kisheria wakati wa kudai uhuru, hasa kwenye mikataba ya kimataifa.

Hakuishia hapo, mama huyu aliweza kushika wadhifa mkubwa ambapo alikuwa ni mkuu wa machifu akipokea kijiti kutoka kwa Chifu Petro Itosi Marealle mwaka 1958. Makabidhiano yalifanyikia Shule ya Mzumbe, na mpaka sasa Mzumbe kuna bweni linaitwa Ntare.

Mengi hayajulikani katika historia ya utoto wa Mwami Theresa Ntare, lakini inaaminika alikuwa mtoto wa kike pekee wa Chifu Ntare. Inaelezwa kwamba Mwami Theresa Ntare alitawazwa uchifu baada baba yake Mwami Ntare kukosa mtoto wa kiume.

Baada kutawazwa uchifu ilibidi atafutiwe mchumba kutoka ukoo wa Chifu Lusimbi wa Kalinzi hivyo akawa ameolewa na kijana wa Kitutsi kutoka Kalinzi akiitwa George Shinganya.

Kulingana na mila za Kiha, Mwami haolewi. Akiolewa inabidi ahame milki yake ya uchifu ili akawe mke wa huyo mwoaji. Hivyo basi, Mwami Ntare hakuolewa na George Shinganya. Bali familia ya Mwami ndiyo iliyolipa mahari kwa familia ya Shinganya. Hivyo, Jina la Shinganya likaondolewa na akaitwa George Ntare.

Baadaye ndoa ya Ntare na George ilivunjika na Mwami akaoana na Mwami Louis Dantes Ngua wa Ufipa (Huyu ana asili ya uchifu wa Ufipa). Kuna nadharia zinazoeleza pia kuwa Mwami Theresa Ntare alipata pia kuwa mke wa Chifu Makwaia wa Usukuma. Lakini hakuna ushahidi wowote juu ya hilo.

Wakati wa zama hizo jamii nyingi za Kiafrika zilitajwa kuwaweka nyuma wanawake hasa katika masuala ya Uongozi. Hilo halikumfanya Mwanamama Ntare asiweze kuongoza vizuri na kishupavu jamii yake ya Waha wa Heru huko Kasulu.

Bibi-Titi-Mohamed-2.jpg

Hakuishia hapo, mama huyu aliweza kushika wadhifa mkubwa ambapo alikuwa ni Mkuu wa machifu wote Tanganyika akipokea kijiti kutoka kwa Chifu Petro Itosi Marealle mwaka 1958. Makabidhiano yalifanyika shule ya sekondari ya Mzumbe, na mpaka sasa Mzumbe kuna bweni linaitwa Ntare.

Mwani Theresa Ntare aliheshimika kama Chifu wa Kasulu yote na sio tu Heru alisimamia vyema msimamo wa Baraza la Machifu mwaka 1958 na kuunga mkono juhudi za TANU katika kudai uhuru.

Mwami Theresa Ntare alikuwa ni mmoja ya wabunge wachache wa Baraza la Kutunga Sheria la Tanganyika kabla hata ya Uhuru wa Tanganyika.

Aliendelea kuwa Mbunge mpaka miaka ya 1980, lakini kabla ya hapo aliachia uchifu Disemba 9, 1962, Katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam nchini Tanganyika. Hapo alikaribishwa kama Malkia wa Heru kwa Ngoma Maalum kutoka Ngome ya Malkia wa Heru kwa heshima kubwa.

Bibi-Titi-Mohamed-1.jpg


Inaelezwa alifariki miaka ya 1990 na mara ya mwisho alikuwa akiishi maeneo ya karibu na barabara inayoelekea Munyegera – Kati ya ilipo shule ya msingi na Kahaga Dispensary (kulikuwa na soko hapo kati miaka ya 1985).

Kwa sasa Mwami wa Heru ni Costa Shinganya au Ntare ambaye ni mtoto wa kwanza wa Mwani Theresa Ntare. Kuna wanaosema Mbunge wa Kigoma mjini, ndugu Zitto Ruyagwa Kabwe ndiye hasa Mwami wa Waha wote. Lakini hili ieleweke yeye amepewa heshima tu ya Mwami Mpole aliyejulikana kama Ruyagwa.

Huyu ndiye Mwami Theresa Ntare VI, Malkia wa Heru kuanzia 16 Aprili, 1946 mpaka 9 Novemba, 1962. Matukio mawili yaliyowatokea yeye na Baba wa Taifa ni: Walizaliwa mwaka mmoja 1922,wamefariki mwaka mmoja 1999.
 
Back
Top Bottom