TANZIA Mwana JamiiForums Miguu ya Kuku/ Mpauko afariki dunia

TANZIA Mwana JamiiForums Miguu ya Kuku/ Mpauko afariki dunia

Baada ya kuona msalaba sasa ndio nmeamini inasikitisha sana ulijitahidi kutukutanisha pamoja wenye tatizo kama lako ili tusijisikie wapweke na tusione tatizo ni letu pekee na tupo wengi kumbe wewe nia ya kujiua ulikuwa nayo bado daah tulikuwa hatuna kitu ila tulijitahidi kufalijiana umekuwa daraja kwetu mimi na mwenzangu maana wewe ndiye uliyetuunganisha tulikuwa hatuna kitu ila tulifarijiana kwia matatizo yetu na kukabiliana na changamoto zetu pumzika kwa amani
 
Maisha kweli ni kitu cha kupita; huyu ndugu niliwahi kuwasiliana naye siku za nyuma kupitia Inbox. Nikamtumia mzigo fulani kwa Moneygram lakini akasumbuliwa sana kuupokea mwishowe baada ya zaidi ya mwezi hivi ukanirudia mwenyewe.

Nasikitika kuwa niliplani kutumia tena kwa njia nyingine lakini baadaye tukakosa mawasiliano hadi leo ninaposoma post hii.

View attachment 1369240

Kwa bahati mbaya sikuwahi kusoma threads zake hata siku moja zaidi ya PM tu.
Nakumbuka alini pm akikuulizia kama nakufahamu, akadai yanatakiwa majina yako ili akamilishe muamala, na haupatikani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi nimemuelewa hoja yake, wewe utakua na shida sio bure.
Acha ujuaji wa kunisemea. Mimi nimesema sentensi chache, hujaelewa nikakuelekeza wewe unakuja na ujuaji wako wa kuweka maneno yako unayojisikia. Unapinga mawazo yangu unaweza yako kwa jina langu.
Yani nishangae kitu nilichofanya? Tena nimefanya kwa miezi miwili yeye kafanya kwa mwezi mmoja. Unashindwa kuelewa kitu kidogo na maelezo ya ziada sasa mambo magumu utayaelewaje.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshana Jr, Natetemeka siamini ninachokisoma..
Mungu pekee anajua ninavojisikia juu ya Robin.
Karibia mwezi mzima namtafuta nijue progress yake then kuna kitu nimeandaa incase alipo( maana lastly alinambia yuko Dar kwa mama mmoja ) hajaanza kuona mwanga nimchukue tuendelee na michakato tuliyoanza anione live nikiendelea nayo apate tumaini.
Baada ya kuwasiliana na kaka mwingine tukagusia issue ya Robin Friday akanambia amefungiwa simu, nikapotezea issue nikijiambia nitamtafuta tena kwa pm Jf au nipige simu mtwara wakanitafutie mawasiliano kwao.

Sijui niandike nini Mimi.
Nina deni kubwa kwa Robin.
Process ya kushughulikia suala lake kuanzia tamisemi mpaka wizarani imekuwa too slow..
Aaahhhh Mungu wangu na Baba yangu!!!
Wacha nishukuru tu sina naweza sema kwa usahihi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana mkuu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Well said my dear, Mungu atusamehe na kutuhurumia
Tumepoteza watu wawili ndani ya muda mfupi ambao walihitaji msaada kwetu ambao ni fasi dwasi na mpauko. Tunatakiwa tujitafakari, tunakwama wapi. Halafu pia wale ambao tumezoea kukejeli kwenye nyuzi za wahitaji tuache hiyo tabia, tunaongeza maumivu kwa wahitaji.

Kama unaona huna uwezo wa kumsaidia kifedha au kwa namna yoyote inayohusisha matumizi ya kile ulichonacho basi msaidie hata ushauri. Kama unaona hata kumpa ushauri huwezi basi ni vyema ukapita kimya.

Dunia inazunguka, inaweza kutokea siku na wewe ukalazimika kuomba msaada humu, na utaweza kuona maumivu ya mtu kukejeli tatizo lako yanavyouma kuliko tatizo lenyewe. Jf ina deni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wanaojiua wanakuwa hawako kweli hali ya kawaida kimawazo. Wewe unasema hivyo kwa sababu uko kwenye hali ya kawaida. Ni kama mtu asiye na homa anayemcheka mtu mwenye homa aliyejifunika blanketi wakati kuna joto kwa sababu ya baridi. La muhimu ni kujichunga na kuomba Mungu tusiwe kwenye hali hiyo. Nikupe mfano. Miaka ya nyuma kuna dada mmoja alijiua kwa kunywa sumu. Siku ya mazishi wakati wanachimba kaburi, jamaa mmoja akawa anajeli na kusema tuchimbe shimo refu kabisa ili asipate nafasi ya kurudi kwani amekufa kwa ujinga wake. Baada ya mwaka yule jamaa naye akafa kwa kunywa sumu.
Nimekusoma sana,nimekuelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nilianza kumfahamu kupitia uzi ule na niliusoma a-z nikaelewa dhamira ya ndani ya mleta uzi na nilijua hatanii japo uwasilishaji wake ni kama masihara.

Nilimfuata PM straight, sasa ya huko PM tuyaache, ila huku ndani kuna watu wana roho zilizopungukiwa ubinadamu. Tupendane ndugu zangu, kejeli na ndugu yake madharau, nk sio fungu letu.
Tatizo kubwa ni kwamba kuna watu wengi wanaanzisha thread za kuomba msaada au kutishia kujiua wakati ni matapeli au wanatania. Kwa mfano huyu marehemu alipoanzisha thread moja alikuwa anaulizia kama utani anataka kujiua na aambiwe njia nzuri. Kwa mtu amabye hakuwa anafuatilia ile thread kwa kusoma yote, au hajasoma thread zake nyingine alizoanzisha moja kwa moja angechukulia kama ni utani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ni mhanga mkubwa wa hili... Nisingekuwa imara ningepata tabu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Jr we angalau una silaha. Si unaweza kuwaroga tu ukamaliza mchezo asubuhi na mapema?

Kuanzia sasa nategemea mods watakuwa proactive kidogo. Itakuwa poa sana na JF pataanza kuwa mahali salama. Kuna sababu akina Zuckerberg wanatumia mamilioni ya dola kupambana na bullying kwenye mitandao yao kwa sababu wanajua madhara yake ni makubwa; na wenyewe wanaweza kuwa liable.
 
Sana waache kutoa lawama.
Kuna watu mpaka muda huu hawawezi kushika simu zao kwa presha ya hili jambo sababau walikuwa ni msaada kwa kijana sasa taarifa kama hizi zinashtua sana.
Alikuwa ndani ya mikono salama humu ndani, pengine kuna mengine ya ndani hatuyajuo yaliyokuwa yanamtatiza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli. Na inavyoonekana marehemu alikuwa na mawasiliano na watu wengi sana huko PM na wengi wao walijaribu kumsaidia kwa kadri walivyoweza. Ni wazi alikuwa amedhamiria kweli kujitoa uhai; na msaada wa kitaalamu kisaikolojia pengine ndiyo ungeweza kusaidia.

Wote waliojaribu kumsaidia na wale ambao walipuuzia maombi yake najua sasa wanajisikia vibaya sana. Hii ni hali ya kawaida. Sense of guilty. Pengine ningefanya hiki au kile marehemu asingejiua. Ukweli hata hivyo ni kwamba mtu akishafikia hatua ya kukata tamaa na akaamua kabisa kabisa kujiua hata wangefanya nini angejiua tu. Labda tiba ya wataalamu wa magonjwa ya akili na watu wa saikolojia ndivyo vingeweza kumletea ahueni.

Wote hawa wanaojilaumu wakae wakijua kuwa siyo kosa lao kuwa marehemu aliamua kujiua pamoja na jitihada zao zote zilizofanya mpaka ada yake ikalipwa, vyeti vyake vikaachiliwa na ahadi ya kazi akapata. Wamshukuru Mungu kwa moyo wao mwema na wasonge mbele. Tukio hili basi liwaachie alama chanya katika mioyo yao kuhusu maisha, upendo, wema na ubinadamu. Mungu Ataponya majeraha yao. Marehemu Alale salama [emoji1545][emoji1545][emoji1545]
 
Uhai mwingine umetutoka.. Ni wa mwana JF mwenzetu... Mpauko! Apumzike kwa amani... Nimepitia mada ya tangazo la kifo chake na mada zake nyingine nyingi... Nimeona sononi na majuto katikati ya maandishi ya wengi
Majuto ya kukejeli
Majuto ya kutochukua hatua kwa wakati sahihi
Majuto ya kuchukulia mizaha
Majuto ya kuupuuzia...
Nina hakika hata viongozi wa JF nao wanajuta kwa namna moja au nyingine.. Pengine kwa kutojali na kuweka barrier kubwa kati yao na wateja wao (wanachama) labda wakiwa busy zaidi na kusajili wanachama wapya, kurekebisha nyuzi, kuzifungia, kuzihamisha kuziondoa na kutoa adhabu
Kuna moja lilipaswa kuwepo na pengine limepuuziwa MAWASILIANO kati ya viongozi na wanachama na sio hivi ilivyo sasa.. Uhafifu mkubwa wa mawasiliano

Kuna sababu kubwa na muhimu sana kwanini watu wanakimbilia JF kama sehemu sahihi ya kusaidika kiroho na kimwili.. Slogans za HOME OF GREAT THINKERS.. where we dare to talk openly, zimewavutia wengi wakubwa kwa wadogo na watu wa kaliba zote kwenye jamii

Mpauko ameondoka.. Hatuishi milele! Lakini je pale alipodhani ni kimbilio sahihi hakujutia kwa aliyokutana nayo? Je wewe u mmoja wao waliomkebehi na kumkejeli au ni mmojawapo uliyempa faraja, tumaini na kumtia moyo?

Tuna ombwe kubwa sana kwenye jamii yetu.. Tumekuwa busy na ya kimwili kuliko ya kiroho... Ya kiroho tumewaachia watu wa dini tukidhani kuwa ni watu sahihi.. Lakini tunasahau kuwa ya kiroho ni zaidi ya mahubiri na mawaidha kwenye masinagogi.. Kule kuna vigezo masharti, mipaka na taratibu... Sio sehemu za kuongea kwa uwazi
Jamii haina muda na wanajamii... Habari mbaya ndio huwa habari kubwa kuliko habari njema! Kushindwa kwa wengine ndio mashangilio na furaha ya wengine..
Wazazi hawana muda na watoto
Mke hana muda na mume
Mume hana muda na mke
Ndugu hawana muda na ndugu
Hakuna mawasiliano ya kifamilia, hakuna mawasiliano ya kikaya hakuna mawasiliano ya kijamii ni kila mmoja na lwake.. Yanafanyika yale ya kimwili tuu tena kwa mipaka na yanayoonekana ni muhimu
Watu hawana pa kukimbilia.. Huko mitandaoni ni ujinga mtupu... Misaada na ushauri unaoombwa ni vituko tupu.. Mtu anaomba ushauri uliojaa mizaha na porojo... Watu wakikimbilia nyumba za imani huko nako kuna yake.. Hakuna cha bure
JF imeonekana kama sehemu sahihi... Je tunalitambua hili? Maombi yameshatolewa mara kadhaa kuwa kwenye maboresho walau liwepo jukwaa la misaada ushauri na kutiana moyo! Misaada si lazima iwe pesa la hasha.. Lakini liwepo jukwaa maalumu kwa mambo hayo...

Natambua mtanziko uliopo kati yetu kwakuwa ni vigumu kumjua nani mkweli nani muongo.. Nani mhitaji wa kweli na nani mzugaji... Tumeshatapeliwa sana hapa kwa kudhani tunasaidia penye tatizo la kweli kumbe hamna kitu... Lakini hii yote imetokana na sisi kudili na mwili zaidi kuliko roho...
Tunahitaji kuwa na jukwaa la kiroho lenye dhima ya kutoa misaada na ushauri wa mambo magumu wanayokutana nayo watu.. Tusiwe busy tu na majukwaa mengine.. Sasa hivi kejeli ni nyingi kwakuwa hakuna jukwaa maalumu la haya mambo... Hatujachelewa bado tunaweza kufanya hata sasa
Mwisho nilikuwa na mawasiliano ya karibu na marehemu Mpauko mwalimu aliyekuwa na tatizo la uziwi... Kwenye kujitambulisha kwangu aliwataja wana JF wawili kama reference Avriel na @manengelo

Kuepuka majuto mengine tusiwadharau na kuwakejeli tena wale wote wanaokuja na shida mbalimbali hapa.. Kama hutoweza kutoa hata neno la faraja basi at least usikejeli... HUJAFA HUJAUMBIKA... Na ya kesho huyajui

Hii barua yake ya kuomba msaada nadhani wengi mnaikumbukaView attachment 1368556

Sent using Jamii Forums mobile app
@maxence melo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu wangu!!!!
Huyu member alikuwa kweli ana matatizo ya kusikia.
Na kuna rafiki humu alikuwa anamuunganishia kazi ya ualimu akamsafirisha toka mkoani mpaka alipokuwa rafiki akafanya interview.
Lakini yule rafiki akaniambia jamaa ni shida sana kuongea nae na kufundisha itakuwa ngumu lakini akampa nauli na kumuahidi shule ikifunguliwa basi itabidi aje wampe probation kama ya mwezu kuona kama ataweza lakini kama asipoweza atamsaidia kivingine hapa sikumbuki alisema hearing aids au sijui nini sikumbuki kwa kweli
Kiukweli sijui ni nini nikajikuta namshawishi yule rafiki ampe nafasi kwani hata mimi nilifundishwa na mwalimu kipofu Advance level na ni mwalinu pekee aliyekuwa anasikilizwa na wanafunzi akaeleweka, ni mwalimu bora kabisa.
Rafiki yule alikuwa busy busy nami busy sana basi hatukuongelea ishu ya huyu mpaka sasa.
Mda huu ninaona hapa amejiua.
Aiseeee nimesikitika sana.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi mwenyewe nimehudhuria sana pale CCBRT Msasani lakini naona kama nimepoteza hela yangu tu.
Yaani kila ikifika leo, ya jana afadhali.
Tatizo kila siku linakuwa.
Udogoni nilikuwa nasikia fresh tu.
Ila navyozidi kukua ndio tatizo linapanuka.
Hakuna hata ndugu mmoja anayenipigia simu zaidi ya kuchati kupitia sms.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi mwenyewe nimehudhuria sana pale CCBRT Msasani lakini naona kama nimepoteza hela yangu tu.
Yaani kila ikifika leo, ya jana afadhali.
Tatizo kila siku linakuwa.
Udogoni nilikuwa nasikia fresh tu.
Ila navyozidi kukua ndio tatizo linapanuka.
Hakuna hata ndugu mmoja anayenipigia simu zaidi ya kuchati kupitia sms.

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana. Hosp wanasema shida ni nini? Ulishajaribu tiba kwa njia ya mitishamba? Pole sana...nakutia moyo mkuu, usije ukakata tamaa. Mungu akuinue kwa upendo mkuu nawe uione asubuhi yako ikiwa njema na yenye kusikia kila jambo! Jipe moyo, tuko pamoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom