TANZIA Mwana JamiiForums mkongwe, Dena Amsi afariki dunia

TANZIA Mwana JamiiForums mkongwe, Dena Amsi afariki dunia

Nimeweza kupata details za mpendwa wetu Dena Amsi kwa mtu wa karibu ana ambaye aliweza kuhudhuria mazishi yake. Dena (Leah F. Komba) alikuwa mdada mwenye kujituma sana na aliweza hata kupata kazi nchini Kenya (akihama taasisi kubwa Tanzania alipofanya zaidi ya miaka 7). Kenya alifanya kazi kwa miaka 3 na miezi kadhaa kabla hajarudi Tanzania na kuajiriwa tena na taasisi moja ya habari Tanzania mpaka umauti ulipomfika. Mungu anaufahamu ukweli wa afya yake mpaka anafariki. Poleni sana ndugu na jamaa na mwanaye wa kiume ambaye atakuwa kwenye 20 years or a bit less (mvulana). Rest in Peace Leah.
Duh.....
 
daah!kifo cha ghafla kinauma
Msiba wa Dena Amsi umetusitua wengi sana maana siku Moja kabla ya kifo chake nilipiga nae story sana nyumbani kwao. Alikuwa mzima kabisa na kiukweli alikuwa MTU wa watu kaniaaidia mambo mengi sana mpaka siku ya mwisho kuonana nae nilikuwa natafuta sanduku la posta la manispaa ya kinondoni alinisaidia akampigia rafiki yake nikalipata. Kwa wale ambao mngependa kuja kuwapa pole wafiwa msiba ulikuwa BUNJU A shule maeneo ya juleva.mungu ailaze pema roho ya Dada yetu Dena Amsi(Leah Flavian komba) jina lake halisi
 
Duh umenishtua sana kumbe Dena Amsi ndio Leah Komba
Binafsi namfahamu marehemu (Leah Komba) nimewahi kufanya field ofisi ambayo alikuwa anafanya kazi na nimewahi kumfanyia kazi zake nyingi nakumbuka mara ya mwisho tuliwasiliana alipata kazi Kenya akahamia Nairobi
Pumzika kwa amani Leah
jf ni msitu ndo maana tunaambiwa tuishi vzr na watu humu
 
Loeli vipi nadhani mwanzo watu walieleweka kuficha privacy ya mtu wewe umechunguza na kuamua kuanika... Humu kuna walioshiriki msiba na mazishi kuna ndugu na jamaa... Walielewa umewahi sana... Inaweza kuwa umeguswa kama sisi ila Mdogo Mdogo me natamani hata tuwape familia rambirambi

Loeli JF-Expert Member
[HASHTAG]#974[/HASHTAG][
Yesterday at 6:48 PM
Nimeweza kupata details za mpendwa wetu Dena Amsi kwa mtu wa karibu ana ambaye aliweza kuhudhuria mazishi yake. Dena (Leah F. Komba) alikuwa mdada mwenye kujituma sana na aliweza hata kupata kazi nchini Kenya (akihama taasisi kubwa Tanzania alipofanya zaidi ya miaka 7). Kenya alifanya kazi kwa miaka 3 na miezi kadhaa kabla hajarudi Tanzania na kuajiriwa tena na taasisi moja ya habari Tanzania mpaka umauti ulipomfika. Mungu anaufahamu ukweliwa afya yake mpaka anafariki. Poleni sana ndugu na jamaa na mwanaye wa kiume ambaye atakuwa kwenye 20 years or a bit less (mvulana). Rest in Peace Leah.
 
Kuna wakati unaweza kudhani kwamba utamuona akitembea, utamuona akicheka na hata kukutania. Amezimika kama taa, Amezimika kama mshumaa katika ya upendo. SICHOK KUKWAMBIA NENDA UKALALE SALAMA, LAKINI UKIMUONA NEEMA MWAMBIE NAMSALIMIA
Mkuu za kupotea Neema yupi
 
Leah Komba daah sijawahi kukujua ndani ya JF ila nimekujua nje ya JF toka 2008 kupitia kwa mdogo ako Stellah , nenda mama kapumzike ila umejua kuniliza dada yangu!!! Wakati mdogo ako stella ananitaarifu kuhusu kifo chako niliona kama ndoto!!! Juzi nakuona kwa mara ya mwisho kwenye jeneza kama umelala baadae utaamka, kumbe utohamka tena!!!....pumzika kwa amani dada angu tupo nyuma yako.
Wekeni picha sasa tumfahamu Marehemu
 
Back
Top Bottom