Mamndenyi
JF-Expert Member
- Apr 11, 2011
- 43,242
- 60,939
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mbarikiwe sana kwa kazi njema.Tumemkabidhi dada Atu dada yake na binamu sh 215,000.
HOE jana aliacha msibani sh 20,000.
Jumla 235,000.
Wabarikiwe sana
Hahahahah loooh!! Shem habari za siku? Hujaacha vituko tu!!!Kuna mmoja alikuwa anamtukana sana mtu humu,akaibukiwa na ID ya kike akadhani dodo limekuja ,wakapanga kukutana akala makofi miguu miguu yake ndo ilimsaidia kukimbia
Mkuu,humu hatuwezi kufanana coz tunatoka different back ground,siku zote simamia unacho kiamini bila kujali maneno ya watu,huwezi kuwabadili watu tabia,ni ngumu sana,Kwanza pale kanisani unawezaje kupiga picha?ni kitu cha ajabu sana cha ajabu mno familia inaombeleza wewe unaenda na simu kupiga picha.
Picha alizotuma hornet kapiga kwa kujiiba sana.
Natamani wangeona jinsi yule dada alivylia na kushukuru.
Humu ndani kuna makolo wengi sana, punguzeni ukolo jamani.
Mjirekebishe.
Daah![emoji24][emoji24]Kwa masikitiko makubwa ninapenda kuwapa taarifa ya mdau mwenzetu humu anayeitwa warumi amefariki usiku wa kuamkia leo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa anapambana kwa ugonjwa wa figo.
Warumi alikuwa kijana wa kiume mwenye umri wa miaka 29.
Taarifa hii nimepewa na dada yake muda huu, msiba unaelekea kwao Tegeta .
UPDATE:
Msiba upo Tegeta Nyuki, ukifika Stand unachukua boda au bajaji unawaambia wakupeleke nyumbani kwa Kiboko, maana msiba upo opposite na utaona geti jeusi liko wazi - ingia.
Msiba utasafirishwa kwenda Mbeya, Nonde Mabatini.
UPDATE.
Misa ya kumuaga itafanyika kesho tarehe 27 August saa 8 mchana Muhimbili.
Muda unaenda hivi sasa ni saa 12 na robo misa inaanza saa 8 muhimbili.
UPDATE.
Msiba utakuwepo mbeya mjini machinjioni Nonde kwa Mwasuluka.
Zaidi, soma:
TANZIA - Rambirambi za mwanachama mwenzetu Warumi
Wanabodi, msiba ni kuzika. Ninawaomba tukamzike mwenzetu, tukamzika vipi?kwa kushiriki ibada ya kumuaga pale kanisani Muhimbili saa 8 mchana. Je, tutaenda kuaga hivi hivi mikono mitupu hapana ninaomba tujichange chochote kabla ya saa 8 mchana tukabidhi kwa familia. Ninaomba rambirambi zote...www.jamiiforums.com
Zile za kwenye ile thread ya ku-selfika?Anyways acha private zilindwe.
Maandiko,
Mathayo 18:18
“Amin, nawaambia, lolote mtakalolifunga duniani litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote mtakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.
Siku nikiondoka wekeni picha yangu, Mshana Jr atakuwa nayo.
Nafikiri wako na tension kubwa maana wajuba humu wamemwaga nyongo sana hivyo ukihoji tu chochote wanajua una washambulia,tuwaelewe tu..Mimi binafsi nimempa faida ya mashaka/ benefit of doubt.....
anaonekana ni mgeni katika ukusanyaji wa michango na kutoa taarifa kwa usahihi
Bado nipo Shem ,humu heri tuishi na watu vizuriHahahahah loooh!! Shem habari za siku? Hujaacha vituko tu!!!
[emoji23][emoji23][emoji23]dah mimi ni moto wa jino kwa jino aisee na sipendagi ujinga wallah na ninapenda kuheshimiana na mtu licha ya kubishana kwa hoja na sio kuzalilishana, mwisho naweza kurudisha na mimi tusi nikala ban bure. Warumi anahitaji tuzo kwa kweli pia Kuna kipindi huwa sijisikii kuingia humu JF na ku comments kabisa huwa nafanya JF detoxication lohUwe mtu usiejali [emoji16]
Binamu alikua hajali umuite dada,kaka, mama, shoga utajaza mwenyewe hajali ye anafocus na ubuyu tu.
Ntammiss yule kaka [emoji17]